Ukiwa nje usiwaamini ndugu Bongo, ndoto ya kurudi nyumbani mazima imefifia kutokana na ujenzi hafifu

Ukiwa nje usiwaamini ndugu Bongo, ndoto ya kurudi nyumbani mazima imefifia kutokana na ujenzi hafifu

Ungetumia contractor kujenga baada ya kuona BOQ wewe ungedeposit then unajua kabisa lini utakabidhiwa nyumba yako.
Siku hizi wapo local engineer wanakubali mnapatana wanajenga kwa phases.

Yani haina stress kabisa, kuna engineer nenda naye sawa kinoma, tukianza phase mpya anaingiza Jeshi tukimaliza anaondowa Jeshi navuta pumzi maana ni jengo la ghorofa moja.
 
Kuna idadi ya kutosha ya watu waliolizwa na wake zao.

Mimi kuna Mshikaji alikuwa Marekani amemtumia mshikaji tu wa mtaani kusimamia nyumba yake mpaka imeisha na jamaa akaendelea kukaa kuilinda nyumba, mshkaji yupo hapa Sasa hivi amekuja likizo amemnunulia jamaa zawadi ya gari IST afanye uber.

Na nyumba iliyojengwa INA standard zote mpaka Rangi zake ni viwango, kwenye hili Mimi naona ni jinsi ya mtu kujipanga siku hizi kuna video call unaona vitu kwa uhalisia.
Kama ulivyoandika hapo juu. Inategemea Nke na Nke Nkuu wangu.
 
Habari zenu wana JF wenzangu, ama baada ya salam ningependa sasa nijielekeze kwenye mada husika.

Ndugu wanajamii forum wenzangu, unapokuwa nje ya nchi mara nyingi unakumbana na changamoto nyingi kutoka kwa ndugu, jamaa na marafiki uliyowaacha nyumbani.

Hii ni kutokana na wao kuona, au kuamini kwamba unao uwezo wa kufanya kila kitu kwao. Na kibaya zaidi hata utapojaribu kufanya baadhi ya vile unavyoweza kufanya bado utaendelea kubebeshwa lawama tu, ili mradi wahakikishe kuwa wew hauwezi ukaishi bila lawama zao.

Mwaka 2019 before corona nilikwenda bongo nikanunua kiji eneo maeneo ya salasala. Mpaka hapo tayari nilikuwa na eneo langu lingine ambalo tayari nimeshajenga kule Kigamboni, sehemu fulan inaitwa yebo yebo. Ila mimi binafsi nilipojaribu kupalinganisha Kigamboni na Salasala maeneo niliyonunua mimi, niliona kwamba Salasala ndio panafaa kuwa makazi yang ya kudumu pindi ntaporudi kuishi bongo mpaka pale muumba ataponichukua.

Kwahiyo nilivyorudi kaburu ikabidi nianze jitihada za ujenzi kule Salasala ili nishushe mjengo nitakaoishi mimi na familia yangu afu ile nyumba ya Kigamboni nitaipangisha. Kwa sasa kule yebo yebo Kigamboni anaishi brother wangu ambae na yey ana kiwanja chake huko huko Kigamboni anajenga, kwahiyo wakati namalizia mjengo wangu wa Kigamboni aliniomba akae kwanza kwa muda ili awe karibu na shughuli yake ya ujenzi afu nyumba yake ikishaisha ndo atapohama na kuniachia nyumba yangu nipangishe, nkasema haina noma bro.

Sasa basi ujenzi wa Salasala niliuanza mwaka 2020 nikitarajia kuwa katikati ya mwaka huu wa 2022 niwe nimeshamaliza afu ikiwezekana mwezi wa 12 nikienda bongo likizo iwe ndo kimoja nisirudi tena Kaburu. Cha kushangaza pamoja na jitihada zote nlizofanya lkn wanaosimamia mjengo wangu ndio wananikwamisha. Nyumba inaenda kimdondo sana mpaka inanikatisha tamaa kama ninaweza kuihamia mwishoni mwa mwaka huu.

Kabla ya kuanza ujenzi huu kuna watu walinishauri kwamba ni bora nimtume mama watoto aende kukaa bongo ili awe anasimamia shughuli za ujenzi kuliko kuwaamini ndugu tu pekee, mimi nikakaidi kwa kuona kuwa kamwe siwezi kumuweka mke wangu mbele ya ndugu zangu.

Sasa matokeo yake majuto ni mjukuu. Na mimi kuhamia Kigamboni staki naona kumenikalia kushoto sana aisee. Wana JF wenzangu mnaonaje, hivi mjengo huu unaweza kuisha kwa mwezi mmoja uliobaki kweli?

Maanake kuishi mbali na nyumbani kwa muda mrefu nako kunachosha.

View attachment 2400496View attachment 2400497
Sibora hawajamalizia wengine unakuta empty
 
Sasa hapo inabidi tuwajadili ndugu au wewe mkuu!?

Mbona Sasa Kwa unachofanya ni kwamba unajitafutia stress mwenyewe halafu zikizidi unatushirikisha member wenzio!!!
Nimekuja hapa kupata ushauri na kupunguza stress baada ya kutuma zingine afu mabadiliko ya ujenzi au muendelezo ni zero.
 
Makosa yako huwezi kuyaona, unapofanya ujenzi siku nyingine kama uko mbali muone Mtaalam akuandalie BOQ hakuna mtu atakuchakachuwa maana ujenzi wote mpaka kitasa upo kwenye BOQ.

Tatizo wabongo tunadharau taaluma za watu na kuamini wahuni wakupigie hesabu za kichwa, kuna vitu tukiacha uswahiliswahili vinaepukika.
Dah umenipa ushauri mzuri kwangu, na hata kwa wengine watakaosoma comment yako pia. Shukran mkuu.
 
Habari zenu wana JF wenzangu, ama baada ya salam ningependa sasa nijielekeze kwenye mada husika.

Ndugu wanajamii forum wenzangu, unapokuwa nje ya nchi mara nyingi unakumbana na changamoto nyingi kutoka kwa ndugu, jamaa na marafiki uliyowaacha nyumbani.

Hii ni kutokana na wao kuona, au kuamini kwamba unao uwezo wa kufanya kila kitu kwao. Na kibaya zaidi hata utapojaribu kufanya baadhi ya vile unavyoweza kufanya bado utaendelea kubebeshwa lawama tu, ili mradi wahakikishe kuwa wew hauwezi ukaishi bila lawama zao.

Mwaka 2019 before corona nilikwenda bongo nikanunua kiji eneo maeneo ya salasala. Mpaka hapo tayari nilikuwa na eneo langu lingine ambalo tayari nimeshajenga kule Kigamboni, sehemu fulan inaitwa yebo yebo. Ila mimi binafsi nilipojaribu kupalinganisha Kigamboni na Salasala maeneo niliyonunua mimi, niliona kwamba Salasala ndio panafaa kuwa makazi yang ya kudumu pindi ntaporudi kuishi bongo mpaka pale muumba ataponichukua.

Kwahiyo nilivyorudi kaburu ikabidi nianze jitihada za ujenzi kule Salasala ili nishushe mjengo nitakaoishi mimi na familia yangu afu ile nyumba ya Kigamboni nitaipangisha. Kwa sasa kule yebo yebo Kigamboni anaishi brother wangu ambae na yey ana kiwanja chake huko huko Kigamboni anajenga, kwahiyo wakati namalizia mjengo wangu wa Kigamboni aliniomba akae kwanza kwa muda ili awe karibu na shughuli yake ya ujenzi afu nyumba yake ikishaisha ndo atapohama na kuniachia nyumba yangu nipangishe, nkasema haina noma bro.

Sasa basi ujenzi wa Salasala niliuanza mwaka 2020 nikitarajia kuwa katikati ya mwaka huu wa 2022 niwe nimeshamaliza afu ikiwezekana mwezi wa 12 nikienda bongo likizo iwe ndo kimoja nisirudi tena Kaburu. Cha kushangaza pamoja na jitihada zote nlizofanya lkn wanaosimamia mjengo wangu ndio wananikwamisha. Nyumba inaenda kimdondo sana mpaka inanikatisha tamaa kama ninaweza kuihamia mwishoni mwa mwaka huu.

Kabla ya kuanza ujenzi huu kuna watu walinishauri kwamba ni bora nimtume mama watoto aende kukaa bongo ili awe anasimamia shughuli za ujenzi kuliko kuwaamini ndugu tu pekee, mimi nikakaidi kwa kuona kuwa kamwe siwezi kumuweka mke wangu mbele ya ndugu zangu.

Sasa matokeo yake majuto ni mjukuu. Na mimi kuhamia Kigamboni staki naona kumenikalia kushoto sana aisee. Wana JF wenzangu mnaonaje, hivi mjengo huu unaweza kuisha kwa mwezi mmoja uliobaki kweli?

Maanake kuishi mbali na nyumbani kwa muda mrefu nako kunachosha.

View attachment 2400496View attachment 2400497
Mwaka 2021 miezi kama hiyo nilikuwa stage kama yako
Muhimu fanya zile kazi ngumu kwanza ziishe

Mfano Shimo la choo pamoja na network nzima ya maji ndani
Kisha angalia levelling ya ndani imekaa poa
Baada ya hapo piga gypusm board ili uki skimm upige kwa pamoja

Kama mafundi waaminifu huna nikupe jeshi langu ndani ya mwezi hadi rangi imekamilika. Walikuwa wanafanya usiku na mchana hapo site kwangu.
 
wakati mwingine ni bora kumtumia contarctor kama mfuko unaruhusu, na kwa sasa wakandarasi wengi mnaweza kubaliana mlipanaje.... lkn pia kuna option ya kutumia mafundi wadogo wadogo... ndugu sometime ni lawama sana!!
Yah ni kweli mkuu, sema mara nyingi binadam huwa tunajifunza kutokana na makosa. So siwezi kurudia kosa tena siku nyingine.
 
Mwaka 2021 miezi kama hiyo nilikuwa stage kama yako
Muhimu fanya zile kazi ngumu kwanza ziishe

Mfano Shimo la choo pamoja na network nzima ya maji ndani
Kisha angalia levelling ya ndani imekaa poa
Baada ya hapo piga gypusm board ili uki skimm upige kwa pamoja

Kama mafundi waaminifu huna nikupe jeshi langu ndani ya mwezi hadi rangi imekamilika. Walikuwa wanafanya usiku na mchana hapo site kwangu.
Ibarikiwe sana mkuu, ngoja ulichoshauri nitakifanyia kazi haraka iwezekanavyo ili program yangu isiharibike.
 
Principal za ujenzi ukiwa mbali ni kama ifuatavyo: 1.Fika mwenyewe utafute fundi wa uhakika na mpatane kazi kwa awamu (kuanza msingi mpaka kumwaga jamvi, kuinua tofali mpaka kufunga lenta, kupaua, kupiga plasta, kupiga gypsum, kupiga rangi etc) 2.Tafuta hardware ya uhakika ambapo vifaa vyako vyote utanunua hapo. 3.Msimamizi wa kuona kazi inaendaje. 4.Vifaa vyote vya ujenzi lipa straight kwa mwenye hardware, hata ukitaka mchanga na kokoto mtumie yeye (kumbuka asiwe na hawa wenye njaa njaa) 5.Fundi mlipe kwa awamu mlivyokubaliana kwa makubaliano ya kutuma video clips zikionyesha work progress.. 6.Walau after every 3 months wewe au mkeo lazima mfike kuona hali halisi.
Huu ushauri una faida kubwa sana kwa sisi wajenzi na wasomaji wengine ambao hawajajaaliwa kujenga, lkn wakiwa na nia ya kujenga siku 1 hata wakiwa mbali.

Shukran zangu za dhati zikufikie huko ulipo mkuu.
 
Yaani wewe, unawaamini ndugu zako ambao hata JF hawaijui? Maana wangekuwa wanaijua usingeweka picha ya hiyo nyumba yako na kuwasema namna hii
Siwasemi vibaya kwa vile sijaweka picha zao hapa JF. Laiti ningeweka picha zao na kuwaanika hapa hapo ningekuwa nimefanya kosa kubwa ambalo hata mimi mwenyew baadae lingenigusa mkuu.
 
Back
Top Bottom