Elections 2015 UKAWA kusimamisha mgombea Urais 2015

Wana jamvi acheni papara someni vizuri post;nimegundua humu ndani vijana wa lumumba huaga wanapasukwa mbaya dr slaa,ktk post yangu prof lipumba mgombea wa muungano
 

Nashukuru ww kwa kutoa mapendekezo ya nani awe nani kutoka ukawa kwenye kugombea,,,,MIMI nakutajia jina la RAIS WA JMT MWAKA 2015 ni MH STEPHEN MASATO WASSIRA,uwezo wake ni mkubwa na anaijua vema historia ya nchi.
 

kwa sababu nchi yetu inamatatizo mengi ya kiuchumi, tumpe Lipumba kwa sababu yeye ni mchumi aliyebobea. Slaa awe waziri mkuu kwa sababu yeye ni msimamizi zaidi! Zitto msaliti hatoiva na Mbowe na Slaa asiwepo! riziki Magembe
 
Last edited by a moderator:
Vigezo kwanza mkuu then uhitaji halafu ndio tujue nani anafaa wapi
 
hii nchi inaitaji rais katili....asie na washkaji...nchi yetu inaendeshwa kirafiki rafiki, mtu una mjuwa nani ndio upate kitu....
 
hapo hapo pa nani awe nani ndiyo vurugu itaanzia. Kwani hata maoni yako ni chanzo cha vurugu. wengi uliyowataja ni cdm Hivyo ratio itaanzisha vurugu. Rais na makamu wote wanatoka bara nayo ni vurugu. Zito hana mahusiano mazuri na wakubwa akiitwa msaliti nayo ni vurugu. Lipunba ana elimu zaidi ya Slaa nayo ni vurugu. na mengine kadha wa kadha.
 
Akihutubia maelfu ya wakazi wa jiji la arusha mapema jana katika mkutano wa [ukawa]katibu mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo,chadema,dr wilbod slaa, alisema,tumefikia makubaliano kama [ukawa] 2015 kumsimamisha mgombea 1 katika nafasi ya urais,lengo letu sio kutafuta vyeo bali kuwakomboa wananchi watanzania waliopigika na mfumo wa chama cha mapinduzi,nilifarijika sana niliposikia maneno haya kutoka kinywani mwake,maana ndio mwisho wa chama cha mapinduzi umewadia,kimsingi ni kujipanga bara bara kusuka kikosi kazi kitakacho fanya kazi ya ziada kuhakikisha ccm haifurukuti kabisa,bg up [ukawa] pa1tutashinda,
 
Pigeni mahesabu ya kula zote za vyama vya ukawa 2010 kisha mlinganishe na za ccm mtapata majibu, msione watu wanajaa ktk mikutano, muulizeni Mrema walikuwa wanalisukuma gari lake for long distance.
Nawaahidi mtagawana mbao baada ya uchaguzi.
 
No, ni mapema mno kuanza kutangaza hivyo hadharani. Hata kama wana mipango hiyo, lingebaki kuwa suala la ndani hadi hapo muda muafaka utakapofika. Akumbuke kwenye msafara wa mamba na kenge wamo! Ikitokea hilo halikufanikiwa itakuwaje? Ataonekana hakuwa makini; gharama nyingine kubwa kisiasa bila sababu za msingi ambayo ingeweza kuepukwa kama angechunga kauli tangu mwanzo.
 
pigeni mahesabu ya kula zote za vyama vya ukawa 2010 kisha mlinganishe na za ccm mtapata majibu, msione watu wanajaa ktk mikutano, muulizeni mrema walikuwa wanalisukuma gari lake for long distance.
Nawaahidi mtagawana mbao baada ya uchaguzi.

kura za jk 2005 na 2010 zinalingana alafu jibu ujijibu mwenyewe.
 

kwa upande mwingine nakubaliana na wewe,lakini watanzania wanahitaji kuandaliwa mapema waelimishwe na kuhelewa, watanzania wengi ni wazito katika maamuzi na hilo [ukawa] wameliona ndio maana wana waandaa mapema,
 
UKAWA wasimamishe mgombea ubunge mmoja kwa kila jimbo kutegemea na kukubalika kwa chama jimboni hapo. Kama ni Arusha basi UKAWA wasimamishe mgombea wa chadema, na kama ni Lindi UKAWA wasimamishe mgombea wa CUF.

Kwa kufanya hivyo viti vingi vya ubunge vitachukuliwa na UKAWA na kuinyima CCM nafasi ya kuwa na viti vingi bungeni.
 
kura za jk 2005 na 2010 zinalingana alafu jibu ujijibu mwenyewe.

Jipeni moyo, wenzeni wanajipanga na uchaguzi mkuu mwakani ukawa wanazunguruka mikoani kupandikiza chuki na uchochezi wa katiba, wakija kushtuka hawana chao, wanaanza kulia tena tumeibiwaaaaaaa!
Hata siku moja hakiri ndogo haiwezi kuitawala. Hakiri kubwa.
 

mkuu bado uko kwenye mawazo ya ubunge? Wenzako wanafikiria mbali zaidi.
 

chuki zipi? Ikiwa chama cha mapinduzi,haki heshim maoni ya wananchi? Ni kuulize swali. Unamfanya kazi wako umemwandika kazi alafu yeye anakwenda kinyume na matakwa yako je atakua mepoteza sifa au ajapoteza sifa? Jibu jaza hapa [ ] alafu kipime chama chako kupingana na maoni ya bosi wake yaani wananchi.
 
Kushindwa kwa ruling party ni pale tu watakapo mchagua candidate wa uraisi ambae ni unpopural,lakini kama watamteua mgombea popural ni matumaini yangu mgombea wa Ukawa hatoweza ku-compete na wa CCM Japo ataleta challenge kiasi fulani.Na ikumbukwe kwamba si kila no kubwa ya watu wanaojitokeza kusikiliza mikutano yao wanawaunga mkono si kweli, ingawa naamini majority wanawaunga mkono na hii ni hata kwa CCM wanapofanya mikutano yao.
 
Na ndo hapo tutakapoona siasa iliyoenda shule 50 kwa 50 bungeni itakuwa poa sana ikiwa hivyo..!!
 

Du hapo ndiyo ukawa utakapo vunjika, unadhani CUF au NCCR-Mageuzi watakubari wagombee majimbo machache? Thubutuuu! Au jimbo la lisu agombee CUF yeye na dada yake viti maalumu wakose unga watakubari?
Waambieni wapime maji kabla ya kuvuka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…