Ukishuka Airport Dar ukapita barabara kuu unaona jinsi nchi na watu wake walivyochoka. Viongozi mnafeli wapi?

Ukishuka Airport Dar ukapita barabara kuu unaona jinsi nchi na watu wake walivyochoka. Viongozi mnafeli wapi?

Mji mzima sahivi barabara zimebomolewa wanajenga mwendokasi sasa ukisema ulalamike pengine hujui kinachoendelea ila pia usifananishe tz na USA bado isee.
Akili za kisiasa zinamtesa mleta mada. Hawezi kuongelea treni ya kisasa kutoka Dar kwenda Mwanza. Kajikitq kwenye negativity tu.
 
Nilishasema yote maisha tu.

Najifikiria na mimi nisingezaliwa familia fulani kwa bahati tu chances are ningekuwa na maisha tofauti sana na yasiyo na relative privileges nyingi sana nilizo nazo.

Imagine unaishi kwenye hizo nyumba za mabati chakavu, halafu kuna mijamaa iko Marekani inasema maneno kama haijawahi kukaa Tanzania.

Yani ushapigwa na maisha, halafu unaona unazodolewa na wabongo wenzako waliokimbikia dunia ambayo huna hata nafasi ya kufika.

Kuna siku nilikuwa nasema Watanzania hawapendi kusoma, nikasema mimi nilijenga utamaduni wa kusoma nika ji challenge kusoma mambo mengi sana, nikapitia Tambaza Library, Tanganyika Library, USIS Library (Peugeot House), British Council, mpaka Goethe Institute na Alliance Francaise. Watu wengi hawasomi.

Jamaa mmoja akaniambia hata kuzijua hizo sehemu ni privilege, hata kupenda kusoma mara nyingi kwenu kutakuwa na msingi wa kupenda kusoma, wazazi waliosoma na wenye maktaba ya nyumbani wana nafasi kubwa ya kuwapa msingi mzuri watoto wao kupenda kusoma.

Kwamba maisha yetu mara nyingi yanafuata mkondo fulani ambao umewekwa kwa bahati, si kwa juhudi, ingawa sehemu ya juhudi oia ipo.

Kwa hivyo, tunaposema habari za mapungufu ya nyumbani, tuwe waangalifu kutowakwaza wenzetu ambao hawajapata nafasi ya kutoka, bila kusahau kuweka msisitizo kwenye kufanya mazungumzo ya kubadilisha mambo yawe mazuri zaidi.
Lakini pia Marekani kufanyika "land of opportunity" na kuwekewa mazingira ya American Dream ni juhudi za dhati za raia wote na founding fathers wao,
 
Hata huko US wanaopiga picha wanajali uzalendo. Nadra sana kuziona mitandaoni picha za watu wanaolala nje pembeni ya njia za watembea kwa miguu. Na wapo wengi sana wanaolala kwenye maboksi.

Zikija picha huku kwetu ni zile za maghorofa marefu ya miji mikubwa, Disney Land na sehemu nzuri nzuri.


Yapo mabadiliko mengi ya mandhari katika majiji yetu lakini kwa kutojipenda kwetu na kukosa uzalendo tunakuwa na wepesi wa kutafuta picha mbaya ambazo zinachangia katika kuwapa watu picha mbaya ya Tanzania.
Ongelea mambo kwa ujumla na ukubwa wake, usichukue tumifano tudogo tudogo twa hapa na pale.
 
Maendeleo hayaji mara moja na ni utekelezaji wa vipaumbele vinavyowekwa kwenye ilani za uchaguzi.

Haiwezekani kwa mara moja tu tukawa tumeshatoka katika mabati yenye kutu, yapo mengi sana yenye kuhitaji kutekelezwa na pesa siku zote huwa hazitoshi kwa kuzilinganisha na wingi wa matumizi.
Marekani miaka ya 1800 ilikuwa inaishi kwa mipango miji,
20240731_075723.jpg
 
Mimi mwaka huu nilienda mwanza takribani miaka 10 ilikua imepita Ila nikaona pamechoka mbaya..

Kuhusu airport dar yes hayo maeneo ni aibu kwa kweli still we have a long way to go (NO POVERTY IS HARD TO FIGHT THAN IGNORANCE) 😔
Hata ukiwa masikini una nguo kuukuu tu basi jitihadi uzifue, yani hata pamoja na hizo nyumba za mabati ya kutu basi hata serikali ingesimamia zijengwe kwa mpangalio na muelekeo maalumu, kuwe na barabara pamoja na sewage system za kueleweka. Ni gharama ndogo sana kuwapanga watu wakae kwa mpangilio.
 
Utafika uliofanyika Kenya Unaonesha watu wa countryside wanatajirika kuliko walioko Miji mikubwa,the likes na hapa Tanzania na Dar yenu.

Kwa Sasa kijjaa wa Mkoani anaelima ana nafasi ya kuwa na maisha mazuri kuliko wa Dar na ndio maana Miji ya Mikoani hakuna mabanda kama ya huko Dar 😆😆😆😆😆
Town pesa ipo mfano huku dar ni Jambo la kawaida kutumia usafir (transport cost 10,000 + chakula let say 4000 + per day easy..

Rent haipungui 50,000+ Bado bill za maji , umeme na taka..

Mkuu uwe na heshima na vijana wa mjini (mawinga)

Huko kijijini unajenga nyumba ya udongo au choma unaezeka nyasi (mabati ya Simba).

Huko kijijini usipo jipanga mwaka mzima unaweza usiwe na Pato hata la 4m maana taarifa research zinasema mnaishi Chini ya 1700 kwa siku..

Still vijana wengi Wana opt Bora Mara 100 kubakia mjini na kuteseka kuliko huko kijijini ( bush)
 
Hata ukiwa masikini una nguo kuukuu tu basi jitihadi uzifue, yani hata pamoja na hizo nyumba za mabati ya kutu basi hata serikali ingesimamia zijengwe kwa mpangalio na muelekeo maalumu, kuwe na barabara pamoja na sewage system za kueleweka. Ni gharama ndogo sana kuwapanga watu wakae kwa mpangilio.
Umeongea jambo la msingi sana

Nyumba za zamani za ilala na Magomeni haikuwa nzuri kama za Oysterbay, lakini Mkoloni wa Kiingereza alipanga vizuri maeneo hayo ya waswahili ( yaani Ilala 'na Magomeni). Lakini serikali zetu za sasa zimefeli mno kwenye kufanya vitu kwa mpangilio
 
Hata ukiwa masikini una nguo kuukuu tu basi jitihadi uzifue, yani hata pamoja na hizo nyumba za mabati ya kutu basi hata serikali ingesimamia zijengwe kwa mpangalio na muelekeo maalumu, kuwe na barabara pamoja na sewage system za kueleweka. Ni gharama ndogo sana kuwapanga watu wakae kwa mpangilio.
Kwa Kweli UMASKINI hufanya nguo ziwe very busy..

Ukijumlisha unakua na nguo chache na zikiwa busy ndio zinapauka kwa Kasi SANAA (maana zitafuliwa na kutumika Mara kwa Mara bila mapumziko)

NB.
Smartness huficha UMASKINI
 
Lakini pia Marekani kufanyika "land of opportunity" na kuwekewa mazingira ya American Dream ni juhudi za dhati za raia wote na founding fathers wao,
Naam,

Nimesisitiza kujikita kwenye kuendeleza nchi bila kuonekana tunanyanyapaa watu wa nyumbani. Hususan wananchibwa kawaida ambao mostly ni wahanga wa mifumo wasiyo na nguvu sana za kuibadili.

Hilo litatengeneza vita ya watu wa nyumbani na wa nje, ambayo haitasaidia watu wa nyumbani wala wa nje.
 
Ongelea mambo kwa ujumla na ukubwa wake, usichukue tumifano tudogo tudogo twa hapa na pale.
Tuachane na hii hulka ya kuidogosha Afrika na Tanzania kwa ujumla. Inaacha makovu mabaya vichwani mwa vijana wadogo wanaingia kwenye maisha wakiwa na mtazamo wenye hasira kwenye kila linalofanywa na serikali.
 
Marekani miaka ya 1800 ilikuwa inaishi kwa mipango miji,
View attachment 3058546
Roma haikujengwa ndani ya siku moja. Kuna mabadiliko hata sasa hapa Dar.

Tazama namna lile daraja lililojengwa pale bandarini zamani pakijulikana kama BP ukiwa unatokea kariakoo namna linavyoipendezesha mandhari ya jiji letu.

Pakijengwa na pale Jangwani kisasa jiji la Dar litakuwa na uzuri fulani ambao haukuwepo kabla.

Tujifunze kuongelea ya kwetu katika namna zilizo chanya.
 
Roma haikujengwa ndani ya siku moja. Kuna mabadiliko hata sasa hapa Dar.

Tazama namna lile daraja lililojengwa pale bandarini zamani pakijulikana kama BP ukiwa unatokea kariakoo namna linavyoipendezesha mandhari ya jiji letu.

Pakijengwa na pale Jangwani kisasa jiji la Dar litakuwa na uzuri fulani ambao haukuwepo kabla.

Tujifunze kuongelea ya kwetu katika namna zilizo chanya.
Umenikumbusha Ile picha iliyo pigwa na AL AHLY waliipiga kwa Aerial 🚡 photography

Wakaonyesha mandhari ya uwanja wa taifa na viunga vyake mabati yalivyo kua yamechoka
 
Roma haikujengwa ndani ya siku moja. Kuna mabadiliko hata sasa hapa Dar.

Tazama namna lile daraja lililojengwa pale bandarini zamani pakijulikana kama BP ukiwa unatokea kariakoo namna linavyoipendezesha mandhari ya jiji letu.

Pakijengwa na pale Jangwani kisasa jiji la Dar litakuwa na uzuri fulani ambao haukuwepo kabla.

Tujifunze kuongelea ya kwetu katika namna zilizo chanya.
Hatuna muda wa kutosha wa kujenga nchi kama waliokuwa nao Roma pia tuna faida kubwa ya kuwa na sehemu nyingi sana za kujifunza jinsi ya kujenga na kupanga nchi tofauti na ilivyokuwa kwa Roma. Dunia leo hii ina nyenzo nyingi za taarifa, teknolojia na maarifa kuliko enzi za Roma ya kale hivyo kuna makosa hayategemewi yafanyike na mambo yanatakiwa yaende kwa speed ya supersonic.
 
😅😅😅

Mwendokasi ikikamilika patavutia kiasi, kiukweli airport tu ndio pazuri kwingine kote hoiiiii!

Mleta mada haujafika sehemu ambayo kila mtu ana spika na kila spika inaongea at the same time.

Chaos.
 
Hatuna muda wa kutosha wa kujenga nchi kama waliokuwa nao Roma pia tuna faida kubwa ya kuwa na sehemu nyingi sana za kujifunza jinsi ya kujenga na kupanga nchi tofauti na ilivyokuwa kwa Roma. Dunia leo hii ina nyenzo nyingi za taarifa, teknolojia na maarifa kuliko enzi za Roma ya kale hivyo kuna makosa hayategemewi yafanyike na mambo yanatakiwa yaende kwa speed ya supersonic.
Kukosoa ni kazi nyepesi, wamepita wakosoaji wengi wanaopewa nafasi serikalini huishia kuendeleza madudu yale yale ya watangulizi wao.
 
Back
Top Bottom