Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Jamani mlitaka sfanye nini wakati hakuna vifaa vya kuokolea muda huo?? Na sio kwamba atakuwa alijiamulia tu mwenyewe, hao wazamiaji hawana vifaa vya kufanyia kazi kwenye mwanga itakuwa gizani?? Ni aibu kwa nchi, hatuko tayari kwenye majanga!! Ya nchi kavu tu yanatushinda itakuwa ya majini??
sasa yale magari Ya kuwasha washa" mnayoyatumiaga wakati wakampeni " si muyauze tu" ili mnunue " vifaa tija" vitakavyo saidia uokozi kwenye majanga kama haya "... Au yale magari wakati huu yanafaida gani"...

au ndio mmekaa mnahofu muda" wote kuwa wa tz wanawaza kuandamana tu ".... mxiiiiiiiiuuuuuww JINGA sana haya ma CCM
 
Kuhusu TBC kujiunga mubashara waoneshe nini sasa ? Ki ubinadamu sio sahihi.mi nimeona clip za ile miili whatsapp sio busara kuionesha kwenye TV
Siyo kuonyesha miili inavyoopolewa. Watangazaji wanatakiwa wawe kribu na kutoa updates, mahojiano na kila habari inayohusiana na ajali. Vipindi vingine vinasitishwa kwa muda.
 
Niliowaona wako busy kuhusu wale wanafunzi wa Arusha hapa sijawaona pia, ubaguzi in
 
CCM mmeua hawa watu kwani mbunge alishapambana sn kivuko kingine kipatikane but nnaendeleza utapeli tu Kwa watanzania.
 
Wakati mzee Mwinyi anajiuzulu alikuwa kwenye zile mahabusu walizojaza watu hadi wakafa ? Kwanini Mzee alijiuzulu badala ya RPC ,OCD nk ?

Mzee Mwinyi alijiuzulu kwasababu yeye wkati ule alikuwa ni waziri wa mambo ya ndani.

Pili, kesi hiz mbili zinatofautiana wakati hili ni janga ile kesi ya Shinyanga haikuwa ni janga.
 
Ndugu wanabodi:
Hivi sisi Watanzania nano katuloga? TBC na vyombo binafsi vimeshindwa kujiunga mubashara kwenye shughuli ya uopoaji maiti lakini hats kupiga nyimbo za maombolezo imeshindikana kweli?

Nimesema shughuli ya uopoaji kwa sababu serikali ingekuwa serious na maisha ya Watanzania wenzetu ingepeleka jenereta jana ili shughuli ya uokoaji iendelee Jana usiku.

Watanzania zaidi ya 126 ni msiba mkubwa wa taifa lakini radio na luninga ya taifa wameshindwa kujiunga mubashara hatua kwa hatua badala yake wanaendelea na mambo yao yasio na maslahi kwa Taifa.

Naamin kwa Wazungu habari ingekuwa ndio hiyo kuwa mubashara muda wote kwa kila kituo cha luninga na redio.Na wasingekubali kusitisha shughuli ya uokoaji eti kisa giza

Tumeshindwa kuthamini uhai wa wenzetu, kweli ngozi nyeusi ni wabinafsi haijapata kutokea
Nashangaa TV zetu zilikuwa busy kuonyesha Royal wedding lakini kwenye tukio hili tunakosa live coverage
 
Back
Top Bottom