Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Poleni mliopatwa na ajali.. Mungu awatie nguvu wafiwa wote.
Japo kila awamu wanatumwaga majini hawa wateule wa NEC.
 
Si utani ngoja nikutajie listi

1. Kingunge alitembelewa mwishowe akavuta

2. Maria na Consolata mwishowe akavuta

3. Samuele Sita mwishowe kavuta

4. Yule aliyechora nembo ya taifa mwishowe kavuta

5. Mzee Majuto naye alivuta

6. Mzee mmoja wa CCM (jina nimelisahau) naye kavuta

7. Wengine niliowasahau nao wamevuta

Yaani hawaponi kabisa!

Duh nimeaanza kumuogopa kwa kweli ata nikiumwa nikimsikia anakuja ntakimbia na dripu zangu maana maisha matamu
Sumaye hakuvuta.
Pengo hakuvuta.
Kijo Bisimba hakuvuta.
..the list goes on. Acheni fikra za kichawi.
 
Hivi vivuko vinahitaji kua na vitu vya kujiokoa wakati wa dharula mfano maboya. N.k. mbaya zaidi kununua mali used. Meli, ndege, vivuko n.k serikali iangalie sana hili suala. poleni sana wafiwa.
 

Hawajapata idadi kamili ya watu waliokuwemo?kwani hicho kivuko ni sawa na daladala la kariakoo ambalo watu hupanda tu?
Ina maana ajali za M.V. Bukoba na Spice Islanders hazijawafunza wahusika wa meli kwenye kutunza kumbukumbu za wasafiri wao.
 
Jiwe huwaga ana gundu ni kama uko hospitali alafu Mortician(jiwe) akaingia wodini lazima gundu litokee tu... alienda msalimia dada yake mwishowe dada akavuta...

Anyway sisi kipaumbele chetu ni CHADEMA ila Kenge yupo wapi au nguvu ya soda ishaisha moto kama wa kiberiti maana alimwambia naniliu kwamba hatatuma salamu za rambirambi

Poleni wenzetu
Dah....akiongeza tena kukaza kiduchu tu...walai wapigaji wataanza kuokota makopo[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji13]
 
Taarifa nilizozipata haraka sasa hivi ni kuwa watu wengi sana wanahisiwa kufa maji baada ya kivuko kubinuka juu chini, chini juu katika kisiwa cha UKALA wilayani Ukerewe.


====
Taarifa Kwa Umma Kutoka Wakala wa Ufundi na Umeme-TEMESA Kuhusu Kuzama Kwa Kivuko Cha MV.Nyerere

View attachment 872340

Kivuko cha MV Nyerere kinachofanya safari zake kati ya Bugorara na kisiwa cha Ukala katika ziwa Victoria kimezama huku taarifa za idadi ya watu waliokuwemo ndani ya kivuko hazijajulikana.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Jonathan Shana amesema kivuko hicho kimezama wakati kikielekea katika Kisiwa cha Ukara. Kiliondoka saa 6 mchana na ilipofika saa nane kamili mchana kilipinduka.

Amesema bado hawajapata idadi kamili ya waliokuwemo kwenye kivuko hicho.

Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa), Hassan Karonda amekiri kuzama kwa kivuko hicho na yuko njiani kulekea huko na watatoa taarifa baadaye.

Kivuko cha MV. NYERERE kilinunuliwa na kuanza kutoa huduma mwaka 2004. Kilifungwa injini mbili mpya zenye thamani ya shilingi milioni 191 JULY 2018. Kivuko cha MV. Nyerere kina uwezo wa kubeba tani 25 sawa na abiria 100 na magari 3 kwa wakati mmoja.


View attachment 872299
Wanajeshi na raia wakitoa msaada wa uokoaji​
Hii mbona inatisha!
Ngoja tusubiri taarifa halisi ili tujue chanzo hasa cha ajali,lkn niwaombe wahusika waje na taarifa sahihi na pale ambapo kutakuwa na uzembe wa kwa watendaji hatua stahiki zichukuliwe..Zaidi ya yote nitoe salaam za pole kwa ndg zangu Wakerewe,maana inaweza kuwa msiba wa kisiwa kizima ikiwemo na sisi tulioko nje ya Ukerewe lkn tukiwa na ndg zetu huko.
 
Hivi vivuko vinahitaji kua na vitu vya kujiokoa wakati wa dharula mfano maboya. N.k. mbaya zaidi kununua mali used. Meli, ndege, vivuko n.k serikali iangalie sana hili suala. poleni sana wafiwa.
Serikali itoe kifuta machozi kwa wafiwa na majeruhi na walipwe bima. Wafiwa waing'ang'anie serikali ikibidi hata kwenda mahakamani waende ili wapate haki yao. Maana tatizo ni ubovu wa kivuko. Please wanasheria baada ya msiba mtoe msaada wa kisheria kwa hao wafiwa ili kufanikisha jambo hilo. Uzembe umekuwa too much.
 
Ukifikilia kwa makini utaona kuna umhimu mkubwa wa kurekodi taarifa za abiria wanao wa majini kuliko abiria wa nchi kavu

Gari ikipata ajali ni rahisi kupata idadi ya waliokua wakisafili, lakini ajari za majini hua tunaishia kukisia tu.... Kadhaa wamekufa.

Wale tunao safili gafla gafla bila tarifa kwa ndg zetu tubadikike.

Idadi kamili wanayo sema wanaona soo....maana sikuizi ili upande meli lazima ujiandikishe majina na uwe na kitambulisho
 
Kwenye uzembe kama huu kuna viongozi hawapaswi kusubiri kufukuzwa kazi bali wajiuzuru tu kama sehemu ya kuwajibika.
 
Ina maana ajali za M.V. Bukoba na Spice Islanders hazijawafunza wahusika wa meli kwenye kutunza kumbukumbu za wasafiri wao.
Maamlaka za bandari Zanzibar na Dar kwa kiwango kikubwa wamedhibiti upandaji meli kiholela uzembe kanda ya ziwa.
 
viongozi wa nchi hii" ni akili mgando". ..inastaajabisha sana na kuumiza wallahi" ndugu zetu wanaishi kwenye mazingira yenye miundo mbinu", haba" .. serikali ya ccm " ndio kwanza ipo busy kwakununua" upinzani", mwisho hupelekea chaguzi kurudiwa" huu ni ufujaji wa kodi za wananchi" wakati bado wanauhitaji mkubwa", wa miundombinu bora". ..Yaliyo tokea leo" iwe fundisho" kwa hili zimwi la hili taifa (ccm)..

halafu bila haya" wanatutajia idadi ya watu"6 wakati meli' imezama chini juu
Hao sita sio watu nafikiri ni magari makubwa Yale TATA au Scania kivuko kile kimeondoka na watu si chini ya 30 siasa mpk kwenye maisha ya watu!!

Wanajaribu kuneutralize situation but only fools can understand them not us anymore!!

Yaani wanakalia misifa tuuu!!wanakera sana hawa watu
 
Nasimama upande wako Bongolala, mamilioni yanatumika kununua wabunge na madiwani wa upinzani na kulazimika kurudia chaguzi kwa gharama kubwa, Pole kwa wote waliohusika katika kadhia hiyo, Mungu awalinde ambao bado wako hai.
Bongolala ni wewe na familia yako walahi!
Shwain kuba kabisa!
 
Back
Top Bottom