Ukienda ugenini Kuna vitoto vinapenda sana sifa

Ukienda ugenini Kuna vitoto vinapenda sana sifa

Nimekuja mkoani kumtembelea bradha Kuna mzigo aliniagiza nimletee.

Hapa kwa bro kuna mtoto wao wa kiume ana umri kama miaka minne au tano hivi. Asee hiki kitoto Ni kitundu sijapata ona. Mbaya zaidi babaake na mama yake wanamlea Kama yai,full kudeka deka hovyo.

Sasa ni heri wangekuwa wanamlea hovyo akawa anawasumbua wenyewe ingekuwa hakuna shida,ila akiwa na wenzie ni kakorofi kanawapiga wenzie.

Nimejilipua zangu fulana kutoka kwa vunja bei,ameshaitanua shingo kwa kunivuta vuta,imekuwa Kama nanyonyesha Sasa. Mara aninyang'anye simu,mara aniparamie usoni Kama mbwa,alafu ana vikucha vikali.

Basi naishia kujichekesha chekesha tu mbele ya mama yake,maisha ya ugenini yana unafiki Sana. Wazazi wake Wala hawastuki,wanaona poa tu mtoto wao anavyoact Kama kingedere. Mamaake ananiambia "shemeji Kama junia anakusumbua mchape" Namchapaje mtoto wa watu ugenini? Kwa nini asimkataze kusumbua wageni na kukachapa kakiendelea kuleta ubishi.

Sasa mamaake akaenda dukani akaniacha na junia tunavutana vutana. Happy ndiyo nikambadikilia nikamwonyesha sura ya ukauzu na kumtoa shingoni maana ilikuwa Kama ananidai kwa jinsi alivyokuwa ananikaba. Nikakashika mikono na kukaminya tuvidole vyake Kama naminya karanga,huku namwambi acha utundu kwa wageni mtoto. Kakaanza kulia kanaelekea dukani kwa mamaake.

Maisha ya ugenini magumu Sana. Nilipanga kukaa siku mbili ila moja tu inatosha kwa kweli.

Wazazi wengine hivi mnaleaje watoto kipuuzi Kama hivi?
Katoto ni ka-attention seeker mpo katika maongezi sebuleni, kenyewe kanapita pita na kuvuta watu nguo ili mradi tu kaonekane kapo live. Mkikapotezea kataangusha hata glass!!


Katoto ka Bro wako ni katoto kako pia, kwahiyo wewe na Bro wako hapo mnaanza kupata hasara.

Halafu wewe naye ni jinga kubwa badala ya kuchukua mamlaka ya kumuonya ulipopewa mamlaka na mama yake (shemeji yako) badala yake ukawa unajichekesha kama zuzu!!🤤-- wewe si ndiye baba mdogo hapo!!

Inaonekana huyo shem wako angekutunuku mzig• pia ungejichekesha ?!!🤣🤣.

Siku zingine usituletee habari za kitoto humu.
 
Fanya shambulizi la kimya kimya hakuna haja ya kushika fimbo.
Shika mkono vizuri kwenye msuli(hawezi kua na msuli) binya na dole gumba kwa nguvu kiasi utakutana na mfupa, kandamiza kama sekunde 10 hivi uone kama katarudia
Hapana mkuu,

huu ni unyanyasaji na ukatili kwa watoto. Ni kusepa tu kuwachia msala wao
 
Halafu huyo mtoto wala sio mtukutu ila yupo excited kumuona Anko wake ndio maana anampandia pandia kwa furaha ila kwa kua watu mmejazwa roho mbaya na ukatili hata furaha ya watoto mnaigeuza chuki,

Hii gender ya Kiume ingeteketea tu [emoji849]
 
Kama wewe sio mnafki kwanini usimkemee hapo hapo mbele ya wazazi wake? Kwanini usubiri hawapo ndio umfinye? Nyie ndio mnalawiti watoto kwa roho mbaya zenu.
Huko kwenye kulawiti umefika mbali Sana.

Alafu usijifanye Kama hujui maisha ya ugenini. Ukienda ugenini lazima unakuwa na kaunafiki fulani,either kutojifanya mlaji,kuwa msataarabu sana au kujifanya unajisikia vizuri mtoto akikuletea ukorofi.

Hii si kwangu tu,ni kwa wengi hutokea unapokuwa ugenini.
 
Mimi huwa navitegesheaga miguu ili adondoke
Fanya hivi wakati unakabeba beba kamata tako moja halafu ufanye kama unaliviringa kwenda kulia....
Kakifanya ng`a na wewe unafanya ng'a,watajua mnacheza ila lazma wakakape panado maana katalalamika siku nzima..
Sikutarajia kukutana na comments za kuchekesha kiasi hiki.

Kumbe humu ndani Kuna magaidi kiasi hiki?
 
Huko kwenye kulawiti umefika mbali Sana.

Alafu usijifanye Kama hujui maisha ya ugenini. Ukienda ugenini lazima unakuwa na kaunafiki fulani,either kutojifanya mlaji,kuwa msamtaarabu sana na Kama hivyo kujifanya unajisikia vizuri mtoto akikuletea ukorofi.

Hii si kwangu tu,ni kwa wengi hutokea unapokuwa ugenini.
Sijawahi kwenda kwa ndugu yangu na kujifanya mnafki, hiyo ni nidhamu ya uoga sikulaumu sababu tumekulia mazingira tofauti ila kwa familia yangu hua najitanua plus madeko kama yote,
Watoto wananipenda na mimi nawapenda sana, nikifika wanajua Rich Aunt is here [emoji847]
 
Mtoto anakutukanaje? Itakua umejiweka kihuni sana,
Mtu aliyekaa kiheshima hawezi kudharauliwa na mtoto hadi kufikia kutukanwa, duh!
Ndio nakuambia huwajui vizuri, kama wazazi hawajafunda vizuri wanawachekea na kuwaacha wakue hovyo hovyo wanashindwa nini kutukana?
Kuna watoto wana tabia mbaya sana labda kama ujawai ishi uswahili/uswazi
 
Mkuu,

Huwezi kufanya huu ugaidi mbele ya babaake na mamaake. Hili kunakuwa swala la wawili,wewe na yeye,ndiyo mnanyooshana viungo. Ila siyo Jambo zuri.
😅😅😅

Hujawai kuona mpo sebuleni mtoto hataki kupita hata karibu yakoo.. kuna mifinyo pia ya siri.. mtoto anashindwa kulia wala kucheka ila anakuwa hakusogelei hata akitumwa kwako unaona kanatingisha tu mageba
 
Ndio nakuambia huwajui vizuri, kama wazazi hawajafunda vizuri wanawachekea na kuwaacha wakue hovyo hovyo wanashindwa nini kutukana?
Kuna watoto wana tabia mbaya sana labda kama ujawai ishi uswahili/uswazi
Kama ni Uswazi basi shida haipo kwa Mtoto bali ni mazingira yaliyomzunguka Mtoto, hapo badala ya kumsulubu Mtoto ni lazima ahamishwe hayo mazingira
 
Back
Top Bottom