Ukiona Rais wa Nchi ana chawa wengi shtuka hakuna kiongozi hapo

Ukiona Rais wa Nchi ana chawa wengi shtuka hakuna kiongozi hapo

Uzuri mama akishachapa KV hana noma na mtu, anasema we kula tu kwa urefu wa kamba yako
 
Chawa wa sasa wanafaidi sana, wanatolewa 'out' za Dubai kila mara.
 
tatizo la kua na njaa sana asubuh asubuh, halafu unaishi nyumba ya kupanga na unamkopo kausha damu lazima utawaza upotofu tu .
Inawezekana kweli mleta mada ana njaa kama unavyosema, ila hoja zake vp?!.
 
Bajeti ya safari tu za mazeri zinauwezo wa kujenga hospital zenye hadhi kadhaa
 
Nilitegemea uje na hoja kama hii hata kama Kwa kuchelewa lakini niliitazamia Kwa sababu zifuatazo:

1. Kwanza, uliamini mtu Fulani angekuwa Fulani na baada ya hapo nawe ungekuwa fulani kutokana na huyo Fulani. Mpaka sasa hauna matumaini ya huyo fulani kama ulivyotarajia hivyo kitendo hicho kinakupa msongo mkali wa mawazo na nilitarajia muda si mrefu utaanza kumsema vibaya Rais.

2. Acha niende Moja Kwa Moja kwenye point bila kumung'unya maneno. Ulitamani sana Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara na Katibu mkuu wa CCM waondoke ili pengine wewe au unayemtaka awe Katibu mkuu au Makamu na mpaka sasa hesabu zako zimegoma kotekote ndio maana umetokea kuwachukia chawa ukiamini ndio wamekutengenezea zengwe.

Hapo inatosha kusema suala la Chawa sio msingi wa hoja yako na msingi mkubwa wa hoja yako ni kuvurugika Kwa mipango yako
 
Inawezekana kweli mleta mada ana njaa kama unavyosema, ila hoja zake vp?!.
zaidi ya wivu, kutia huruma, mihemko na chuki binafsi dhidi ya walio karibu au wanaomuunga mkono Rais atatoa hoja wapi pamoja na wewe mwenyewe labda na vibaraka unaowaunga mkono kwa uchache 😜
 
Ukiona Rais wa Nchi ana chawa wengi tambua mtu huyo hana uwezo wowote wa kuongoza Nchi.

Rais debe tupu lazima Nchi yake itakubwa na yafuatayo;

....uongozi duni.

....huduma za jamii kulemaa.

....upungufu wa umeme.

....ufisadi kutamalaki.

....ubinafsishaji wa mashirika ya umma ki ufisadi.

....safari nyingi za nje zisizo na maana yeyote.

Kwa muktadha huo, endapo Nchi yako ina Kiongozi mwenye machawa wengi tambua huna Rais bali unaongozwa na debe tupu!
.
 
Mabwege nyie wivu unawasumbua, Rais wetu ana wapenzi wengi nchi nzima, hakuna cha chawa, chawa wako kwenye nguo zako. Kumpenda rais wetu na kumwuunga mkono siyo uchawa. Kwanza Rais hata hawafahamu.
Kwa kuws keenu hakuna mgao wa umeme na wewe una punguzo maalumu vutuo vyote vya mafuta nchini na zaidi sana serikali inakupatia ruzuku ya basics basi ni haki yako kuimba pambio za kusifu.

Sisi wenye nchi tumegoma. Hatukubali samia na ccm yake waendelee kuvuruga nchi
 
Inaonyesha, jaribio la kijana kuukwaa u- KM Kwa Hila limekwama Rasmi.
 
Back
Top Bottom