Ukishuka Airport Dar ukapita barabara kuu unaona jinsi nchi na watu wake walivyochoka. Viongozi mnafeli wapi?

Ukishuka Airport Dar ukapita barabara kuu unaona jinsi nchi na watu wake walivyochoka. Viongozi mnafeli wapi?

Ndio maana mkuu wa mkoa wakati ule alisema bomoeni vibanda na ni marufuku kufanya biashara maeneo hayo.
Mnawatia aibu.
Inatakiwa mgeni akifika tuonekane wote tuna pesa.
 
Mod naomba univumilie niteme nyongo!.

Yaani kama ulitoka nje ukashuka airport Dara miaka 8 iliyopita, ukashuka miaka mitano iliyopita na ukashuka leo, unakutana na barabara ni lami siyo lami, vumbi tupu, makorongo matupu, mitaro ya waziwazi iliyojaa maji machafu, yaani kanchi kamechoka kamechoka kwelikweli. Hivi nyie watawala mnaoshinda kwenye ndege kila kukicha mnnaenda kwenye nchi za watu huwa hamuoni huko kwa wenzenu kukoje?

Yaani just imagine, barabara ya mwanzo ambayo wageni wanapita kabla hawajaenda popote nchini wanakutana na kituko cha barabara ile. First impression inayopatikana hapo ni ya kanchi masikini ka watu masikini, ka viongozi hopeless!

Yaani hako kabarabara kako hivyohivyo miaka nenda rudi pachovu choka mbaya, yaani vagalanti hovyohovyo.

Nyie watawala mnatutia aibu, mnajionaje fahari kuwa viongozi msioweza kudeal na issues ndogo namna hiyo kama hiyo ya kuipa nchi "reception" ya maana?

Kwa kweli aibu naona mimi.

Miviongozi kazi kujilimbikizia mali, kutwa kucha kwenye ndege, misafara ya mamia ya magari, lakini barabara tu ya airport wanayopita daily kwenda huko nje ya nchi kuuza sura imewashinda!. Sijui hii mijitu ikoje?

Kila siku ukipita maendo hayo unakutana na miradi uchwara as if wanajenga, lakini miaka yote huo ujenzi huwa hauishi, ni magumashi, hakuna lolote la maana linaloonekana!. Yaani choka mbaya choka mbaya, hovyo hovyo kabisa!.

Nyie viongozi wa nchi hii badilikeni. Incompentency yenu ndo inatufanya sisi huko duniani tuonekane kama nyani tu. Nchi zina marasilimali kibao halafu unakutana na kinchi kimechokaaa. Hii inakuwaje.

Yaani unapita barabarabani pembeni unakutana na mamitaro makubwaaa hayajafunikwa ambayo kwanza ukifuatilia vizuri hayana exit ya mitoni wala sewage system yoyote ya maana, yaani yapo ceremonial tu.

Mamitaro makubwa hayajafunikiwa na yamekaa kama mahandaki ya vita kuu ya kwanza ya dunia. Hivi hawa wenye dhamana ya utawala wakienda huko kwa wenzetu wanajifunza chochote kweli?.

Achilia mbali hilo. Ukishuka airport njiani unakutana na wabongo wamechoka mbaya, hali ngumu, wamekonda, wameweka vimizigo vyao barabarani masikini wanahustle. Hii iko hivyo miaka nenda rudi. Wakati huo kuna watu wanaitafuna nchi hii kwa kula na kusaza. Ni lini wansnchi wataanza kula matunda na mema ya nchi?. Watawala wanawaza siasa tu, siasa tu.

Pia soma
- Kwanini Watanzania na Tanzania ni masikini pamoja na rasilimali (resources) tulizonazo?
Achana na kushuka. Ukifika nyakati za usiku ukiwa angani angalia chini yani mitaa haeleweki nyumba zmesongamana. Hovyo hovyo
 
hata ukienda mkoani tu, ukakaa muda fulani, kukirudi dsm unaona namna raia barabarani wanavyotembea wakiwa wamechoka, wamejaa mawazo,wamekata tamaa, wana sura za umasikini na hasira, joto daladala dart everything, ni kwamba wamevurugwa mbaya. na ukitaka kuwafahamu vizuri mchokoze mmoja uone hasira atakazomalizia kwako.
Baada ya muda mrefu kupita miaka 10 juzi hapa nikaenda mwanza nikakuta pamechoka 😔😔
 
Ndio maana mkuu wa mkoa wakati ule alisema bomoeni vibanda na ni marufuku kufanya biashara maeneo hayo.
Mnawatia aibu.
Inatakiwa mgeni akifika tuonekane wote tuna pesa.
Sio suala la kuonekana wenye pesa, hata kama uwezo wa raia ni kujenga mabanda basi wasimamiwe wayajenge hayo mabanda kwenye mpango unaoleweka.
 
sura za watu wa mwanza zina furaha na matumaini kuiliko za hawa wa hapa dsm. i tell you.
Mikoa mingi tanzania hata ukienda vijijini huko utakuta watu japo ni masikini lakini wana nyuso za furaha zilizojaa matumaini. Yaani utaona nyuso angavu.

Njoo dar sasa. Kila unaemuangalia usoni yaani ni amejichokea, anaonekana amekata tamaa, ana hasira, kakunja sura. Kila mtu kakaa kishari shari utadhani yuko vitani huko south sudan.
 
Mikoa mingi tanzania hata ukienda vijijini huko utakuta watu japo ni masikini lakini wana nyuso za furaha zilizojaa matumaini. Yaani utaona nyuso angavu.

Njoo dar sasa. Kila unaemuangalia usoni yaani ni amejichokea, anaonekana amekata tamaa, ana hasira, kakunja sura. Kila mtu kakaa kishari shari utadhani yuko vitani huko south sudan.
Hivyo ndivyo mlipuko hujengwa. Siku moja sura hizo hizo ndizo zitakazo zaa purukushani ya kutisha.
 
Naunga mkono hoja. Tuwasaidie mainjinia wetu sijui Tarura au Tanroads nchi zote afrika barabara ya kuelekea airport inakuwaga haina usumbufu haina foleni. Jengeni barabara ya juu from kamata tu airport na from buguruni tu airport ya juu kwa juu.

Huwa viongozi kila siku manenda nchi za nje hamuwezi kuleta ideas za mazingira mazuri.
 
Lucas Mwashambwa njoo unyooshe maelezo huku
Kazi yake kuponda maticha tuu,kamwashambwa hakana kitu hata hapo Halifax Kuna flyover kama zote Kenyewe kamekazana na mada Moja tuu kajinga sana haka ka pot,niseme tuu tuko hovyo,hata pale Arusha ni kama kijiji,ukienda Moshi ni kama forgotten town ni hovyo,ukienda.magogoni wasanaii wote wameishiwa sehemu ya kupiga picha ni vigorofa pacha vya bandari pekeeake hakuna jingine,vijitu vichafu mpaka vinasahau kuoga,Bongo uchwara sana alafu watu wale wanaleta shida na kijani yao.as if wako ok kumbe majanga,chama choka wanauza Hadi bandari
 
Naunga mkono hoja. Tuwasaidie mainjinia wetu sijui Tarura au Tanroads nchi zote afrika barabara ya kuelekea airport inakuwaga haina usumbufu haina foleni. Jengeni barabara ya juu from kamata tu airport na from buguruni tu airport ya juu kwa juu.

Huwa viongozi kila siku manenda nchi za nje hamuwezi kuleta ideas za mazingira mazuri.
Hawa muda wote wanawaza jinsi ya kuiba kura tu,ovyo sana hii mijitu
 
Mikoa mingi tanzania hata ukienda vijijini huko utakuta watu japo ni masikini lakini wana nyuso za furaha zilizojaa matumaini. Yaani utaona nyuso angavu.

Njoo dar sasa. Kila unaemuangalia usoni yaani ni amejichokea, anaonekana amekata tamaa, ana hasira, kakunja sura. Kila mtu kakaa kishari shari utadhani yuko vitani huko south sudan.
Watu wengi wa Dar hapa ni masikitiko makubwa matumaini yamepotea kabisa usoni.
 
Yaani kama ulitoka nje ukashuka airport Dar miaka 8 iliyopita, ukashuka miaka mitano iliyopita na ukashuka leo, unakutana na barabara ni lami siyo lami, vumbi tupu, makorongo matupu, mitaro ya waziwazi iliyojaa maji machafu, yaani kanchi kamechoka kamechoka kwelikweli. Hivi nyie watawala mnaoshinda kwenye ndege kila kukicha mnnaenda kwenye nchi za watu huwa hamuoni huko kwa wenzenu kukoje?

Yaani just imagine, barabara ya mwanzo ambayo wageni wanapita kabla hawajaenda popote nchini wanakutana na kituko cha barabara ile. First impression inayopatikana hapo ni ya kanchi masikini ka watu masikini, ka viongozi hopeless!

Yaani hako kabarabara kako hivyohivyo miaka nenda rudi pachovu choka mbaya, yaani vagalanti hovyohovyo.

Nyie watawala mnatutia aibu, mnajionaje fahari kuwa viongozi msioweza kudeal na issues ndogo namna hiyo kama hiyo ya kuipa nchi "reception" ya maana?

Kwa kweli aibu naona mimi.

Miviongozi kazi kujilimbikizia mali, kutwa kucha kwenye ndege, misafara ya mamia ya magari, lakini barabara tu ya airport wanayopita daily kwenda huko nje ya nchi kuuza sura imewashinda!. Sijui hii mijitu ikoje?

Kila siku ukipita maendo hayo unakutana na miradi uchwara as if wanajenga, lakini miaka yote huo ujenzi huwa hauishi, ni magumashi, hakuna lolote la maana linaloonekana!. Yaani choka mbaya choka mbaya, hovyo hovyo kabisa!.

Nyie viongozi wa nchi hii badilikeni. Incompentency yenu ndo inatufanya sisi huko duniani tuonekane kama nyani tu. Nchi zina marasilimali kibao halafu unakutana na kinchi kimechokaaa. Hii inakuwaje.

Yaani unapita barabarabani pembeni unakutana na mamitaro makubwaaa hayajafunikwa ambayo kwanza ukifuatilia vizuri hayana exit ya mitoni wala sewage system yoyote ya maana, yaani yapo ceremonial tu.

Mamitaro makubwa hayajafunikiwa na yamekaa kama mahandaki ya vita kuu ya kwanza ya dunia. Hivi hawa wenye dhamana ya utawala wakienda huko kwa wenzetu wanajifunza chochote kweli?.

Achilia mbali hilo. Ukishuka airport njiani unakutana na wabongo wamechoka mbaya, hali ngumu, wamekonda, wameweka vimizigo vyao barabarani masikini wanahustle. Hii iko hivyo miaka nenda rudi. Wakati huo kuna watu wanaitafuna nchi hii kwa kula na kusaza. Ni lini wansnchi wataanza kula matunda na mema ya nchi?. Watawala wanawaza siasa tu, siasa tu.

Pia soma
- Kwanini Watanzania na Tanzania ni masikini pamoja na rasilimali (resources) tulizonazo?
Waambie wasubiri tunakopa wata-NENEPA.
 
Back
Top Bottom