Ukishuka Airport Dar ukapita barabara kuu unaona jinsi nchi na watu wake walivyochoka. Viongozi mnafeli wapi?

Nchi ya watu wachovu.
Viongozi ni kana kwamba wanaona fahari kuongoza wachovu.
Wako busy kujijenga wao na familia zao.
Ndiyo maana nikiwaonaga hata wanaoteuliwa kushika nafasi mbalimbali, ni wale wenye kilo nyingi (hadi wengine wanaambiwa wapunguze kidogo!).
Ooh Tanzania nchi yangu!
 
Nitarudi kuipopoa nchi yangu
 
Mliosomeshwa vizuri wote mmekimbia

Mmeacha waganga njaa

What do you expect ?
 
Tatizo ni Ccm
 
Hata barabara zinajengwa kihuni. Barabara zote za mitaa baada ya mwaka tangu zijengwe zinaanza kubomoka na zinaachwa hivyo hivyo. Wanajenga barabara kisiasa ili wazifungue wakati wa uchaguzi. Wanajua wakijenga haraka haraka na zikaanza kufanya kazi hadi ikifika uchaguzi mkuu zitakuwa zimeharibika hivyo watakosa cha kuwadanganyia watu.
 
Ukizingatia Nyerere road ni vumbi tupu,watu wanaotumia barabara ile wanakuwa na vumbi as if wametoka kigoma,juzi kati kuna boda boda alinichukulia kimzigo airport,daah kufika mjini anaonekana meno tuπŸ˜€.....ujenzi wa pale haukustahili kuwa slow vile,ilipaswa iwe day and night...... kwasababu pale ndiyo lango la nchi
 
Uko sahihi,unajiuliza wanafeli wapi? Ni hapa mnapotumia matrilioni ya hela kuwekeza kwenye liabilities badala ya sekta ambazo Zina watu wengi.πŸ˜†πŸ˜†πŸ˜†πŸ”₯πŸ‘‡πŸ‘‡


Samia ndio kajaribu kugusa ila Kwa kuwa Kuna rundo la wajinga hawaoni hili.

Hii Nchi inatakiwa tupate Rais aliyesomea Uchumi ndio itakwamuliwa.

Maisha ya Watanzania ni ya kifukara sana Wala sio Siri ndio uhalisia wenyewe
 
Ndio maana mkuu wa mkoa wakati ule alisema bomoeni vibanda na ni marufuku kufanya biashara maeneo hayo.
Mnawatia aibu.
Inatakiwa mgeni akifika tuonekane wote tuna pesa.
Na huyo Mgeni mwenyewe ana pesa!? Siyo kaja kuchuma,wakati sisi tunaamini kwenye falasafa ya Mgeni njoo mwenyeji apone!!
 
Tanzania hii ni Nchi ya shaghalabaghala ambayo jamii yake haijali,haithamini Wala haijitambui.

Swala sio viongozi Baki aina ya jamii ambayo haiana Ustaarabu ndio matokeo yake haya sasa.

Athari za ujamaa na uswahili zitatutafuna sana.

Nilisikitika kuona Jamaa mmja wa Burundi anajenga apartments nzuri sana kule Bujumbura nikalinganisha na vile vijumba vya Iyumbu Dom nikajua tuna Nchi ya hovyo sana.
 
Lucas Mwashambwa njoo unyooshe maelezo huku
Lucas ndio mwenye dhamana ya kujenga hii Nchi na nyie mnakuwa mnafanya nini?

Kwanza mipango ya Nchi hii Huwa haiko coercive yaani ni Bora liende.Mfano unakuta mtu anajua hii ni Barabara anatakiwa asimike Bomba za maji ila hafuati usahihi unatakiwa ndio maana unakuta mradi ukianzanaanza kuingia gharama zingine za kuhamishwa miundombinu ambayo ilitakiwa kuwa imewekwa sehemu inapostahili ila hawakufanya hivyo.
 
Kusema ukweli Dar hasa kama huna kipato unaishi kwa stress na mahangaiko kuliko mtu aliyeko Sengerema kijijini huko!
Utafika uliofanyika Kenya Unaonesha watu wa countryside wanatajirika kuliko walioko Miji mikubwa,the likes na hapa Tanzania na Dar yenu.

Kwa Sasa kijjaa wa Mkoani anaelima ana nafasi ya kuwa na maisha mazuri kuliko wa Dar na ndio maana Miji ya Mikoani hakuna mabanda kama ya huko Dar πŸ˜†πŸ˜†πŸ˜†πŸ˜†πŸ˜†
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…