Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

1. Inasemekana kivuko kimefanyiwa ukarabati miezi kama miwili iliyopita kwa kuwekewa injini mpya za thamani ya milioni 190 ( kama sijakosea).
2.Tahadhari nadhani ambayo haijazingatiwa itakuwa ni uwezo halisi wa kivuko kubeba mzigo na mzigo halisi uliobebwa. Hata hivyo kuhusu uwezo wa kivuko unaweza kutupa elimu maana kwa jinsi ulivyokokotoa uwezo wa vivuko unaweza kutusaidia kivuko hiki kilikuwa na uwezo kiasi gani. Kwani kwenye pointi hii ulikazia kabisa kuwa " haiwezekani"!
3.Pia kitendo cha kutojua idadi kamili ya abiri haikubariki wakati siku hizi naona wanatoza nauli na kutoa tiketi za electronic. Lazima kumbukumbu ziwepo vinginevyo kuna udanganyifu mkubwa unafanyika.
4.Kuna uwezekano wa kuwa labda ni majanga ya asili, kwani kipindi hiki kumekuwa na upepo wenye kasi kubwa na wa kushtukiza. Hata hivyo(kama ajali hii imetokana na upepo) hii inaonyesha yawezekana hakuna ushirikiano wa kutosha kati Mamlaka ya hali ya hewa na wamiliki wa vivuko(TEMESA) ama wamiliki na makapteni wanapuuzia taarifa wanazopewa na wataalamu wa hali ya hewa.
6. Nimakosa kuingiza masuala ya kisiasa tena ambayo hayana ushahidi kwenye masuala ya majanga kama haya. Vinginevyo, ieleweke kuwa unakusudia kuhujumu utawala sa serikali ya sasa kwa kuigombanisha na wananchi kwa malengo " maalumu". Kama huna lengo hilo jitahidi kukwepa kutumia maneno yanayoweza kuashiria hilo.
===
Inauma sana taifa kupoteza watu wake kwa namna hii.
Inawezekana...Meli zote zinakuwa na mstari wa usalama.ambao maji hayatakiwi yauguse huo mstari...maji yakiugusa inamaanisha uzito umezidi.. Tatizo ni stability.,,Meli ilikata kona vibaya/ ghafla hivyo mizigo ikahamia upande mmoja, ikakosa balance ikapinduka...
 
Imagine doesn’t count!
Grow up kido!
hata sayansi iliyopelekea tukawa na dreamliner ilianza na assumption mkuu.
ninasema hivyo maana kwenye matukio kama haya ukifanikiwa kukutana na waanga huwa kuna story nyingi. Hata ninachokisema kinawezekana. Labda kama wahusika walijiridhisha hakuna aliyehai ambaye amebaki hivyo watakuja kuokoa kesho tu taratibu kwenye mwanga. Ila maoni Yangu Bora wangefanya kimyakimya, maana siku meli ikipinduka na giza likianza kuingia nitajua sitegemei kuokolewa hadi asubuhi.
 
Hivi RC, Msimamizi wa bandari Mwanza, RPC, DC, Kiongozi wa Zimamoto leo walipata usingizi kweli? huku roho za Watanzania zikiteketea ziwani? I cant imagine uongozi wa dizaini hii, na utasikia hakuna atakayewajibika.
Unajiuliza swali ambalo hauna jibu alafu unahitimisha kuonyesha walilala.
Unapojaribu kutafuta upenyo hapa ili uongeze political mileage lazima utakuwa na mtazamo kama wako.
 
Nikukumbushe tu 90% ya wavuvi wanaingia ziwan usiku na kutekeleza shughuli zao usiku,,,na tecnologia ya kuzuia Giza mkuu inakua tatizo?.. Boti za kuwasaka wavuvi haramu zipo kibao na zinafanya kazi 24HRS ,,ila za kuokoa watu ambao na hakika baadhi walikua hai hazipo
Hapa kwetu wanakesha kwa mambo ya hovyo kama
Mkesha wa mwenge, Uchaguzi dhidi ya vyama pinzani wanakesha nk.
Uokozi wanataka break!!
 
Samahani kwa kusema hivi ila ninadhani kwa namna fulani waokozi walikua sahihi kusitisha zoezi kwenye mazingira yafuatayo:-

Kama teknolojia na njia zetu za uokozi si fanisi kwa wakati wa usiku, hivyo kuendelea na uokozi inakua si salama kwanza kwa waokoaji wenyewe na pia mafanikio yake ni madogo mno, ni afadhali kusitisha zoezi hadi kutakapokucha.

Hakuna anayenufaika na vifo vya ndugu zetu, sitaki kuamini kwamba zoezi lilisitisishwa "JUST FOR LEISURE", kwa sasa bado hatuna uwezo mkubwa sana wa kufanya uokozi wakati wa usiku, na isingekua habari njema leo hii kusikia kwamba tumefanikiwa kuokoa wawili na tumepoteza waokozi nane.

Mwenyezi Mungu atupe nguvu na roho ya ustahimilivu watanzania katika kipindi hiki kigumu. Amen
Tuna helkopta zinaruka juu kulinda wateule,nchi jirani zina vifaa kedekede mf. Kenya. In a matter of hour or two, watakuwa wamefika site!! Kipindi cha Mkapa na MV Bukoba, kuna kikosi kilitoka Zenj na SA walifanya kazi day& night. Nashauri, pamoja na juhudi zote, tusitangulize visingizio vya giza!! Tuongeze juhudi na tuimarishe mahusiano mema na majirani zetu ili tunakotindikiwa tupate msaada. Mungu weka mkono wako katika hili.
 
Akili za viongozi wa awamu hii ni Mungu tu ndiye anayezijua, hivi utasitishaje kuokoa mtu anayetapatapa kujiokoa kwenye maji, mtu ambaye ukichelewa hata kwa dakika moja tu anazama, halafu useme subiri nitakuja kesho asubuhi, inaingia akilini kweli?

Ningekuwa mimi Magufuli wote waliohusika na kusitisha kazi ya kuokoa leo wasingeingia ofisini.

RIP waliotangulia mbele ya haki, ugua pole majeruhi.

View attachment 872858
Hapo wanebugi
 
Huyu RC angekuwepo mama yake miongoni mwa abiria sizan kama wangesitisha zoezi,,,,,,,na bado kile cha kigambon maana geti linafunguliwa watu wanaenda tu wote hakuna idad maalum
 
Hivi kwamfano malaika mkuu Gabriel Makufuli angekuwepo ndani ya hiyo meli sipati picha wale vikaragosi wake venye wangehangaika kumuokoa.
 
20180921_070315.jpg
 

Attachments

  • 20180921_070315.jpg
    20180921_070315.jpg
    135 KB · Views: 26
1. Inasemekana kivuko kimefanyiwa ukarabati miezi kama miwili iliyopita kwa kuwekewa injini mpya za thamani ya milioni 190 ( kama sijakosea).
2.Tahadhari nadhani ambayo haijazingatiwa itakuwa ni uwezo halisi wa kivuko kubeba mzigo na mzigo halisi uliobebwa. Hata hivyo kuhusu uwezo wa kivuko unaweza kutupa elimu maana kwa jinsi ulivyokokotoa uwezo wa vivuko unaweza kutusaidia kivuko hiki kilikuwa na uwezo kiasi gani. Kwani kwenye pointi hii ulikazia kabisa kuwa " haiwezekani"!
3.Pia kitendo cha kutojua idadi kamili ya abiri haikubariki wakati siku hizi naona wanatoza nauli na kutoa tiketi za electronic. Lazima kumbukumbu ziwepo vinginevyo kuna udanganyifu mkubwa unafanyika.
4.Kuna uwezekano wa kuwa labda ni majanga ya asili, kwani kipindi hiki kumekuwa na upepo wenye kasi kubwa na wa kushtukiza. Hata hivyo(kama ajali hii imetokana na upepo) hii inaonyesha yawezekana hakuna ushirikiano wa kutosha kati Mamlaka ya hali ya hewa na wamiliki wa vivuko(TEMESA) ama wamiliki na makapteni wanapuuzia taarifa wanazopewa na wataalamu wa hali ya hewa.
6. Nimakosa kuingiza masuala ya kisiasa tena ambayo hayana ushahidi kwenye masuala ya majanga kama haya. Vinginevyo, ieleweke kuwa unakusudia kuhujumu utawala sa serikali ya sasa kwa kuigombanisha na wananchi kwa malengo " maalumu". Kama huna lengo hilo jitahidi kukwepa kutumia maneno yanayoweza kuashiria hilo.
===
Inauma sana taifa kupoteza watu wake kwa namna hii.
Tatizo zinajaza sana mkuu... Kuna siku nilipanda Mv Victoria kutoka Mwanza kwenda Bukoba...Ile meli ilikuwa imejaza hatari hata sehemu ya kukaa hamna.....
 
Labda wangebaki ili kufurahisha watu kuwa bado wanaendelea na zoezi la uokoaji. Hivi kivuko kilichozama chote toka asubuhi ndani ya maji, kuna mategemeo ya kumtoa mtu akiwa bado anapumua baada ya masaa takriban kumi?
Uokoaji ni fani pia, siasa ziwekwe kando. Na baada ya masaa kadhaa kupita, halikuwa zoezi la uokoaji tena. Maiti haiokolewi.
Kwa hiyo mtu akifa basi hana thamani? Yaani sijakuelewa kabisaaa!
 
Kuna kipindi wajukuu zetu watatamani kufukua makaburi yetu wapime hivi vichwa vya karne hii vinawaza nini...
 
Kwa hiyo mtu akifa basi hana thamani? Yaani sijakuelewa kabisaaa!
Sijamaanisha hivyo. Ila ktk zoezi lolote la uokoaji, maisha ya muokoaji ndio kipaumbele cha kwanza. Namaanisha mazingira ya shughuli hiyo ya uokoaji. Ilifika wakati kilichokuwa kinatolewa ni miili tu na sio watu walio na pumzi. Hivyo kama itafika muda zoezi likawa gumu kulisitisha ni wazo zuri. Halihusiani na wewe unavyosema uthamani wa mwili. Thamani iko pale pale. Hapa ishu ni zoezi la utoaji wa miili na sio uokoaji tena. Kuokoa binadamu maana yake baada ya kuokolewa basi bado ana pumzi. Mtu asiye na pumzi haokolewi. Unaokoa maisha.

Kuna kitu kwenye hii shughuli kinaitwa;
RESCUE vs RECOVERY.

In rescue, the team puts all efforts in hope that there is still life left AND in recovery, the team concludes that there is no life so even the mode of 'rescuing' is different.
 
Back
Top Bottom