Ukiona siri za jumba jeupe zinavuja, basi hiyo ni taa nyekundu kwa kiongozi wa nchi

Ukiona siri za jumba jeupe zinavuja, basi hiyo ni taa nyekundu kwa kiongozi wa nchi

Hao mabwana wanazo mbinu nyingi za kulazimisha ushauri wao wa kizalendo utiliwe maanani.

Hiyo ya kupenyeza taarifa nyeti kwa vyombo vya habari, wanaharakati na wapinzani ni moja ya njia za awali tena za 'amani'.

Wakiona mambo yanaharibika sana basi watalazimika kutumia mbinu mbaya zaidi. Uwezo huo wanao.

Kwa hali ilipofika sasa ya safari za SIRI za kiongozi kuanikwa tena zikiwa kwenye hatua ya mipango inapaswa kuwa 'wake up call' kwa kiongozi husika.

Kumbuka, mamlaka ya kwenye karatasi hayana maana yoyote ikiwa wale unaowategemea ku enforce mamlaka yako hawako upande wako.
Kaona mchwa waharibifu wanabungua kijiji roho ime muuma taratibu hazimruhusu kuchukua hatua kaamua kutafuta spika (wanaharakati) kuvujisha taarifa nyeti sauti ipazwe.. ili wanakijiji wajue hatari iliyopo ndipo tulipo fikia hamna usiri.
 
Ni dhambi kubwa kuzushia kifo watu

Lakini pia kifo kikija, hakina namna nyingine zaidi ya kujulikana kwa kila mtu, maana hakifichiki, kikikuondoa, macho ya kila mtu yatashuhudia kuwa wewe haupo tena katika hali ya uzima, na kwamba wewe ni mfu, na watu wasipoweka wazi hilo, bado mfu ataoza tu!
 
Nyingine wanavujishaga makusudi

Ila kuna moja nzito na I verify kwanza hapa

Nzito mno!

Nilitaka nichape Uzi Ila nikagundua kuna code ziko wazi sana nikauweka pending (Draft)

Ila nikiwaza CHATU kufa wakifuatana si vema sana!
Britanicca
Mmh!

Nisisitize tu hapa, haina haja kutamani au kuwaza tu kuwa, miongoni mwetu wanadamu kuwepo na mmoja wetu wa kutamani kuwaondoa uhai wengine kwa sababu tu eti apate uhuru kwenye mambo yake afanyayo au matamanio yake binafsi ya hapa duniani akisahau kwamba, kifo hakina adui wala rafiki
 
Nyingine wanavujishaga makusudi

Ila kuna moja nzito na I verify kwanza hapa

Nzito mno!

Nilitaka nichape Uzi Ila nikagundua kuna code ziko wazi sana nikauweka pending (Draft)

Ila nikiwaza CHATU kufa wakifuatana si vema sana!
Britanicca
Hakuna taatifa nzito hapa duniani labda tupate kitu kigeni nje ya dunia yetu hiyo ndio itakuwa taarifa nzito!.
muda wowote mtu yoyote unaweza ukasikia amelamba ardhi kitu ambacho ni kawaida kete ya uhai kila mmoja atairudisha tu!.

labda mniambie annunaki wanakuja duniani ama viumbe vya ajabu vimeingia dunia hiyo ndio taarifa nzito!
 
Safari nzima ya mheshimiwa ya huko nje ya nchi tangu iko kwenye mipango ya awali kabisa ilivuja.

Jambo la hatari sana, yaani mpaka usafiri watakaotumia, mpaka orodha ya akina nani watakwenda.
Katika dunia hii ambayo ndege aliyotumia rais inajulikana ni 5H-TCR na unaweza kuifuatilia online kuona iko wapi, serikali inawezaje kuficha nyendo za rais?

Na kwa nini serikali katika nchi ya kidemokrasia isiwe wazi kuhusu nyendo za rais?
 
Nyingine wanavujishaga makusudi

Ila kuna moja nzito na I verify kwanza hapa

Nzito mno!

Nilitaka nichape Uzi Ila nikagundua kuna code ziko wazi sana nikauweka pending (Draft)

Ila nikiwaza CHATU kufa wakifuatana si vema sana!
Britanicca

Weka uzi, jambo kama lime au litatokea hakuna mtu wa kuzuia isipokuwa Mungu...
 
Katika dunia hii ambayo ndege aliyotumia rais inajulikana ni 5H-TCR na unaweza kuifuatilia online kuona iko wapi, serikali inawezaje kuficha nyendo za rais?

Na kwa nini serikali katika nchi ya kidemokrasia isiwe wazi kuhusu nywndo za rais?

JPM na sasa Samia ambaye amekuwa na tendency kutumia ndege za ATCL haswa ile Boeing Max
 
Kwani taarifa si zinaweza kuvuja kutokea upande alioomba kwenda kutembea?
Taarifa kuvuja maana yake ni nini?

Taarifa gani?

Habari za safari za rais, au afya ya rais, zinatakiwa ziwe wazi, wananchi wana haki ya kujua rais yuko wapi, anafanya nini.

Hili ni jambo la kawaida katika nchi za kidemokrasia.

Sasa tunaweza kuona taarifa zinavuja kwa sababu hatujazoea serikali kuwa wazi.

Lakini, suala la muhimu zaidi ni kuwa, kwa nini taarifa hizi hazitolewi kwa uwazi na serikali?

Kama Ikulu haitoi taarifa, na kupata taarifa hizi ni haki ya wananchi, kwa nini Ikulu haitoi taarifa hizi ambazo ni haki ya kikatiba ya wananchi?
 
Back
Top Bottom