KERO Ukiwa na mkopo Songesha hupati mkopo benki

KERO Ukiwa na mkopo Songesha hupati mkopo benki

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Hili ni janga zaidi kwa wale wanaowasajilia line ndugu jamaa na marafiki zao.

Unamsajilia mtu line na haya maisha yetu ya utafutaji leo umehama au yeye amehama mkoa anaenda anaitia kwenye kausha damu siku imepotea uwezo wa kui-renew hana anatafuta mtu mwengine anamsajilia nyingine huku nyuma line aliyoisongeshea msala unabaki kwako siku umepata shida ukijijua kabisa kwamba wewe ni msafi unakopesheka unashangaa unakutana na muhuri mwekundu madai umekuwa mdaiwa sugu,ukimpigia jamaa akupe ABCs ya kilichokuwa kinaendelea humpati.

Jioni hii nilikuwa nazungumza na jamaa yangu yupo Airtel akaniambia line zote zilizokopewa zikitoweka hewani iwe kwa bahati mbaya (kupotea /mmiliki kufariki) au kwa makusudi (kuzimwa/kuvunjwa baada ya kukopa pesa au salio) hazitagawiwa kwa mtu mwengine kama ilivyo kawaida hata kikipita kipindi cha siku 90 (miezi mitatu) mpaka itakapojulikana hatma ya wamiliki wake nini kimewakuta,jamaa wameamua kukomaa.
Umesema sahihi Mkuu, ndiyo maana una nafasi ya kutambua namba zilizosajiri Kwa kitambulisho chako.

Ukiona vipi kazifungie
 
Lakini sidhani kama Songesha wanatoa Mkopo zaidi ya milioni 1, hopefully watakuwa down
Haijalishi kiwango. WaTz mmewekewa Credit Bureau sasa hivi ukiharibu mkopo unakuwa blacklisted hukopesheki. Mtoa mkopo kabla ya kukupa mkopo a anacheki na credit bureau status yako(credit score) ikoje. Kama ulikimbia deni sehemu unakosa sifa.
 
Ni mpumbavu pekee anayeweza kukataa kumkopesha mtumishi wa Umma 20,000,000 kisa anadaiwa na songesa 20,000. Narudia tena ni mpumbavu pekee.
Huyo anaekataa wala hajui kisa ni 20k ya songesha. System tu itamwambia huyo hakopesheki. High risk,poor credit score.
 
Nina hakika mabenki yanayo tegemea faida kwa kukopesha watumishi yatapoteza wateja wengi mnoo. Maana kiukweli asilimia kubwa wana vimikopo walivyo default.

Jana nilikuwa benk ya CRDB,wanasema maombi ya wateja wapatao 10 kwa ajili ya mikopo yamekataliwa na system kwa sababu ya udaiwa sugu. Yule loan officer alikuwa anasikitishwa na hyo Hali na akawa anasema wanafanya communication na makao makuu ili waachie tu hyo mikopo.
Shida kwa hao maofisa, mmoja wa hao 10 aki default wakaguzi wakaona system ilimkataa yeye akalazimisha itakula kwake.
 
Makampuni ya simu hayana leseni ya kukopesha.Yanayokopesha ni mabank yaliyoingia mikataba na kampuni za simu....
 
Ishu sio kuwa na songesha , M-Pawa Wala mkopo sehem nyingine, inatakiwa iwe kwenye Hali nzuri. Ni mlipaji.

Sheria za benki kuu zinataka watu wote wanaotoa huduma za mikopo kupeleka taarifa za wakopaji wote credit bureau. Mtu yeyote anaetaka mkopo, wanaingia huko wanachungulia kama umewahi kuwa mdaiwa sugu unahatari ya kukosa mkopo.

Nnachosisitiza, fanya songesha, mpawa, bustisha na mengine yanayofanana na hayo lakini lipa Kwa wakati.
 
tz ustaarabu wa fedha hatuna..... songesha imeahanisaidia sana kwenye miamala midogo midogo ila nikiweka pesa tu nawalipa kwahiyo sijawahi pata adha ya kushindwa kupata huduma sehemu.....

unakuta mtu anasongesha miamala akimaliza anaona kashawini laini haitumii tena wakati ukilipa songesha unajiwekea uwezo mkubwa zaidi wa kusongesha miamala leo hata nikipelea 200k nasingesha muamala kama kawa na nikipata hela naweka nalipa tatizo linakuja mtu anasongesha vocha anasongesha 10k anatoa muamala anakwenda kunywa visungura unatarajia muda wa kulipa anajiskiaje na pesa alotumia sehemu isiyoweza ingiza pesa nyingine....


tumerahisishiwa sana kufanya miamala ila tunajiwekea ugumu sisi wenyewe

jiulize mtu songesha tu inamshinda sasa atajenga kweli? anaweza kuendesha biashara na ikaleta faida? watu kama mleta mada ndio huchukua mkopo bank anakwenda kujenga nyumba ya kuishi au kununua gari la kutembelea.....
 
Songesha na mikopo mingine ya simu imepelekea watumishi kunyimwa mikopo wanapoenda bank kukopa, na hii ni kutokana na mamlaka zinazosimamia mikopo kuweka utaratibu wa madaraja high risk, risk na low risk katika kadiri mteja anaposongesha.

Hilo limetokea leo mimi mwenyewe nilipoenda bank na kuingia kwenye mfumo wa ESS Utumishi, bank walivyoingia na kutumia mkopo ukawa rejected, nikaenda Voda nikawalipa Songesha yote lakini bado mfumo ulisoma high risk.

Nawashauri wale ambao hamjaingia kwenye hili jini songesha msijaribu, mbeleni litawaleta shida.

Mamlaka zinasimamia Mikopo hili la simu hasa mikopo ya Nivushe, Songesha, Gold, Bustisha ziwe na term of condition, yaani taratibu za mwanachama kukubali.
Hata hii elgu kumi.niliyokopa.nikiw porini ,ininyime m15 Benki
 
Nina hakika mabenki yanayo tegemea faida kwa kukopesha watumishi yatapoteza wateja wengi mnoo. Maana kiukweli asilimia kubwa wana vimikopo walivyo default.

Jana nilikuwa benk ya CRDB,wanasema maombi ya wateja wapatao 10 kwa ajili ya mikopo yamekataliwa na system kwa sababu ya udaiwa sugu. Yule loan officer alikuwa anasikitishwa na hyo Hali na akawa anasema wanafanya communication na makao makuu ili waachie tu hyo mikopo.
Shida kwa hao maofisa, mmoja wa hao 10 aki default wakaguzi wakaona system ilimkataa yeye akalazimisha itakula kwake.
ila mkuu tunatia aibu yaani mtu anakimbia na afarobaini pesa ndogo kabisa wakati akilipa anaweza kusongesha miamala zaidi tz tunatia aibu kinoma
Halafu akinyimwa mkopo mkubwa anaweza 'yaani uninyime 40m kwasababu ya deni la 40k'
 
Shida kwa hao maofisa, mmoja wa hao 10 aki default wakaguzi wakaona system ilimkataa yeye akalazimisha itakula kwake.

Halafu akinyimwa mkopo mkubwa anaweza 'yaani uninyime 40m kwasababu ya deni la 40k'
kama mtu kashindwa kukurudishia 40k unaweza kumpa 100k kama ni ww hebu sema tu kwa uelewa wa fast
 
Shida kwa hao maofisa, mmoja wa hao 10 aki default wakaguzi wakaona system ilimkataa yeye akalazimisha itakula kwake.
Mnajaribu kutumia nguvu nyingi kuelezea kitu ambacho hakipo. Ukiwa blacklisted kwasababu ya mkopo haĺafu ukalipa na umewekewa hiyo status mnayosema, sio kwamba unakosa mkopo. Unachotaiwa kufanya ni kuchukua kitu kinaitwa "loan clearance statement" taasisi iliyokuwa inakudai ikitoa hiyo statement status ya high risk inaondolewa.

Mfumo huo umeanzishwa maalumu kuweza ku track madeni ya mtu kabla hajaingia kwenye mkopo mwingine, sio ku block mtu asiweze kukopa.

Ndiomaana nasema humu kuna wachangiaji wa mada hii ambao ni wafanyakazi wa hizi songesha and the like maana hamsemi uhalisia

Sent from my SM-E045F using JamiiForums mobile app
 
Mnajaribu kutumia nguvu nyingi kuelezea kitu ambacho hakipo. Ukiwa blacklisted kwasababu ya mkopo haĺafu ukalipa na umewekewa hiyo status mnayosema, sio kwamba unakosa mkopo. Unachotaiwa kufanya ni kuchukua kitu kinaitwa "loan clearance statement" taasisi iliyokuwa inakudai ikitoa hiyo statement status ya high risk inaondolewa.

Mfumo huo umeanzishwa maalumu kuweza ku track madeni ya mtu kabla hajaingia kwenye mkopo mwingine, sio ku block mtu asiweze kukopa.

Ndiomaana nasema humu kuna wachangiaji wa mada hii ambao ni wafanyakazi wa hizi songesha and the like maana hamsemi uhalisia

Sent from my SM-E045F using JamiiForums mobile app
Naweza kubaliana na wewe kwenye hiyo document ya so called loan clearance statement lakini kufutika hizo alama za kupitiliza siku ya ulipaji wa mkopo kufutika kwake baada ya miaka sita na limeshakuwekea doa kwenye taasisi nyingine kukopa na kama watakukopesha basi kwa riba kubwa sana.
 
Haijalishi kiwango. WaTz mmewekewa Credit Bureau sasa hivi ukiharibu mkopo unakuwa blacklisted hukopesheki. Mtoa mkopo kabla ya kukupa mkopo a anacheki na credit bureau status yako(credit score) ikoje. Kama ulikimbia deni sehemu unakosa sifa.
Kama tumefikia huko ni jambo jema sana, Watanzania wengi sio waaminifu.

Kuna Mzee mmoja alikuwa yupo radhi akupe hela ukisema unaomba lakini sio kukukopesha.

Maana anajua tulivyowasumbufu kulipa 🙌
 
Back
Top Bottom