Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Hivi boti za doria za polisi na JWTZ hazina taa, mbona zina tochi kubwa kwa juu zenye uwezo wa kumlika zaidi ya mita 200.

Hizo boti zipo ni juzi tu tulitangaziwa kuwa serikali imenunua boti za doria za kisasa na kupelekwa ziwa Vitoria na zanzibar.

Kuwa na hizo boti (kuzimiliki) ni jambo moja, ni jambo jema. Lakini je, hiyo jana zilikuwepo site ? Kama hazikuwepo (kwa sababu yoyote ile) zoezi lisingeweza kuendelea. Uwezo wetu wa kukabiliana na majanga bado uko chini, Mungu saidia leo kiza isiwe ni kikwazo maana bado muda upo wa kupeleka kila aina ya vifaa ili ku "improve the methods"
 
Tuna helkopta zinaruka juu kulinda wateule,nchi jirani zina vifaa kedekede mf. Kenya. In a matter of hour or two, watakuwa wamefika site!! Kipindi cha Mkapa na MV Bukoba, kuna kikosi kilitoka Zenj na SA walifanya kazi day& night. Nashauri, pamoja na juhudi zote, tusitangulize visingizio vya giza!! Tuongeze juhudi na tuimarishe mahusiano mema na majirani zetu ili tunakotindikiwa tupate msaada. Mungu weka mkono wako katika hili.
Hatukujifunza kwa MV Bukoba kosa lilelile linajirudia, vikosi vyetu havina maandalizi mazuri. Sisi tuna maziwa tuna bahari tuna mito, tunajua ajari kama hizi lazima zitatokea kwanini tusiimarishe vikosi vyetu vya uokozi?

Katika karne hii bado tunasingizia giza, ingekuwa vita tungesitisha sababu ya giza, siku hizi kuna vifaa vya kuona gizani (night vision goggles) nafikiri lazima jeshi linazo.
 
Hivi vivuko huwa vinajaza mpaka inasikitisha!
Usifikiri hao watu wako kama wewe na kuchukua tahadhari! NO WAY!
Mara nyingine unaona kabisa watu wanafanya mambo na ni completely suicidal act!
Kama wanavyo panda mshikaki kwenye bodaboda au pickup kwa Nyuma!
Mambo mengine huwa yanabadilika kwa wakati wake, lakini kuinyoshea kidole Serikali ni kutafuta LAANA KUTOKA KWA MAMA TANZANIA walahi!
Be realistic kijana mdogo ehhh jamani!
That’s all
Tunaachaje kuilaumu serikali ?!, pale kuna wasimamizi ambao ni watumishi wa hiyo serikali, na wanalipwa mishahara ambayo ni kodi zetu, kama wamekaa tu wanaangalia watu wanapanda bila Control hii ni failure government, Bernard Membe alisema hii serikali imefeli mapema kabisa, serikali ndio msimamizi na ina vyombo vya ulinzi, (Polisi na migambo ambao kazi yao huwa ni kupiga wapinzani)
 
Ila watanzania lazima ukubali uzembe wetu sisi kama raia. Nimeshangazwa ma picha hiyo hapo juu ya raia waliangalia na caption yake inasema RAIA WAKIWA MITA CHACHE TOKA ILIPOZAMA BOTI. Tujifunze kuogelea, idadi zitapungua ingawa najua kuna mida kunakuwa ma panick ktk ajali.
 
Tunaachaje kuilaumu serikali ?!, pale kuna wasimamizi ambao ni watumishi wa hiyo serikali, na wanalipwa mishahara ambayo ni kodi zetu, kama wamekaa tu wanaangalia watu wanapanda bila Control hii ni failure government, Bernard Membe alisema hii serikali imefeli mapema kabisa, serikali ndio msimamizi na ina vyombo vya ulinzi, (Polisi na migambo ambao kazi yao huwa ni kupiga wapinzani)
Hata enzi za serikali ya akina Benard Membe, kivuko hiki kilikuwapo na kilijaza watu.
 
kwahyo wewe ulitaka atoe jibu gani kwa mfano?

kuna utofauti gani maiti ikitolewa kwenye maji jana au leo?

itafufuka? itapunguza machungu ya wafiwa? au labda ww unahisi vipi yani?

huwezi riski maisha ya watu walio hai kwa sababu ya mtu ambaye ameshapoteza uhai hyo ipo hivyo dunia nzima....

sema kuna watu mnajifanya mnajua kuongea na kuongoza nchi wakati hata familia ya kuiongoza bado hujaipata..

embu basi sema ulitaka waendelee kutoa maiti hadi usiku wa manane? unajua changamoto za uokoaji majini?

Mkuu naomba nikujibu kwa ufupi tuu uelewe majanga yote yanatokea katika mazingira magumu na ndio maana waokoaji wanasomea sio kila mtu anaweza kuokoa iwe majanga ya maji au moto.

pili umeongelea huwezi kuhatarisha maisha ya walio hai kwa ajili ya uokoaji hiyo haipo na umezungumzia duniani sijui ya wapi hiyo dunia...waokoaji wengi wanahatarisha maisha ndio maana hata unaona wanafanya kazi ya hatari ili kuokoa maisha ya walioathirika huko wiki iliyopita waokoaji wawili walikufa SA gorofa ya nane baada ya kwenda kumuokoa mtoto ambae alipona kule Thailand waokoaji waliwaokoa wale watoto kwenye mazingira magumu muokoaji mmoja alifariki kwa kukosa hewa ya oxygen ila watoto wote walipona na ndio maana waokoaji wapo katika jeshi la Zimamoto katika Nchi zilizoendelea...
 
Mimi hoja yangu imejikita kwenye usahihi wa kusitisha zoezi siku ya jana kwa sababu ya giza, na nikaeleza kwamba ilikua ni sawa kufanya vile kutokana na njia ambazo zilikua zinatumika. Na ili zoezi lisiendelee "kulala" ni lazima tu "improve the methods" ili ziwe fanisi na salama kwa waokoaji hasa wakati huo wa usiku na tuwaotoe ndugu zetu (hai au la) kule chini. Na mapendekezo uliyoyatoa hapo juu ni ya msingi kabisa ili kufanikisha zoezi zima. Kwa sababu yoyote ile, kwa uzembe au makosa ya mtu yeyote yule, kama njia za uokozi zilizokua zikiendelea kutumika hazikua salama na fanisi hiyo jana usiku, ilikua sahihi kusitisha zoezi lile hadi asubuhi. Suala la kwanini bado tunatumia njia "za kizamani" kufanya uokozi ni suala jingine (with respect to maamuzi ya jana)
Yani wewe jamaa
Yan kuku tu vitoto wake wakinyeshea mvua atawafunika kwa mbawa zake hata anaeeza asitoke kwenda bandani
Je binadam
Unaanzisha usafiri wa majin afu hujui kama kuna majanga?
 
Kweli inasikitisha vyombo vya usalama kwenda kulala huku watanzania wanaangamia wameshindwa kufanya kazi hata kwa shift?? Kwa technolojia ya Leo ni aibu kusema eti kuna Giza , so sorry kwa wafiwa
 
Daah afu linatokea lijitu ambalo vivu la kufikia na kusema wanaoishi Dsm wanapoteza muda wakati maisha ya mikoani yana risk sn hasa inapotokea maafa makubwa
 
NIMEUMIA SANA

Anaandika Kijana Msomi
Rashid Chilumba

Nimesikia zoezi la uokoaji kwenye ajali ya kivuko Mwanza limesitishwa hadi kesho kutokana na kiza, sasa kesho mtakwenda kuokoa au kuokota Maiti?

Hapo Mwanza kuna kikosi cha Jeshi, boti za doria za polisi, helikopta na vivuko vingine? Hivi kweli vyote hivyo havina taa kubwa za kuwezesha zoezi la uokozi kuendelea usiku kucha? Kama havina tulivinunua vya kazi gani?

Ni aibu kwa viongozi kusema tunaenda kulala eti kuna giza ziwani wakati kuna dazani ya watanzania wenzetu tunaowahudumia wamezama ziwani tena siyo kwa uzembe wao bali kwa ujuba na tabia ya kutokujali maisha ya watu na kutosimamia usalama wao.

Mkuu wa mkoa, RPC, mkuu wa kamandi ya Jeshi la Wananchi, Mkuu wa Bandari Mwanza mnapata wapi ujasiri wa kwenda kulala na kuna watu watoto wao, baba zao, Mama zao wamo majini na hawajui kama watawapata wakiwa hai? Hivi ingelikuwa ni jamaa zenu wa karibu mngepata ujasiri wa kusimamisha zoezi kwa sababu ya kiza?

Katika dunia ya leo seriously kabisa mnasema kiza kinawazuia kuokoa watu? Aiseee.... Kwa hiyo hao waliozama ikiwa kwa bahati bado wapo hai hadi sasa mnategemea Israeli atawangoja ninyi hadi kesho jua litapochomoza? Huu ni uzembe wa hali ya juu mno.

Kweli kabisa mnashindwa kufunga tochi kubwa kama zile za bandari kwenye helikopta moja ya polisi hapo na boti nne tano mkaingia kuwaokoa watanzania wenzetu? Hata ikiwa ni wafu lakini faraja ni kupata japo miili yao hadi kesho samaki, mawimbi ya ziwa nk inaweza kuwa imewapoteza zaidi.

Leo nimeumia sana, makosa yale yake ya Mv Bukoba, Spice Islander, Skagit yamejirudia Mv. Nyerere na watu wanaenda kulala usiku umeingia na vyombo vya habari vinaonesha shilawadu na kutoa dakika kiduchu kwa habari muhimu na msiba mkubwa huo wa taifa.

Na tena mlionywa mara kadhaa kuwa chombo ni kibovu. Mkuu wa bandari ya mwanza bado yupo na wadhifa wake na msimamizi wa Sumatra kanda ya ziwa kesho ataenda pia ofisini.

Mungu awapumzishe waliotangulia na atawalipa waliowasababishia kuzama kwenu kwa uzembe wao.

Cc
Dotto Bulendu
Malisa GJ
Kheri James

Tusaidiane kusema Ndugu zangu. Tunawezaje kwenda kulala na watanzania wenzetu wako majini sasa hivi?
Ndiyo matunda ya Absolute power, Tume kufuru ya uchaguzi, kufurahia uonevu na ukatili wa vyombo vya Dola dhidi ya raia wasio na hatia.
 
Nimemskia mmoja wa viongozi wetu wanoishi kwa kodi zetu, akihojiwa na BBC Leo asubuhi kwamba kwanini walisitisha uokoaji. Utumbo aliojibu ndo ulio nichosha.


Kwamba, waaliingia kwenye meli na kujiridhisha kwamba hakuna alie hai ambae anahitaji msaada, isitoshe pia waokoaji walikuwa wamechoka kutokana wanatumia mitumbwi kubeba maiti hivyo tukaamua kusitisha uokoaji mpaka kesho.

Huu uongozi wa awamu hii naona kila mtu kichaaa.
Hakika wewe ni mwendawazimu kuu walahi
 
Kuwa na hizo boti (kuzimiliki) ni jambo moja, ni jambo jema. Lakini je, hiyo jana zilikuwepo site ? Kama hazikuwepo (kwa sababu yoyote ile) zoezi lisingeweza kuendelea. Uwezo wetu wa kukabiliana na majanga bado uko chini, Mungu saidia leo kiza isiwe ni kikwazo maana bado muda upo wa kupeleka kila aina ya vifaa ili ku "improve the methods"
Vifaa vya uokozi lazima ziwe standby hujui ajari itatokea lini na wapi, boti za doria zinafanya kazi 24hrs, nyingi ziko Mwanza jijini, kwa speed za boti hizo kutoka Mwanza hadi kisiwa cha Ukara sidhani itatumia hata nusu saa, afterall ajari imetokea saa 8 kulikuwa na uwezekano mkubwa wa kufika pale mapema na kuanza maandalizi ya kukabiliana na giza kwa kuandaa taa.

Mbali na boti za polisi za doria kuna helikopta za polisi na jeshi zisingeshindwa kufika pale na kumulika wakati zoezi likiendelea. Ni uzembe fulani tu umefanyika.
 
Back
Top Bottom