Ukiona mfanyakazi anamiliki vitu havilingani na mshahara wake hiyo ni Red flag

Ukiona mfanyakazi anamiliki vitu havilingani na mshahara wake hiyo ni Red flag

mhn! naogopa nikikambia kuwa unaishi kizamani utachukia! lakini ndio hivyo.
wakati huo mshahara ndio ulikuwa chanzo pekee kwa mfanyakazi kuishi na kiukweli kulingana na mahitaji ya wakati huo alikuwa anaweza kumudu maisha yake ya kawaida.
lakini kwa sasa mambo ni tofauti mshahara ni moja ya chanzo cha mapato. mfano mtu akiwa na mshahara anaweza kumudu kujiunga na VICOBA na kuweza kukopa zaidi ya 3,000,000 akawekeza kwenye biashara nyingine inayoweza kumwakikishia pato la shilingi 20,000 kwa siku sawa na laki sita kwa mwezi bado hajauza supu na chakula ambayo tufanye kwa siku inaleta 10,000 sawa na 300,000
chanzo kingine inawezekana familia imeuza mali ya urithi kama nyumba akapata mgao wa 150m sasa kwanini asinunue gari?
viko vyanzo vingi zaidi ya kipato zaidi ya wizi
Masanja yupo efm lakini naendesha mav8 nae Huyu vipi? Ya gharama kuliko boss wake majizo
 
Ukiona mfanyakazi wako anamiliki vitu havilingani na mshahara unaomlipa lazima upate wasiwasi , mfano haiingii akilini kwa mtu anayelipwa laki 3 halafu ananunua Gari la milioni 60 , au anaishi maisha yanayozidi mshahara wake. Waajiri kuweni makini hizo ni Red flag za kupigwa
Kabla yakumuwekea reg flag mfanyakazi wako kwanza jiulize ofisi yako inaweza kuibiwa hiyo million 60 ukute thamani ya ofcn yote ni 30 million tu.
 
Kama na biashara au kilimo ila kazi anapata ujuzi na ni kwa sababu zingine huyo nae utasemaje?
 
Sasa lengo la kazi ni Nini? Ili umchunguze mfanyakazi wako maendeleo yake? Boss mzuri unapaswa utamani mafanikio ya watu wako maana kufanikiwa kwao ni mafanikio zaidi kwako.

Tamaa za wizi mara nyingi zinatokana na kutowapa stahiki zao Kwa wakati na wanapokua hapo motivated. Maboss wajifunze uongozi bora
Nyie wachangiaji kwa kweli mmenitia moyo sana nilikuwa nawaza jinsi ya kwenda na hili gari langu kazini ...sasa majibu ya kumpa boss akileta maneno ninayo.
Mmenifariji sana .
Kazi iendelee
 
Mshahara laki3 , Gari ya milioni60...!!🙄🙄

Kumbe ukikljitahidi sana unaweza ukaubeba mlima Kilimanjaro 😂!
 
Ukiona mfanyakazi wako anamiliki vitu havilingani na mshahara unaomlipa lazima upate wasiwasi , mfano haiingii akilini kwa mtu anayelipwa laki 3 halafu ananunua Gari la milioni 60 , au anaishi maisha yanayozidi mshahara wake. Waajiri kuweni makini hizo ni Red flag za kupigwa
SIO KWELI Mkuu.
Nilikuwa na mshahara wa Tsh 35,000/= miakq 20 iliyopita na ulitosha kufanya maendeleo. Hata tukipokea lak 3 sasa hivi mimi na wewe. Mimi utatosha na nitafanya la kufanya kupitia hiyo laki 3 mkuu.
Sio kila mwenye mshahara mdogo ni mwizi hapana. Unapokea laki 3 umepanga,una mke na watoto ,una mchepuko, una watoto kibao unadaiwa matumizi hiyo haita kutosha.!
 
Ukiona mfanyakazi wako anamiliki vitu havilingani na mshahara unaomlipa lazima upate wasiwasi , mfano haiingii akilini kwa mtu anayelipwa laki 3 halafu ananunua Gari la milioni 60 , au anaishi maisha yanayozidi mshahara wake. Waajiri kuweni makini hizo ni Red flag za kupigwa
Hili ni tatizio la kurithi jina la ukoo pekee, wengine wanatoka familia zinazojiweza, hivyo wanarithi na mali pia. Ila kusudi uweze kufaulu darasani nadharia yako ni sahihi kwani ndivyo ulivyofundishwa.
 
Mbona mke wangu namuachia afu tatu na kila siku tunakula wali kuku? Acha unoko.
 
Ukiona mfanyakazi wako anamiliki vitu havilingani na mshahara unaomlipa lazima upate wasiwasi , mfano haiingii akilini kwa mtu anayelipwa laki 3 halafu ananunua Gari la milioni 60 , au anaishi maisha yanayozidi mshahara wake. Waajiri kuweni makini hizo ni Red flag za kupigwa
Hizo ni redflag lakini hazimaanishi kwamba ni upigaji 100% na inategemeana na mtu husika , mimi nilianza ajira huku napiga mishe mishe zingine , so nilikuwa naweza tumia zaidi ya my salary sometimes.

Ofisi niliopo kuna watu mishahara yao ni ya kawaida ila wanamagari ya mil 80, 90, 120 na nikawaida kabisa maana wanabackup za issue zingine sio salary tu mzee.

labda uzungumzie ofisi za umma ambapo ndio kunakuwa na fraud sanasana.
 
Kuna jamaa alizindua nyumba yake ya gorofa moja akaalika marafiki wa kazini mwezi uliofata akafanyia bonge la audit na kuachishwa kazi
Labda walimuonea wivu tu wenzake ,maana kama angekuwa mwizi asingealika wafanyakazi wenzake. Ghorofa moja sasa ndugu si hata mil 150 mtu ananyanyua? kama karithi?,kauza kiwanja? kakopa ?

Kaka alikuwa mwizi basi ni mjinga kabisa
 
Watu hawaelewi ila watu unaofanya nao kazi hawapaswi kujua mambo yako. Kutaneni kazini au baa achaneni huko huko. Mimi ni Nina kijumba Cha kuzugia kabisa siku kama naumwa au Nina tatizo wanakuja kuniona hapo na wanajua ndio kwangu.

Nilikajenga maalum Kwa ajili ya kazi hiyo. Kilichofuata jamaa wananidharau na kunipuuzia wakati wangejua namiliki ukwasi wa mabillion
Yaani una ukwasi wa mabilioni halafu unaishi kama digidigi kisa ajira ambayo haikupi hata kipato cha kujenga nyumba ya maana bila kuonekana mwizi?
Jamani mnapotunga hizi stori muwe mnapima uhalisia.
 
Yaani una ukwasi wa mabilioni halafu unaishi kama digidigi kisa ajira ambayo haikupi hata kipato cha kujenga nyumba ya maana bila kuonekana mwizi?
Jamani mnapotunga hizi stori muwe mnapima uhalisia.
Mwamba umechanganua umeshtuka story ni ya kupangwa
 
Yaani una ukwasi wa mabilioni halafu unaishi kama digidigi kisa ajira ambayo haikupi hata kipato cha kujenga nyumba ya maana bila kuonekana mwizi?
Jamani mnapotunga hizi stori muwe mnapima uhalisia.
Ukwasi wa mabilioni? hao wanaokuja kukuona lazima watakuwa kwao nyumba sio issue ,so jamaa anatupiga fix
 
Ukiona mfanyakazi wako anamiliki vitu havilingani na mshahara unaomlipa lazima upate wasiwasi , mfano haiingii akilini kwa mtu anayelipwa laki 3 halafu ananunua Gari la milioni 60 , au anaishi maisha yanayozidi mshahara wake. Waajiri kuweni makini hizo ni Red flag za kupigwa
😄😄😄Yaani wewe ukiwa ni boss sehemu fulani utateseka sana Kwa mentality yako ya namna hii.
Fungua ubongo vizuri mzee.
 
Hii philosophy ni kufikiri kimaskini. Hili nilikuja kulitambua baada ya jamaa mmoja tuliye ajiriwa naye, alikuwa na maisha ya kawaida kabisa ya kupanda Daladala na wakati mwingine alikuwa anaweza kukupiga kibomu cha fifty au zaidi. Ila hakuwa mzulumati. Akikopa anarudisha mwisho wa Mwezi.

Baadae akawa amefiwa na mzazi. Issue za Mirathi hazikukawia, watoto wakagawana Mali na mkwanja. Yeye akabahatika kupata 280m. Halafu bado akaendelea kubakia Low Key.

Sasa mtu kama huyo akija kuomba kazi kwako, leo na kesho ukamuona ana drive Anaconda au Subaru X-Brake, utaanza kumfuatilia !?

Binafsi nashauri tuache kufikiri kizamani.
 
Na ukiona mtu ana frame kubwa pale sinza alafu ndani ya hiyo fremu kaning'iniza vinguo viwili tu, huku nje kapaki V8 kali/Sport car hiyo ni redflag.
 
Watanzania wengi ni very sadist. Ona huu uzi.
Wabongo wengi ni wapigaji sasa hapa wanapeana sapoti za kijinga. kuna jamaa namfaham alikuwa mshkaji tu tupo naye kijiweni siku zote mara akapata kazi sehem flani. siku iyo ghafla kanicheki anataka kuanzisha kiprojekti chake cha milioni 10 nikajua uku tyr kumekucha. mara naskia kafukuzwa kazi.
 
Back
Top Bottom