Ujumbe muhimu: Mashabiki wenzangu wa Simba tulifeli hapa

adriz

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2017
Posts
12,207
Reaction score
26,521
Ningependa moja moja kuwapongeza watani zetu Yanga kwa ushindi wa jana.

Baada ya kufanya tathimini yangu fupi mitandaoni na vijiweni nimegundua kuna mabadiko makubwa kati ya mashabiki wa Simba na Yanga kutokana na mambo wanayojadili kuhusu timu yao.

Nikianza na Yanga haswa hapa Jf kwenye jukwaa lao utakuta wanajidili kikosi chao na kutathimimi mapungufu na maboresho hata hapa Jf demigod pamoja na upopoma wake lakini alianzisha uzi wa kuiushauri klabu yake kuwa isiweke kambi nje ya nchi badala yake iwe hapa hapa kwani muda walioanza kambi ni sio rafiki hatimaye uongozi ukafanya hivyo japo sina uhakika kwamba mawazo walitoa kwenye uzi wake hapa jukwaani.

Tukirudi upande wetu misimu ya nyuma tulikuwa na mtindo wa kujadili wachezaji na mwendo wa timu kwa ujumla hata msimu ukiisha hapa Jf tutakutana na nyuzi kibao za napendekeza na maboresho nk lakini hali imeanza kubadilika tokea msimu uliopita kuanza mashabiki wa Simba tumekua tukitumia nguvu kubwa na kujadili na kushadadia mambo ambayo hayana msingi kwa klabu sisemi kama ni ubaya kujadili ili kunogesha mambo ila tumekithirisha mno mifano naweka hapo chini;

1. Habari za ng'ombe wa Mayele mpaka kungundua mbavu zake zina mpangilio upi.

2. Sopu and Sakho cup ilikuwa kama tumebeba Uefa vile.

3. Rank za CAF. Kama zinadumu milele au fifa ndio wametoa.

4. Sakata la Manara.

5. Jezi mpya za Yanga ikafikia hatua mpaka kugundua msikiti na Hamza .

6. Kuliponda Kombe alilobeba Yanga NBC Premier League kea kusema ni blender wengine eti kama mchoro wa virus.Wakati huo wachezaji wanabweteka kwa kuona Sawa maana nguvu imehamia kuponda Kombe kuliko kuwafanya wajute kukosa ubingwa.

7. Ongezeeni wadau.
#GuyuMoya#GuvuMoya

#UziTayari
 
Mashabiki wenzangu tunakumbuka shuka wakati kumekucha sasa kila mtu mchambuzi na tunajadili timu habari za udaku ,Jezi ,Ki Azizi domo lepe ,Picha ya chama kuwepo kwenye ramani ya Afrika ya super League tumeachana nazo kabisa..
Nimesahau kukutag @Mgagunzi maana baada ya kuwafunga wana kwaya ulileta usi Simba lidude flani kikubwa saaana bila kuchambua kitimu kwa ujumla.
 
Simba wakiulizwa ni kwa nini huwa wanafungwa na Yanga kila sikuπŸ‘‡πŸ˜πŸ˜πŸ˜
Your browser is not able to display this video.
 
Mabadiliko ya kocha yalituponza. Kumuondoa Chama na kutopanga washambuliaji wazuri
 
Mngeshinda haya yote yasingekuwa na maana. Kubalini matokeo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…