Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali

Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali

Mie naona ili kuepuka kabisa ukabila katika maofisi ni vyema usaili kwa ajili ya kazi ufanywe na wageni. Ikiwezekana wafanye wazungu ambao hawajui kabila la mtu na wala hawajali dini ya mtu. maana kama wenyewe hatuwezi kutenda haki na pia kuaminiana ni vyema watusaidie watu wengine. Jamani tujitahidi kuwasomesha watoto wetu ili baadaye kusiwe na watu watakaojidai kuwa wao wamesoma zaidi!!
 
Msijali Ndugu Mwanangu Hatakuwa Profesa ,
Kwa sasa anapiga soka ,mipango yote akachezee hata Leeds kwa malkia ,so idadi yetu kwenye hizo ofisi ulizozitaja haitaongezeka 🙂
 
As long mtu ana sifa apewe nafasi,hiv nitamtosa wakwetu mwenye sifa nimchukue mtu from nowhere! Akiharib utamfatia wap? Kwanza hapa inajenga undugu na ufanisi kazini coz wote ni wachapakazi na wana sifa
 
Mjadala ulishafungwa na bandiko la nne tu, sasa mnaendelea kujadili nini?
 
samvulechole... hakuna hoja ambayo ni ngeni hapa.. madai ya makabila hayo kupendelewa hayakuanza leo! tangu mara tu baada ya uhuru kulikuwa na tuhuma hizo hizo.. so.. there is nothing there..! Hata hivyo hatari unayoweza kuleta siyo ukabila bali ubaguzi, kuwa kama mtu anatoka kwenye makabila hayo basi asipewe nafasi fulani kwa vile watu fulani wanadhani kuna ukabila! Nitakupa mfano, kuna wanasheria watatu wote ni maprofesa... kuna Prof. Mwakalindile (Sheria, uzoefu miaka 30), Prof. Mtimba (mmakua, uzoefu miaka 10, sheria), na Prof. Chanda (Mzigua, sheria uzoefu miaka 5). Assuming maeneo ya fani zao ni sawa, ceteris paribus Rais anataka kumteua mshauri wa kisheria.. nani apewe kwa haki? Wengi watasema prof. Mwakalindile! Sasa kwa kufanya hivyo hata hivyo kuna wanyakyusa wawili tayari hapo ikulu ambao wameshapata nafasi zao, je tumnyime Mwakalindile kwa vile itaonesha ukabila?

Kabla hatujafikia hapo pa kudai ukabila tujiulize: "Kwanini inaonekana kuna wasomi wengi wa makabila hayo matatu Wachaga, Wahaya, na Wanyakyusa"? Je, tupunguze wanafunzi wanaotoka kwenye makabila hayo na kuwapa nafasi watu wa makabila mengine ili kuleta uwiano (parity)? Je tukiamua kufanya hivyo hatutakuwa tunaanza ubaguzi wa kikabila?

Tarehe 9 Disemba 1968 Nyerere alitumia siku ya Jamhuri kuzungumzia "Vitu ambavyo ni lazima Tuvisahihishe", vitu ambavyo baada ya uhuru havikwenda vilivyotarajiwa. Alizungumzia ukabila; kwanza alisema hivi:

"the man who talks about tribalism being practised without having any evidence for his statement is often a man who wants to stir up tribalism. Even if that is not his purpose, the result can be just the same. People will begin to think that there is tribalism, and, once people begin to think in these terms, then tribalism has begun to enter tinto our society"

Kuhusu Wahaya, Wanyakyusa, na Wachaga kupata nafasi nyingi katika serikali, Mwalimu alisema hivi miaka karibu 30 iliyopita:

"..the work of the civil servants and people in the parastatal organizations does require education..it so happened that the Tanzanians who had the opportunity for higher education under the colonialists were mostly Wahaya, Wachagga, and Wanyakyusa. And because most of the education was provided by missionaries, most of these people are also Christians. That was our inheritance. These conditions will change, but they have not changed yet. And for these reasons, when we get rid of the Europeans who were doing responsible jobs, and give these jobs to Tanzanians, the people who get them come mostly from one or other of these three tribes".

Akaongeza pia,

"Therefore, if you ask me why Wahaya, Wachagga, and Wanyakyusa have most of the jobs which require higher education, the answer is very obvious. They were the ones who received higher education during colonial times. I'd say: investigate the position in politics where a man is not asked about his educational qualifications. Look at the Parliament, the National Executive and Central Committee of TANU, and at the Cabinet. How many Wanyakyusa, Wahaya, or Wachagga are members? You will find that perhaps there aren't any, or there are one or two. This is the truth"

kwa umahiri wake wa maneno JKN akatoboa ukweli huu

"Anyone who refuses to accept a very obvious truth like this, and says that the reason is tribalism, must provide us with the evidence for his statement. If he cannot provide any evidence, we must conclude either that he is a fool, or that he is strirring up tribalism deliberately. He is the sort of (a) person who begs work on a tribal basis, and when he is refused because he does not have the capabilities, he pretends he was refused on tribal grounds."

Akasema pia ni jukumu la serikali kusaidia sehemu ambazo bado ziko nyuma kielimu. Na alimaliza kwa kusema:

".. if a Mchagga, a Mhaya, or a Mnyakyusayoung man were refused work simply because of his tribe - when he is capable and there is no other Tanzanian with the qualifications - then we would be practising a very stupid and very evil kind of tribalism such as that which caused the establishment of Biafra. I beg you, my brothers, avoid ANYTHING WHICH COULD BRING OUR COUNTRY INTO THIS KIND OF DISGRACE" (emphasis mine)
(From: Uhuru na Maendeleo pp 76,77)

so what say you?

Mzee mwanakijiji, majawabu ya Nyerere yalikuwa very valid wakati huo, kwa sasa tukikuta kabila moja kwenye idara moja sio sawa. makabila yote sasa yana watu waliosoma.
 
Kwenye suala hili nasikitika sana kwani kuna juhudi za makusudi za kutaka kufukarisha matajiri badala ya kuwa na juhudi za makusudi za kutajirisha maskini.
Na mbaya zaidi kwani kwenye masuala haya hakuna shortcut. Shule lazima usome miaka 14 au zaidi ndipo uwe na degree. Njia muafaka ni kujenga shule katika maeneo ya nchi yetu ambako wapo wachache serikalini.
Mwanakijiji anaongelea affirmative action ni kweli tunahitaji kwa baadhi ya wenzetu kwani binafsi nitajiskia vibaya kuona kuna mtindiga graduate halafu hana kazi. Huyu atatumiwa na wazee wa kwao kujustify kuwa kusoma hakuna maana ni kupoteza muda tu.
Tatizo la kuimplement affirmative action kwenye nchi yetu kwa sasa ni kwamba nchi "haina wenye nchi" wale aliokuwa nao Nyerere ambao unaweza ukawapa kazi ya kufuatilia mambo hayo ya kuona ni jinsi gani wenzetu wachache pale wanapojitokeza wanatendewa haki bila kuathiri wengine.
 
Wasukuma waacheni tu...hawana ukabila Nyerere alifanikiwa kuwanyima kupendeleana. Kama baba yako ni Mkurugenzi wewe msukuma usitegemee mteremko. Hata hivyo wanasema miaka hii baada ya 2015 uchumi wa Tanzania utategemea Science (Mahospitali, viwandani n.k) I bet! Wasukuma watakuwa kila mahali maana madaktari wasukuma ni wengi sana, wahandisi balaa na mtaani watafurika maana hadi sasa tunakadiria zaidi ya 1/3 ya watanzania ni wasukuma na zaidi ya 2/3 wanazungumza kisukuma. La msingi ni kutangaza Wasukuma kuanzia sasa siyo Kabila (tuwape hadhi tofauti....amua tuwaitaje?) na lugha yao ni lugha rasmi kwa taifa la Tanzania baada ya Kiingereza na Kiswahili
 
daah mi kabila langu muwanji. joto la jiwe naliona saizi na degree yangu mkononi ukizingatia kabila letu halijashika idara yoyote hata umgambo
 
Sipendi ukabila.naomba watz tujitahidi kwenye elimu ili wote twende pamoja tusiachane.tunalalamika humu ndani lakini ukweli tuliopita shule na kukaa mitaani tunaujua.taasisi nyingi za elimu nilikopita nakumbuka usongo wa hao jamaa kutoka hizo kabila 3.hawana utani hata kidogo.nakumbuka negligence yetu wengi wakati walimu wanatupigia kelele tusome,negligence iliyokuwa influenced na mazingira yetu nyumbani,ratiba na tabia za wazazi wetu,tamaduni za koo na kabila zetu n.k.huko mitaani pia zipo tofauti.hawa jamaa wana discipline ya maisha ambayo wengi wetu tunaona mateso kuifuata lakini this is what makes the difference.mie nadhani tubadili tamaduni zetu kwanza kabla hatujanyooshea vidole wachaga na wengine wenye maendeleo.ukweli unauma!namkumbuka rafiki yangu mmoja aliyekuwa akitimuliwa ada mara kwa mara wakati tukiwa shule na kuja kunilalamikia kuwa mama yake(single parent) alimwambia hana hela lakini kesho yake walisafiri kwenda kwao Tanga kufagilia makaburi na kufanya matambiko shughuli iliyomgharimu mama huyo pesa nyingi tu!ni vitu vidoogo sana ndio vinatuletea tofauti kubwa ktk maisha.
 
Wasukuma waacheni tu...hawana ukabila Nyerere alifanikiwa kuwanyima kupendeleana. Kama baba yako ni Mkurugenzi wewe msukuma usitegemee mteremko. Hata hivyo wanasema miaka hii baada ya 2015 uchumi wa Tanzania utategemea Science (Mahospitali, viwandani n.k) I bet! Wasukuma watakuwa kila mahali maana madaktari wasukuma ni wengi sana, wahandisi balaa na mtaani watafurika maana hadi sasa tunakadiria zaidi ya 1/3 ya watanzania ni wasukuma na zaidi ya 2/3 wanazungumza kisukuma. La msingi ni kutangaza Wasukuma kuanzia sasa siyo Kabila (tuwape hadhi tofauti....amua tuwaitaje?) na lugha yao ni lugha rasmi kwa taifa la Tanzania baada ya Kiingereza na Kiswahili

Hahahaha! wasukuma eeh! wewe huwajui vizuri wachaga usijidanganye kabisa,wachaga wame dominate kilamahali na wengi kweli mashuleni na vyuo vikuu.mimi nafanya kazi sehemu ya science wachaga kibao! nenda muhimbili,nenda engineering UDSM,wako kibao sababu wachaga wako very aggressive ndugu yangu.Ukiniambia wasukuma nakushangaa kabisa! wachaga,wahaya,wanyakyusa wana juhudi sana ktk elimu,angalia hata shule nyingi zimerundikana Kilimanjaro,Mbeya,BKB na siku hizi na Iringa wanakuja juu.shinyanga Mmm!
 
J.J.Mungai once said "tukiruhusu watu wenye performance za hali ya juu kwenda shule za sekondari, basi shule hizo zitajazwa na watu wanafunzi wa kutoka Mara...hivyo lazima tubane ili na maeneo mengine wapate nafasi za sekondari" Hii ilichangia sana kudidimiza baadhi ya maeneo jamani..kwa lengo zuri tu kuweka uwiano kumbe ndo ilkuwa kuua maendeleo ya mikoa na watu wake wale...Madingi kibao kule ni mageneous kinyama, lakini hawakupata fursa ili wenzao wapate kwenda shule na ku-avoid u-dominance wa watu wa mahali fulani kuonekana wao wako juu...
 
Wasukuma waacheni tu...hawana ukabila Nyerere alifanikiwa kuwanyima kupendeleana. Kama baba yako ni Mkurugenzi wewe msukuma usitegemee mteremko. Hata hivyo wanasema miaka hii baada ya 2015 uchumi wa Tanzania utategemea Science (Mahospitali, viwandani n.k) I bet! Wasukuma watakuwa kila mahali maana madaktari wasukuma ni wengi sana, wahandisi balaa na mtaani watafurika maana hadi sasa tunakadiria zaidi ya 1/3 ya watanzania ni wasukuma na zaidi ya 2/3 wanazungumza kisukuma. La msingi ni kutangaza Wasukuma kuanzia sasa siyo Kabila (tuwape hadhi tofauti....amua tuwaitaje?) na lugha yao ni lugha rasmi kwa taifa la Tanzania baada ya Kiingereza na Kiswahili

wewe hapana chezea MANGI hata kidogo!!! hata mngekuwa nusu ya watanzania bado sisi ni zaidi na acheni kudanganyika na sijui ukabila , watu wanachapa kazi nyie mnaendeleza misifa ya kijinga tu, mtasema sana siye twasonga mbele! karbuni katika ulimwengu wa kazi na juhudi bila kukata tamaa.
 
well done mkkj,

ndugu yangu samvulachole, umeanza kujihami ati topic haitawapendeza baadhi ya wachangaiji...wewe ulitaka kila mtu akubaliane na yasemwayo hata kama ni pumba?

Taonesha wewe mwenyewe ndo mkabila ma mdini, ndo maana ukachambua hobi uliyonayo..!!!

Hayo makabila ulotaja hakika kumejaa wasomi...hata ukinuna...! Sasa ulitegemea hapo kwenu samvulachole toka alfajiri umevalia msuli wachwza bao barazani ndo ulinganishe na kule kwa walima ndizi bk?

Wenzio wamekwenda shule, wakapata nafasi nzuri kazini kwao, wewe utabaki mhudumu na mfagizi wa ofisi tuuu>! Hadi utakapoelimisha kizazi kijacho cha huko samvulachole..!

mkabila huyoooooooooo
 
j.j.mungai once said "tukiruhusu watu wenye performance za hali ya juu kwenda shule za sekondari, basi shule hizo zitajazwa na watu wanafunzi wa kutoka mara...hivyo lazima tubane ili na maeneo mengine wapate nafasi za sekondari" hii ilichangia sana kudidimiza baadhi ya maeneo jamani..kwa lengo zuri tu kuweka uwiano kumbe ndo ilkuwa kuua maendeleo ya mikoa na watu wake wale...madingi kibao kule ni mageneous kinyama, lakini hawakupata fursa ili wenzao wapate kwenda shule na ku-avoid u-dominance wa watu wa mahali fulani kuonekana wao wako juu...

mhhhhh
 
Ya ikulu na hizo idara zingine siyajuwi ila TRA ni kiboko kwa ukabila. Wewe kama si mpare au mchagga na mtoto wa mjomba kupata kazi pale ni vigumu.
 
nilopokuwa chuo kulikuwa na wachaga zaidi ya robo kamasio nusu.....mkinga 1,,wasukuma hawakuwa zaidi ya 20..wahaya kama 30..+wengine warabu na wahindi kama wawili wawili waioppenda kujulikana ukabila wapia walikuwepo,,,,,ila wachaga walikuwa wengi zaidi kimakundi waislamu ndio usisema walikuwa chini ya robo ya darasa.....tegemea tuipata kazi wote swala la ubaguzi lisitokee ni ajabu............
 
mbona hautaji ukabila pale Muh2 na, UDSM?

PRO shayo, Pro Kinasha, Pro Mushi, Pro Temu, Dr Kisanga, Dr Temu, Dr Lema, Dr Mtei, Dr Kundi, Dr Matee, na wengineo. ukienda Muh2 utawakuta wanatibu nashangaa hawa hawauliziwi.
 
Back
Top Bottom