KERO Ukiwa na mkopo Songesha hupati mkopo benki

KERO Ukiwa na mkopo Songesha hupati mkopo benki

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Kifupi benki yeyote hutakopesheka si ulisajili laini Kwa kitambulisho cha taifa .Unadhani rekodi zako zitapotea hata ukienda kukopa popote watakudai kitambulisho Cha taifa wakiingizia tu huyu hapa wanakuona tapeli wa kukopa alishakopa kabla akiingia mitini
Si kweli hata kidogo, labda ungesema baadhi ya hivyo vibenki uchwara vilivyoingia ubia na makampuni ya simu
 
SONGESHA na MIKOPO mingine ya simu imepelekea watumishi KUNYIMWA mikopo WAnapoenda bank kukopa, na hii ni kutokana na mamlaka zinazosimamia mikopo kuweka utaratibu wa madaraja high risk,risk na low risk katika kadiri mteja anaposongesha.

Hilo limetokea Leo Mimi mwenyewe nilipoenda bank na kuingia Kwenye mfumo wa ess utumishi, bank walivyoingia na kutumia mkopo ukawa rejected,nikaenda voda nikawalipa SONGESHA yote lakini Bado mfumo ulisoma high risk.

Nawashauri wale ambao hamjaingia Kwenye hili jini SONGESHA msijalibu mbeleni litawaleta shida

Mamlaka zinasimamia Mikopo hili LA simu hasa Mikopo ya nivushe, SONGESHA, Gold, bustisha ziwe na term of condition, Yani taratibu za mwanachama kukubali
Nadaiwa mgodi, songesha,mpawa ,salary advance na mkopo nimevuta.... Acha ulaghai .....
 
Ni CRDB? Maana ndo wameanza kufanya hivyo
CRDB na NMB ni kama umechukua salary advance ukahamisha mshahara ndio wanakuripoti hiyo imemkuta mshkaji mi sikuhamisha mshahara na salary advance nilichukua ...na nikaprocess mkopo CRDB hata siku haikuisha imo..... Ila madeni ya mitandao ya simu sio kweli....
 
Hahaha...........bora kama wamefanya hivyo, maana Vijana wasio waaminifu wamekuwa wanakopa na kuvunja laini zao 🙌
Hili ni janga zaidi kwa wale wanaowasajilia line ndugu jamaa na marafiki zao.

Unamsajilia mtu line na haya maisha yetu ya utafutaji leo umehama au yeye amehama mkoa anaenda anaitia kwenye kausha damu siku imepotea uwezo wa kui-renew hana anatafuta mtu mwengine anamsajilia nyingine huku nyuma line aliyoisongeshea msala unabaki kwako siku umepata shida ukijijua kabisa kwamba wewe ni msafi unakopesheka unashangaa unakutana na muhuri mwekundu madai umekuwa mdaiwa sugu,ukimpigia jamaa akupe ABCs ya kilichokuwa kinaendelea humpati.

Jioni hii nilikuwa nazungumza na jamaa yangu yupo Airtel akaniambia line zote zilizokopewa zikitoweka hewani iwe kwa bahati mbaya (kupotea /mmiliki kufariki) au kwa makusudi (kuzimwa/kuvunjwa baada ya kukopa pesa au salio) hazitagawiwa kwa mtu mwengine kama ilivyo kawaida hata kikipita kipindi cha siku 90 (miezi mitatu) mpaka itakapojulikana hatma ya wamiliki wake nini kimewakuta,jamaa wameamua kukomaa.
 
CRDB na NMB ni kama umechukua salary advance ukahamisha mshahara ndio wanakuripoti hiyo imemkuta mshkaji mi sikuhamisha mshahara na salary advance nilichukua ...na nikaprocess mkopo CRDB hata siku haikuisha imo..... Ila madeni ya mitandao ya simu sio kweli....
Inaweza ikawa ni bahati yako au tawi walilokuhudumia hawaja-update bado system zao ili ku-copy na sheria mpya zilizoingizwa (tukumbuke haya malalamiko yameanza leo so labda ni sheria imeanza kutumika kuanzia jana au juzi).

Haiwezekani kila mtu analalamika kutakuwa na tatizo mahali.
 
Hili ni janga zaidi kwa wale wanaowasajilia line ndugu jamaa na marafiki zao.

Unamsajilia mtu line na haya maisha yetu ya utafutaji leo umehama au yeye amehama mkoa anaenda anaitia kwenye kausha damu siku imepotea uwezo wa kui-renew hana anatafuta mtu mwengine anamsajilia nyingine huku nyuma line aliyoisongeshea msala unabaki kwako siku umepata shida ukijijua kabisa kwamba wewe ni msafi unakopesheka unashangaa unakutana na muhuri mwekundu madai umekuwa mdaiwa sugu,ukimpigia jamaa akupe ABCs ya kilichokuwa kinaendelea humpati.

Jioni hii nilikuwa nazungumza na jamaa yangu yupo Airtel akaniambia line zote zilizokopewa zikitoweka hewani iwe kwa bahati mbaya (kupotea /mmiliki kufariki) au kwa makusudi (kuzimwa/kuvunjwa baada ya kukopa pesa au salio) hazitagawiwa kwa mtu mwengine kama ilivyo kawaida hata kikipita kipindi cha siku 90 (miezi mitatu) mpaka itakapojulikana hatma ya wamiliki wake nini kimewakuta,jamaa wameamua kukomaa.
Laini akipewa mtu mwingine huwezi kudaiwa?
 
Unataka kusema Mteja wa Vodacom Songesha anaweza kuwa na Deni linaloweza kuathiri kukopeshwa na Benki?

Kivipi jambo hilo likahusiana?
Huo mkopo iliutoa ni benki. Voda ni mlipaji na mpokeaji wa rejesho. Hivyo jina lako lipo kwenye vitabu vya benki x. Kalipe na usipolipa utaonekana were mifumo kuwa sio mteja mzuri
 
Yaani bank wakatae kula hela ya mtumishi 200k kwa mwezi kisa alikopa 20k Songesha? We utakua haukopesheki.
Maswala ya mikopo chechefu ni very sensitive.

Zamani benki zilikuwa na uwezo wa kuhesabu mkopo chechefu kama "hasara" kwa benki i.e inapunguza faida i.e inapunguza mzigo wa kodi. Baada ya kuja database ya taarifa za wateja, benki kabla ya kutoa mkopo ni lazima wapitie huko kwanza kujiridhisha kuhusu tabia za mkopaji. Ikitokea bank wametoa mkopo either kwa kutoangalia au kutozingatia taarifa za database, na huo mkopo ukashindwa kulipika; imekula kwa bank.
 
SONGESHA na MIKOPO mingine ya simu imepelekea watumishi KUNYIMWA mikopo WAnapoenda bank kukopa, na hii ni kutokana na mamlaka zinazosimamia mikopo kuweka utaratibu wa madaraja high risk,risk na low risk katika kadiri mteja anaposongesha.

Hilo limetokea Leo Mimi mwenyewe nilipoenda bank na kuingia Kwenye mfumo wa ess utumishi, bank walivyoingia na kutumia mkopo ukawa rejected,nikaenda voda nikawalipa SONGESHA yote lakini Bado mfumo ulisoma high risk.

Nawashauri wale ambao hamjaingia Kwenye hili jini SONGESHA msijalibu mbeleni litawaleta shida

Mamlaka zinasimamia Mikopo hili LA simu hasa Mikopo ya nivushe, SONGESHA, Gold, bustisha ziwe na term of condition, Yani taratibu za mwanachama kukubali
Hiyo benki ni wapumbavu kabisa.Walipaswa wakupe mkopo haraka kwa sababu ulionesha wewe ni muhitaji hadi ukakopa SONGESHA.Wewe ni mlengwa wa TASAF II Phase 3 unaevaa suti.Haujahitimu.
 
Kama si mwaminifu wa kurejesha mkopo wao lazima wakublack list.

Nimekaa na Airtel money vizuri kwa miaka kadhaa, Sasa wananiamini wanaweza kunikopesha hadi 1.6 m bila shida. Kaeni vizuri na wanaowakopesha kwa kuwa waaminifu na kulipa deni kwa wakati mliokubaliana.
Tatizo riba zao sio rafiki, mfano mzuri ni SONGESHA. Hawa ni sawa sawa na kausha damu tuu. Mkopo mzuri niliouona kwasasa ni "saraly advance" only 5% na ndani ya mwezi lazima urudishe deni la watu utake usitake. Sasa hawa kina Songesha kila unavyochelewesha deni lao rate inapanda, hizi mamlaka zinazo blacklist hawalioni hili?

Sent from my SM-E045F using JamiiForums mobile app
 
Tatizo riba zao sio rafiki, mfano mzuri ni SONGESHA. Hawa ni sawa sawa na kausha damu tuu. Mkopo mzuri niliouona kwasasa ni "saraly advance" only 5% na ndani ya mwezi lazima urudishe deni la watu utake usitake. Sasa hawa kina Songesha kila unavyochelewesha deni lao rate inapanda, hizi mamlaka zinazo blacklist hawalioni hili?

Sent from my SM-E045F using JamiiForums mobile app
Umasikini kmnioko.Mtu unakopa hadi buku/1000/one tau?Duh!Tufumbe macho tuombe ufukara utokomee mbali.
 
Wengi wetu tunafikiri mikopo ya mitandao ya simu kwa sababu huwa hawataki vielelezo vingi zaidi ya namba za NIDA tulizosajilia basi mtu anaweza akakopa halafu akawakimbia kwa kuhama line.

Lakini wao walishalijua hili mapema so inaonekana walipoenda kuomba license ya kufanya hii biashara waliomba pia wawe na uwezo wa kuingilia taarifa binafsi za wateja wao kwenye mizunguko yao ya fedha nje ya mitandao yao ili inapotokea mteja kukosa uaminifu kwao wawe na uwezo wa kuzishawishi taasisi nyengine zizuie mikopo watakapoenda kuwakopa mpaka watakapowalipa na hili linafanikiwa kwa sababu ya namba za NIDA tulizosajilia.

Ukienda popote kukopa wakiingiza ID card # yako kama una kimeo unawekwa uchi,na ukweli ktk hilo wamefanikiwa sana nimemsoma mdau mmoja humu asubuhi akilalamika songesha ya 5K imemfanya awe na sifa ya kutokopesheka hata alipoilipa still akaonekana ni mzigo hakopesheki,nadhani wanatumia ile kanuni ya ”ukikosa uaminifu kwa kitu kidogo huwezi kuwa muaminifu na kitu kikubwa”
Hawana leseni ya kutoa mikopo hili hata waziri wa fedha aliwahi kulitolea fufafanuzi bungeni. Kinachofanyika ni uholela tu kama nchi yetu ilivyo holela

Sent from my SM-E045F using JamiiForums mobile app
 
Wasiwasi wangu hii mada imeanzishwa na mmoja wa wafanyakazi wa hizi kampuni za simu na amewaalika wenzake waje wachangie kwa nguvu zote ili wanaodaiwa walipe madeni. Hii nguvu inayotumika hapa sio kawaida. Nina deni Songesha zaidi ya laki moja na nusu kwa mwaka sasa, na wiki iliyopita nimepata mkopo wangu saaafi kabisa kutoka benki

Sent from my SM-E045F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom