Julian Emmanuel
Member
- Mar 6, 2007
- 38
- 6
Tukatae tukubali ukabila upo, hauwezi kuisha ila unaweza kunyimwa nafasi ili kisiwe kigezo katika mambo yanayohusu umma.
ukabila nini labda ? maana naona wengine hatujui chimbuko la ukabila.
Ukabila ni kipengele ndani ya ubinafsi. neno binafsi lina tokana na mimi au sisi. Kila mwanadamu ana ubinafsi. huanza kujiangalia yeye "yaani mimi" akiridhika yeye kama eye au akiona peke yake hawezi basi hukimbilia kundi gani ambalo na yeye atakuwemo ndani yake linaloweza kurahisisha yeye kupata anachokitaka kama kakosa au ni nani yuko karibu na yeye ambaye baada ya yeye kupata huyu hajapata "yaani anaangalia sisi"
Ubinafsi huu hujitokeza kama mtu binafsi, au kimakundi kama familia, koo, kabila, dini, jinsia, makundi kama ya siasa, mpira, jamii nakadhalika.
Mimi naamini watanzania wote ni wabinafsi kama walivyo wanadamu wote. Kila mwanadamu anaangalia nafsi yake, na ubinafsi ndio chimbuko la wivu, kwani mtu hujiuliza kwanini sio yeye apate kile ila anacho mtu mwingine, kwa nini asiwe yeye bali ni mtu mwingine.
Kutokana na utofauti wa wanadamu kimatamanio ubinafsi wetu hujionyesha katika mambo tofautitofauti kila mtu katika jambo lake ingawa kuna mambo tunafanana wakati mwingine.
ubinafsi unapokuta nchi inayolegea katika uongozi mara nyingi sura kama hizi za kikabila, kidini, kifamilia, kikoo nakadhalika hujitokeza.
tukiangalia hapa tanzania tuangalie hivi kweli tukiangalia mfumo wa ajira kama mada ilikopitia kweli kuna usimamiaji wa kuhakikisha ushindani wa kiutendaji unatumika katika kuajiri au tunaajiriana kwa kujuana, wataalamu wanasema ili upate ajira kiushindani unahitaji "know how" lakini kwa tanzania unahitaji "know who"
sasa katika mfumo huu wa kuajiriana kwa kujuana tutakataaje kuwa ukabila haupo?, ufamilia haupo?. Hivi katika tanzania hii ni nani ataacha kumfanyia mpango ndugu yake ili apate ajira kama anajulikana na anaushawishi wa kumpatia ndugu yake ajira?
Siku zote ukaribu wa watu huanzia nyumbani "undugu". ukikutana na mtu mbali na kwenu mnaotokea sehemu moja utamuona ndugu yako na hapo usisi huanza, ukiwa mfano ulaya ukaona mtu anaongea kiswahili unamuona ndugu yako. katika nchi watu huonana ndugu kuanzia familia, ukoo, kabila, dini na kadhalika na hivyo pale ambapo hakuna ufuatiliaji wa sheria kuhakikisha kuwa watu hawatumii nyadhifa zao kuridhisha nafsi zao, katika ajira sura za kibinafsi hujitokeza katika mrorongo kama ulivyoorodheshwa hapo juu.
Hivyo ubinafsi katika Tanzania, katika nyanja ya ajira umejitokeza sana kifamilia ambapo unakuta familia fulani wameshikilia nyadhifa kubwa kubwa au zilizonona kimapato, sio kwa ushindani wao bali kwa kuwa na "good god father in family". sio lazima tutajane
kwa yale makabila ambayo wanakabila wake wamekuwa wakijisikia kwa mtu kujitaja mbele za watu kuwa mimi kabila fulani kutoka na picha fulani kwenye kabila hilo wamejikuta wakitambuana mijini na kujiona wako karibu na wale ambao mfumo wa ajira wa zamani ulikuwa umkipatia nafasi kila mtu ulikuwa umewawekea wajumbe wa kutosha katika nyadhifa muhimu wamenufaika na na mfumo huu wa sasa wa kuajiriana kwa kujuana inayotokana na uzembe katika uongozi katika kusimamia taratibu.
Kwa ujumla ubinafsi ndio chachu ya maendeleo, bila wewe kujiuliza kwa nini wewe uwe masikini wakati kuna watu wengine matajiri huwezi kupiga hatua, bila kujiuliza kwa nini familia yenu masikini au ikose vitu fulani na familia nyingine ziwe mbele huwezi kwenda. Bila kujiuliza kwa nini kabila lako liwe masikini wakati makabila mengine yamepiga hatua mbele, bila kujiuliza kwa nini sisi watanzania tu masikini hakika hatuwezi kupiga hatua. siri ya mafanikio ni kutoridhika na kile ulichonacho au na pale ulipo.
ila bila serikali kusimamia sheria ili kila mtu atambue mipaka yake na watu wakaanza kutumia mali za umma kama ni zao binafsi, ana mwajiri ndugu yake kwa sababu ni ndugu yake sio kwa sababu yeye ndiye bali zaidi ki taaluma kwa nafasi hiyo, au jamaa yake au rafiki yake wa kweli hapo ubinafsi utabadilika na kuwa chanzo cha kurudi nyuma na unaweza kuwa chanzo cha vurugu pale wale ambao hawana ndugu zao kwenye mfumo kuwaingiza watakapokata tamaa.
MTU YEYOTE AKIPEWA WADHIFA WA KUAJIRI AKAMUAJIRI NDUGU YAKE WA KULAUMIWA NI YULE ALIYEMPA WADHIFA HUO AU ANAYESTAHILI KUMSMAMIA. hivyo katika sekta ya umma kuajiriana kidugu wa kulaumu ni serikali. na serikali ya tanzania ni uongozi wa watanzania.
katika sekta binafsi usindani kwenye soko ndio utawafanya watu watoe ajira kwa ushindani na sio kwa kujuana
ukabila nini labda ? maana naona wengine hatujui chimbuko la ukabila.
Ukabila ni kipengele ndani ya ubinafsi. neno binafsi lina tokana na mimi au sisi. Kila mwanadamu ana ubinafsi. huanza kujiangalia yeye "yaani mimi" akiridhika yeye kama eye au akiona peke yake hawezi basi hukimbilia kundi gani ambalo na yeye atakuwemo ndani yake linaloweza kurahisisha yeye kupata anachokitaka kama kakosa au ni nani yuko karibu na yeye ambaye baada ya yeye kupata huyu hajapata "yaani anaangalia sisi"
Ubinafsi huu hujitokeza kama mtu binafsi, au kimakundi kama familia, koo, kabila, dini, jinsia, makundi kama ya siasa, mpira, jamii nakadhalika.
Mimi naamini watanzania wote ni wabinafsi kama walivyo wanadamu wote. Kila mwanadamu anaangalia nafsi yake, na ubinafsi ndio chimbuko la wivu, kwani mtu hujiuliza kwanini sio yeye apate kile ila anacho mtu mwingine, kwa nini asiwe yeye bali ni mtu mwingine.
Kutokana na utofauti wa wanadamu kimatamanio ubinafsi wetu hujionyesha katika mambo tofautitofauti kila mtu katika jambo lake ingawa kuna mambo tunafanana wakati mwingine.
ubinafsi unapokuta nchi inayolegea katika uongozi mara nyingi sura kama hizi za kikabila, kidini, kifamilia, kikoo nakadhalika hujitokeza.
tukiangalia hapa tanzania tuangalie hivi kweli tukiangalia mfumo wa ajira kama mada ilikopitia kweli kuna usimamiaji wa kuhakikisha ushindani wa kiutendaji unatumika katika kuajiri au tunaajiriana kwa kujuana, wataalamu wanasema ili upate ajira kiushindani unahitaji "know how" lakini kwa tanzania unahitaji "know who"
sasa katika mfumo huu wa kuajiriana kwa kujuana tutakataaje kuwa ukabila haupo?, ufamilia haupo?. Hivi katika tanzania hii ni nani ataacha kumfanyia mpango ndugu yake ili apate ajira kama anajulikana na anaushawishi wa kumpatia ndugu yake ajira?
Siku zote ukaribu wa watu huanzia nyumbani "undugu". ukikutana na mtu mbali na kwenu mnaotokea sehemu moja utamuona ndugu yako na hapo usisi huanza, ukiwa mfano ulaya ukaona mtu anaongea kiswahili unamuona ndugu yako. katika nchi watu huonana ndugu kuanzia familia, ukoo, kabila, dini na kadhalika na hivyo pale ambapo hakuna ufuatiliaji wa sheria kuhakikisha kuwa watu hawatumii nyadhifa zao kuridhisha nafsi zao, katika ajira sura za kibinafsi hujitokeza katika mrorongo kama ulivyoorodheshwa hapo juu.
Hivyo ubinafsi katika Tanzania, katika nyanja ya ajira umejitokeza sana kifamilia ambapo unakuta familia fulani wameshikilia nyadhifa kubwa kubwa au zilizonona kimapato, sio kwa ushindani wao bali kwa kuwa na "good god father in family". sio lazima tutajane
kwa yale makabila ambayo wanakabila wake wamekuwa wakijisikia kwa mtu kujitaja mbele za watu kuwa mimi kabila fulani kutoka na picha fulani kwenye kabila hilo wamejikuta wakitambuana mijini na kujiona wako karibu na wale ambao mfumo wa ajira wa zamani ulikuwa umkipatia nafasi kila mtu ulikuwa umewawekea wajumbe wa kutosha katika nyadhifa muhimu wamenufaika na na mfumo huu wa sasa wa kuajiriana kwa kujuana inayotokana na uzembe katika uongozi katika kusimamia taratibu.
Kwa ujumla ubinafsi ndio chachu ya maendeleo, bila wewe kujiuliza kwa nini wewe uwe masikini wakati kuna watu wengine matajiri huwezi kupiga hatua, bila kujiuliza kwa nini familia yenu masikini au ikose vitu fulani na familia nyingine ziwe mbele huwezi kwenda. Bila kujiuliza kwa nini kabila lako liwe masikini wakati makabila mengine yamepiga hatua mbele, bila kujiuliza kwa nini sisi watanzania tu masikini hakika hatuwezi kupiga hatua. siri ya mafanikio ni kutoridhika na kile ulichonacho au na pale ulipo.
ila bila serikali kusimamia sheria ili kila mtu atambue mipaka yake na watu wakaanza kutumia mali za umma kama ni zao binafsi, ana mwajiri ndugu yake kwa sababu ni ndugu yake sio kwa sababu yeye ndiye bali zaidi ki taaluma kwa nafasi hiyo, au jamaa yake au rafiki yake wa kweli hapo ubinafsi utabadilika na kuwa chanzo cha kurudi nyuma na unaweza kuwa chanzo cha vurugu pale wale ambao hawana ndugu zao kwenye mfumo kuwaingiza watakapokata tamaa.
MTU YEYOTE AKIPEWA WADHIFA WA KUAJIRI AKAMUAJIRI NDUGU YAKE WA KULAUMIWA NI YULE ALIYEMPA WADHIFA HUO AU ANAYESTAHILI KUMSMAMIA. hivyo katika sekta ya umma kuajiriana kidugu wa kulaumu ni serikali. na serikali ya tanzania ni uongozi wa watanzania.
katika sekta binafsi usindani kwenye soko ndio utawafanya watu watoe ajira kwa ushindani na sio kwa kujuana