Ukipata milioni unaila siku tatu, ikibaki elfu kumi unaishi nayo week. Hii kitaalam mnaiitaje?

Mzee wako ni legend kama mzee wangu tofauti yao mzee wangu alishatangulia mbele za haki akatuachia msala.
 
Ni kweli kabisa mkuu nakubaliana na yote uliyoyasema, kamari ni addiction ambayo ilinitesa sana namshukuru Mungu nilifanikiwa kuacha baada ya kujitathimini na kuona nateketeza hela ambazo nazitafuta na kuzipata kwa shida.

Sifa za kuonekana zinawamaliza wengi, kama huyo jamaa ni kawaida kujitapa alitumia kiasi kikubwa cha pesa kulewa na starehe nyingine, alafu baada ya kuyasema hayo bado atalia shida.
 

ndo maana wanakwambia umasikini unaanzia kwene akili
 
Ni nguvu ya soko mkuu, ukiwa na milioni hata Zuchu atakupenda lakini ukiwa na elfu kumi hata mbwa anakukimbia
 
Watu wanaitawanya milioni ndani ya masaa we unasema siku 3, hukuwahi kufika bar ukakuta watu wanamwaga Hennessy chini.
 
Watu wengi sana wanateseka kwa kujitakia tu...ndo maana sio ajabu kuona watu wakitumbua tu pesa za kazi au za mikopo ya biashara..yote ili awe tu gumzo mjini๐Ÿคง๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿšฎ
 
Watu wengi sana wanateseka kwa kujitakia tu...ndo maana sio ajabu kuona watu wakitumbua tu pesa za kazi au za mikopo ya biashara..yote ili awe tu gumzo mjini๐Ÿคง๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿšฎ
Ukizifuga kuna mpuuzi atakuja kuzifuja km aliwahi kuzitafuta
 
hii pia ni hatua
uko njiani kufanikiwa kwakuwa ushalijua tatizo.
 
Watu wengi sana wanateseka kwa kujitakia tu...ndo maana sio ajabu kuona watu wakitumbua tu pesa za kazi au za mikopo ya biashara..yote ili awe tu gumzo mjini๐Ÿคง๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿšฎ
Na mwisho wa hayo yote huwa ni maumivu makali ya kupigika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ