Ukishuka Airport Dar ukapita barabara kuu unaona jinsi nchi na watu wake walivyochoka. Viongozi mnafeli wapi?

Mji mzima sahivi barabara zimebomolewa wanajenga mwendokasi sasa ukisema ulalamike pengine hujui kinachoendelea ila pia usifananishe tz na USA bado isee.
Akili za kisiasa zinamtesa mleta mada. Hawezi kuongelea treni ya kisasa kutoka Dar kwenda Mwanza. Kajikitq kwenye negativity tu.
 
Lakini pia Marekani kufanyika "land of opportunity" na kuwekewa mazingira ya American Dream ni juhudi za dhati za raia wote na founding fathers wao,
 
Ongelea mambo kwa ujumla na ukubwa wake, usichukue tumifano tudogo tudogo twa hapa na pale.
 
Marekani miaka ya 1800 ilikuwa inaishi kwa mipango miji,
 
Mimi mwaka huu nilienda mwanza takribani miaka 10 ilikua imepita Ila nikaona pamechoka mbaya..

Kuhusu airport dar yes hayo maeneo ni aibu kwa kweli still we have a long way to go (NO POVERTY IS HARD TO FIGHT THAN IGNORANCE) πŸ˜”
Hata ukiwa masikini una nguo kuukuu tu basi jitihadi uzifue, yani hata pamoja na hizo nyumba za mabati ya kutu basi hata serikali ingesimamia zijengwe kwa mpangalio na muelekeo maalumu, kuwe na barabara pamoja na sewage system za kueleweka. Ni gharama ndogo sana kuwapanga watu wakae kwa mpangilio.
 
Town pesa ipo mfano huku dar ni Jambo la kawaida kutumia usafir (transport cost 10,000 + chakula let say 4000 + per day easy..

Rent haipungui 50,000+ Bado bill za maji , umeme na taka..

Mkuu uwe na heshima na vijana wa mjini (mawinga)

Huko kijijini unajenga nyumba ya udongo au choma unaezeka nyasi (mabati ya Simba).

Huko kijijini usipo jipanga mwaka mzima unaweza usiwe na Pato hata la 4m maana taarifa research zinasema mnaishi Chini ya 1700 kwa siku..

Still vijana wengi Wana opt Bora Mara 100 kubakia mjini na kuteseka kuliko huko kijijini ( bush)
 
Umeongea jambo la msingi sana

Nyumba za zamani za ilala na Magomeni haikuwa nzuri kama za Oysterbay, lakini Mkoloni wa Kiingereza alipanga vizuri maeneo hayo ya waswahili ( yaani Ilala 'na Magomeni). Lakini serikali zetu za sasa zimefeli mno kwenye kufanya vitu kwa mpangilio
 
Kwa Kweli UMASKINI hufanya nguo ziwe very busy..

Ukijumlisha unakua na nguo chache na zikiwa busy ndio zinapauka kwa Kasi SANAA (maana zitafuliwa na kutumika Mara kwa Mara bila mapumziko)

NB.
Smartness huficha UMASKINI
 
Lakini pia Marekani kufanyika "land of opportunity" na kuwekewa mazingira ya American Dream ni juhudi za dhati za raia wote na founding fathers wao,
Naam,

Nimesisitiza kujikita kwenye kuendeleza nchi bila kuonekana tunanyanyapaa watu wa nyumbani. Hususan wananchibwa kawaida ambao mostly ni wahanga wa mifumo wasiyo na nguvu sana za kuibadili.

Hilo litatengeneza vita ya watu wa nyumbani na wa nje, ambayo haitasaidia watu wa nyumbani wala wa nje.
 
Ongelea mambo kwa ujumla na ukubwa wake, usichukue tumifano tudogo tudogo twa hapa na pale.
Tuachane na hii hulka ya kuidogosha Afrika na Tanzania kwa ujumla. Inaacha makovu mabaya vichwani mwa vijana wadogo wanaingia kwenye maisha wakiwa na mtazamo wenye hasira kwenye kila linalofanywa na serikali.
 
Marekani miaka ya 1800 ilikuwa inaishi kwa mipango miji,
View attachment 3058546
Roma haikujengwa ndani ya siku moja. Kuna mabadiliko hata sasa hapa Dar.

Tazama namna lile daraja lililojengwa pale bandarini zamani pakijulikana kama BP ukiwa unatokea kariakoo namna linavyoipendezesha mandhari ya jiji letu.

Pakijengwa na pale Jangwani kisasa jiji la Dar litakuwa na uzuri fulani ambao haukuwepo kabla.

Tujifunze kuongelea ya kwetu katika namna zilizo chanya.
 
Umenikumbusha Ile picha iliyo pigwa na AL AHLY waliipiga kwa Aerial 🚑 photography

Wakaonyesha mandhari ya uwanja wa taifa na viunga vyake mabati yalivyo kua yamechoka
 
Hatuna muda wa kutosha wa kujenga nchi kama waliokuwa nao Roma pia tuna faida kubwa ya kuwa na sehemu nyingi sana za kujifunza jinsi ya kujenga na kupanga nchi tofauti na ilivyokuwa kwa Roma. Dunia leo hii ina nyenzo nyingi za taarifa, teknolojia na maarifa kuliko enzi za Roma ya kale hivyo kuna makosa hayategemewi yafanyike na mambo yanatakiwa yaende kwa speed ya supersonic.
 
πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…

Mwendokasi ikikamilika patavutia kiasi, kiukweli airport tu ndio pazuri kwingine kote hoiiiii!

Mleta mada haujafika sehemu ambayo kila mtu ana spika na kila spika inaongea at the same time.

Chaos.
 
Kukosoa ni kazi nyepesi, wamepita wakosoaji wengi wanaopewa nafasi serikalini huishia kuendeleza madudu yale yale ya watangulizi wao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…