Ukitaka kujua ufisadi wa CCM angalia kiasi hiki walichotoa USAID mwaka 2023. Kwanini bado tunalipia huduma za afya?

Ukitaka kujua ufisadi wa CCM angalia kiasi hiki walichotoa USAID mwaka 2023. Kwanini bado tunalipia huduma za afya?

Saa nyingine hizi huwa sio fedha kama fedha

Marekani ni ngumu sana kukupatia fedha, anachofanya ni kukupa ARV au chanjo zikiwa overpriced ndo maana utaona kwamba wametoa kiasi kikubwa cha pesa ila sivyo ilivyo

Same same wanachofanyiwa Ukraine, wanapewa silaha obsolete halafu Marekani wanaweka high price ionekane ni mabilioni ya fedha

Unaelewa maana ya neno DISBURSEMENT au tukurudishe shule?
 
Wakuu,

Wakati napita pita zangu mitandaoni nimkeutana na hili bandiko linaloonesha kiasi cha pesa ambacho Marekani iliipa Tanzania mwaka 2023 kama msaada.

Inawezekanaje kwamba tulipewa msaada wa USD Milion 512 ndani ya mwaka mmoja kwenye sekta ya afya pekee alafu bado wagonjwa wanalala chini? Hizi hela zilienda wapi?

Hii chati inaonesha kuwa kwa mwaka 2023 Tanzania ndio iliongoza kupokea fedha nyingi Afrika kutoka Marekani kwenye sekta ya Afya, hizi zilienda kwa nani?

Yaani Mkuu wa Mkoa anajitokeza hadharani kusema wanawake ambao hawana hela ya kununua gloves wakajifungulie nyumbani meanwhile kuna kiasi kingi hiki cha fedha tulipewa na Marekani?

Naomba kusaidiwa nani alikuwa ni Waziri wa Afya mwaka 2023 na kwanini bado tunalipia huduma za afya wakati tulishapokea kiasi kingi hivi cha pesa kutoka kwa wahisani.

Inawezekanaje kwamba tulipewa msaada wa USD Milion 512 ndani ya mwaka mmoja kwenye sekta ya afya pekee alafu bado wagonjwa wanalala chini? Hizi hela zilienda wapi?🥺🥺😭😭
 
Chama chakavu kimezitumia hizo pesa kuwanunulia makatibu wao waenezi wa wilaya zote V8 na nyingine wametumia kununulia mabasi ya kijani, boda boda na bajaji kwa ajili ya kusomba wananchi kuwapeleka kwenye mikutano wakati wa kampeni za uchaguzi wakati huo huo wanaomba msaada kutoka Japan kwa ajili kutengenezea matundu ya vyoo mashuleni. Aibu!
 
Inawezekana wakasema wametoa hicho kiasi lakini kwa masharti kwamba asilimia fulani ielekezwe kwenye kampeni fulani.

Mfano kama zile kampeni za dondosha mkono sweta.

Au asilimia fulani itafanya trainings kwa kipindi hiki mpaka hiki.

Au hii asilimia nyingine mtanunua kondomu (ambazo ndiyo unazikuta vyooni za bure)

So siyo kwamba unagewa mpunga ujipangie matumizi
 
Kuna muda unaanza kuona anayofanya Trump ni sawa.

Hivi pesa yote hii si ingetosha kumaliza masuala ya afya
Hv Kuna wakati mmemuona trump hayuko sawa, kama upo wakati huo basi jueni mna matatizo makubwa mno, haiwezekani miaka 60 ya uhuru nchi ambayo imebarikiwa kila aina ya rasirimali bado haziwezi hata kujenga matundu ya choo..achilia mbali madawati ya wanafumzi, wanachoweza ni kuhonga rasirimali Kwa wageni Kwa mikataba ya kipuuzi, pamoja na kumiminiwa misaada lkn wamekosa vipaumbele na kuendekeza anasa za watawala huku huduma za kijamii zikizorota! Hata kama ni wewe unatoka hela zako kumsaidia mtu unaedhani ni maskini lkn kumbe mtu huyo anatumia kidogo anachokipata kuhonga na kunywa pombe sijui kama utaendelea kutoa msaada.
 
Kuna muda unaanza kuona anayofanya Trump ni sawa.

Hivi pesa yote hii si ingetosha kumaliza masuala ya afya
Mimi nimefanyakazi kwenye USAID Funded Projects pesa nyingi hubaki huko huko Marekani. Kwanza viongozi wa ngazi za juu za project lazima wawe Wamarekani na wanalimpwa mara 10 zaidi ya Mtanzania pia kuna wafanyakazi ambao wako based US lakini wanakuwa wanalipwa pesa hizo za project na pesa hizo zinalipwa kwenye account za mhusika huko huko USA, vifaa vyote vinatoka Marekani kwa bei ya juu sana. Pia mkiwa mnasafiri lazima mtumie ndege za US flag. Hivyo pesa ambazo zitakuwa zimewanufaisha watz kati ya hizo ni asilimia robo tu lakini kwenye matangazo wanatoa pesa zote wameleta TZ. Wamarekani ni matapeli sana.
 
Inawezekana wakasema wametoa hicho kiasi lakini kwa masharti kwamba asilimia fulani ielekezwe kwenye kampeni fulani.

Mfano kama zile kampeni za dondosha mkono sweta.

Au asilimia fulani itafanya trainings kwa kipindi hiki mpaka hiki.

Au hii asilimia nyingine mtanunua kondomu (ambazo ndiyo unazikuta vyooni za bure)

So siyo kwamba unagewa mpunga ujipangie matumizi

Hata kama

Yaani Trilioni 1 zote zitumike kwenye training na kununulia condoms?

Hizo hela zote zinazobaki zinaenda wapi?
 
Kilichokereketa kuliko yote ni kuiondoa bima ya afya ya watoto ambao hawafanyi kazi wala kibarua chochote..........hii ni mbaya sana..........sasa laana ya haya yote wacha Trump asimamie ukucha .........ili fukuto lake liwatoe madarakani kwa kujisahau
 
Back
Top Bottom