Mkandara;10113797]Mkuu wangu wakati mwingine unauliza maswali ya ajabu kabisa. Unaposema Tanganyika inanufaika nini na huu Muungano una maana gani? Hivi nikuulize wewe hilo deni la taifa ni kiasi gani?
Swali hilo ni la 'ajabu' kwasababu linakukera kwa kutambua jibu lake si zuri kwa wazanzibar unaowatetea. Chanzo cha swali hilo kinatokana na wazanzibar wanaosema 'Muungano huu hauwasadii, wananyonywa na kuonewa''Swali Tananyika inafaidika na nini.
Hapa unafahamu wazi kuwa Tanganyika hainufuaiki na lololte katika muungano. Zama za muungano wa kisiasa zimekwisha, sasa ni zama za muugano wa kiuchumi.
Katika uchumi znz haina fao la aina yoyote kwa Tanganyika.Hivyo muungano huu ni kuwasaidia wazanzibar kwasababu Watanganyika hawanufaiki. Hakuna la maana zaidi ya kupoteza, kubeba zigo lisilo na square likisumbua mgongoni.
au wewe utajibu vipi mtu akikuuliza unafaidika vipi na ndoa yako? Ni kipi kilichopo ktk ndoa yako ambacho huwezi kukipata pasipo ndoa hiyo? pengine wewe mwenzangu una akili sana tujuze nadhani ndio swali lako kwenye Utanganyika au sivyo?.
Kuna faida za kujenga familia na kizazi. Faida za kiuchumi na kijamii.
Lakini katika ndoa hiyo kama mke atasema hana faida nayo, nitampa talaka. Nami nikigundua hakuna faida ya ndoa zaidi ya migogoro jibu ni talaka.Matatizo ndani ya ndoa yanazungumzika, mke anapokuwa barabarani akidai mume mwizi,huyo si mke ni mjinga au mwendawazimu, mwache, Mpe talaka haraka akafungue genge lake la nyanya.
Swala sio Tanganyika inanufaika vipi bali ni ukweli kwamba mikopo tunachukua, hivyo kama tunaenda kulewea, tunaibiana kujenga miradi binafsi au kuhamishia ktk mabenki ya nje haya sii maswala ya kujadili hapa. Kinachojadiliwa hapa ni mikopo inachukuliwa na bara kwa jina la Muungano na kwa minajiri ya miradi isokuwa na Muungano - Kaput!.
Swadakta, ndiyo maana tunasema iwepo Tanganyika,Magufuli ajenge barabara za Tanganyika na Mansour ajenge za znz.
Huwezi kusema Tanganyika inanufaika na misaada na mikopo wakati wazanzibar wanalala hawajui gharama za ulinzi na usalama ambazo hawawezi kulipia hata 2%. Hilo jina Tanzania unalosema linaiba linalipiwa na wenyewe.
Zanzibar kwa maneno ya Salimin Awad wa CCM amesema hawalipi.
Ni hivi, Magufuli hana uwezo wa kufanya kazi znz kwasababu kuna magufuli wa znz.
Hebu nieleze kama ni misaada na mikopo (hoja ya kipuuzi sana) kwa wasomi, maana msomi anapofikiria misaada na mikopo inasikitisha, unaingalia vipi.Kiasi gani znz inapata kupitia jina la Tanzania.
Nikupe namba kidogo, znz inapata 4.5 ya pato la Tanzania. Ukichukua pato hilo kama Trilioni 12 ambapo znz haina mchango, kwa mwaka mmoja inapata 540 bilioni.
Kwa minajili tu ya mjadala tuseme ni bilioni 400. Mapato ya znz 2014 ni bilioni 400 na bajeti ni bilioni 710.
Tofauti ya bajeti na mapato inapatikana kwa hizo 4.5. Kamuulize Salimini Awad wa Baraza la wawakilishi.
Kamuulize Omar mzee, na Shein.
In other words, kile cha Mtanganyika bila mikopo na misaada kinagawanywa kwa wazanzibar.
Arguably wanasema ni pesa za benki kuu. Leo wakilipwa kiasi chote hawawezi ku generate kiasi kikubwa zaidi ya hicho. Yaani mapato yanayotoka Tanganyika ni makubwa kuliko wanayofanyia kazi.
Kumbuka naongelea 12 Trilioni bila misaada au mikopo.
Watanganyika tunasema, no ! tunataka kila mtu aende Washington kwa Bretton Institutions akakope kwa jina lake alipe kwa jina lake, atumie kwa jina lake na mafisadi waibe katika nchi yake.
Wazanzibar wanaoona fahari kukopa (aibu kubwa sana kwa wasomi kuzungumzia) waende Paris Club na Bretton na Oman na kwingine wakakope na kupewa misaada yao bila kuingiliwa.
Inawezekana kama tutatenga shughuli kwa serikali ya Tanganyika na Zanzibar.
Hakuna tatizo na mafisadi kwasababu ni watu na mfumo unaweza kuwakomesha siku moja akipatikana kiongozi mweledi.
Ni tatizo na mfumo wa wizi unaofanywa kwa jina la muungano. Kasehemu kadogo kasiko na mchango kanachukua pande kubwa bila sababu, hilo Watanganyika hatukubali sasa.
Halmashauri 54 za Tanganyika kwa mwaka 2014 zimetengewa bilioni 540.
Hizi zinawakilisha sehemu kubwa ya uchumi, population na size mara zaidi ya 400 ya znz.
Kituko ni kuwa Zanz yenye watu wachache kuliko halmashuri yoyote kati ya hizo 54 inapewa zaidi ya bilioni 500 kwa pesa za moja kwa moja na gharama zinzaotokana.
Mfano, wabunge 81 wa znz wanaokuja Dodoma wanalipiwa bilioni 9.6 sawa na halamashrui moja ya Tanganyika kwa mwaka.
Leo mnasema misaada, huo si msaada ni kitu gani. Leo tunajeshi linagharimu trilioni 1.2, mambo ya ndani bilioni 900 na mambo ya nje bilioni zaidi ya 400 kwa ujumla wa trilioni 3. Kati ya hizo znz inachangia sifuri, I mean zero.
Leo mnasema hawapati msaada! msaada gani zaidi ya huo.
Watanganyika tunataka tuone znz ikikopa huko nje na kupewa misaada yake bila kuwaingilia.
Lakini pia yunataka tuone wanachangia nini katika huu uungano. Hata kama ni milioni moja lazima wachangie ili waone uchungu na umuhimu wake.Hatuwezi kuendelea kulea kelele tu, tunasema ruksa nendeni Paris na Washington
Serikali 3 ndilo jibu tu
Mimi na wewe tunajua fika kwamba ni asimia 10 hadi 20 tu ndio hutumika kama gharama halali ya ujenzi wa miradi hiyo ya kitapeli, wakati asilimia 80 inawekwa kibondoni mwa viongozi wetu wakishirikiana na Makabaila. Hili sio swali la kuniuliza mimi mkuu wangu hata kidogo. Ni hawa wameifanya mikataba hii kuwa ya siri ili wapate kuendelea kutuibiwa wananchi bora wenzetu Wazanzibar wameshtuka kuliko sisi tusioona mbali zaidi ya marefu ya kero zetu..
Ndio maana tunataka tuwaondoe katika mtego wa ufisadi, waende kukopa na kupata misaada yao. Tunataka Tanganyika ili tuhangaike na matatizo yetu bila kuwapa wazanzibar.
Afadhali wameshtuka, watuunge mkono kila mtu na serikali yake.Kwanini tuwape taabu. Serikali 3 zinawasaidia wao si sisi.
Sasa haya sii ya kuniuliza mimi ati Tanganyika inafaidika nini na Muungano wakati tunaibiwa na viongozi ambao hawana msalie, aidha uwape serikali 2 au 3 pasipo kubadilisha mfumo huu mbaya wa Kiutawala ambao mikataba ya uwekezaji nchini ni siri ya serikali tawala. Siri ya nani ktk uwekezaji nchini uliona wapi kama sio jeuri ya kuwaibia wananchi na hasa kuficha machafu yao.
Sawa , tunachosema mafisadi ni sawa na vibaka. Wanaiba tu.
Tunataka znz wasiibiwe na njia rahisi ni wao kuwa na mamlaka kamili ya kuendesha mambo yao. W
aende Oman na Washington kukopa, wakusanye kodi zao na kwavile hawana mafisadi watumie katika miradi yao.
Walipie ulinzi na usalama, mambo ya ndani na kila gharama zao. Hawana sababu ya kujifunga na Tanganyika yenye maifsadi. Maifsadi watuachie tuhangaike nao.
Njia nyepesi ni serikali 3. Wakikataa serikali 3 nao ni wezi wakubwa tu kama maifasadi.
Na naweza kukujibu kihuni vile vile kwa kusema wewe huoni maendeleo ya Tanganyika? Tanganyika ile ya Nyerere sawa na hii ya leo?. Fedha zinazokopwa nje leo zinajenga mabarabara, madaraja ambayo JK kapewa sifa kubwa lakini deni lote ni la Taifa. Mkapa alijenga daraja kubwa na uwanja wa mpira wa Kimataifa. Au unataka nikwambie ya kwamba Tanganyika ilifaidika na Muungano kutokana na Hayati Karume ndiye alojenga jengo la Yanga pale jangwani na pia kuchangia kwa asilimia kubwa Klabu ya Simba?.
Hapa swali linabaki tunafaidika nini kwa kuwa na znz katika uchumi wetu.
Kama Watanganyika, hatuna faida ya aina yoyote, narudia hata leo muungano ukivunjika hakuna Mtanganyika atakayejiuliza kwanini. Huko Manyoni kuna watu hawajui znz ni nini.
Ali Swalehe anasema hivi, amezunguka mikoani na kugundua kuwa Tanganyika ina WAPUMBAVU waisojua muungano.
Ni kweli anachosema ingawa lugha yake ni mbovu, nani anashughulishwa na znz kule Manyara.
Inamhusu nini maana Manyara haitegemei znz kwa jambo lolote. Inamhusu nini mtu wa Dar es Salaam au Tanga.
Elimu ya kwa Watanganyika imefanikiwa sasa wanadai nchi yao na hakuna wa kuwazuia.
Zanzibar kila la heri kama mnataka muungano ni kwa kuwajibika, adabu na heshima!ala.
Mlipiwe bill halafu mlete mdomo.
Kinyume chake njia nyeupee, vunja jahazi tugawane mbao maana sisi hatuwahitaji.
Mkuu acha hizo leo tuna mipango ya Ujenzi wa bandari na airport mpya Bagamoyo, daraja la Kigamboni, madaraja ktk kila kivuko cha mito, Meli za Kigoma, Lake Nyasa na Victoria kote huko ni miradi ya serikali kuu sio ya watu binafsi kama ilivyo Zanzibar na hii yote ni mikopo ya Kimataifa ambayo Pasipo Muungano pengine tusingeifanya maana kama Zanzibar watakuwa na International Airport na bandari ya Free Port hakuna haja wala sababu ya Ujenzi wa miradi hiyo mipya
Kwamba tusijenge bandari zetu tusubiri wazanzibar. Ney.
Tunajenga ya mwambani, tunajenga ya Bagamoyo tunapanua ya Dar. Airport ya Kilimanjaro ni kwa Watanganyika na tutajenga nyingine nyingi tu. Watalii watakuja Kilimanjaro, wakibaikisha pesa wataenda znz.
Soko la Afrika mashariki tuna access nalo, tunajenga bandari. Hiyo bandari huru ya znz ni kwa ajili yao.
Sisi ndio soko la znz na tunaelekea kuchukua umiliki wa soko letu kwajili ya watu wetu siyo wa nchi jirani ya zanzibar.
Huu upuuzi wa kusubiri znz wajenge kwasababu ni wazuri sana hatuukubali.
Wao hawana mchango wanataka miradi ya nini. Waende Oma na Washington wakakope, wajenge International airport yao, wajenge bandari huru yao na kila kitu chao , hatuna taabu.
Hiyo isiwe sababu ya kwanyima wakaazi wa Tanga fursa za uwepo wa bandari yao, wakaazi wa Kilimanjaro au Mpanda kufanya maendeleo yao.
Wao hawataki utanzania na wameukana, sasa huruma ya nini.
Wao ni wznz bwana tunawaacha kama walivyo.
Sisi Watanganyika tutaendelea kama Watanganyika. Hawataki Utanzania kwanini unawalaizimisha mkuu. Let them go!
Zamani walikuwa anatisha tisha kuvunja muungano. Ule upambavu wa Watanganyika aliosema Ali Salehe umeondoka, Watanganyika wameshaelewa hawahitaji znz kwa lolote lile. Leo niambie, umesikia mznz gani akinyanyua pua na kusema tunavunja muungano. Tanganayika tunasema kama wazn wanataka kuvunja muungano wasije Dodoma, sisi tutaendelea na bunge la katiba kuandika katiba ya Tanganyika. Hatuwahitaji, hawana msaada wala hatuna sababu za maana za kuwa nao zaidi ya kwausaidia. Hatuwahaitaji the least to say