Ukitaka kujua Watanzania wajinga nenda Facebook kaangalie wanavyokomenti kwenye habari muhimu na habari za udaku

Lisuu aliniboa sana alivyoanza kumpinga Magu. Magu alikuwa sahihi sana. Lisu alipewa hela apingane na anachofanya magu. Toka pale niliachana na chadema na genge lake. Sishabikii chama chochote. Waache wamalizane tu.
 
Kule kuna watu wamenunuliwa na kuwekewa bando na kijana,kwamba akiongea apongezwe na kusifiwa hata akiongea yasiyoeleweka.Ukimponda kijana watakuponda haswa.Ndio maana vijana ni wa kushauri wajitambue na kujua kesho yao.
 
Ni upepo tu, kwa wabongo ikitoka connection moja tu hawa washasahau kila kitu kama kuku wa kienyeji na maisha yanaendelea. Ukiwa serious sana na wabongo utateseka sana wakati wenyewe hawana hata habare!
 
Uganda? 😂😂😂
 
Haha, kwanza kuhusu akili hili si suala la ukabila wala ukanda akili ni Tunu ya mtu binafsi, inachangiwa na uelewa wa vitu upambanuzi na kutafakari, watanzania ni watu wenye brain nzuri mno na wapo na reasoning nzuri, haimaanishi kukaa kimya kwa watanzania ndy ujinga wao.

Najua umeangalia ujasiri wa wakenya na wauganda juu ya kuzipinga Serikali zao pale ambapo kuna kitu hakiendi sawa, watanzania wanafikra pana ndy mana hadi leo amani ipo na utulivu licha ya mambo ya kutatanisha yanayotokea kila siku, wananchi wa Tanzania wanatamani kutumia njia bora ambayo haitosababisha vifo, majeraa, njaa, wala vita kwa maslahi ya maisha ya vizazi vijavyo.

Tatizo kubwa ni namna ya kupata majibu ya maswali magumu yaliyopo kwa watanzania.
Hapa kuna umuhimu wa kushirikiana na taasisi za haki za binadamu ili kuweza kuzungumza kwa amani na kupata masuluhisho ya matatizo yetu wala sio kustrike then baadae ndiyo tutambulike kwamba tunaakili sana kwasababu tuna ujasiri wa kuichallenge serikali na kuitishia kuiondoa madarakani.

We are very intelligent people as Tanzanians.
Na tutapata njia bora kuliko mataifa mengine katika kutatua matatizo yetu naamini hivyo.

Huu ndiyo wakati wa kutumia NGOs kutoa elimu juu ya haki ya binadamu na wananchi wote kwa ujumla na kuunda mifumo mizuri ya kuhoji serikali na kutatua matatizo yetu peacefully, habari za vita na maandamano tuwaachie wengine.

Nyerere kwa kutumia maarifa alimuondoa Muingereza kwenye nchi hii, bila bunduki wala panga ni kwa maarifa tu na kutumia majukwaa husika, sasa kwanini akili zetu tuzielekezee kwenye matendo kama ya wakenya na wauganda?
 
Tanzania taifa la misukule na maiti kama Jomo Kenyatta alivyowahi sema , yule mzee aliona mbali sana .
Humu tz binadamu ni wachache , kuna maiti na misukule
 
Tuna kizazi chenye upeo mdogo sana ndugu.
 
Yaani hilo na mimi nilishalisema nyuma. Kwa kweli ukisoma comments za watu kwenye issue mbalimbali unagundua mengi hasa kwenye uwezo wao wa kumake a case, uwezo wao wa kuelewa hata issues ndogo tu, roho zao mbaya, wivu, kutokuwa serious na mambo mengi. Ni hatari kwa kweli.Ila kuna magroup yaliyoenda shule kwa kweli ukisoma urgument zao wewe mwenyewe unakubali.
 
Wat do u nou abt propaganda?
 
Hivi alikoswa koswa vipi?
 
Yaani wengi ni kama matahira vile .
Hasara kwa taifa.
Level ya Watanzania wengi ni kujadili mambo ya Dida mashamsham na Mondi vs Kiba
 
Yaani hadi leo bado hatuna njia ya kuihoji serekali na kuiwajibisha? Ni lini mtapata hiyo njia?

Nyerere hakutumia maarifa kupata uhuru wa Tanganyika, bali Tanzania haikuwa koloni kama yalivyo makoloni mengine, bali ilikuwa chini ya UN, hivyo muongeaji yoyote angepewa uhuru ule. Achana historia za upotoshaji.
 
Ukoloni ni hali ya taifa moja lenye nguvu kulitawala taifa lingine dhaifu katika nyanja zote za kiuchumi ,kijamii na kiutamadunj.
Je waingereza hawakuwa na tabia hii dhidi ya watanganyika?
Na kabla ya uhuru Nyerere alienda Kwenye mkutano wa UN uliofanyika UN je alienda kufanya nini?
Baada ya hapo Nyerere alienda Marekani akapokelewa na John Firtzgerald Kennedy alienda kuplead nini?
Kama sio kuomba uhuru wa Taifa hili.

Kama ilikuwa sio koloni je Uingereza ilikuwa inafanya nn nchini?

nakubaliana na wewe kwamba ilikuwa ni mandator territory sawa but serikali iliyokuwa inatawala ni ya nchi gani? Je ni serikali ya UN au ni serikali ya Uingereza?

Unapaswa ujue Tanganyika ilikuwa ni miongoni mwa mataifa yaliyochukuliwa na upande wa pili wa mabepari pale upande wa Waingereza na washirika wake ilipowashinda wajerumani kwenye vita ya pili ya mabepari duniani iliyopewa jina la vita vya pili vya Dunia.

Tanganyika ilichukuliwa kutoka kwa mjerumani kuja kwa mwingereza, UN imetumika kama sehemu ya ku pacify the situation ili resistances zipungue duniani ila ukoloni ni ule ule, haijalishi ni muingereza au ni mjerumani wote ni wakoloni.
 
Hivyo unamaanisha Nyerere alikuwa ni muongeaji tu 🤔
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…