Ukiwa nje usiwaamini ndugu Bongo, ndoto ya kurudi nyumbani mazima imefifia kutokana na ujenzi hafifu

Ungetumia contractor kujenga baada ya kuona BOQ wewe ungedeposit then unajua kabisa lini utakabidhiwa nyumba yako.
Siku hizi wapo local engineer wanakubali mnapatana wanajenga kwa phases.

Yani haina stress kabisa, kuna engineer nenda naye sawa kinoma, tukianza phase mpya anaingiza Jeshi tukimaliza anaondowa Jeshi navuta pumzi maana ni jengo la ghorofa moja.
 
Aisee ndugu noma sana. Ukiwaamini wanakupiga, usipowaamini wanakulaumu.

Pambana mkuu, nyumba itaisha tu hiyo.
Wengi ni wajanja wajanja. Laiti marehemu mzee wangu angekuwepo huu ujinga usingefanyika.
 
Kama ulivyoandika hapo juu. Inategemea Nke na Nke Nkuu wangu.
 
Sibora hawajamalizia wengine unakuta empty
 
Sasa hapo inabidi tuwajadili ndugu au wewe mkuu!?

Mbona Sasa Kwa unachofanya ni kwamba unajitafutia stress mwenyewe halafu zikizidi unatushirikisha member wenzio!!!
Nimekuja hapa kupata ushauri na kupunguza stress baada ya kutuma zingine afu mabadiliko ya ujenzi au muendelezo ni zero.
 
Dah umenipa ushauri mzuri kwangu, na hata kwa wengine watakaosoma comment yako pia. Shukran mkuu.
 
Mwaka 2021 miezi kama hiyo nilikuwa stage kama yako
Muhimu fanya zile kazi ngumu kwanza ziishe

Mfano Shimo la choo pamoja na network nzima ya maji ndani
Kisha angalia levelling ya ndani imekaa poa
Baada ya hapo piga gypusm board ili uki skimm upige kwa pamoja

Kama mafundi waaminifu huna nikupe jeshi langu ndani ya mwezi hadi rangi imekamilika. Walikuwa wanafanya usiku na mchana hapo site kwangu.
 
wakati mwingine ni bora kumtumia contarctor kama mfuko unaruhusu, na kwa sasa wakandarasi wengi mnaweza kubaliana mlipanaje.... lkn pia kuna option ya kutumia mafundi wadogo wadogo... ndugu sometime ni lawama sana!!
Yah ni kweli mkuu, sema mara nyingi binadam huwa tunajifunza kutokana na makosa. So siwezi kurudia kosa tena siku nyingine.
 
Ibarikiwe sana mkuu, ngoja ulichoshauri nitakifanyia kazi haraka iwezekanavyo ili program yangu isiharibike.
 
Huu ushauri una faida kubwa sana kwa sisi wajenzi na wasomaji wengine ambao hawajajaaliwa kujenga, lkn wakiwa na nia ya kujenga siku 1 hata wakiwa mbali.

Shukran zangu za dhati zikufikie huko ulipo mkuu.
 
Yaani wewe, unawaamini ndugu zako ambao hata JF hawaijui? Maana wangekuwa wanaijua usingeweka picha ya hiyo nyumba yako na kuwasema namna hii
Siwasemi vibaya kwa vile sijaweka picha zao hapa JF. Laiti ningeweka picha zao na kuwaanika hapa hapo ningekuwa nimefanya kosa kubwa ambalo hata mimi mwenyew baadae lingenigusa mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…