Hivi boti za doria za polisi na JWTZ hazina taa, mbona zina tochi kubwa kwa juu zenye uwezo wa kumlika zaidi ya mita 200.
Hizo boti zipo ni juzi tu tulitangaziwa kuwa serikali imenunua boti za doria za kisasa na kupelekwa ziwa Vitoria na zanzibar.
Hatukujifunza kwa MV Bukoba kosa lilelile linajirudia, vikosi vyetu havina maandalizi mazuri. Sisi tuna maziwa tuna bahari tuna mito, tunajua ajari kama hizi lazima zitatokea kwanini tusiimarishe vikosi vyetu vya uokozi?Tuna helkopta zinaruka juu kulinda wateule,nchi jirani zina vifaa kedekede mf. Kenya. In a matter of hour or two, watakuwa wamefika site!! Kipindi cha Mkapa na MV Bukoba, kuna kikosi kilitoka Zenj na SA walifanya kazi day& night. Nashauri, pamoja na juhudi zote, tusitangulize visingizio vya giza!! Tuongeze juhudi na tuimarishe mahusiano mema na majirani zetu ili tunakotindikiwa tupate msaada. Mungu weka mkono wako katika hili.
Tunaachaje kuilaumu serikali ?!, pale kuna wasimamizi ambao ni watumishi wa hiyo serikali, na wanalipwa mishahara ambayo ni kodi zetu, kama wamekaa tu wanaangalia watu wanapanda bila Control hii ni failure government, Bernard Membe alisema hii serikali imefeli mapema kabisa, serikali ndio msimamizi na ina vyombo vya ulinzi, (Polisi na migambo ambao kazi yao huwa ni kupiga wapinzani)Hivi vivuko huwa vinajaza mpaka inasikitisha!
Usifikiri hao watu wako kama wewe na kuchukua tahadhari! NO WAY!
Mara nyingine unaona kabisa watu wanafanya mambo na ni completely suicidal act!
Kama wanavyo panda mshikaki kwenye bodaboda au pickup kwa Nyuma!
Mambo mengine huwa yanabadilika kwa wakati wake, lakini kuinyoshea kidole Serikali ni kutafuta LAANA KUTOKA KWA MAMA TANZANIA walahi!
Be realistic kijana mdogo ehhh jamani!
That’s all
Pumbavu mkubwa wewe na waliyokutuma, mbwa koko wewe, mimi nimeshindwa kukusambehe kwa upumbavu wako nyau wewe
kesho wakimtatua marinda yeye atakuja lalama hapa kama akirudi salama,washakusoma wenye kazi zao watakutafutaHeshima kwa wakubwa ni kitu cha bure kabisa.....sio sawa kwa hili.
Hata enzi za serikali ya akina Benard Membe, kivuko hiki kilikuwapo na kilijaza watu.Tunaachaje kuilaumu serikali ?!, pale kuna wasimamizi ambao ni watumishi wa hiyo serikali, na wanalipwa mishahara ambayo ni kodi zetu, kama wamekaa tu wanaangalia watu wanapanda bila Control hii ni failure government, Bernard Membe alisema hii serikali imefeli mapema kabisa, serikali ndio msimamizi na ina vyombo vya ulinzi, (Polisi na migambo ambao kazi yao huwa ni kupiga wapinzani)
kwahyo wewe ulitaka atoe jibu gani kwa mfano?
kuna utofauti gani maiti ikitolewa kwenye maji jana au leo?
itafufuka? itapunguza machungu ya wafiwa? au labda ww unahisi vipi yani?
huwezi riski maisha ya watu walio hai kwa sababu ya mtu ambaye ameshapoteza uhai hyo ipo hivyo dunia nzima....
sema kuna watu mnajifanya mnajua kuongea na kuongoza nchi wakati hata familia ya kuiongoza bado hujaipata..
embu basi sema ulitaka waendelee kutoa maiti hadi usiku wa manane? unajua changamoto za uokoaji majini?
Yani wewe jamaaMimi hoja yangu imejikita kwenye usahihi wa kusitisha zoezi siku ya jana kwa sababu ya giza, na nikaeleza kwamba ilikua ni sawa kufanya vile kutokana na njia ambazo zilikua zinatumika. Na ili zoezi lisiendelee "kulala" ni lazima tu "improve the methods" ili ziwe fanisi na salama kwa waokoaji hasa wakati huo wa usiku na tuwaotoe ndugu zetu (hai au la) kule chini. Na mapendekezo uliyoyatoa hapo juu ni ya msingi kabisa ili kufanikisha zoezi zima. Kwa sababu yoyote ile, kwa uzembe au makosa ya mtu yeyote yule, kama njia za uokozi zilizokua zikiendelea kutumika hazikua salama na fanisi hiyo jana usiku, ilikua sahihi kusitisha zoezi lile hadi asubuhi. Suala la kwanini bado tunatumia njia "za kizamani" kufanya uokozi ni suala jingine (with respect to maamuzi ya jana)
Mnunuzi wa hicho kivuko ni nani??Hapo ingekuwa ni sisi chadema tuna vikao vyetu au mkutano wasingechoka kabisa
Ndiyo matunda ya Absolute power, Tume kufuru ya uchaguzi, kufurahia uonevu na ukatili wa vyombo vya Dola dhidi ya raia wasio na hatia.NIMEUMIA SANA
Anaandika Kijana Msomi
Rashid Chilumba
Nimesikia zoezi la uokoaji kwenye ajali ya kivuko Mwanza limesitishwa hadi kesho kutokana na kiza, sasa kesho mtakwenda kuokoa au kuokota Maiti?
Hapo Mwanza kuna kikosi cha Jeshi, boti za doria za polisi, helikopta na vivuko vingine? Hivi kweli vyote hivyo havina taa kubwa za kuwezesha zoezi la uokozi kuendelea usiku kucha? Kama havina tulivinunua vya kazi gani?
Ni aibu kwa viongozi kusema tunaenda kulala eti kuna giza ziwani wakati kuna dazani ya watanzania wenzetu tunaowahudumia wamezama ziwani tena siyo kwa uzembe wao bali kwa ujuba na tabia ya kutokujali maisha ya watu na kutosimamia usalama wao.
Mkuu wa mkoa, RPC, mkuu wa kamandi ya Jeshi la Wananchi, Mkuu wa Bandari Mwanza mnapata wapi ujasiri wa kwenda kulala na kuna watu watoto wao, baba zao, Mama zao wamo majini na hawajui kama watawapata wakiwa hai? Hivi ingelikuwa ni jamaa zenu wa karibu mngepata ujasiri wa kusimamisha zoezi kwa sababu ya kiza?
Katika dunia ya leo seriously kabisa mnasema kiza kinawazuia kuokoa watu? Aiseee.... Kwa hiyo hao waliozama ikiwa kwa bahati bado wapo hai hadi sasa mnategemea Israeli atawangoja ninyi hadi kesho jua litapochomoza? Huu ni uzembe wa hali ya juu mno.
Kweli kabisa mnashindwa kufunga tochi kubwa kama zile za bandari kwenye helikopta moja ya polisi hapo na boti nne tano mkaingia kuwaokoa watanzania wenzetu? Hata ikiwa ni wafu lakini faraja ni kupata japo miili yao hadi kesho samaki, mawimbi ya ziwa nk inaweza kuwa imewapoteza zaidi.
Leo nimeumia sana, makosa yale yake ya Mv Bukoba, Spice Islander, Skagit yamejirudia Mv. Nyerere na watu wanaenda kulala usiku umeingia na vyombo vya habari vinaonesha shilawadu na kutoa dakika kiduchu kwa habari muhimu na msiba mkubwa huo wa taifa.
Na tena mlionywa mara kadhaa kuwa chombo ni kibovu. Mkuu wa bandari ya mwanza bado yupo na wadhifa wake na msimamizi wa Sumatra kanda ya ziwa kesho ataenda pia ofisini.
Mungu awapumzishe waliotangulia na atawalipa waliowasababishia kuzama kwenu kwa uzembe wao.
Cc
Dotto Bulendu
Malisa GJ
Kheri James
Tusaidiane kusema Ndugu zangu. Tunawezaje kwenda kulala na watanzania wenzetu wako majini sasa hivi?
Hakika wewe ni mwendawazimu kuu walahiNimemskia mmoja wa viongozi wetu wanoishi kwa kodi zetu, akihojiwa na BBC Leo asubuhi kwamba kwanini walisitisha uokoaji. Utumbo aliojibu ndo ulio nichosha.
Kwamba, waaliingia kwenye meli na kujiridhisha kwamba hakuna alie hai ambae anahitaji msaada, isitoshe pia waokoaji walikuwa wamechoka kutokana wanatumia mitumbwi kubeba maiti hivyo tukaamua kusitisha uokoaji mpaka kesho.
Huu uongozi wa awamu hii naona kila mtu kichaaa.
Vifaa vya uokozi lazima ziwe standby hujui ajari itatokea lini na wapi, boti za doria zinafanya kazi 24hrs, nyingi ziko Mwanza jijini, kwa speed za boti hizo kutoka Mwanza hadi kisiwa cha Ukara sidhani itatumia hata nusu saa, afterall ajari imetokea saa 8 kulikuwa na uwezekano mkubwa wa kufika pale mapema na kuanza maandalizi ya kukabiliana na giza kwa kuandaa taa.Kuwa na hizo boti (kuzimiliki) ni jambo moja, ni jambo jema. Lakini je, hiyo jana zilikuwepo site ? Kama hazikuwepo (kwa sababu yoyote ile) zoezi lisingeweza kuendelea. Uwezo wetu wa kukabiliana na majanga bado uko chini, Mungu saidia leo kiza isiwe ni kikwazo maana bado muda upo wa kupeleka kila aina ya vifaa ili ku "improve the methods"