Ujumbe kwa Prof. Assad: Hatutaki Rais anayesikiliza kila mtu na la kila Mtu!

Ujumbe kwa Prof. Assad: Hatutaki Rais anayesikiliza kila mtu na la kila Mtu!

Kati ya Prof Assad na wewe Mzee Mwanakijiji naona wewe ndiyo IMEFYATUKA vibaya. Hivi kweli unathubu kuunga mkono maamuzi ya KIIMLA yaliyofanywa na Magufuli kama Jeshi kuingia biashara ya korosho, kuwabomolea nyumba wakazi wa Kimara-Kinamba bila fidia, kujenga uwanja wa 3km runway kijijini kwake Chato, kukataa kutunza takwimu za COVID-19 na kuwapima Watanzania.

Rais ana wasaidizi wake na wapo pale kumsaidia. Hakuna binadamu anayejua kila kitu.

Hatutaki turudi kwenye ile hali ya ya yule hayawani tuliyemzika Chato ambaye akiamua kukupiga risasi anatuma kikundi chake kama alivyomfanyia Tundu Lissu
Ukionekana unaleta namna gani vp unashughulikiwa tu hata Kikwete alimshughulikia Ulimboka.
 
Tena kiuhalisia walitaka si asikilize ushauri wa kila mtu, Bali walichotaka ni kumfanya asikilize ushsuri wa kila mpumbavu aliyejiona ana nguvu Fulani, Viongozi wa Dini, Viongozi wa Taasisi, Siasa, Wafanyabiashara, Wawekezaji, Matajiri, nk...

Makundi yote hayo yalitaka kumpanda kichwani wasijue ni Kisiki Kizito. Matokeo yake ndio kutengeneza hoja mufilisi kupitia vibaraka wao kama Assad.

Ni wa kupuuzwa tu.
Kinachoonekana nchi yetu ilishatekwa. Mabeberu waliwekeza kwa watu kiasi kwamba walitegemea enzi za Dkt Magufuli wakisema kitu basi wasikilizwe ili mambo yao ya kuiibia nchi yaendelee, na ndicho Dkt Magufuli aliwahi kusema serikali yake haiambiwi kitu na mtu yeyote, wakakasirika sana. Sasa kwa Mama inaonekana wanatamani sana tena sana akubali kila aina ya ushauri kitu ambacho ni hatari sana
 
ukweli mpaka sasa Watanzania hatujajua tunataka nini, hata hicho tunachotaka tukipewa bado tutasema hapana hatukutaka hivi..

Kifupi, Watanzania ni kama binadamu aliyeruka stage katika ukuaji wake, binafsi naamini zipo stage ambazo Watanzania na WaAfrica tumeziruka na ndio chanzo cha kila kero tuliyonayo leo hii..

Yapo ya msingi sana yanayoonekana live ambayo kwa nguvu zetu wote tungeyapambania tungeweza kujinasua.... Mfano ELIMU DUNI KWA WATU WETU NI JANGA MPAKA SASA, kwa pamoja tungepigania hili kuna mambo tungeweza kuweka sawa sawia kabisa bila hata hii Katiba mpya.

MENTALITY YA KUJITEGEMEA NA WATU KUFANYA KAZI KWA BIDII, hili nalo halina na halihitaji Katiba mpya ila linaweza kuanza sasa au leo, Watu wote wafanye kazi kwa bidii na akili zetu zitoke kwenye mentality ya kumtegemea Mzungu baadala yake turudi kwenye akili za kujitegemea na kuwajenga watu wetu huko..

UZALENDO NA UPENDO BAINA YA WATANZANIA WENYEWE, sidhani kama hili nalo ambalo pia ni tatizo kwenye jamii linahitaji katiba mpya na ikija watu ndio watakuwa Wazalendo...Watanzania wenyewe kwa wenyewe tuna tatizo la kutopendana na kutokuwa wazalendo kwa Taifa letu kiasi.... Mentality hii inahitaji nguvu ya pamoja na mipango ya pamoja ili wote tulipende taifa letu na wenyewe pia kama watanzania tupendane popote pale...
Ulichokieleza ni wote tunahitaji kubadilika ili tuweze kuyafikia mabadiliko tunayohitaji ila ubaya ni kwamba huwa hatuhitaji kubadilika ila tunataka mabadiliko na ndio maana tunalilia katiba mpya kwa kudhani kwamba kila kitu kitajiseti tu chenyewe.
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Mojawapo ya maajabu makubwa ni hili la watu kuamini kuwa ujio wa Katiba Mpya utawapa Rais ambaye ataweza kudhibitiwa na "taasisi". Kwamba, Katiba Mpya itazuia Rais kufanya lolote na kuwa atakuwa analazimishwa kusikiliza mashauri mbalimbali. Prof. Assad ni miongoni mwa watu ambao amejionesha kukerwa mno na jinsi Magufuli alikuwa; hasikilizi, hapigwi maneno ya wataalam, na watendaji wenye maneno ya kitalaamu. Inawezekana siyo yeye tu bali wapo wengine ambao nao walikuwa wanakerwa kuwa Magufuli "hasikilizi". Na tunawaona wengine ambao nao wanafikia mahali pa kusema "Magufuli hakufanya lolote".

Sasa, wanataka tuwe na Rais ambaye anapewa ushauri na kila mtu na anatakiwa kusikiliza kila ushauri kwani asipousikiliza au kuukubali basi anakuwa "haambiliki". Inanikumbusha maneno yaliyosemwa wakati wa Nyerere; aliitwa pia "Haambiliki". Ati Magufuli alikuwa anawakera kwa sababu walitaka awasikilize na asiwaulize; akubali bila maswali! Sasa inawezekana wanaona Rais Samia ni wa kuambiwa kila kitu; kwamba wanampa mashauri ya kila namna na anaonekana anayafuata. Inawezekana wanaona kuwa Rais Samia anawakubalia kila mashauri hata ambayo matokeo yake siyo mazuri. WAnachofurahia ni kuwa wamelipata "sikio la mama".

Ndio maana tunaweza kuona wanashindana kukandia awamu ya tano (ambayo wao walikuwemo). Inaonekana kabisa kuwa ili mama akupe sikio inabidi umpapase kwa maneno mazuri ya kumkandia mtangulizi wake. Magufuli hakujenga kiwanda hata kimoja, uwekezaji ulipungua, maisha yalikuwa Magumu, watalii walikimbia, uchumi ulidorora... wanasema na kusema ili waseme "ila sasa awamu ya sita" mambo yamekavaa vizuri! Wanajaribu kutenda kana kwamba Rais Samia alishinda uchaguzi mahali bila ya Magufuli! Lakini hawa wanaotaka Rais anayesikiliza kila ushauri inabidi tuwakatae.

Tunawapinga na kuwakataa kwa sababu wanataka kumchukua Rais kuwa mateka wa fikra zao na mashauri yao. Watamshauri akikataa wataanza kusema "Rais hatusikilizi tena". Ukweli ni kuwa Rais - hata ije Katiba Haramu Mpya - hatakiwi kukubali ushauri wa kila mtu, hata kama ni maprofesa kama Assad. Anatakiwa kusikiliza na kuuliza; hatakiwi kukubali bila maswali! Na ni hatari zaidi kumtaka Rais awafurahishe kwa kuwa karibu na watu wenye kumsifia na kumwambia mambo mazuri.

Profesa Assad na watu wenye fikra kama zake hawamtakii mema Rais, wanamtega, na wanajaribu kumfanya awe Rais wa picha!

Hili tunawakatalia; waache ufyatu!

MMM
Mi nilijiuliza kitu kimoja! Why Prof Assad ameitwa kwenye kikosi kazi na si Ludovick Utouh? Nikakumbuka kuwa "Anaemlipa mpiga zumari ndiye anaechagua wimbo".

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yule fala wenu alikuwa kichaa..Mfano mdogo maamuzi yake ya kipumbavu ndio yalisababisha Mazao yoote kuporomoka bei na yakawa yanaoza tuu Kisa yeye halimi ..

Huyo punguani wenu aliharibu uhusiano na Nchi zote majirani,wabia na washirika wa maendeleo nk..

Nchi ikafikisika akaanza kupora watu hela mara aseme atabadili sarafu Ili walioficha pesa ndani ziwaharibikie,akaanza kuuza vitambulisho kwa wanyonge wake,kubambikia Kodi,kufanya maigizo nk..

Akashindwa kuajiri na kupandisha mishahara na madaraja kwa watumishi miaka yote 6 huku akisingizia kujenga sgr and such nonsense wakati hadi anakufa alishindwa kukamilisha km 200 tu za sgr..

Huoni ulivyo mjinga na mpumbavu kama huyo unaemshabikia? Majitu kama yule huwa yanauwawa kote Dunia,ni hasara tupu maana kwa miaka 6 tumefanya marktime..
Maneno yako tu yanaonyesha una chuki ya kwako dhidi yake..kiongozi hachaguliwi kufurahisha mtu mmoja mmoja! Pili, si mara ya kwanza bei za mazao kushuka, hata huko nyuma zmewahi kushuka! lkn ni nani kati ya viongozi wote alikuwa mtetezi wa kweli wa wakulima? Uhusiano gani uliharibika, mbona AfDB wamefadhili miradi mingi kipindi chake kuliko wakati wowote..ni ujinga kutetea uhusiano wa kinafiki na kinyonyaji kiongozi mwenye uchungu na hali ya maisha ya watu wake na rasilimali za nchi hawezi kukubali uhusiano wa kudharauriana! Wajibu mkubwa wa serikali na kiongozi mkuu ni kuzuia mfumuko wa bei na si kupandisha mishahara..kwanza kuthubutu tu kuanzisha JNHPP, SGR, madaraja makubwa, meli na vivuko nk inahitaji ujasiri wa aina yake, yeye aliweza, mbona wengine walishindwa..hakuna mtu ataishi milele hapa take that note! everyone will die, be t ulikuwa mwema sana, uliuwa wengine, vyovyote..huhitaji kukumbushwa jambo hili km una akili timamu! Kiongozi huwezi ukawa na furaha kuongoza nchi imejaa udhalimu kila mahali tena wa wazi..nadhani ulikuwa unamsikia yeye hakuwa anaogopa kifo, nani mwingine ulimsikia anasema hivyo! aliyoyafanya yalitosha kwa muono wa aliyemuumba na kumjalia kupata hiyo nafasi..hiyo siyo kesi yetu, tumia vzr akili ulizopewa kijana usije kufuru bure kwa chuki zisizo na kichwa wala miguu..
 
Watoto wa mjini muda wenu huu kutamba megeni nchi mtakavyo, Jiwe alikuwa mshamba ndio maana alikuwa anawazingua na kuwafanya mupitie kipindi kigumu. Unajua Jiwe alikuwa anazingua aliifunga nchi kwa ushamba wake ila sasa mama kafungua si unaona hata panya road nao wamepata uhuru wao achilia hao wauza ngada waliyokuwa wamefulia unga hakuna mateja hawakuwa na jinsi kuacha unga, sasa hivi siwaoni kule muhimbili sijui ndio wamerudi walipotoka.

Ila mama yupo vizuri ndio raha ya watoto wa mjini.
 
Sidhani kama Prof. Assad alimaanisha hivyo,kuwa tuwe na Rais anayemsikiliza kila mtu. Kumekuwepo na madhara makubwa sana ya kuwa na viongozi wasioshaurika viongozi wanaodhani na kuamini wao wana akili kuliko watu wote. Hata mipango/miradi yao mingi ni ya kukurupuka pamoja na kuwa na nia njema. Nia njema haihalalishi njia mbovu. Lakini naamini wapo watu walioshauri kwa utalaam walikuwa nao na hawakupewa nafasi.
Nilichoelewa anachomaanisha ni kuwa na mfumo imara wa kumdhibiti Rais dhidi ya matumizi mabaya ya madaraka.
Marekani ingekosa mfumo imara,watu Kama Rais Trump kwa yale aliyokuwa akijiapiza kuyafanya akichaguliwa kuwa Rais, sijui kama hata nyie mnaoishi huko mngesalimika na bila shaka na ule ukuta wa kuitenga Mexico ungekuwa umeisha.
Mfumo imara utamlazimisha Rais kuheshimu sheria na katiba ya nchi.
Mfumo imara hautaruhusu kuunda sheria kandamizi, kama za vyombo vya habari, au kuunda sheria za kulinda watu wasishtakiwe wakiwa madarakani ndo tunajikuta na watu Kama kina Ndugai anafanya anachotaka kwenye mhimili mzito Kama bunge kisa anayo kinga.
Mfumo imara utazaa bunge huru,leo bunge letu linategemea na nani ni spika kwa wakati huo, angalia kwa kesi zile zile alivyoamua Ndugai na kesi zile zile anavyoamua Tulia.
Mfumo imara utatupa mahakama huru, angalau kidogo kama mahakama zilee chini ya Mzee Nyalali au Barnabas Samata,ulikuwa huwezi kuwaona kwenye shughuli zozote za propaganda,siyo hawa wa sasa, mara kwenye makinikia na wao wapo,halafu sijui kama wenye hayo makinikia,hawaridhiki unawategemea waziamini mahakama zetu,wakati umemuona CJ yuko kiti cha mbele anasikiliza anatikisa na kichwa kwa huzuni. Mfumo imara utatupa tume ya uchaguzi huru siyo hii ambayo nayo inaushangaa uchaguzi wa 2020 ulivyoendeshwa.
Mfumo imara utaweka mipaka ya kiutendaji kwa vyombo vyetu vya dola.
Polisi au JWTZ watajihusisha na majukumu yao ya kikatiba tu na kamwe haitawezekana kuwatumia kisiasa.
Mfumo imara utawapa wananchi heshima kuwa wao ndio wamiliki wa nchi hii na raslimali zake, na siyo kuambiwa eti Rais ametoa fedha za mradi huu kana kwamba ni za kwake na ni hisani yake,utaondoa kauli za kuzimu kama zile,eti mkichagua upinzani hatuwaletei maendeleo,kauli za kibaguzi na wizi mkubwa,unawanyima maendeleo wakati na wao ni wachangiaji wazuri wa pato la nchi kupitia Kodi zao.
Mfumo imara utajenga watanzania wenye kujiamini,wenye kujua haki zao na kuzisimamia na siyo,tabia ya sasa ya kuwa na watu wanafiki wasioaminika,kwao ni kujipendekeza kwenda mbele kisa Rais aliyeko ni kabila lake, au wa dini yake au chama chake.
Tunatamani kuwa na wasomi angalau kidogo wa enzi zile za kina Prof. Chachage, Haroub Othman, Mwesiga Baregu, Mwaikusa na wengine ambao wakikutana Nkurumah hall mpaka nchi jirani zinafuatilia.
Tuwe na wataalam wenye exposure ya kutosha kusimamia raslimali zetu, na siyo tunayoyashuhudia sasa. Tunao wahandisi wazuri midomoni wape kazi sasa ushangae. Bidhaa nyingi tunazoona toka china ukisikia wanaozitengeneza hata diploma kama wanazo ni wa kuhesabu. Hivyo lazima tuwajengee uwezo wataalam wetu kwa kukusudia.
Ni ngumu sana kuamini Maendeleo yetu yatategemea wawekezaji kutoka ulaya na Asia bila kuhakikisha tunawawezesha watu wetu kupata utalaam na wao kuwa na uwezo wa kuanzisha viwanda wenyewe. Wakati Saab scania wanafungua tawi lao hapa Tanzania 1972, pia na Brazil walianzisha, leo ya kwetu imekufa wakati ya Brazil wanatengeneza scania 95% ni 5% tu wanaagiza Sweden.
Hatuwezi kujilaumu na kujuta bado tunayo nafasi ya kufanya vizuri zaidi.
Tupiganie tupate mfumo imara.
 
Naona hukumuelewa Prof. Mussa Assad.

Yeye hakumaamisha kwamba Rais anapaswa kumsikiliza kila mtu hapana, Tatizo kubwa ni Rais kushindwa kuwasikiliza wataalamu. Kuwa Raisi Haina maana unamfahamu kila kitu.

Kila Nyanja ina wabobezi wake kitaaluma, na ni lazima tuheshimi ushauri wa kitaalamu tunaopewa na wenye taaluma zao.

Huwezi jiamulia Tu as if Hii nchi ni familia yako. Ikiwa wanaukoo hukaa kikao kushauriana kwa pamoja na kufikia muafaka iweje nchi yenye watu zaidi milioni 60 iamuliwe na akili ya mtu mmoja?
Matokeo ya maamuzi binafsi yasiyozingatia weledi tumeyaona.
Zamani nilikuwa nakuelewa sana Mzee Wangu Mwanakijiji Ila siku hizi sijui umekuwaje.
 
Muovu kwa nani hasa..hivi kuna kesi hata moja ya mtu kuonewa bila kosa, mbona ingawa hayupo hakuna kesi mahakamani ya mtu kufanyiwa uonevu? Ni matendo gani mabaya dhidi ya raia yalifanyika awamu ya 5 tu tofauti na awamu nyingine..hivi tathmini ya Rais km ni mzr au mbaya ni ile ya kila mtu anasema km mtanzania au anasema kwa niaba yake mwenyewe? Nadhani kiongozi yupo kwa ajili ya watanzania waliopo na watakaokuwepo..mimi nikimchukia Rais kwa sabb alielekeza wenye vyeti vya kughushi waondolewe kazini na mimi ni mmojawao si sahihi! Haki huinua taifa..taifa haliwezi kujengwa kwa wizi, kupendeleana na kubembelezana..lazima kila mtu apende hata alazimishwe na sheria kuishi kwa HAKI na kufikiria maslahi ya wengine..ni km mashutumu mengi kwa awamu ya 5 ni yale ya ubinafsi zaidi kwa mgongo wa demokrasi na uhuru wa mtu mmoja mmoja..ni mambo madogo sana kulinganisha na mengi makubwa yaliyofanyika.
Kwa jinsi mifumo yetu ilivyo, unategemea uende mahakamani kushtaki utawala mbovu wa kiongozi hasa kwa ngazi ya urais? Watu walivunjiwa nyumba hapo kukiwa na zuio la mahakama, na aliyeagiza hayo ni rais. Mkuu naona unaongea nadharia ukihisi tumesahau. Huenda ulikuwa mfaidika wa uovu ule hivyo huamini ukweli uliopo. Naona kama unanipotezea muda, nikianza kuweka ushahidi hapa utakuwa huna lolote jipya zaidi ya kusema yaliyopita si ndwele.
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Mojawapo ya maajabu makubwa ni hili la watu kuamini kuwa ujio wa Katiba Mpya utawapa Rais ambaye ataweza kudhibitiwa na "taasisi". Kwamba, Katiba Mpya itazuia Rais kufanya lolote na kuwa atakuwa analazimishwa kusikiliza mashauri mbalimbali. Prof. Assad ni miongoni mwa watu ambao amejionesha kukerwa mno na jinsi Magufuli alikuwa; hasikilizi, hapigwi maneno ya wataalam, na watendaji wenye maneno ya kitalaamu. Inawezekana siyo yeye tu bali wapo wengine ambao nao walikuwa wanakerwa kuwa Magufuli "hasikilizi". Na tunawaona wengine ambao nao wanafikia mahali pa kusema "Magufuli hakufanya lolote".

Sasa, wanataka tuwe na Rais ambaye anapewa ushauri na kila mtu na anatakiwa kusikiliza kila ushauri kwani asipousikiliza au kuukubali basi anakuwa "haambiliki". Inanikumbusha maneno yaliyosemwa wakati wa Nyerere; aliitwa pia "Haambiliki". Ati Magufuli alikuwa anawakera kwa sababu walitaka awasikilize na asiwaulize; akubali bila maswali! Sasa inawezekana wanaona Rais Samia ni wa kuambiwa kila kitu; kwamba wanampa mashauri ya kila namna na anaonekana anayafuata. Inawezekana wanaona kuwa Rais Samia anawakubalia kila mashauri hata ambayo matokeo yake siyo mazuri. WAnachofurahia ni kuwa wamelipata "sikio la mama".

Ndio maana tunaweza kuona wanashindana kukandia awamu ya tano (ambayo wao walikuwemo). Inaonekana kabisa kuwa ili mama akupe sikio inabidi umpapase kwa maneno mazuri ya kumkandia mtangulizi wake. Magufuli hakujenga kiwanda hata kimoja, uwekezaji ulipungua, maisha yalikuwa Magumu, watalii walikimbia, uchumi ulidorora... wanasema na kusema ili waseme "ila sasa awamu ya sita" mambo yamekavaa vizuri! Wanajaribu kutenda kana kwamba Rais Samia alishinda uchaguzi mahali bila ya Magufuli! Lakini hawa wanaotaka Rais anayesikiliza kila ushauri inabidi tuwakatae.

Tunawapinga na kuwakataa kwa sababu wanataka kumchukua Rais kuwa mateka wa fikra zao na mashauri yao. Watamshauri akikataa wataanza kusema "Rais hatusikilizi tena". Ukweli ni kuwa Rais - hata ije Katiba Haramu Mpya - hatakiwi kukubali ushauri wa kila mtu, hata kama ni maprofesa kama Assad. Anatakiwa kusikiliza na kuuliza; hatakiwi kukubali bila maswali! Na ni hatari zaidi kumtaka Rais awafurahishe kwa kuwa karibu na watu wenye kumsifia na kumwambia mambo mazuri.

Profesa Assad na watu wenye fikra kama zake hawamtakii mema Rais, wanamtega, na wanajaribu kumfanya awe Rais wa picha!

Hili tunawakatalia; waache ufyatu!

MMM
Assad angekuwa jasiri asingekanusha siku ile Ikulu kuwa hatukuibiwa 1.5T
 
Kwa jinsi mifumo yetu ilivyo, unategemea uende mahakamani kushtaki utawala mbovu wa kiongozi hasa kwa ngazi ya urais? Watu walivunjiwa nyumba hapo kukiwa na zuio la mahakama, na aliyeagiza hayo ni rais. Mkuu naona unaongea nadharia ukihisi tumesahau. Huenda ulikuwa mfaidika wa uovu ule hivyo huamini ukweli uliopo. Naona kama unanipotezea muda, nikianza kuweka ushahidi hapa utakuwa huna lolote jipya zaidi ya kusema yaliyopita si ndwele.
Hata jengo la TANESCO lilivunjwa pale ubungo..dalili za a corrupt society ni matumizi yasiyofaa ya court injunction, moja ya sifa mbaya za watu wa nchi hii ni ukiukaji wa sheria makusudi, mf. uvamizi wa maeneo makusudi.. wakiambiwa wanakimbilia kuweka zuio mahakamani..jambo la maendeleo ya nchi liko juu ya ubinafsi wa wachache, kiongozi hodari hahitaji kufundishwa hili..ningekuwa nakupotezea muda huo muda unaotumia kila siku kumtukana mtu tena asiyekuwepo si ungeutunza ukusaidie kufanya mambo ya maana kuliko kuupoteza hapa..wewe orodhesha maovu usilete hoja mufilisi unauliza maswali na kujibu mwenyewe..dunia ya leo si lazima muhalifu umshitaki kwny mahakama za ndani ndio maana kuna mahakama ya Africa hapa, hata ile ya the Hague ipo kwa ajili ya jinai zinazofanywa na viongozi dhidi ya watu wake.
 
Hata jengo la TANESCO lilivunjwa pale ubungo..dalili za a corrupt society ni matumizi yasiyofaa ya court injunction, moja ya sifa mbaya za watu wa nchi hii ni ukiukaji wa sheria makusudi, mf. uvamizi wa maeneo makusudi.. wakiambiwa wanakimbilia kuweka zuio mahakamani..jambo la maendeleo ya nchi liko juu ya ubinafsi wa wachache, kiongozi hodari hahitaji kufundishwa hili..ningekuwa nakupotezea muda huo muda unaotumia kila siku kumtukana mtu tena asiyekuwepo si ungeutunza ukusaidie kufanya mambo ya maana kuliko kuupoteza hapa..wewe orodhesha maovu usilete hoja mufilisi unauliza maswali na kujibu mwenyewe..dunia ya leo si lazima muhalifu umshitaki kwny mahakama za ndani ndio maana kuna mahakama ya Africa hapa, hata ile ya the Hague ipo kwa ajili ya jinai zinazofanywa na viongozi dhidi ya watu wake.

Yeye mwenyewe alikuwa jizi la kura sasa sijui ni uadilifu gani alikuwa anasimamia. Tunamshukuru Mungu kwa kutuondolea yule kiongozi muovu bila damu kumwagika.
 
..tunataka Rais anayepanda HAKI.

..Jpm alikuwa kiongozi asiyependa haki, alikuwa na hulka ya ukatili.
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Mojawapo ya maajabu makubwa ni hili la watu kuamini kuwa ujio wa Katiba Mpya utawapa Rais ambaye ataweza kudhibitiwa na "taasisi". Kwamba, Katiba Mpya itazuia Rais kufanya lolote na kuwa atakuwa analazimishwa kusikiliza mashauri mbalimbali. Prof. Assad ni miongoni mwa watu ambao amejionesha kukerwa mno na jinsi Magufuli alikuwa; hasikilizi, hapigwi maneno ya wataalam, na watendaji wenye maneno ya kitalaamu. Inawezekana siyo yeye tu bali wapo wengine ambao nao walikuwa wanakerwa kuwa Magufuli "hasikilizi". Na tunawaona wengine ambao nao wanafikia mahali pa kusema "Magufuli hakufanya lolote".

Sasa, wanataka tuwe na Rais ambaye anapewa ushauri na kila mtu na anatakiwa kusikiliza kila ushauri kwani asipousikiliza au kuukubali basi anakuwa "haambiliki". Inanikumbusha maneno yaliyosemwa wakati wa Nyerere; aliitwa pia "Haambiliki". Ati Magufuli alikuwa anawakera kwa sababu walitaka awasikilize na asiwaulize; akubali bila maswali! Sasa inawezekana wanaona Rais Samia ni wa kuambiwa kila kitu; kwamba wanampa mashauri ya kila namna na anaonekana anayafuata. Inawezekana wanaona kuwa Rais Samia anawakubalia kila mashauri hata ambayo matokeo yake siyo mazuri. WAnachofurahia ni kuwa wamelipata "sikio la mama".

Ndio maana tunaweza kuona wanashindana kukandia awamu ya tano (ambayo wao walikuwemo). Inaonekana kabisa kuwa ili mama akupe sikio inabidi umpapase kwa maneno mazuri ya kumkandia mtangulizi wake. Magufuli hakujenga kiwanda hata kimoja, uwekezaji ulipungua, maisha yalikuwa Magumu, watalii walikimbia, uchumi ulidorora... wanasema na kusema ili waseme "ila sasa awamu ya sita" mambo yamekavaa vizuri! Wanajaribu kutenda kana kwamba Rais Samia alishinda uchaguzi mahali bila ya Magufuli! Lakini hawa wanaotaka Rais anayesikiliza kila ushauri inabidi tuwakatae.

Tunawapinga na kuwakataa kwa sababu wanataka kumchukua Rais kuwa mateka wa fikra zao na mashauri yao. Watamshauri akikataa wataanza kusema "Rais hatusikilizi tena". Ukweli ni kuwa Rais - hata ije Katiba Haramu Mpya - hatakiwi kukubali ushauri wa kila mtu, hata kama ni maprofesa kama Assad. Anatakiwa kusikiliza na kuuliza; hatakiwi kukubali bila maswali! Na ni hatari zaidi kumtaka Rais awafurahishe kwa kuwa karibu na watu wenye kumsifia na kumwambia mambo mazuri.

Profesa Assad na watu wenye fikra kama zake hawamtakii mema Rais, wanamtega, na wanajaribu kumfanya awe Rais wa picha!

Hili tunawakatalia; waache ufyatu!

MMM
Mzee umeibukia wapi
 
hivi wabongo tunataka Rais wa aina gani? anaesikiliza au asiesikiliza? tusifungane midomo tupige kura tujuane!!
Sidhani kama Magufuli alikuwa hasikilizi. Mara ngapi tuliona anasikiliza vilio vya watu kila anapokuwa ziarani sehemu mbalimbali?? Kuna wa kusikiliza ila kuna wa kutimua hapo hapo. Nakumbuka kuna mkurugenzi ama das aliwahi kujikanyaga maelezo akampa nafasi mwingine kuelezea na akamsikiliza vizuri hadi huyo aliyetoa maelezo ndo akapewa uongozi wa juu na kumvua aliyeshindwa. Danadana hatuzitaki
 
Mawazo yaliyofilisika kutoka Ubongo uliofilisika

Ni lazima tuwe na Katiba ambayo Rais atatenda kulingana na matakwa ya Watanzania lakini kutenda ndani ya Sheria. Ni hatari sana kuwa na Kiongozi ambaye neno lake ni amri na kila mtu analifuata. Ni hatari kuwa na Kiongozi ambaye anasababisha Mihimili mingine kuwa dhaifu na kufanya maamuzi ambayo aidha yanakwamisha demokrasia au yanakwamisha ustawi wa maisha ya Raia wa Tanzania.

Tunafahamu unaumia sana Magufuli kushambuliwa, lakini hakuna namna, alifanya Maamuzi mengi ya pupa na ya hovyo kwa Taifa hili. Laiti tungekuwa na Katiba bora basi maamuzi yake mengi yangekuwa under review by other organs na hivyo kuzuia hasara kwa nchi yetu.

Katiba Mpya ni sasa. Katiba Mpya ndiyo hitaji letu
Eti hasara. 😁😁 tunajua chadema hasara yenu ni kutokuingia mjengoni tu. Hakuna machungu ya taifa hapa, kama mliyemuita mwizi mlimteua agombee urais na kumnadi kwa mbwembwe zote mnayo machungu na nchi hii kweli?
 
Kwamba Assad na wengineo wakisema kuwa Magufuli alikuwa hasikilizi maneno ya wataalamu, haimaanishi kuwa "Sasa, wanataka tuwe na Rais ambaye anapewa ushauri na kila mtu na anatakiwa kusikiliza kila ushauri kwani asipousikiliza au kuukubali basi anakuwa "haambiliki". "
Jibu lako lina maana kuwa Magufuli alikuwa hasikilizi, lakini siyo kweli kwani kuna mifano mingi sana inayoonyesha akiwa anasikiliza ushauri. Tatizo la Assad ni kuwa alitaka Magufuli amsikilize na achukue ushauri wake yeye moja kwa moja, jambo ambalo siyo kweli, kwani Magufuli naye alikuwa na analytical skills za kujua namna ya kuacheive malengo yake. Ukimpa ushauri ambao hauko kwenye malengo yake anakuachia hapo hapo.
 
Back
Top Bottom