Ukiambiwa kuna viwanja vya bure uchague tu sehemu ya kujenga na kuishi kati ya Vikindu, Kibaha, Chanika na Bagamoyo, utachagua kujenga wapi?

Ukiambiwa kuna viwanja vya bure uchague tu sehemu ya kujenga na kuishi kati ya Vikindu, Kibaha, Chanika na Bagamoyo, utachagua kujenga wapi?

Nitachagua kibaha sababu ni mji unakua kuna nafasi naweza kufanya maendeleo mengine kama kufuga ni rahisi kupata masoko upande wa kibamba na chalinze maana kibaha ipo hapo kati.
Vikindu nafasi ipo ila ukuaji wake sio kama kibaha, chanika mmh huko pashakua uswazi na bagamoyo bado hapajaendelea kivilee.
 
Wengi wanaosapoti Kibaha wanapaangalia pale Maili Moja, Kwa Mfipa, Kwa Mathias hadi Kongowe tena barabarani. Hivi mmewahi kuingia huko ndani ndani kwenye viwanja vinakouzwa? Ni uzaramoni haswaaaaa, ni uswahili sana.

As for Bagamoyo, ule mji mimi hapana. Haujawahi kunivutia.
Labda maeneo kama Zinga huku nyuma kabla hujafika Bagamoyo kwenyewe. Bagamoyo ni mji usioendelea kwa miaka mingi.

Chanika, sehemu nzuri mwisho pale Taliani. Huko mbele sijui Zingiziwa, kwa Mpango sjui wapi huko ni mateso tu. Na uswahilini sana.

Vikindu, ubaya wa Vikindu ina jamii mchanganyiko lakini wamekaa vikundi vikundi. Unaweza kwenda sehemu wamejaa Wapare watupu mtaa mzima viwanja vyote wanamiliki wao. Kuna sehemu unaenda wamejaa Wamakonde watupu, ipo sehemu ina Wandengereko tupu. Hawa wengi ni zao la machinga wa Mbagala na waliouza nyumba za urithi au zao wenyewe Tandika na Mbagala/Magomeni wamekimbilia huko.

Ceteris Paribus, Kibaha is promising. Ile barabara kutoka pale Maili Moja wanataka iwe njia 4 hadi Chalinze so kutakuwa magoli sana. Maroli hayatakuja mjini kwa sababu Kwala wanajenga bandari kavu.

Kumbuka mkoa wa Pwani ndio mkoa pekee Tz usiokuwa na Manispaa.
 
Kwa sehemu iliyochangamka kama Chanika na ilivyokuwa maarufu mpaka leo kuwa na kiwanja cha 1.7 mill huko ni sawa na kutoa bure.

Tungetegemea huko viwanja visipungue 8mill hadi tunavyoongea hapa
Me kuna wadau wako huko kiwanja mpak 20mil vipo mpka 100mil hii ni barabarani

Bei ya kiwanja inategemea. Kiwanja chenyewe kiko katika mazingira gani.
 
Niaje waungwana,

Kama swali linavojieleza hapo juu, ukiambiwa uchague sehemu moja tu ya kujenga kwa ajili ya makazi kati ya Chanika, Kibaha, Vikindu na Bagamoyo ila kiwanja unapewa bure.

Ndugu muungwana hebu tuambie utachagua kujenga na kuishi wapi? Na kwanini?
Nenda Chanika mkuu imekuwa sana na mahitaji sio tatizo
 
Kama mimi binafsi huwa napenda kulinganisha maeneo husika na kuona fursa zilizopo ili kuchagua sehemu sahihi ya kuishi.

Ni muhimu pia kuzingatia mambo kama miundombinu, huduma za umma, elimu, na fursa

Hata hivyo, naweza kukusaidia kwa kukupa taarifa kuhusu maeneo hayo ili uweze kufanya uamuzi wako mwenyewe.

1. Vikindu: Vikindu ni sehemu iliyoko katika Wilaya ya Mkuranga, Mkoa wa Pwani, Tanzania. Inapatikana umbali wa takribani kilomita 45 kutoka Dar es Salaam. Maeneo ya karibu na pwani yanaweza kuwa na vivutio vya kipekee, lakini umbali kutoka Dar es Salaam unaweza kuwa changamoto ikiwa unahitaji kufanya shughuli nyingi jijini.

2. Kibaha: Kibaha ni mji ambao ni makao makuu ya Wilaya ya Kibaha, Mkoa wa Pwani, Tanzania. Ni eneo linalokaribia Dar es Salaam, umbali wa takribani kilomita 35, na inaunganishwa vizuri na barabara kuu na njia ya reli. Kuishi Kibaha kunaweza kukuruhusu kufurahia urahisi wa kufika Dar es Salaam na huduma zake, wakati ukijivunia mazingira ya mji mdogo na utulivu.

3. Chanika: Chanika ni eneo lililopo katika Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam, Tanzania. Ni sehemu ya mijini zaidi ikilinganishwa na maeneo mengine uliyotaja. Kuishi Chanika kunaweza kukupa faida ya kuwa karibu na vituo vya biashara, huduma za umma, na miundombinu ya jiji. Hata hivyo, unaweza kukabiliwa na msongamano wa trafiki na kelele za mji mkubwa.

4. Bagamoyo: Bagamoyo ni mji wa kihistoria ulioko katika Mkoa wa Pwani, takribani kilomita 75 kaskazini mwa Dar es Salaam, Tanzania. Mji huu una historia ndefu ya biashara na utamaduni na inaonekana kama sehemu ya urithi wa dunia na UNESCO.

Kuchagua kujenga na kuishi Bagamoyo kunaweza kuwa chaguo nzuri kwa sababu ya mambo yafuatayo:

Utamaduni na Historia, Mandhari ya Pwani,
Amani na Utulivu, Karibu na Dar es Salaam
Well done mkuu
 
Chanika ni Bora kuanzia Buyuni Taliani Nyeburu Nguvu kazi hadi maeneo ya Kwa ngwale ardhi yake ni tambarare inapitika mda wote hakuna miinuko mikali au mabonde
Unaweza kupata eneo kubwa la kujenga kwa gharama nafuu
Kwa Sasa hakuna sana uswahili maana wahamiaji ni wengi sana
Ni rahisi kufika mjini hasa asubuhi kuanzia 11 hadi 1 nje ya hapo utakutana na foleni ya tazara itakuchelewesha
Ok brother acha ushauri wako niufanyie kazi.
 
Hakuna afadhali hata sehemu moja...

Wanaotaja Kibaha wanaitazama Maili moja tu labda, lakini Kibaha ni kubwa na ndani ndani kuna mambo ya kiduanzi na ushirikina kama ilivyo Bagamoyo na Vikindu, na palipo na ushirikina sahau maendeleo...
Mbona watu wanadai sehemu kubwa ya Kibaha kwa sasa imejengeka, uswahili umepungua maana wale waswahili wenyewe original wengi wameshakufa, na wengine wameuza maeneo yao au viwanja vyao na kuwaachia wageni mji.

Sasa nashangaa wewe unapapinga mkuu!
 
Ni bora pale chanika,baada ya wiki mbili nitakua nishakitia sokoni nirudi kupanga mjini😎
Kwani hata maeneo mengine si unaweza kukitia sokoni tena kwa bei kubwa zaidi ya Chanika au kwako wewe unaona Chanika kunauzika zaidi ya maeneo mengine?
 
Niaje waungwana,

Kama swali linavojieleza hapo juu, ukiambiwa uchague sehemu moja tu ya kujenga kwa ajili ya makazi kati ya Chanika, Kibaha, Vikindu na Bagamoyo ila kiwanja unapewa bure.

Ndugu muungwana hebu tuambie utachagua kujenga na kuishi wapi? Na kwanini?
Bagamoyo
 
Nitachagua kibaha sababu ni mji unakua kuna nafasi naweza kufanya maendeleo mengine kama kufuga ni rahisi kupata masoko upande wa kibamba na chalinze maana kibaha ipo hapo kati.
Vikindu nafasi ipo ila ukuaji wake sio kama kibaha, chanika mmh huko pashakua uswazi na bagamoyo bado hapajaendelea kivilee.
Ok boss, naona Kibaha inazidi kuibuka kidedea katika mjadala wetu, sio kama Chanika na Vikindu yake.
 
Kama mimi binafsi huwa napenda kulinganisha maeneo husika na kuona fursa zilizopo ili kuchagua sehemu sahihi ya kuishi.

Ni muhimu pia kuzingatia mambo kama miundombinu, huduma za umma, elimu, na fursa

Hata hivyo, naweza kukusaidia kwa kukupa taarifa kuhusu maeneo hayo ili uweze kufanya uamuzi wako mwenyewe.

1. Vikindu: Vikindu ni sehemu iliyoko katika Wilaya ya Mkuranga, Mkoa wa Pwani, Tanzania. Inapatikana umbali wa takribani kilomita 45 kutoka Dar es Salaam. Maeneo ya karibu na pwani yanaweza kuwa na vivutio vya kipekee, lakini umbali kutoka Dar es Salaam unaweza kuwa changamoto ikiwa unahitaji kufanya shughuli nyingi jijini.

2. Kibaha: Kibaha ni mji ambao ni makao makuu ya Wilaya ya Kibaha, Mkoa wa Pwani, Tanzania. Ni eneo linalokaribia Dar es Salaam, umbali wa takribani kilomita 35, na inaunganishwa vizuri na barabara kuu na njia ya reli. Kuishi Kibaha kunaweza kukuruhusu kufurahia urahisi wa kufika Dar es Salaam na huduma zake, wakati ukijivunia mazingira ya mji mdogo na utulivu.

3. Chanika: Chanika ni eneo lililopo katika Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam, Tanzania. Ni sehemu ya mijini zaidi ikilinganishwa na maeneo mengine uliyotaja. Kuishi Chanika kunaweza kukupa faida ya kuwa karibu na vituo vya biashara, huduma za umma, na miundombinu ya jiji. Hata hivyo, unaweza kukabiliwa na msongamano wa trafiki na kelele za mji mkubwa.

4. Bagamoyo: Bagamoyo ni mji wa kihistoria ulioko katika Mkoa wa Pwani, takribani kilomita 75 kaskazini mwa Dar es Salaam, Tanzania. Mji huu una historia ndefu ya biashara na utamaduni na inaonekana kama sehemu ya urithi wa dunia na UNESCO.

Kuchagua kujenga na kuishi Bagamoyo kunaweza kuwa chaguo nzuri kwa sababu ya mambo yafuatayo:

Utamaduni na Historia, Mandhari ya Pwani,
Amani na Utulivu, Karibu na Dar es Salaam
We kaka una akili sana nyingi Wacha niku follow
 
Back
Top Bottom