Ukifuatilia sana yanayojiri huko Israel, Lebanon, Iran, Palestina, Russia na Ukraine unaweza fikiri Dunia itawaka moto usiku huu na Kuteketea kabisa

Ukifuatilia sana yanayojiri huko Israel, Lebanon, Iran, Palestina, Russia na Ukraine unaweza fikiri Dunia itawaka moto usiku huu na Kuteketea kabisa

Heart Wood.

JF-Expert Member
Joined
Nov 16, 2014
Posts
982
Reaction score
1,179
Wakuu,

Kichwa cha thread chahusika.

Yaani ukijifanya kuwa mfuatiliaji sana wa kinachojiri huko kwa wenzetu unaweza pata wasiwasi na kuhisi dunia itafikia mwisho usiku wa leo. Kumbe maisha yapo tu na yataendelea kuwepo sana.

Mwanzoni wakati nasikia Russia ikiwapiga beat Ukraine pamoja na NATO nilidhani Ulaya yote itaangamia, lakini wapi. Mpaka sasa jioni hii watu pande za Ulaya wanakula tu mvinyo kama kawa.

Sasa dawa ya kukomesha hofu tunayolazimishwa na media ni nini?

Ni kupuuzia kila kitu kinachoendelea na kuendelea kupambana na maisha yako tu. Usiache kabisa kufuatilia kinachojiri ila ukishasoma hizo habari we achana nazo na uendelee na maisha yako.

Nilitumia njia hii wakati wa COVID ikanisaidia. Mwanzoni nilikuwa nafuatilia sana habari za COVID kisha nikawa napata hofu, ila tangu nilipoanza kupuuza habari zake COVID ilipita na maisha mpaka sasa yanaendelea kama kawa hapa Duniani.

Mwisho wa thread.
 
Wakuu,

Kichwa cha thread chahusika.

Yaani ukijifanya kuwa mfuatiliaji sana wa kinachojiri huko kwa wenzetu unaweza pata wasiwasi na kuhisi dunia itafikia mwisho usiku wa leo. Kumbe maisha yapo tu na yataendelea kuwepo ....
Sawa umeeleweka!
 
Hizo ni vita za ndugu kuziingilia na kuchagua upande ni upimbi wa hali ya juu.. Wanajuana hao waache watangane wakichoka watarudi mezani kuyajenga
 
Usife presha, huko middle east (Iran vs Israel vs Arab Nations) wana battle lao Hilo haliishi Hadi mwisho wa dunia...huko Russia na Ukraine ni ndugu wa damu, waache nao wauane wakichoka watatulia...Tena ni kwamba miaka hii Kuna afadhali kubwa, enzi hizo za kina mongols, Romans(west and eastern Romans), ottoman, Persian kingdoms, unavamiwa Kwa lazima bila taarifa yyte, kama ni mwanaume unachanwa na panga kama nyama buchani, unachukuliwa utumwani Kwa lazima. Sasa hv Kuna sheria za kivita kabisa wakati ukikutana na Genghis Khan wa mongols kipindi hicho anakutafuna Hadi utumbo.
 
Back
Top Bottom