Ujumbe wa JWTZ kuhusu kutoroka kwa Luteni Kanali Coelestine Seromba

Ujumbe wa JWTZ kuhusu kutoroka kwa Luteni Kanali Coelestine Seromba

Status
Not open for further replies.

nngu007

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2010
Posts
15,860
Reaction score
5,801
23/08/2013

JWTZ litatoa taarifa kuhusu kutoroka kwa Luteni Kanali Coelestine Seromba. Kwa mujibu wa taarifa kutoka Makao Makuu ya Jeshi hilo, taarifa hizo zitatolewa Agosti 24.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Habari na Uhusiano Makao Makuu ya Jeshi.
Dar es Salaam.

Kwa Mawasiliano zaidi 0715-270136 au 0754-270136


Tanzania Daima Jumapili limekariri msemaji wa JWTZ akikiri kuwa ni kweli mwanajeshi ametoroka lakini tayari alikuwa chini ya uchunguzi na alikuwa amekabidhi vitu vyote muhimu.



JWTZ yakanusha ofisa wake kutoroka na nyaraka


na Abdallah Khamis

JESHI la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), limetoa ufafanuzi juu ya kutoroka kwa ofisa wa jeshi hilo, Luteni Kanali Colestine Serombe na kusema kuwa ofisa huyo hakufanikiwa kuondoka na nyaraka yoyote muhimu ya jeshi hilo.

Mbali na kusema Luteni Kanali Serombe hajaondoka na nyaraka muhimu za jeshi hilo, pia wamesema ofisa huyo aliyetoroka ni Mtanzania na kwamba kabla ya kuroroka alikuwa akikabiliwa na tuhuma dhidi ya makosa ya kijeshi.

Jeshi limelazimika kutoa kauli hiyo baada ya baadhi ya vyombo vya habari vya ndani na nje ya nchi kusema kuwa ofisa huyo aliyetoroka ni miongoni mwa maofisa wachache walio na asili ya Rwanda ndani ya jeshi hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, msemaji wa jeshi hilo, Meja Erick Komba, alisema Luteni Kanali Serombe alizaliwa katika Kijiji cha Rukira kilichopo mkoani Kagera na kupata elimu ya msingi katika Shule ya Msingi Rukira kabla ya kwenda sekondari za Rulenge na baadaye Minaki alikosoma kidato cha tano na sita.

"Ametoroka usiku wa Desemba 17 kuamkia 18 mwaka jana baada ya kuwa na makosa ya kijeshi …tulimuweka chini ya uchunguzi kwa ajili ya kumfungulia mashtaka, sasa labda hiyo ndiyo inaweza kuwa sababu ya kutoroka kwake, kwa kuwa suala la utoro ni uamuzi wa mtu kama ambavyo wengine wanaamua kujiua wakiwa na sababu zao," alisema Meja Komba.

Kuhusu madai kuwa ofisa aliyetoroka alikuwa mkuu wa kitengo cha teknolojia ya habari na mawasiliano, Meja Komba alisema hilo si la kweli na kwamba Luteni Kanali Serombe alikuwa ni mkufunzi wa wanafunzi wa kijeshi wanaosoma masuala ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (IT).

Alisema kulingana na cheo cha Luteni Kanali Serombe na madaraka aliyokuwa nayo alikuwa na uwezo wa kusoma baadhi ya taarifa ambazo zilimfikia kwenye ofisi yake kwa ajili ya utekelezaji au kwa taarifa.

"Katika kipindi chake cha utumishi kwa muda mrefu alikuwa mkufunzi wa masomo ya kompyuta katika kituo chetu, kwa mantiki hii taarifa nyingi alizokuwa nazo zilikuwa ni zile za wanafunzi, yaani mahudhurio, matokeo na nyingine zinazomhusu mwanafunzi," alisema Meja Komba.

Aliongeza kuwa jeshi lilipoanza uchunguzi dhidi ya makosa ya Luteni Kanali Serombe kitu cha kwanza kilichofanyika ni kuhakikisha anakabidhi vitendea kazi vyake vyote kwenye uongozi, huku akibainisha kuwa walichomwachia ni elimu aliyonayo.

"Labda sasa anaweza kuitumia elimu hiyo huko alikotorokea kufungua chuo cha kompyuta na wananchi wakapata ujuzi huo," aliongeza Meja Komba.
 
Huyo Mnyarwanda atakuwa kwa Kagame na siri za jeshi.
 
Sasa wanakimbizwa na nini? Si wangesubiri tu mpaka hyo kesho?
 
Sasa kama ni kesho kulikua na haja gani ya kutoa shallow statement kama hii?This is shame.Tena imeletwa na kurugenzi kabisa?Hivi kwenye millitary propaganda wataweza kweli kwa staili hii?

lol.. mimi ninataka kuwatetea...labda ni August 24...ya 2014???
Mnajuaje kama ni kesho 🙂

Anyway japo mimi si mtaalamu wa sheria lakini even from legal point of view hiyo "barua" ni kinyesi... August 24 ya mwaka gani??? Huyo aliyeiandika ana elimu kiasi gani?? Anajua kitu kingine chochote zaidi ya kucheza na magobole?????
I doubt!!!
 
hapa napita tu, nadhani leo wanapima upepo ili wafahamu namna bora ya kuchakachua ! Otherwise wangesubiri hiyo kesho !!
 
Imefika wakati wa Kuirejesha Rwanda kwenye Himaya ya Tanganyika... ni Jimbo letu lile
 
Huyo Mnyarwanda atakuwa kwa Kagame na siri za jeshi.

Halafu tunajisifia kwamba tuna jeshi thabiti,atakuwa ameenda kuyaanika yote,yaani kwa kifupi katuacha uchi huko kwa kagame.
 
...ndo maana sikuzote nasema likagame linaweza kutuchapa tu,jiulize wangapi bado wamejificha serikalini.sasa tupo uchi mbele ya wanyaruanda,ole wetu tuwaguse tunakula kichapo kikali sana,ikowapi tiss...
acha upuuzi ww boya na kushabikia ujinga, hujui kama vita ikitokea familia yako poa itadhurika, kuwa mzalendo na Taifa lako utumwa huo kushabikia vya wenzio
 
Du! Haya sasa kumbe matope hadi jwtz inatofauti gani mgambo anaruka na kukanyagana abei nahene nashoga shinyanga
 
...ndo maana sikuzote nasema likagame linaweza kutuchapa tu,jiulize wangapi bado wamejificha serikalini.sasa tupo uchi mbele ya wanyaruanda,ole wetu tuwaguse tunakula kichapo kikali sana,ikowapi tiss...

tunaweza tukatake advantage ya hizo missing docs kumchapa kagame.
 
Mkuu jiandae kung"olewa meno na kucha
 
Hahahahahaahahahahaaha
nilipoifungua hii thread kidogo nimtukane mleta mada kwa kudhani anataka tuitembelee blog yake kwa kuwa hajaweka huo ujumbe wa jeshi.

Sasa kumbe ujumbe wenyewe ndio huo ambao unasomeka,,,,,,majanga
 
Jamaa wanapima upepo,mnajua ukweli kiasi gani?wakipitia pitia jf wakaona kimya,basi hiyo siku watakuja na stori za kuchonga,kweli chuo cha sanaa hawakukosea kujenga bagamoyo.
 
Huyo Lt Col.seromba atapatikana ktk karo la maji machafu katika moja ya makambi ya Jeshi akikosekana huko basi itakuwa mabwepande!
 
Hii ni TZ na sio Serikali ya Rwanda hawa wanaoleta upuuzi wa kufikirika kikombe chao cha Sifongo watakinywa tu maana wamekipenda kwa kifupi ni hivi > hata Rwanda iungane na UG kui attack Tz< tutaumia lakini wataumia zaidi wao na hawatashinda ukibisha andamana.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom