Ukiacha Dar es Salaam, mikoa iliyobaki ujanja wao ni mchana tu, ikifika saa tatu usiku kila mtu yupo kwake

mdukuzi

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2014
Posts
20,925
Reaction score
51,688
Mikoani mmepoa sana,kuna mikoa ikifika saa tatu huwezi kuona mtu nje,still wanaamka saa moja, mnakuwa mbafanya nini ndani muda wote.

Saa sita za usiku DSM kuna watu ndio wanajiandaa watoke
Saa saba usiku wauza chipsi bado wanamenya viazi.

Juzi kuna mtuhumiwa kampiga na kitako cha bastola mwenzake saa 12 asubuhi wakiwa kwenye club ya usiku.

Kuna mikoa sungusungu wanaanza doria saa tatu,ukizubaa unakamatwa na kuulizwa eti unatoka wapi usiku huu ,saa tatu ni usiku??

Mnalala sana mikoani
 
Juzi kati nilikesha pale buguruni chama, yaani mpaka asubuhi hauoni tofauti yoyote zaidi ya kwamba usiku wanazidi makahaba na wawinda makahaba.
Lakini pilika pilika zingine zote ziko sawa na mchana
 
Sema moderator kaedit cha habari kilikuwa kinasema "ntu" Sasa mtu unauza chips maana yake hela mnaisaka kwa tochi sisi huku samoja tushafunga hesabu😂trilion moja kwa siku
 
Napenda maisha ya mkoani yalivyo na utulivu bila usumbufu usiokuwa na sababu.. Good life

Sasa dar kamji kieneo kadogo Ila watu wanafukuzia milioni sita. Kwa nini kusiwe na mahangaiko
 
Napenda maisha ya mkoani yalivyo na utulivu bila usumbufu usiokuwa na sababu.. Good life

Sasa dar kamji kieneo kadogo Ila watu wanafukuzia milioni sita. Kwa nini kusiwe na mahangaiko
Mkoani watu hawachakariki sana ndio maana matajiri wachache wanajulikana mkoa mzima na masikini ni wengi sana.
 
Mimi ndio nataka kutoka hapa niingie kitaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…