Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali

angalieni huko nyuma nilipomuambia ayaweke hadharani aliyonitumia kwenye PM, nimemwambia si mara moja amenijibu nini? Huwezi kusema vitu kama hivyo ukaviweka in strict confidence, ukimya wake na kupuuzia kwake ombi langu kumenipa haki ya kuweka hadharani alichosema.. one can not be a bigot in private!!

Kama ningetaka kuweka hadharani bila kumpa nafasi ya kunikataza ningefanya hivyo!

Halafu Dua, niliposema hilo la vitu exclusive you know better ilikuwa inahusu nini. Mtu hawezi kunitumia PM za kunitukana, kutishia maisha mtu/watu n.k ukitegemea kuwa that is a private conversation. Itakuwa ni kutowajibika kwa upande wangu nikijifanya kufumbia macho maandishi ya namna hiyo!

Na badala ya kuangalia alichosema bila kujali mazingira ya kauli hiyo watu wanageuza kuwa mimi ndiyo hoja! Baada ya kukemea kauli za kibaguzi watu wanaguswa na maneno ya tafsiri yangu ya kuelewa kinachomsukuma ndugu yetu.

Hili haliwezi kufumbiwa macho, you can make me the topic if you want, but inapobidi tutaita kijiko kijiko. Mtu yeyote anayo haki ya kunikosoa mimi kama maandishi yangu yanachochea uhalifu au hisia za kibaguzi. Na ikionekana hivyo au ikitafsirika hivyo niko tayari kuweka sawa, kukiri nimekosea na kuomba mwongozo.

Sisi wote ni binadamu, hukosea lakini tunakuwa waungwana pale tunapokiri makosa yetu badala ya kujifanya hatuyaoni!!!
 

Kama Mswahili kweli kasema yote hayo, then mswahili is wrong. Lakini kinachoniudhi mimi, ni wewe kung'ang'aniza, just because tunakubaliana kuna ishu kitengo fulani. Then that makes us wakabila. Hiyo inauma, na nimekuomba before u-apologise au ujieleze vizuri na umejiona you are too big to apologise. Hapo juu nimeweka bold (na kuna thread nyingi umeongea kwa wingi). unatumia wingi. Kuna marafiki zangu 3 wamenipigia simu, wananiuliza, mbona huyu jamaa anacreate impression wewe ni mmoja wa wakabila?? For you to group me as mkabila is very wrong, and I take it very personal. My girlfriend of 5 years is a mchagga. Nina marafiki wengi wachagga kuliko kabila jingine. Nimesoma Moshi, na ni kama 2nd home kwangu within Tanzania. Nachokuomba, differentiate between mtu kusema kuna tatizo fulani sehemu fulani, na kuwa mkabila.
Ndio nakuuliza, wewe uliyekuwa unachangisha watu tumsaidie muuza madawa, tukuite wewe pia muuza madawa? Tumesoma watu Tanzatl walikwambia usidanganye watu.......ukasema utapataje info Brazil. Watu tukanyamaza tunakuona unabwabwaja tu.
Because you sources of information have time and time proven to be shady, I do not believe Mswahili said those things. YOU COULD HAVE COOKED THAT. Sikubaliani na mawazo hayo....unayoclaim ni maneno ya Mswahili. Atakuja ajitetee mwenyewe. Na kama ni mawazo yake, basi namsikitia.
Who are you to make us believe what you say? Wewe ndio umeifanya topic iwe yako........maana you are the one who pasted that message. And we are supposed to believe you?? Umeshindwa kufanya interview unakuja na tactic nyingine.
You can control other people's minds, but not this dude here!! Jaribu tena!!
 
Swali hayo yalitokea katika mazingara yapi? Hilo ndio nililotaka kujua na sasa umesema mwenyewe, kumbe mlikuwa mnatukanana/alikuwa anakutukana, mbona wanabodi wakitumiwa matusi na vitisho wanasema. Kyoma amesema hapa etc. etc.. If that was the case then mwenyewe umemaliza i.e amekutumia PM na kukutukana. Mbona hukulisema hili kabla ya kuweka hiyo story? Kulikoni? Au ndio kumkoma nyani giladi or whatever kama Mzee Es asemavyo? Kwa hiyo ugomvi wenu umeamua kuuleta hapa siyo? Hii inaleta even more serious issue, Je ni tangu lini mnatukanana/anakutukana? Je wewe huwa unamwambia nini wakati akitoa matusi kama hayo na kutishia maisha yako? Ingekuwa vizuri wakati unaweka hayo ungetuonya kwamba member huyu i.e Mswahili amesema hivi na vile na mimi nimesema hivi etc. kuliko ulivyofanya na unategemea sisi tuseme unavyotaka.

Nafikiri tujadili issues bila kuangalia nani kaileta, if it helps walalahoi then that is well and good kuliko kujaribu ku-score cheap points.

Maneno haya confidentiality of information zenu zitabaki confident hayana maana kama mimi na wewe leo tukikosana then unamwambia kila mtu. Je ulikuwa unataka kumrubuni Mswahili kwa yale aliyokuandikia in private?

Anyway to me you're not an issue, issue ni jinsi ulivyolichukulia hili jambo la ugomvi wenu ili tukemee kitu ambacho hatufahamu mwanzo wake and now unakuja open kule mlikoanzia. Sihitaji kuwa malaika kwa hili lakini sio punguani kufahamu kuwa member hahitaji kutishiwa maisha yake au kutukanwa.
 
You may be entitled to your own opinions, but you are not entitled to your own facts!!!!!!!!!
 
Dua, with due respect to mwanakjj I bet ana personal grudge zake na mswahilli. Maana this was unprecedent disclosure. Perhaps mswahili should come here to put the record strait... PM.....usilete kauli za Bush..(you are either with us, or with terrorist!) Kila mtu anahaki ya kutoa maoni yake....no body is a holocaust revisionist, but again we should not allow such parochial way of reasoning to muzzle legitimate debates of issues touching our daily lives! Asante.
 
aisee interesting....mwenye mapenzi haonii ,ingawa macho anayoo...

tukubaliane jambo moja hata kama walikua wanatukanana na mswahili ninge ignore kama mjj angekuwa ametukanwa personelly...lakini hapa kauli aliyotoa mswahili ni uchochezi fulani dhidi ya kabila la wachagga...na zaidi akaenda mbali zaidi kuulizA KAMA WAISRAEL WALIKUWA 6MILLION [ WAKAMALIZWA UJERUMANI] WACHAGGA WANAFIKA MILLIONI 6???? KWA KWELI SIELEWI KAMA MTANZANIA YEYOTE ATASHINDWA KUKEMEA HATA HILI...UNLESS MAONI YA KUMTETEA MSWAHILI KWA HILI YANATOKA KWA MTU MMOJA[AU ORGANISED CLIQUE]
 
Ngoja niweke mambo fulani sawa.

Defunc.. siyo kusudio langu hata kidogo kuacha taswira kuwa kila anayesema "wachagga ni wakabila" ni mkabila! Inawezekana anasema kutokana na ujuzi wake. Kwa vile mtu huyo ana marafiki, ndugu n.k ambao ni wachagga basi ni vigumu kuweza kugundua kama ana ukabila au la! Je mtu mwenye rafiki mchagga anaweza kuona ukabila wa wachagga isipokuwa wale waliokaribu naye? Kuna wanaotetea hoja za mswahili kwa sababu moja tu nayo ni kukubali kuwa Wachagga ni wakabila. Kama wewe si mmoja wao nakuomba radhi.

Dua, mimi sikuwa natukanana na Mswahili au yeye kunitukana. Bado sijatukanwa na mtu yeyote chemba wote wanaotaka kunitukana wamefanya hapa hapa hadharani. Maandishi ya Mswahili kwangu ni kuwa alikuwa anajibu swali langu ambalo nimeliandika hadharani (ukurasa wa 98) ambapo nilimuuliza a very pointed question. Jibu lake ndio hilo nililoliweka kwanza hapa. Nilipoandika swala la "fyeka fyeka" hadharani, mswahili akajibu kwa jibu la pili mnalolisoma hapa.

Mikuki, mimi sina grudge na Mswahili zaidi ya kutofautiana kimtazamo. Kwa vile maswali yangu niliuliza hadharani na yeye kaamua kunijibu kwenye PM inaniweka mimi njia panda. Mimi sikumuuliza kwenye PM. Na kabla sijaposti hapa hadharani nilimpa nafasi (angalia ukurasa wa 98, 99) kwa yeye kuniruhusu au kutoniruhusu. Na angalia ni muda gani uliopita kabla sijaamua kuweka hadharani.

Inawezekana kuna watu wangependa aliyosema Mswahili chemba yasijulikane na yabakie sirini huku akiendelea hadharani demonizing the whole population of Chagga! Wale ambao tunawafahamu wachagga, tuna marafiki wachagga au tumeoa au kudate uchagani tungetoka hadharani na kumpinga bila kumuonea haya. In time of human sufferings it is not the actions of our enemies that hurt us most but the silence of our friends! Some peole would have like me to remain silent, that I shouldn't have exposed the motivations behind Mswahili's postings on this Ukabila issue. I DO NOT apologize for doing so.

Suala la mimi kuomba watu wasaidie kwenye msiba wa Tobi ni suala ambalo linakosoleka and I take fully responsibility for that. I take such a responsibility just like when I asked people to help the Mazula family, the Rupia family, the Semgaya family etc! For those who remember, as soon as the issue of his involvement with some illegal dealing surfaced I was the first person to take responsibility. Of course my critics will not point that out! Na ninaahidi kwa kadiri nina uwezo wowote, I'll continue to help whenever I can within reason.
 
Hebu tuwekeni sawa wazee, hili suala la msiba wa Tobi ni la nini? Exactly kuna nini kilitokea maana nimesikia sana hii habari ikiwa linked na wewe Mzee MMJ, eti ni la nini?
 
Mzee ES.... Tobi alikuwa akiishi uingereza akaenda Brazili ambako alifia huko. Nikaombwa na watu kuweka tangazo kwenye KLH News ili watu waisaidie familia kusafirisha mwili wake nyumbani TZ, which I did. Mazishi yakafanyika. Baadaye ya siku chache natumiwa email na watu kuniambia kuwa huyo kijana alikwenda huku akishughulika na madawa ya kulevya. Mara moja nikatangaza kwamba kama kutangaza habari kama hizi ni vizuri kuwa na facts zote. Nikaomba radhi wasikilizaji na kueleza kuwa mimi sikujua mahusiano hayo. Sasa toka hapo imekuwa ni nira juu ya shingo yangu!!
 

Unaona sasa? This proves you had it in your mind, wengine wote ni wakabila. Mwenendo wako wa kuwa-include wote umeanza tangu mwanzo. Na kuna post nilikuomba u-apologise. Uka ignore, na nimekuwa nikisoma jinsi unavyozidi....kudondosha maneno ya 'kufyeka...mapanga' sijui nini. Ina maana hayo maneno ulikuwa unaunganisha na watu wote wanaoongelea ukabila TRA. That is the issue.....TRA. Anywhere else, sijasema wachagga ni wakabila, and I dont believe so. Kama mswahili kasema hivyo, deal with the individual, dont generalise wote. Na nilishasema, ukienda kitengo kingine, unaweza kukuta wasukuma, au wakurya ni wakabila....i.e kuchaguana kwa ukabila. Ishu hapa ilikuwa TRA. Lakini wewe ulivyokuwa ukijaribu ku-stir it in a smart way, efforts zako ndio zaweza sababisha misunderstandings na chuki zisizokuwa na basis. Mwanakijiji, you are an intelligent person and I respect your work, but you are not the only intelligent person out there.
Mimi sio mmoja wao mwenye chuki hiyo unayofikiria, and you know that, so that is not a full apology. That is an indecisive, conditional apology.
For you, working in the media, you need to be NEUTRAL.....then when you have all facts, choose sides.
 

Mmmh,
Kusaidia sio ishu, watu wote tutakutwa na majanga. Hapo nilipoweka bold na underline, unatwist ukweli wa mambo yalivyokuwa. Wakati maiti bado iko Brazil, kuna watu pale Tanzatl walikua wanakukosoa usipotoshe watu. (Bahati mbaya, Tanzatl wamei-revamp. Kwahiyo hizo threads hazipo). So sio kweli ulijua kuhusu haya mambo baada ya mazishi. You knew before hand, kwasababu uliongea na 'wasemaji' wawili tofauti, na wakakwambia vitu viwili tofauti and you flipped. But you still continued campaigning for help. It was a very humaritarian deed, lakini watu uliokuwa unaomba mchango walikuwa wanajua kinachoendelea, and you were NOT TELLING THE TRUTH and not WILLING to research. Dont twist the truth. Please dont!!
 
Ni mTanzania gani huyo (au baadhi ya waTanzania gani) anayetamani wananchi wenziwe wapatwe na mabaya kiasi cha kutaka kuwahamisha nchini mwao, (waende wapi, au watupwe baharini?); au kuwaulia mbali kama Mayahudi walivyouliwa na Hitler! If this is not shocking enough, what will outrage you?

Huu sio utani.
Jambo ninalomvulia kofia Mswahili ni kwamba sio mnafiki kama baadhi ya watu wengine wanavyojitahidi kujificha katika kivuli cha utetezi kwa kupindisha hoja inayojadiriwa. Tokea wakati wa michango yake akijiita Chinga, hadi leo amekuwa mkweli na 'consistent' katika michango yake kuhusu wachagga na watu wa "Kanisa."

Kutokubaliana na Mkjj katika swali la Ukabila au hoja nyinginezo zozote hakuwezi kabisa kuwa kisingizio cha kuhalalisha kuunga mkono au kutetea mtazamo potofu kama huu unaoonyeshwa na Mswahili.

Katika Tanzania yetu ninayo imani kubwa kuwa hakuna kabila lenye chuki zidi ya waChagga kiasi cha kufikia hatua ya Wahutu na Watutsi iliyosababisha kutokee mauaji ya watutsi na baadhi ya wahutu ambao hawakukubaliana na siasa za chuki. Lililopo Tanzania, na ambalo dalili zake zinajionyesha hata humu kwenye majadiliano ya JF, ni baadhi ya wadini wenye siasa kali za kidini wanaofanya kila aina ya njia kuvuruga hali ya amani iliyopo nchini. Watu hawa hawawezi kuridhishwa na 'appeasement' ya aina yoyote ile. Hata kama leo hii kungetokea Tanzania iwe nchi ya dini moja tu, bado matatizo yatakuwa ni yaleyale; kama inavyojionyesha katika baadhi ya nchi zisizokuwa na dini nyinginezo.

Kwa bahati mbaya, watu kama Mkjj wanaojitokeza kwa njia moja au nyingine kupingana nao, mapigo yanageuziwa kwao ili kuwanyamazisha hata kisingizio ni mjadala wa ukabila wa wachagga. Kutokubaliana hoja hakuwezi kuamsha chuki kiasi kinachoonyeshwa hapa. Kwani haiwezekani kujadili ukabila au udini bila ya kuweka hisia za chuki?

Nilishawahi kusikia kuwa kuna baadhi ya watu wanapokwenda hospitali na kuwakuta madaktari wa 'kanisa' huwa wanagoma kutibiwa. Hii iliwahi kutokea Temeke; lakini mfano wa Mswahili na waChagga ni mara yangu ya kwanza kuusikia. Pengine 'context' ingekuwa ni tofauti maneno mahsusi yangetumiwa.

Hili ni swali: Hivi Dau ndio Dua? Maanake Mswahili anapommwagia sifa Dau, Dua naye anamkingia kifua!
Lakini siamini kuwa Dua ni mtu mwenye msimamo alionao Mswahili. Michango yake ya EAF haionyeshi mwelekeo wa kuwakataa waTanzania wengine kwa sababu tu za dini au ukabila wao.

Tutambuane kama waTanzania kwanza kabla ya chochote. Sio dini wala makabila yanayowatambulisha watanzania. Ni uTanzania wao ndio unaowatambulisha popote pale duniani. Tofauti za udini au ukabila tuzimalize bila ya kusambaratisha uTanzania wetu. Kamwe haitaweza kutokea pawepo taifa la wahaya, wangoni, wakurya n.k., au Tanzania ya watu wa 'kanisa' au wa 'misikiti.' pekee. Tukubali, tusikubali sisi ni waTanzania, na daima itabaki hivyo hivyo..... utake au usitake. So what will you do? You can go and hang if you disagree.
 
Somehow, You sound like Br.Robert!
 

What is the big deal here?
Whether the deceased Tanzanian (ndugu) was a drug dealer, was it not proper to facilitate transfer or burial of the body?

I'm curious. What if Mkjj had revealed the (truth?); did he have all the facts?
 
What is the big deal here?
Whether the deceased Tanzanian (ndugu) was a drug dealer, was it not proper to facilitate transfer or burial of the body?

I'm curious. What if Mkjj had revealed the (truth?); did he have all the facts?
Nimesema kutoa msaada sio ishu. Mtu yeyote anaweza pata matatizo. The issue is, mimi na wengi, hatuwezi kutoa mchango kama tunadanganywa. Na kama tunajua watu wanaficha ukweli, hiyo itaondoa spirit ya kusaidiana waTanzania huko mbeleni.
Drugs kill, and they kill bad. I, and many people dont like being associated with drugs. In my travels, I have met many drug dealers, we talk and thats it, we agree to disagree on what they do, lakini generally they are nice people like you and me. When drug dealers make money, they own the world. Drugs are killing people all over the world. Drug dealers have money. When they are flossing that money, do they know you? When your relatives are dying, do they know you? Do you know how drugs mess people up?
Do I need to spell it out to you where the problem is???
Kuna mtu namjua kafariki hivi majuzi Ugiriki. Nilitoa mchango wangu. Huyu mtu nilijua ni muuza madawa. Lakini kwavile ukweli nilikuwa najua, nilitoa msaada kwa mTanzania mwenzangu. Besides, huyu mtu alitoa msaada wa muda wake wakati mimi natembelea Ugiriki.
If you tell me the truth, then I will judge..........lakini kupotosha ukweli wakati najua ukweli, haifai!!
 
Unajua siku zote ni tatizo sana watu wanapokuja hapa na beef ambazo hazi-make a sense au za binafsi, nimeisikia habari ya Tobi na Mzee MMJ kwa muda mrefu laikini sikujua what was the deal, sasa kama Mzee MMJ unavyosema ni kweli then someone is lying or not telling the truth,

Kwa sababu whta kusaidia kusafirishwa mwili wa marehemu has anything to do na anyechangisha pesa kwa ajili ya kusafirisha mwili? I do not get it?

I mean let me get this straight, kuna mbongo amekufa majuu, akatokea mbongo mwingine akaamua kuchangisha kusaidia kusafirisha mwili wa marehemu, huyu mbongo wa pili alipaswa kujua yule marehemu alikuwa akifanya kazi gani kabla ya kufa? Na angejua alipaswa kuacha kuchangisha hizo hela ili mwili wa marehemu ubaki au uzikwe city, can someone help me here,

I mean something is missing here!
 
Ktk vile vifo vilivyotokea Brazil walipigwa Risasi wa Tanzania wawili Hivi yule wapili mwili wake ulishia wapi?Samahani kwa kuwatoa nje ya mada zaidi kwani tulishatoka nje Lakini Kidogo
 

please read the above post. yule mtanzania mwingine mbona hakuchangiwa pesa na yeye?kwanini kazikwa Brazil?

Mzee Es, mimi sina bifu. Niliumizwa kuitwa mkabila, just because anamwona Mswahili ni mkabila. Lakini ishu ni TRA. Ndio na mimi nikauliza, je MKJJ ni haki kumwiita muuza madawa kwa msaada wake aliotoa kwa marehemu muuza madawa (wakati alikuwa ana mislead watu?? na watu wakamwambia ajisahihishe).
Sijamlaumu yeye kutoa msaada, msaada ni msaada tu. Ninachosema, huyu anatwist facts to work in his favour. Other than that, hayo mambo mengine, I dont care really. Sijawahi kukutana na MKJJ na siwezi kuwa na bifu naye. I respect his efforts very much. Lakini asitumie position yake kutwist ukweli in his favour.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…