Nimesikitishwa sana na taarifa ya mkuu wa mkoa wa Mwanza akisema eti zoezi la uokoaji wa maiti na wahanga wa ajali ya kivuko cha MV Nyerere ihairishwe kwa sababu ya giza.
Najaribu kuwaza mpaka miaka hii na karne hii ambayo sayansi na technology ni kubwa lakini bado Giza linakuwa ni changamoto kwa nchi ya Tanzania.
Kupitia matangazo ya DW,wanasema mpaka jana saa mbili usiku walikuwa wakisikia milio ya watu wakingonga gonga kwa ndani kuashiria kuwa bado wapo hai.
Hii ina maana kama zoezi la uokoaji lingekuwa linaendelea hadi usiku huenda na wao wangeokolewa.
Kuna mbunge wa upinzani alishawahi kutoa tahadhari lakini haikupewa uzito wa juu.Hii tabia ya kupuuza puuza itaendelea mpaka lini?
Anyway,Wapunzike kwa Amani