Ukisikiliza audio ya kocha wa Yanga, ameongea ukweli mtupu. Uongozi wa Yanga haupendi kuambiwa ukweli

Ukisikiliza audio ya kocha wa Yanga, ameongea ukweli mtupu. Uongozi wa Yanga haupendi kuambiwa ukweli

You can't be serious!! Yaani viwanja vya mikoani wamekuwa wakilazimisha mpira uchezwe kwa sababu za kisiasa au ni kwa sababu ndo viwanja vyenyewe vilivyopo?!

Hivi mtu ambae amefundisha mpira DRC, Rwanda, Gabon na hata Kenya bado alienda Tanzania huku akiamini viwanja vya Tz vitakuwa bora sana ukilinganisha na nchi zingine alizowahi kufundisha soka?! Ina maana alitarajia kukuta vyumba bora vya kubadilishia kuliko alivyoviona kwenye hizo nchi zingine?

According to Wikipedia, hapa chini ndio timu ambazo Luc Eymael amezifundisha kwa nyakati tofauti tofauti!

Over the past 10 years, hakuna club yoyote ambayo amekaa kwa zaidi ya mwaka mmoja... hivi huoni kwamba huyo mtu ana matatizo?! To be honest, mimi binafsi niliwashangaa sana Yanga kumchukua mtu mwenye CV ya aina hiyo! Hivi hata wewe kama ni HR, unapokea CV ya mtu ambae hatulii na ofisi moja; huwezi kuhisi there's something wrong with him/her?!

Na hilo wala halishangazi kwa sababi Agent mmoja kutoka South Africa amesema wazi kwamba:-
According to tovuti ya kickoff.com, huyo Agent anamfahamu vizuri Eymael kwa sababu amewahi kufanya nae kazi!

Kwahiyo mengine aliyosema ni porojo tu kwa sababu Eymael sio mgeni wa viwanja vya hovyo kwa sababu sehemu kubwa ya career yake amefanyia Afrika, tena South of Sahara!
Nyinyi ndio walewale hivi unapomchezesha mchezaji kwenye viwanja vibovu unategemea nini hujali afya ya mchezaji. Kwanza hata mpira wenyewe hauna ladha ya kuangalia ni siasa ndio inafanya mpira uchezwe viwanja vibovu jiulize ni viwanja vingapi vya mkoani vinaweza kupitishwa kuchezewa michuano ya kimataifa
 
Nyinyi ndio walewale hivi unapomchezesha mchezaji kwenye viwanja vibovu unategemea nini hujali afya ya mchezaji. Kwanza hata mpira wenyewe hauna ladha ya kuangalia ni siasa ndio inafanya mpira uchezwe viwanja vibovu jiulize ni viwanja vingapi vya mkoani vinaweza kupitishwa kuchezewa michuano ya kimataifa
Wakati unadai sie ndo wale wale; jibu maswali niliyokuuliza:

1. Wakati anafikiria kufundisha soka Tanzania alidhani viwanja ni kama vya Ulaya wakati tayari alishakuwa na uzoefu na viwanja vya Afrika?!

2. Suala la viwanja Yanga anahusika nalo vp?!

3. Na huko kwingine ambako na kwenyewe hakuwahi kutulia, ni kipi kilimwondoa?! Viwanja vibovu, wi-fi, gari au nini hasa?!

NOTE: Wakati unadai mie ndo wale wale tu, ninachoona wewe ndie wale wale tu... watu mnaojaribu kutafuta sababu za ku-justify lugha za hovyo za Eymael!

Na unathibnitisha kwamba nawe ni wale wale tu kwa sababu nimekuwekea maelezo hadi ya Agent kutoka South Africa aliyesema wazi kwamba Luc sio mtu wa kutulia sehemu moja, na hata ukiangalia CV yake inaonesha hivyo!

Sasa na wenzako mnaojaribu kutafuta sababu za ku-justify alichofanya Eymael, unataka kusema wewe ndo unamfahamu sana Luc kuliko mtu ambae amefanya nae kazi, na mtu mwenyewe wala hana ushabiki wa Simba vs Yanga?!

Na wakati mnajaribu ku-justify kwa hoja zisizo na kichwa wala miguu, Luc Eymael mwenyewe anawaambia Yahoo Sports kilichomfanya a-panic ni kwa sababu alikuwa harrassed na shabiki wa:-

Simba.png


Ambapo anaendelea:-

“I didn't go for the interview, just went straight to my hotel. All people were calling me [names] but I did not want to respond.

“Then there is this one guy from Simba who kept harassing me, and I reacted.”
Sasa kama alikuwa harassed na Shabiki wa Simba, how come povu awatolee Yanga, na kuita mashabiki wa Yanga wanabweka kama Monkey or Dogs?

Ajabu ya nchi hii, habari ya Luc Eymael imeripotiwa na media mbalimbali duniani... hadi Uhindini lakini ni Watanzania peke yao ndio wanaojaribu kutafuta sababu za ku-justify kitendo cha Luc Eymael!
 
Nina wasiwasi sana na afya ya akili ya huyo kocha. Anaonekana ni mtu mwenye msongo sana wa mawazo na hili liko wazi pale utakapoamua kusikiliza taratibu ile "audio" bila kuweka ushabiki wa Simba na Yanga. Kwa sababu kachanganya mambo mengi kwenye chungu kimoja. Ukichambua vizuri ametukuna/kutuhumu kuanzia viongozi wa Yanga, viongozi wa TFF, mashabiki wa Yanga, Simba kama timu kwa ujumla wake, chama na serikali (juu ya ubovu wa viwanja vya mpira) na watanzania wote kwa ujumla. Na mbaya zaidi katuletea mpaka mambo yake ya binafsi kuwa mke wake "haienjoy" kuwepo hapa nchini Tanzania. Kimsingi hapa kama huyu kocha angekuwa timamu kichwani hizo tuhuma zake zote angeziwasilisha kwenye uongozi kupitia ripoti yake baada ya ligi kumalizika. Na uongozi baada ya kupata ripoti ya kocha ungefuata taratibu katika kuyatafutia ufumbuzi malalamiko yake kuanzia yale uongozi wenyewe wa Yanga wangemalizana huko ndani, yale TFF na serikali viongozi wangeyawasilisha kimya kimya kwenye ngazi husika huko serikalini na mwisho zile kelele za wanachama/mashabiki hapo ndio kazi ya afisa habari kumalizana na wanachama/mashabiki wa Yanga. Lakini njia ya huyo kocha kubwabwaja kwenye vyombo vya habari moja kwa moja anakuwa sio mstaarabu na hana weledi na kazi yake kwa hiyo hafai kabisa kuwa mwajiriwa kwenye taasisi kubwa kama Yanga.

Kwanza niwapongeze sana viongozi wa Yanga pamoja na baadhi ya mapungufu yao waliyonayo lakini kwa hili wamechukua hatu zinazostahili kwa haraka sana. Hongereni sana viongozi wa Yanga.

Ila suala la huyu kocha na la mchezaji Morison liwazindue sasa viongozi wa Yanga wachukue hatua ya kukaa chini na mdhamini wao GSM. Badala ya mdhamini kuleta kocha au mchezaji na kuja kuwabwagia angalau wakae wajadiliane ili waweze kupata watu sahihi kwa ajili ya kuja kuzipigania "brand" za GSM na Yanga kwa pamoja. Kwa sababu nikiangalia ajira ya kocha na usajili wachezaji mpaka ligi ilipoisha wiki iliyopita naona ni hasara tupu kwa usajili wa wachezaji takribani 20 ukiondoa Haruna Niyozima pekee ndiye mwenye manufaa kwa timu. Na GSM asione aibu ajifunze jinsi Simba inavyopitia mchakato wa kupata makocha kwa kutumia jopo la wataalamu wa ndani wa kina Kayuni, Madadi, na wengineo.

Mwisho vilabu vyetu viwe makini vinaposajili wachezaji hasa wa nje kwani wa ndani wanafahamika tabia zao. Naamini kabisa iwapo "GSM" angefanya "homework" kidogo tu mtandaoni wa kupitia "CV" na habari kuhusiana na Eyamel na Morison hakika asingepata hii hasara na aibu. Siku hizi kila kitu kipo mtandaoni ni suala la kutenga muda tu ili kupata unachokihitaji. Ukiingiza tu jina la mtu zinakuja habari na historia yake yote. Kama mimi mtu wa kawaida tu nikiangalia tu historia na habari za Eyamel na Morison naona ni watu ambao hawafai kuajiriwa mahali kwa malengo ya muda mrefu vipi huyo GSM ambaye ana wataalamu wengi karibu yake (kutokana na aina ya biashara zake) ambao wangeweza kumsaidia kitaalamu kabla hata ya kuwasiliana nao sembuse kumwajiri huyo Eyamel na kumsajili Morison Yanga.
 
Angeongelea tu hayo yanayohusu mazingira magumu ya kazi (usafiri, nyumba, viwanja vibovu, marefarii wabovu au wanapendelea), ingeweza kutosha na pengine hata angepata watetezi wengi tu. Hakuwa na sababu ya kufananisha mashabiki na nyani wakati anajua kuna upepo mbaya wa wabaguzi wengine wa rangi (sio yeye) ambao katika soka wamekuwa wakilitumia sana jina la nyani au kurusha ndizi uwanjani kwa blacks kuwalinganisha na nyani. Hapo ndipo alipochemka, na kwa kweli itamletea matatizo zaidi kama itafika huko juu kwa wenye soka
Kwani uongo??? SASA chura si manyani tu nyieee??
 
Sawa nyani
Habari wadau,

Nimesikiliza Audio ya kocha wa Yanga maneno aliyoyasema ni ya kweli tupu. Mimi ni mwanayanga ila sijasikia sehemu akitutukana.

Viongozi wa Yanga wameibadilisha tafsiri ya maneno ya kocha ili walinde vibarua vyao na kujitetea maovu yao kwa mashabiki.

Kocha amesema anashangaa mashabiki wa Yanga wakiwa wanazomea hovyo hovyo tu kama sio binadamu wenye akili, kama nyani ama mnyama ambaye hana IQ.

Hii viongozi wa Yanga wameibadili na kusema amesema wanaYanga wote ni manyani.

Binafsi nimewai kuona mtu akiambiwa anaongea kama chiriku ila sijawai kuona akisema ameambiwa yeye ni chiriku.

Mtu anaambiwa ana tamaa kama fisi, aimaanishi yeye ameambiwa ni fisi

Viongozi wa yanga wajanja sana, wanajua madudu yao wamemuangushia kocha jumba bovu

Kocha huyu mzungu hajamsajili yikpe wala molinga wala mchezaji yeyote, sasa waliosajili madudu wanamuangushia jumba bovu.

Kwa maneno ya kocha Mkataba wa Yanga na kocha aliambiwa anapewa nyumba nzuri sehemu salama Dar, akaambiwa analipiwa DSTV, akaambiwa atalipiwe wireless internet ila Yanga hawajatimiza hata moja.

Walisema atapewa gari limsaidie usafiri Dar hajapewa.

Viongozi wamejaa uswahili Swahili kocha analalamika.

Sasa why wabadilishe maana.

Hoja inajibiwa kwa hoja, ilipaswa hoja za kocha zijibiwe kwa hoja kama je alitimiziwa masharti ya mkataba wake yote?

Sikiliza audio hapo chini kisha utoe hukumu.

Mchawi ya Yanga ni Msolla, Mkwassa na waswahili wengine.

Pongezi sana kwa Simba na Mo kwa kuachana na Waswahili na kuweka mzulu awaongoze.

 
Kaka siamini kama hili unaongea wewe, hivi Dstv haizidi laki na nusu, unalipwa mshahara Mil 10 unashindwa kujiwekea kweli mpaka usubiri viongozi?
Luc kweli kazingua ila Yanga nayo ibadilike hivi kweli unashindwa hata kumpa kocha DSTV, wifi,gari?
 
Habari wadau,

Nimesikiliza Audio ya kocha wa Yanga maneno aliyoyasema ni ya kweli tupu. Mimi ni mwanayanga ila sijasikia sehemu akitutukana.

Viongozi wa Yanga wameibadilisha tafsiri ya maneno ya kocha ili walinde vibarua vyao na kujitetea maovu yao kwa mashabiki.

Kocha amesema anashangaa mashabiki wa Yanga wakiwa wanazomea hovyo hovyo tu kama sio binadamu wenye akili, kama nyani ama mnyama ambaye hana IQ.

Hii viongozi wa Yanga wameibadili na kusema amesema wanaYanga wote ni manyani.

Binafsi nimewai kuona mtu akiambiwa anaongea kama chiriku ila sijawai kuona akisema ameambiwa yeye ni chiriku.

Mtu anaambiwa ana tamaa kama fisi, aimaanishi yeye ameambiwa ni fisi

Viongozi wa yanga wajanja sana, wanajua madudu yao wamemuangushia kocha jumba bovu

Kocha huyu mzungu hajamsajili yikpe wala molinga wala mchezaji yeyote, sasa waliosajili madudu wanamuangushia jumba bovu.

Kwa maneno ya kocha Mkataba wa Yanga na kocha aliambiwa anapewa nyumba nzuri sehemu salama Dar, akaambiwa analipiwa DSTV, akaambiwa atalipiwe wireless internet ila Yanga hawajatimiza hata moja.

Walisema atapewa gari limsaidie usafiri Dar hajapewa.

Viongozi wamejaa uswahili Swahili kocha analalamika.

Sasa why wabadilishe maana.

Hoja inajibiwa kwa hoja, ilipaswa hoja za kocha zijibiwe kwa hoja kama je alitimiziwa masharti ya mkataba wake yote?

Sikiliza audio hapo chini kisha utoe hukumu.

Mchawi ya Yanga ni Msolla, Mkwassa na waswahili wengine.

Pongezi sana kwa Simba na Mo kwa kuachana na Waswahili na kuweka mzulu awaongoze.


Kwa hiyo hata kauli yake kuwa TFF ipo kwa ajili ya Simba ni sawa siyo?!?!?!
 
Kwanza inabdi ujue alikuwa na sababu gani kuwaa attack mashabiki kwa maneno makali km hawajaelimika, iQ zao ndgo km manyani blabla nyingi wakati ugomvi wake yeye ni kati ya viongoz wa timu na yeye na sio mashabiki. Kwanza hana busara principal za uongozi hajui ni mbaguzi dhahiri halina kukwepesha chochote. Na pia nataka nikujuze mm ni shabiki wa Simba tena damu ila apa nazungumza km muafrika mtanzania. Hajapangiwa nyumba,gari,dstv bla bla zote ila lakujiuliza mashabiki wanahusika vipi hapo je ndio waliotakiwa walipe hayo mahitaji yake au...kwa maoni yangu kakosea Sana tena sio kawakosea yanga tuu, kawakosea watanzania pia na waafrika kwa ujumla. Umaskini wetu usiwe sababu ya mpuuzi mmoja kutuongelea maneno machafu alafu avumiliwe.
Huyu kocha bwege sana
 
Back
Top Bottom