Ujumbe muhimu: Mashabiki wenzangu wa Simba tulifeli hapa

Ujumbe muhimu: Mashabiki wenzangu wa Simba tulifeli hapa

Huyu njaakalihatari anaelekea kwenye ukichaa sasa ,jamani msichukulie mpira seriaz sana kumbukeni mna familia na mambo mengine muhimu ambayo yanawategemea.
Screenshot_20220815_060700.jpg
 
Ningependa moja moja kuwapongeza watani zetu Yanga kwa ushindi wa jana.

Baada ya kufanya tathimini yangu fupi mitandaoni na vijiweni nimegundua kuna mabadiko makubwa kati ya mashabiki wa Simba na Yanga kutokana na mambo wanayojadili kuhusu timu yao.

Nikianza na Yanga haswa hapa Jf kwenye jukwaa lao utakuta wanajidili kikosi chao na kutathimimi mapungufu na maboresho hata hapa Jf demigod pamoja na upopoma wake lakini alianzisha uzi wa kuiushauri klabu yake kuwa isiweke kambi nje ya nchi badala yake iwe hapa hapa kwani muda walioanza kambi ni sio rafiki hatimaye uongozi ukafanya hivyo japo sina uhakika kwamba mawazo walitoa kwenye uzi wake hapa jukwaani.

Tukirudi upande wetu misimu ya nyuma tulikuwa na mtindo wa kujadili wachezaji na mwendo wa timu kwa ujumla hata msimu ukiisha hapa Jf tutakutana na nyuzi kibao za napendekeza na maboresho nk lakini hali imeanza kubadilika tokea msimu uliopita kuanza mashabiki wa Simba tumekua tukitumia nguvu kubwa na kujadili na kushadadia mambo ambayo hayana msingi kwa klabu sisemi kama ni ubaya kujadili ili kunogesha mambo ila tumekithirisha mno mifano naweka hapo chini;

1. Habari za ng'ombe wa Mayele mpaka kungundua mbavu zake zina mpangilio upi.

2. Sopu and Sakho cup ilikuwa kama tumebeba Uefa vile.

3. Rank za CAF. Kama zinadumu milele au fifa ndio wametoa.

4. Sakata la Manara.

5. Jezi mpya za Yanga ikafikia hatua mpaka kugundua msikiti na Hamza .

6. Kuliponda Kombe alilobeba Yanga NBC Premier League kea kusema ni blender wengine eti kama mchoro wa virus.Wakati huo wachezaji wanabweteka kwa kuona Sawa maana nguvu imehamia kuponda Kombe kuliko kuwafanya wajute kukosa ubingwa.

7. Ongezeeni wadau.
#GuyuMoya#GuvuMoya

#UziTayari
Kwa bahati mbaya kwangu sikuwahi kukufuatilia miongoni mwa mashabiki wa Simba humu JF. Leo nimegundua busara na hekima ulizonazo na nakuongeza kwenye orodha yangu ya mashabiki wa Simba ndani ya JF àmbao ni Genta, Cocastic, Scars.
Baada ya ligi kumalizika Genta aliandika Uzi ulioshambuliwa Sana kuhusu madhaifu ya Simba. Kati ya maeneo aliyogusia na Mimi binafsi kumuunga mkono na Uongozi wa Simba pamoja na Benchi la Ufundi wameacha hivyo hivyo ni eneo la Kiungo mkabaji. Tulisema na narudia kusema Simba inashindwa kujua kuwa Mkude siyo DM? Mmemsajili V.A lakini inaonekana kocha mpya hajamkubali japokuwa Mimi namhusudu Sana mbali ya kasoro yake ya ball control.
Ukiangalia magoli aliyofungwa Simba juzi, assisters wamepita free eneo la DM wa Simba. Anayebisha aangalie upya magoli yale mawili. Ukitaka kuona umuhimu wa DM makini angalia upya tukio la Kadi ya njano ya Feitoto dhidi ya Okwa na uniambie Kwa nini aliamua kumvuta jezi Kwa gharama ya Kadi japokuwa yeye hakuwa DM.
Kumekuwa na ushabiki usio na faida na wengine wakidhani mashabiki hawana nguvu kwenye timu. Hebu angalia pale Man U Ten Hag anataka kumsajili mchezaji mashabiki wanasema akija aidha hatutakuja uwanjani au tukija tutamzomea, na hajasajiliwa. Leo humu watu wanasifia hata visivyositahaili ilimradi ni vyao, wanakosoa hata yasiyoatahili ilimradi si yao. Hao si mashabiki ni Washangiliaji, na humu JF washangiliaji ni wengi kuliko mashabiki. Pole kwako wewe unayejua soka.
 
Mngeshinda haya yote yasingekuwa na maana. Kubalini matokeo!
Hakuna sehemu alipokataa matokeo. Shabiki mzuri utamjua hata akishinda unamuona anakosoa madhaifu. Lakini humu Yanga wameshinda lakini ni Mtu mmoja tu alionyesha madhaifu machache ya Yanga.
 
Mimi kwa upande wangu naona kinacho waponza simba ni kuwekeza zaidi kwenye maneno, kuliko vitendo.
Na wasipobadilika, aisee watasahau kuifunga Yanga na pia kuchukua ubingwa wowote ule kwenye hii miaka ya karibuni.

Yaani wanachonga mno! Kejeli nyingi! Na hii ni kuanzia kwa CEO wao Barbara, Msemaji wao Ahmed Ali, na mashabiki wao kwa ujumla. Wapunguze kuchonga! Na badala yake wacheze mpira. Kwa miaka ya karibuni, simba wamewekeza sana katika mpira wa maneno nje ya uwanja! Halafu wakiingia uwanjani, mambo yanakuwa tofauti kabisa.

Ona walivyo mvimbisha kichwa Enock Inonga kwa kumkamia kwake Mayele, na kilichomkuta jana!
Tate,
Hili la kuwekeza kwenye maneno timu zote za Kariakoo mko vizuri. Nadhani ni Kwa vile mko karibu na Soko kuu. Ukimtaja Ally usimsahau Manara.
 
Jamani Simba wenzangu haraka tumuwahi njaakalihatari naona anaelekea kuchanganyikiwa sasa kila muda anaandika nyuzi za malalamiko halafu pumba tupuView attachment 2323594
Greatest Of All Time umesema ukweli kuwa kuna mashabiki mambumbumbu kabisa mfano hai huu hapa.
Huyo wala usimfuatilie utapoteza Muda. Yuko na mwenzake ni maarufu wa kuanzisha nyuzi za matokeo lakini ni mweupe kichwani kama pamba ya Simiyu.
 
Ningependa moja moja kuwapongeza watani zetu Yanga kwa ushindi wa jana.

Baada ya kufanya tathimini yangu fupi mitandaoni na vijiweni nimegundua kuna mabadiko makubwa kati ya mashabiki wa Simba na Yanga kutokana na mambo wanayojadili kuhusu timu yao.

Nikianza na Yanga haswa hapa Jf kwenye jukwaa lao utakuta wanajidili kikosi chao na kutathimimi mapungufu na maboresho hata hapa Jf demigod pamoja na upopoma wake lakini alianzisha uzi wa kuiushauri klabu yake kuwa isiweke kambi nje ya nchi badala yake iwe hapa hapa kwani muda walioanza kambi ni sio rafiki hatimaye uongozi ukafanya hivyo japo sina uhakika kwamba mawazo walitoa kwenye uzi wake hapa jukwaani.

Tukirudi upande wetu misimu ya nyuma tulikuwa na mtindo wa kujadili wachezaji na mwendo wa timu kwa ujumla hata msimu ukiisha hapa Jf tutakutana na nyuzi kibao za napendekeza na maboresho nk lakini hali imeanza kubadilika tokea msimu uliopita kuanza mashabiki wa Simba tumekua tukitumia nguvu kubwa na kujadili na kushadadia mambo ambayo hayana msingi kwa klabu sisemi kama ni ubaya kujadili ili kunogesha mambo ila tumekithirisha mno mifano naweka hapo chini;

1. Habari za ng'ombe wa Mayele mpaka kungundua mbavu zake zina mpangilio upi.

2. Sopu and Sakho cup ilikuwa kama tumebeba Uefa vile.

3. Rank za CAF. Kama zinadumu milele au fifa ndio wametoa.

4. Sakata la Manara.

5. Jezi mpya za Yanga ikafikia hatua mpaka kugundua msikiti na Hamza .

6. Kuliponda Kombe alilobeba Yanga NBC Premier League kea kusema ni blender wengine eti kama mchoro wa virus.Wakati huo wachezaji wanabweteka kwa kuona Sawa maana nguvu imehamia kuponda Kombe kuliko kuwafanya wajute kukosa ubingwa.

7. Ongezeeni wadau.
#GuyuMoya#GuvuMoya

#UziTayari
Kwahiyo washabiki wa yanga hawaisemi simba?
 
Kwahiyo washabiki wa yanga hawaisemi simba?
Simba tukikithirisha kiasi ambacho tukasahau kukosa na kurekebishwa mapungufu ya timu yetu mfano rahisi angalia sasa nyuzi za malalamiko ambazo kimsingi ushauri na napendekeza hayo yangekua yametolewa tokea awali ingesaidia.
 
Huu uzi wa kujadili kistaarabu tafadhali tumia lugha nzuri mambo ya ushangingi hayana nafasi hapa.
Mkuu tumekuwa tukipishana kauli kwenye mada mbali mbali ila kwa hili NAKUUNGA MKONO badilisha mtazamo wa mashabiki wenzio hapa jukwaani




Sema wanangu mnapuyanga sanaa😂😂😂😂😂
 
Simba SC kupoteza mchezo wake dhidi ya Yanga SC ni matokeo ya mpira, kwangu naona uwepo wa Nabi muda mrefu pale Yanga umemsaidia kuwajua vizuri wachezaji wake na awatumie vipi, ukilinganisha na kocha wa Simba SC ambaye bado ni mgeni.

Zile sub alizofanya Nabi ndio chanzo cha yote haya, anajua matumizi sahihi ya wachezaji wake, kocha wa Simba SC alikuwa kama anabahatisha kwa zile sub zake sababu ya ugeni wake.
 
Simba SC kupoteza mchezo wake dhidi ya Yanga SC ni matokeo ya mpira, kwangu naona uwepo wa Nabi muda mrefu pale Yanga umemsaidia kuwajua vizuri wachezaji wake na awatumie vipi, ukilinganisha na kocha wa Simba SC ambaye bado ni mgeni.

Zile sub alizofanya Nabi ndio chanzo cha yote haya, anajua matumizi sahihi ya wachezaji wake, kocha wa Simba SC alikuwa kama anabahatisha kwa zile sub zake sababu ya ugeni wake.
Fukuza fukuza makocha imechangia Simba kudorora,kweli kabisa Nabi mechi zake nyingi zinaamuliwa na subs zake matata mfano fainali FA na nyinginezo ligi kuu.
 
Back
Top Bottom