Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

DW: Idadi ya waliokufa baada ya kuvuko cha MV Nyerere kuzama katika eneo la Ziwa Victoria mkoani Mwanza nchini Tanzania imeongezeka na kufikia zaidi ya 100. Jitihada ya uokoaji zimeendelea tena leo baada ya kusitishwa kwa muda jana usiku. Kutoka katika eneo la Busia. Mwenzetu Sudi Mnette amezungumza na mwandishi wa habari Jovitha Kaijage aliyesema kuna wasiwasi wa kuongezeka kwa idadi ya vifo.
 
Huko ni kwetu na nilipanda kivuko hicho mwaka Jana mwezi wa 9. Tulikua abiria zaidi ya uwezo wa meli. Niliongea na captain na tukajenga urafiki huku nikimweleza juu ya jambo hili. Kibaya zaidi nimesoma karibu na Bugolora Alhamisi abiria na mizigo kuelekea Ukara huwa utitili. Serikali inajua vyema lakini wao hujikita kwenye mapato kuliko tahadhali ya kupoteza maisha ya watu. Mungu iumbe upya Tz. CCM inatumaliza na kututeketeza bila mapenzi yako.
 
Nimesikitishwa sana na taarifa ya mkuu wa mkoa wa Mwanza akisema eti zoezi la uokoaji wa maiti na wahanga wa ajali ya kivuko cha MV Nyerere ihairishwe kwa sababu ya giza.
Najaribu kuwaza mpaka miaka hii na karne hii ambayo sayansi na technology ni kubwa lakini bado Giza linakuwa ni changamoto kwa nchi ya Tanzania.

Kupitia matangazo ya DW,wanasema mpaka jana saa mbili usiku walikuwa wakisikia milio ya watu wakingonga gonga kwa ndani kuashiria kuwa bado wapo hai.
Hii ina maana kama zoezi la uokoaji lingekuwa
Yaani hata mm nimeshangaa sana hii nchi sjui tulilogwa na nani??
 
Nimesikitishwa sana na taarifa ya mkuu wa mkoa wa Mwanza akisema eti zoezi la uokoaji wa maiti na wahanga wa ajali ya kivuko cha MV Nyerere ihairishwe kwa sababu ya giza.
Najaribu kuwaza mpaka miaka hii na karne hii ambayo sayansi na technology ni kubwa lakini bado Giza linakuwa ni changamoto kwa nchi ya Tanzania.

Kupitia matangazo ya DW,wanasema mpaka jana saa mbili usiku walikuwa wakisikia milio ya watu wakingonga gonga kwa ndani kuashiria kuwa bado wapo hai.
Hii ina maana kama zoezi la uokoaji lingekuwa
Watu wanacheza Mpira usiku we unasema hamuwezi kuokoa watu wana kufa na maji uck kucheza mpira na kuokoa maisha ya watu bora nn
 
Funny Enough mwezi huu wakaji Magufuli anazindua ujenzi wa meli mpya nilimsikiliza mwanzo mwisho.

Yule mkurugenZi wa mambo ya usafiri majini alikuwa kaimu na rais kamfanya awe kamili hapo hapo.

Rais aliwalaumu sana kwa uzembe na aka quote ule uzembe wa mv bukoba.

Rais alikuwa anaongea kwa uchungu sana tena sana.

Na akawaagiza waanzishe tiketi za electronics.
Aliwaambia anajua wanayoyafanya na aliwaasa waache upuZi na ujanja ujanja.

Nina uhakika kwa research yangu niliyoifanya. Tiketi zilizouzwa kihalali zilikuwa ni 70. Na magari mawili na mizigo basi.

Ila kivuko kilibeba watu zaidi ya mia nne.(imagine kivuko kina uwezo wa kubeba watu 101 ila wamezidi watu miatatu).

Tiketi zingine wahudumu walipiga pesa kwa ujanja ujana pamoja na kwamba rais mwezi huu aliidhinisha pesa za mishahara yao.

Jiulizeni walikaa zaidi ya miezi kumi hawalipwi mishahara sasa walikuwa wanaishije?

Ndio upumbavu kama huu.

Nashauri hawa jamaa wanyongwe.


Uzembe unaanzia kwa mkuu wa mkoa kushuka chini.
Wote ni wazembe askari wote walikuwa wanaona jinsi wananchi wanavyojazwa kwenye kivuko.

Shiriki la usafiri majini linasema eti haijulikani watu wangapi walikuwa kwenyw kivuko hicho.
Hili ni jibu kutoka kwa wataalamu ambao wamesoma na wanasimamia rasilimali zetu.
 
Kwa kweli hawa wahusika wa kivuko ni wahuni sana.

Haiwezekani meli yenye capacity ya watu 100 ibebe watu zaidi ya 400.

Ukijaribu kuwaelimisha watakwambia katengeneze meli yako upande ujinafasi.

Hata kwenye madaladala watu wanajazwa nyomi kama siafu.

Kila kitu shithole.
 
Back
Top Bottom