Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

bado sijaelewa! Safina ya Nuhu na Sumatra na hicho ulichoandika
 
C bora wafe madiver wanne lkn wananchi 10 wakaokolewa. Ebu acheni siasa. Hivi unajua wanaccm mtakuja kulia kuliko Opposition. Kwasababu nyie mtakuwa Malia na kusema mwno kwa sababu sanamu mmelichonga wenyewe na kuliweka. Ni hapo sasa mtakapokuwa mnalia, Opposition wanawang'ong'a TULIWAAMBIA!!! Halafu siyo mbali yaani soon
Mkuu ungeenda kudive ili uokoe
 
Majibu ya sasa ya Mongela ni baada ya kuteleza na kusema sababu ni giza. Kilicho dhahiri ni kwamba taifa halina vikosi vya uokoaji imara. Uokoaji ni vita, sawa na kuvamiwa. Utalala wakati adui anakuja? Divers walichoka, no support team, hapakuwa na namna.
 
Wakati Mungu anamuamrisha Nabii Nuhu ajenge boti kubwa lenye uwezo wa kubeeba viumbe na baadhii ya binadamu nadhani nuhu mwenyewe alijua mawazo ya munguni huwa hayana makosa,na kweli safari ilikuwa salama salimini.

Sasa ngoja uyasikie ya SUMATRA hawa jamaa walipopewa mamlaka ya kudhibiti chombo hicho chicho ndio unasimia vilio kila teo ni kwa nini chombo kilichopendekezwa kubeba kizazi cha watu wema ambacho katika maoni yangu ndio chombo salama muliko vyote SUMATRA wazembee kiasi hicho.

Kama SUMATRA wangelipewa jukumu la SAFINA si wangemgomea NUHU mwamba "Mzee hapandi mnyama yoyote hapa tunaijaza hii boti na mapipa ya mvinyo kwanza halafu hivyo vingine vitakuja juu yake"
View attachment 875233
SUMATRA WANGEPEWA KAZI YA KUISIMAMIA SAFINA MAMBO YANGEKUWA HIVI.
Sumatra hawapewi fedha za kutosha za usimamizi, pesa nyingi inanunulia ndege na wapinzani
 
bado sijaelewa! Safina ya Nuhu na Sumatra na hicho ulichoandika
Mamlaka iliyooe kusimamia ni SUMATRA majini na nchi kavu lakini uzembe wao umekubuhu chombo kihajazwa kupita kiasi hawakagui wao kazi yao ni kutega pale ubungo.
 
Hivi kuna sababu yoyote ile ya msingi kwa nini Mkurugenzi wa OSHA na menejimenti yake wasiwajibike?

Mkurugenzi wa OSHA anawajibika kwenye wizara iliyo chini ya waziri Jenista Mhagama

sasa cha kujiuliza je, ni kweli huyu Mkurugenzi na menjimenti yao wamewasilisha barua zao za kuwajibika/kujiuzulu kwa Waziri Mhagama na kama wamefanya hivyo mbona umma haujajulishwa? Na je waziri Mhagama alichukua hatua gani?


Je hii OSHA is it good for purpose?
 
Angewaambia pia wajijue jue..(kwa sauti ya Mbowe)

Hapa kazi tu
Wewe jitu huwa nakuchukia..hivi kwa mfano jiwe akimtumbua mkuu wa mkoa wa Mwanza sasa hivi kwa kutoa ile kauli ya kusitisha zoezi la uokoaji..na kusubiri uopoaji wa miili ya wahanga kesho yake..hamtaanza kumgeuka kweli na kuanza kumwagia misifa Jiwe?..kweli fisiem ni mafisi tu!
 
Wewe jitu huwa nakuchukia..hivi kwa mfano jiwe akimtumbua mkuu wa mkoa wa Mwanza sasa hivi kwa kutoa ile kauli ya kusitisha zoezi la uokoaji..na kusubiri uopoaji wa miili ya wahanga kesho yake..hamtaanza kumgeuka kweli na kuanza kumwagia misifa Jiwe?..kweli fisiem ni mafisi tu!

Kwanini hukwenda wewe kuokoa au hata kuvuta ndugu zako pia kama uliona ni vyema wangeendelea.. kwani leo umekatazwa pia.. jipange nenda usiku ukafanye yako.. wala hakuna atakaye kujali utakuwaje.. usisahau kujivalisha matairi mwilini maana hata kuogelea hujui na boti unaisikia kama usikiavyo baisikeli.
 
Hapa ndipo kama nchi tunapokuwa wapumbavu kwa ujumla wetu.
Siku ya alhamis SAA 1.22 jioni nikiwa eneo la tukio nilimuona na kumsikia Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongela akitangaza kusitisha zoezi la uokozi kwa sababu ya giza. Na nikiri wazi sikumsikia akisema ameshauriwa na wataalamu au yalikuwa mawazo yake. Wakati anatoa tangazo lake kulikuwa na divers ndani ya kivuko ambao walitoka na miili kadhaa saa mbili kasoro hivi. Mara baada ya kutangaza kusitishwa kwa zoezi vilio vilisikika mwaloni toka kwa ndugu waliokuwa na matumaini labda kuna watu wako hai ndani. Baada ya kusoma mawazo ya waombolezaji Mkuu wa wilaya ya Ukerewe akalazimika kutuliza hali ya hewa kwa kusema, namnukuu; Ndugu zangu katika hali ya kawaida mtu hawezi kukaa ndani ya maji kwa masaa zaidi ya manne bado akawa hai kama hana vifaa vya kumsaidia kupumua, Sisi viongozi wenu tuna huzuni kama ninyi lakini kazi hii haiwezi kufanyika gizani, mwisho wa kunukuu". Kwa vile watanzania huwa tunaona kauli za viongozi ni kauli za mbingu wengi walitii lakini wachache wenye uchungu walitoa hoja wakaonekana wabishi mbele ya viongozi. Hilo ziwa lililochafuka SAA 1 jioni hapa Ukara ni lipi? Au waliondoka nalo sisi hatukuliona? Kivuko kimezama chini ya mita 100 toka ufukweni, wazoefu wa ziwa mnajua vizuri, hivi hata ziwa likichafuka kwa umbali huo na kwa watu wenye vifaa watashindwa kuendelea na kazi?
Kesho yake baada ya kelele za wananchi na mitandaoni zoezi lilifanyika hadi usiku siku ya Ijumaa. Hizi sababu za ziwa kuchafuka tumeanza kuzisikiaIjumaa jioni baada ya Waziri Mkuu kuwepo na walikuwa wanaongea kama kujikosha tu na Leo ndo zimeletwa hapa kama sababu rasmi.
Siasa zinatufanya watanzania tukose mawazo ya kuhoji hata vitu vya msingi. Nawashangaa vijana wa ccm mitandaoni mnavyokosa utu na kushabikia makosa ya kiutendaji kwa vile tu aliyekosea ni wa Chama chenu. Sidhani kama kuna mwanaccm mwenye uchungu na aliyepotelewa na ndugu/jamaaa/rafiki kama ilivyonitokea Mimi anayeweza kuunga mkono mawazo yenu. Mimi nilisafiri Jumanne na kivuko hicho hicho na alhamis kikapata ajali, lakini maneno ya usalama mdogo ndani ya kivuko yalikuwepo, na bado tulijaa ingawaje si kama siku ya gulio Bugolora. Siku za Gulio mpaka mitumbwi toka Chifule na Chibasi huwa inasadia kutokana na wingi wa watu.
Mbunge wa Ukerewe kawa mkweli kwamba kivuko kilifanyiwa ukarabati, napo ni kuwekewa injini mpya tu na hoja kuu hata kwenye baraza za madiwani ni kupatiwa kivuko kipya na kikubwa zaidi.
Acha nikae kimya Nina majonzi.
Pole sana Bila bila
 
Kuhusu OSHA anza na wewe mwenyewe hapo kazini kwako.
1: Je, umeshawahi kufanyiwa medical check up?
2: Je, wafanyakazi wanaoacha kzi wanafanyiwa exit medical chek up?
3: Je, kuna fire extinguisher hapo kazini kwenu?
4: Je, kuna emergency assembly point hapo kazini kwenu?
5: Je, kuna Health Committee hapo kazini kwenu?

Kuhusu barabarani.
1: Je, dereva anapozidisha abiria na wanasimama wengi, ulishawahi kushughuliki ahili tatizo?
2: Je, magari ambayo hayana mikanda (safety belt) ulishawahi kushughuliki hilo tatizo?
3: Je dereva anapozidisha mwendo, ulishawahi kukemea au abiria wenzako walikushangaa

Unaweza kuorodhesha mengi ambayo huna wa kumlaumu bali ni sisi wenyewe kabla ya kumlaumu Magufuli na watendaji wake.
Naona mfanyakazi wa OSHA unatetea ujira wako
 
It doesn't make any sense....mkuu wa mkoa kwa hili nitamlaumu sana.....zoezi linasitishwaje kivuko kimezama na watu wengi hivi

Ilikuwaje hadi leo hujajitolea kwemda kuokoa usiku.. mna jua kuandika huku nyuma hata majirani zenu hamuwajali.. kuwa umbele na kuhatarisha maisha yenu.. mmejaa porojo tu

Acheni kuendelea kuumiza wafiwa na maneno yenu..
 
Back
Top Bottom