Nimekusoma vizuri mtaalam wanguKwanini?
Sehemu zinazopimwa kwa futi hata siyo pa maana.
Eneo la mita 20 kwa mita 20 mnajikuta mpo watu wawili.
Kiwanja kimoja kinapimwa futi 50 kwa 40 maana yake ni mita 12 kwa 17 chenye mita za mraba 204 wakati cha mita 20 kwa mita 20 kina ukubwa mita za mraba 400.
Hali kama hiyo ipo eneo lote la Wilaya ya Temeke (Mbagala ikiwemo), Homboza, Mkuranga-Vikindu, Kisemvule, na mikoa ya Kusini.
Kinachokuja hapo ni uswazi na vijumba vichafu.
Waswahili hawana utamaduni wa kujenga vyoo bora kwa hiyo hata ukijenga chako kizuri bado mtaa utakuwa mchafu na wewe utakuwa mchafu tu.
Priority ni KibahaNiFirstaje waungwana,
Kama swali linavojieleza hapo juu, ukiambiwa uchague sehemu moja tu ya kujenga kwa ajili ya makazi kati ya Chanika, Kibaha, Vikindu na Bagamoyo ila kiwanja unapewa bure.
Ndugu muungwana hebu tuambie utachagua kujenga na kuishi wapi? Na kwanini?
Niaje waungwana,
Kama swali linavojieleza hapo juu, ukiambiwa uchague sehemu moja tu ya kujenga kwa ajili ya makazi kati ya Chanika, Kibaha, Vikindu na Bagamoyo ila kiwanja unapewa bure.
Ndugu muungwana hebu tuambie utachagua kujenga na kuishi wapi? Na kwanini
Kwanini mkuu kwani hujui Kwa Sasa CHANIKA ni chaguo namba 1 Kwa wajenzi kwine huko mbwembwe tuUmeandika ukiwa serious mkuu au unapima upepo kwanza?
Inamaana wewe Kibaha imekukalia kushoto mkuu, au unamaanisha huko kuna hadhi kubwa hivyo sikutakiwa kupataja katika list hii?Nafikiri ulitakiwa kutaja Bagamoyo, Chalinze, Kisarawe na Mkuranga kwa sababu kwa sasa miji inakuwa kuelekea huko japo ukuwaji ndio unatofautiana, binafsi siyo tu kupewa bure bali hata ungeniambia nitoe hela kununua kiwanja kati ya hizo wilaya nilizokutajia, bila kupepesa macho ningechagua Bagamoyo hata kama cha Huko ndio kingekuwa na bei kubwa kuliko hizo sehemu nyingine
Ok mkuu, hapa naona kila muwamba ngoma anavutia upande wake. Kuna mmoja amesema Vikindu ndo mpango mzima, kwengine kote michosho tu πππKwanini mkuu kwani hujui Kwa Sasa CHANIKA ni chaguo namba 1 Kwa wajenzi kwine huko mbwembwe tu
Chani babu kuko njema ktk nyanja zote miundo mbinu huduma za kijamii kama usafili hospital mahakama vituo vya police NK nkOk mkuu, hapa naona kila muwamba ngoma anavutia upande wake. Kuna mmoja amesema Vikindu ndo mpango mzima, kwengine kote michosho tu πππ
Mkuu nashukur sana tena sana kwa ushauri wako wenye kuelimisha na kutia moyo.Kama ulivyosema kuwa kila mwamba ngoma ngozi huvilutia kwake. Wengi wapendekaeza tu eneo bia kutoa sababu za msingi.
Ila mkuu kuchagua mahali au eneo kunatokana na hitaji au lengo kuu. Mimi naamini katika michango ya watu hapa nadhani kuna iliyogusa lengo lako.
Yuko mmoja ambaye nadhani amechanganua kila maeneo bila upendeleo akielezea uzuri na ubaya wa kila eneo. Huyu amemaliza kila kitu. Kazi kwako.
Sasa katika malengo yako angalia wapi panafaa kutokana na ufafanuzi alioeleza.
Kila la heri. Ila karibu Vikindu, hutajuta.