Ukiondoa Ukakasi wa Kauli za RC Chalamila Mnyonge Mnyongeni Ila Haki Yake Mpeni, Waafrika Tunapenda Kulelewa Mpaka Imekuwa Ulemavu

Ukiondoa Ukakasi wa Kauli za RC Chalamila Mnyonge Mnyongeni Ila Haki Yake Mpeni, Waafrika Tunapenda Kulelewa Mpaka Imekuwa Ulemavu

You mean unataka tuwajibike na sio kulalamikia wengine for our shortcomings? Hatukubali.

On the other end, watu lazima walalamike wanapoona wanalipa kodi zinaenda kununua V8 kila siku wakati vifaa tiba vya bei ndogo kabisa vinakosekana. Kulikua na ulazima gani wa ku update gari zote za serikali wakati za zamani bado zinafanya kazi? Vipaumbele vimekua vipaunyuma. Wananchi wana haki ya kuhoji matumizi ya kodi zao.
Sasa mkuu unamaanisha kwamba serikali viongozi watumie Noah, rumion, crown na juke let say kutoka DSM mpaka mwanza, bukoba, RUVUMA au rukwa? Tuwe wakweli tu.

Hii nchi Kuna muda unahisi kama matatizo na umasikini tulionao ukikaa sawa kabisa utakuta sisi wananchi wa chini ndyo tunachangia pakubwa kuifikisha mpaka hapa ilipo
 
Sasa mkuu unamaanisha kwamba serikali viongozi watumie Noah, rumion, crown na juke let say kutoka DSM mpaka mwanza, bukoba, RUVUMA au rukwa? Tuwe wakweli tu.

Hii nchi Kuna muda unahisi kama matatizo na umasikini tulionao ukikaa sawa kabisa utakuta sisi wananchi wa chini ndyo tunachangia pakubwa kuifikisha mpaka hapa ilipo
Viongozi ni reflection ya jamii wanayoingoza
 
Tanzania bila kuweka sheria Kali ya kuzuia hii kasi ya kuzaliana ....tutalaumiana sana. Serikali haiwezi kukidhi mahitaji ya familia kubwa inayokua kwa kasi ya mwanga kwa rasilimali hizi hizi.
Iwekwe sheria ya kuzaa watoto wawili tu hadi idadi isimame kwenye million 65. Anayezingatia vigezo na kutii apewe ruzuku au zawadi.
Hiki kitu ukiwaambia watz hawakuelewi, ila truth to be told. Kwma population ya sasa inawaelemea, wakifika mara mbili yake wata colapse kabisa
 
Nimesoma paragraphs 3 tu. Umeandika US3NGE, samahani.

Kodi tunazolipa zina msaada gani? Kuna nchi hapahapa Africa zina free healthcare. Ghana tu wana free maternal healthcare.
Sijui ni kaka"

Naomba nikueleze jambo moja... Unapopata nafasi ya kuwa msomi hata kwa bahati mbaya...

Jitahidi kuutumia usomi na kufanya tafiti kwenye hizo taasisi zinazosaidia akina mama kujifungua...

Inahuzunisha sana' tumekalia kila siku kuambiwa na kuimbiwa vya bure bure ndio vinavyoleta matokeo ya Magonjwa ya hovyo hovyo

Hizo health facility zinazalisha vya kutosha kuweza kuhudumia kundi la akina mama wajawazito 40 mpaka 100 kwa mwezi?


Tuko kwenye mifumo ya kuhitaji vituo vijihudumie vyenyewe, je vinaweza kujiendesha?

Facility inahudumia watu mfano 200 mpaka 300 kwa mwezi free, hizo Dawa na vifaa tiba mtanunua na nini?


Kuna wakati wasomi mnapaswa kuwa wakwanza kuwafundisha na kuwaelimisha ndugu' na Wana nchi kuchangia huduma ili hivi vituo viweze kuinuka na kujiendesha....

Nawaza wadau wa maendeleo wakijitoa siku moja sijui hivi vituo kama vitakuwa na uwezo wa kununua hata packet moja ya kidonge sidhani....

Badilika msomi
 
Sasa mkuu unamaanisha kwamba serikali viongozi watumie Noah, rumion, crown na juke let say kutoka DSM mpaka mwanza, bukoba, RUVUMA au rukwa? Tuwe wakweli tu.

Hii nchi Kuna muda unahisi kama matatizo na umasikini tulionao ukikaa sawa kabisa utakuta sisi wananchi wa chini ndyo tunachangia pakubwa kuifikisha mpaka hapa ilipo

Umeelewa hoja yangu?

Nimeuliza kuna ulazima gani wa ku update gari zote za serikali wakati zilizopo zinafanya kazi? LC200 bado imara kufika popote pale ila LC300 zilipotoka wamechukua mpya, hivyo ndo vipaumbele? Wananchi wanapohoji kwanini wanunue vifaatiba msiwazogoe wakati wanaona kodi zao zinatumika ndivyo sivyo.
 
USA ni taifa lililofeli ?
100%

Mtu 1 kati ya watu 5 Marekani ana deni kutokana na matibabu ya kiafya. Marekani wanatumia 17.6% (2024) ya pato la taifa kwenye afya na bado wanatoa huduma zenye gharama kubwa, ukilinganisha na Uingereza ambayo ina mfumo wa huduma za afya wa Kitaifa (NHS), ambao ni mfumo wa umma unaolipiwa na serikali kupitia kodi.

Uingereza, huduma nyingi zinatolewa na serikali na kila mtu ana uwezo wa kupata huduma bila kujali hali yake ya kifedha. Marekani, mfumo wao una mgawanyiko, ambapo kuna bima binafsi, bima kupitia ajira, na pia Medicare & Medicaid za serikali. Mgawanyiko huu unasababisha ufanisi mdogo, gharama za huduma kuwa juu, na upatikanaji wa huduma kutofautiana kulingana na bima na hali ya kifedha ya mtu.
 
50,000/- kwajili ya kujifungua ni gharama?
Siyo kila mtanzania ana uwezo wa kumudu hizo gharama. Ndiyo maana kama taifa ni lazima pia, kuwe na mipango dhabiti ya kuinua uchumi wa taifa na mtu mmoja-mmoja ili kuongeza walipa kodi na kupunguza namba ya umasikini. Kama taifa inasikitisha kuona vipaumbele vyetu ni vingine kabisa.
 
NCHI INAZAMA KWA KUKUMBATIA UJINGA

Je, umewahi kujiuliza kwa nini nchi hii haipigi hatua licha ya kuwa na rasilimali, amani, na nafasi za kujikwamua? Sababu iko wazi: tunakumbatia ujinga na kusambaza mzigo wa maamuzi yetu mabaya kwa wengine.

Mtu anataka kondomu afadhiliwe, akishindwa kuitumia na kupata VVU, anataka dawa za kufubaza ugonjwa zitolewe bure. Akimpa mwanamke mimba, anataka mtoto azaliwe kwa ufadhili wa serikali. Watu hawa ndio wale wale ambao wakifika hospitali kujifungua, hawana hata shilingi 5,000 ya kununua glovu za daktari, lakini wanaamini ni haki yao kupata kila kitu bure. Kwa nini? Kwa sababu wameshawishika kuwa serikali inapaswa kuwajibika kwa kila uamuzi wao mbovu maishani.

Hili suala linafanana kabisa na chuki dhidi ya kauli za RC Chalamila. Yaani mtu amebeba ujauzito bila kuwa na uhakika wa hata shilingi elfu tano ya vifaa vya kujifungulia, halafu anakuja hospitali akiamini kila kitu kitaangukia bure kutoka kwa serikali. Hebu fikiria—ikiwa hata hela ya kondomu siku hiyo haikuwepo, serikali ndiyo ije kubeba mzigo wa mtoto wako? Na kama kweli huna uwezo hata wa kununua glovu, unadhani kweli utakuwa na uwezo wa kumlea huyo mtoto?

Ni mentality hii hii tunayoiona kwa ARV. Mtu anaamua kufanya zinaa bila kinga, akipata UKIMWI anataka matibabu yatolewe bure. Ndio maana mpaka misaada ya Wamarekani inahitajika kulisha taifa linalozaliana bila mpango. Watu milioni 60, lakini wanaochangia mfuko wa bima hawafiki hata milioni 5. Hao wachache ndio wanapaswa kubeba mzigo wa wengine wote? Na bado tunajiita taifa huru!

Tuache unafiki. Hii siyo tena hoja ya CCM au CHADEMA. Ukifukuza CCM na kuleta upinzani, hakuna miujiza itakayofanyika. Historia imetufundisha kuwa mabadiliko hayaji kwa kubadilisha majina ya viongozi, bali kwa kubadili tabia na mtazamo wa jamii. Tanzania ina watu milioni 60, lakini wenye mchango wa moja kwa moja kwenye pato la taifa hawazidi milioni 10. Unadhani nchi yoyote inaweza kuendelea ikiwa idadi kubwa ya watu wake ni mizigo?

Tazama tofauti kati ya Kenya na Switzerland. Miaka ya 1960, nchi hizi zilikuwa na idadi sawa ya watu, lakini leo Kenya ina watu zaidi ya milioni 50, wengi wao wakiishi kwenye umasikini, huku Switzerland ikiwa na milioni 7 wanaoishi maisha mazuri. Unadhani ni kwa bahati mbaya? Hapana. Ni kwa sababu kule watu walitumia akili, huku kwetu wengi wanaamini "Mungu atajalia" huku wakizaliana bila mpango na kutegemea serikali iwahudumie.

Kama hatutabadilika, tusitarajie maendeleo. Tusipokuwa wakweli kwa nafsi zetu, tutaendelea kulalamika huku tukizidi kuzama kwenye lindi la umasikini wa kujitakia.
Ushawahi kujiuliza kwanini hujawahi kusikia mtanzania yeyote amekwenda airport kupanda ndege za Air Tanzania bure?
Jibu ni kwamba serikali haijawahi kuwambia hivyo. Sasa unakuta waziri ili serikali ipate sifa anawambia akina mama wajawazito kutibiwa, huduma na dawa ni bure, same kwa elimu halafu wanaenda wanakuta si bure.
Mkosaji hapa ni serikali ambayo haitaki kuwambia ukweli. Leo waziri kaulizwa bungeni bado anasema ni bure.
Wambieni ukweli kuwa labda utachangia lakini si bure.
 
Hivi vitu bila kufanya Mahesabu kila siku mtakua ni watu wa kulalamika,

Bajeti ya Afya 2023 ilikua ni Trilioni 1.2 kwa Nchi ambayo ina watu zaidi ya milioni 60 hio ni kama 20,000 kwa mwaka kwa kila mtu. Unaweza nipigia mahesabu 20,000 inatoaje huduma za Afya mwaka mzima bure? Kwa Pato la Taifa letu hata tukisema tunatumia 50% ya pato la Taifa kwenye Afya tu bado haitoshi kutoa Huduma bure, bado hapo mtu anataka Atibiwe bure, Elimu bure, ajengewe barabara etc.
20250131_190408.png
 
Chalamila ni CCM na serikali iliyopo madarakani inaongozwa na CCM na ilani ya CCM huduma ya kujifungua ni bure na kiukweli wananchi sidhani kama wanashindwa kuwa na hela kidogo ya kuchangia bali viongozi wenyewe wa serikali wamewalemaza na tena wanazungumza live bila chenga kwamba KUJIFUNGUA NI BURE na kama kuna Mtumishi wa afya amelipisha fedha mwananchi akalalamika ikafika kwenye vyombo vya habari itaitwa na PRESS kukemea kilichofanyika.

Hata hivyo ukijifingulia hospital za umma ni BURE except kama utaenda kijifungulia hospitali ya RUFAA bila kupewa rufaa hapo ndo kuna kulipia. Msiwasimange wananchi wakati wao wenyewe kina Chalamila (Serikali) ndo wanawaambia kujifungua ni bure hivyo hiyo buku 5 unayoiona ndogo wenzako wanaona wanapigwa

Ni kuwapa taarifa sahihi tu wananchi, mbona mwananchi huyo huyo kwenye elimu ameambiwa elimu bure (elimu bila malipo) analipia mahitaji kibao kuliko hata ile ada iliyofutwa alafu ashindwe kulipia huduma ya kujifungua ambayo ni BURE na hata kama kuna complication atapakiwa kwenye AMBULANCE kwenda hospitali ya rufaa nako pia ni BURE kwa kuwa alianzia hospitali za chini.

Wapeni wananchi taarifa sahihi msiwasimange
 
Nimesoma paragraphs 3 tu. Umeandika US3NGE, samahani.

Kodi tunazolipa zina msaada gani? Kuna nchi hapahapa Africa zina free healthcare. Ghana tu wana free maternal healthcare.
Kaka jitahidi ukiweka mimba uwe responsible, mengine yawe ziada tuu.
 
Sijui ni kaka"

Naomba nikueleze jambo moja... Unapopata nafasi ya kuwa msomi hata kwa bahati mbaya...

Jitahidi kuutumia usomi na kufanya tafiti kwenye hizo taasisi zinazosaidia akina mama kujifungua...

Inahuzunisha sana' tumekalia kila siku kuambiwa na kuimbiwa vya bure bure ndio vinavyoleta matokeo ya Magonjwa ya hovyo hovyo

Hizo health facility zinazalisha vya kutosha kuweza kuhudumia kundi la akina mama wajawazito 40 mpaka 100 kwa mwezi?


Tuko kwenye mifumo ya kuhitaji vituo vijihudumie vyenyewe, je vinaweza kujiendesha?

Facility inahudumia watu mfano 200 mpaka 300 kwa mwezi free, hizo Dawa na vifaa tiba mtanunua na nini?


Kuna wakati wasomi mnapaswa kuwa wakwanza kuwafundisha na kuwaelimisha ndugu' na Wana nchi kuchangia huduma ili hivi vituo viweze kuinuka na kujiendesha....

Nawaza wadau wa maendeleo wakijitoa siku moja sijui hivi vituo kama vitakuwa na uwezo wa kununua hata packet moja ya kidonge sidhani....

Badilika msomi
Kila mwaka zinapotea pesa nyingi za walipa kodi kutokana na matumizi mabaya ya rasilimali, wizi, udanganyifu, uhujumu uchumi, rushwa.

Tatizo kubwa ni kwamba system yetu ilishafeli kitambo sana, kwa nchi yetu imekuwa kawaida kuona watumishi wa umma wanachezea au kutumia rasilimali isivyotakiwa, hakuna uwajibishaji kwa watu wanaofanya makosa yanayogharimu taifa pesa nyingi sana. Halafu muda huohuo mwananchi wa kawaida tu anahamasishwa alipe kodi, pesa zinazoenda kufanya kazi nyingine nje na mipango.

Nchi yetu ina namba ndogo sana ya watu wanaolipa kodi na huwezi kuwalaumu wananchi. Itakuwa rahisi sana watu kulipa kodi kwa hiari pale watakapoona serikali yao inafanya jitihada kuboresha maisha yao na taifa kwa ujumla bila kujali cheo, undugu, au kabila. Imeshakuwa kawaida kwa nchi hii ili upate huduma bora basi lazima ujuane na mtu (connection) au uwe kwenye mfumo.
 
Kujifungua ni bure, ila vifaa ndio vya kugharamia hii mbona iko wazi
 
Back
Top Bottom