Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Nimesoma kwa kina andiko lako Pascal Mayalla, naamini mtu yeyote aliyesoma shule na hiyo elimu ikamstaarabisha hawezi kukubaliana na hoja yako kwamba eti watu hawawajibiki kwa makosa ambayo ama ni moja kwa moja wamehusika au ni kwa migongo ya wsnawaongoza, Tumeshuhudia, akina Tibaijuka. Muhongo, Kitwanga. Nape, Nchemba, Je hao walipowajibika ilikuwa enzi ya Baba wa Taifa hili? Hasira yako hakika inatokana na ndugu yako kuwajibika ? Au inatokana na chuki yako binafsi? Binafsi nakufahamu sana pengine kuliko hata unavyojifahamu wewe. Kila Mara mandiko yako huwa ni ant system, lakini unasahau kuwa Taifa hili limekusomesha , linakupa fursa ya kujivinjari mitandaoni kwa gharama nafuu kabisa, kuwa na shukrani kwa Serikali yako. Siyo kila siku kuibeza.


Tibaijuka. Muhongo, Kitwanga. Nape, Nchemba,... Hawa waliwajibika ???
 
Wakijiuzulu watoto wao utawalipia karo na kuwapa chakula?

Mkuu Tanzania Uongozi ni biashara kama biashara nyinginezo. Uwajibikaji ni sifuri. Ndo maana wakiteuliwa wanafanya sherehe na kuiba. Hakuna kitu kama kuhudumia wananchi.

The sad part of it, hao hao viongozi kesho watakuja kuomba kura kwa kutumia hicho kivuko kama mtaji. NA wananchi walivyo na akili nyingi watawachagua kwa kishindo!

Africa bado tuna safari ndefu sana!
Masanja. uko sahihi kabisa."Uongozi NI BIASHARA". Na siku ya kura watakitumia chombo hicho hicho.
Too sad!/Huizuni kubwa.
 
Pengne walipokuwa wamekaa uzito ulibalance,kutoka kwao kukasababisha uzito uzidi upande m1.
Yaani mkuu kwenye geti la kutokea ndio pazidiwe uzito wakati ndio sehemu kubwa ya kukaa,, na sio kwamba ni wote walikuja hapo kwa wakati mmoja, kwani kulikuwa na magari, ingekuwa imepigwa na dhoruba tungesema labda uzito umehamia upande mmoja ghafla!!! Lakini kwa watu kutembea tu!! Vyombo vingi vya majini vinakuwa na matatizo ya imbalance kwenye maji!! Ambacho ni kitu muhimu sana kwenye chombo kinachoelea
 
Rais Magufuli ameagiza kuwa kufuatia ajali ya MV Nyerere Bendera ya Taifa itapepea nusu mlingoti kwa siku tatu kuanzia kesho Septemba 22, 2018-Katibu Mkuu Kiongozi.

Katibu Mkuu Kiongozi,Dodoma
 
Yaani mkuu kwenye geti la kutokea ndio pazidiwe uzito wakati ndio sehemu kubwa ya kukaa,, na sio kwamba ni wote walikuja hapo kwa wakati mmoja, kwani kulikuwa na magari, ingekuwa imepigwa na dhoruba tungesema labda uzito umehamia upande mmoja ghafla!!! Lakini kwa watu kutembea tu!! Vyombo vingi vya majini vinakuwa na matatizo ya imbalance kwenye maji!! Ambacho ni kitu muhimu sana kwenye chombo kinachoelea
Nimekuelewa mkuu..dah nothing to say
 
Mbona bendera hazipepei nusu mlingoti.Kuna nini kinaendelea Tanzania.
Kabisa kabisa. Hi;li n ijanga la la kitaifa na halijitaji SNAILPACE/MWENDO wa KONOKONO katika kuhuzunika na WAFIWA!
 
Ndugu wanabodi:
Hivi sisi Watanzania nano katuloga? TBC na vyombo binafsi vimeshindwa kujiunga mubashara kwenye shughuli ya uopoaji maiti lakini hats kupiga nyimbo za maombolezo imeshindikana kweli?

Nimesema shughuli ya uopoaji kwa sababu serikali ingekuwa serious na maisha ya Watanzania wenzetu ingepeleka jenereta jana ili shughuli ya uokoaji iendelee Jana usiku.

Watanzania zaidi ya 126 ni msiba mkubwa wa taifa lakini radio na luninga ya taifa wameshindwa kujiunga mubashara hatua kwa hatua badala yake wanaendelea na mambo yao yasio na maslahi kwa Taifa.

Naamin kwa Wazungu habari ingekuwa ndio hiyo kuwa mubashara muda wote kwa kila kituo cha luninga na redio.Na wasingekubali kusitisha shughuli ya uokoaji eti kisa giza

Tumeshindwa kuthamini uhai wa wenzetu, kweli ngozi nyeusi ni wabinafsi haijapata kutokea
 
Ila ccm mmechemsha Sana kwenye ajali ya mv Nyerere....mabilioni ya kuwanunua madiwani na wabunge mnayo ila hata vibatari vya kuokolea wahanga kwenye ajali hiyo hamna....[emoji41]
 
Tuko pamoja nao ndg Wa marehemu pia tunatoa pole kwa wafiwa wote
Nalog off
 
Mkuu wa mkoa na timu yake wanaamua kwenda kulala ili waje kesho yake asubuhi kuendelea na uokoaji...
Tena wanautangazia Umma wa Watanzania kwamba "tunakwenda zetu kulala na tukutane kesho". Kuna familia zaidi ya 350 zitakuwa hazikupata usingizi hiyo jana
 
Back
Top Bottom