Ukiwa umeenda kuosha gari zingatia haya

Ukiwa umeenda kuosha gari zingatia haya

2009 NILIACHA NOAH SINZA WAOIOSHA GARI

NKAENDA GUEST

MAVIMKOJOÒ NIKO B BAR NAPIGIWA SIMU KAKA UKO WAPI NA BOSS WA CAR WASH

KUFIKA NAMBIWA AISEE KUNA KAKA NILIMTUMA XXXX NYOKOOO NKAMWAMBIAA NDUGU NAOMBA GARI YANGU

AKAJIBU IPO SEMAA WAMEMGUSA GARI FLAN NKAJIBU NATAKA GARI NKAITA NDUGU YANGU MWANASHERIA AKAJA

AKAMSAINISHA AKAPIGA SIMU TUKACHKUE GARI WIKI INAYOFWATA

HUKU MBEZI BEACH NJIA YA RAINBOW TO TANKIBOVU MAKABURINI KUNA KONA MAMAYEEE

USIKUUU IMOO OOOOO

HIOOKONAA NYOKOOO BALAAA KUNA NYUMBA YA MTU KILA UKIAMKA ASBH GARI IMEINGIA NDAN HAHAHAA ALIOGA HELA YULE MAZA SIJUI KAMA YUKO HAI LOH

Uandishi mwingine bwana, kama mtu aliyekula kitu cha Arusha...
 
Wengine wajanja hela hawagusi.. wao wanadeal na vitu ambavyo ww kivyovyote kujua itakuchukua muda sana.. mfn una flash drives nyingi ktk gari na sehem uliyoweka inaonyesha hujapagusa siku nyingi au hauna access napo mara kwa mara.. lazima apite nayo.
Kuna wangese walipita na cologne yangu Dunhill Pursuit. Iliniuma sana ilikuwa 100ml 3/4 full.
 
2009 NILIACHA NOAH SINZA WAOIOSHA GARI

NKAENDA GUEST

MAVIMKOJOÒ NIKO B BAR NAPIGIWA SIMU KAKA UKO WAPI NA BOSS WA CAR WASH

KUFIKA NAMBIWA AISEE KUNA KAKA NILIMTUMA XXXX NYOKOOO NKAMWAMBIAA NDUGU NAOMBA GARI YANGU

AKAJIBU IPO SEMAA WAMEMGUSA GARI FLAN NKAJIBU NATAKA GARI NKAITA NDUGU YANGU MWANASHERIA AKAJA

AKAMSAINISHA AKAPIGA SIMU TUKACHKUE GARI WIKI INAYOFWATA

HUKU MBEZI BEACH NJIA YA RAINBOW TO TANKIBOVU MAKABURINI KUNA KONA MAMAYEEE

USIKUUU IMOO OOOOO

HIOOKONAA NYOKOOO BALAAA KUNA NYUMBA YA MTU KILA UKIAMKA ASBH GARI IMEINGIA NDAN HAHAHAA ALIOGA HELA YULE MAZA SIJUI KAMA YUKO HAI LOH
Andikka vizuri
 
kuna vitu umeongea vina ukweli kabisa hasa kupekuw pekuwa kwenye gari na kama umeacha labda beats zako unakuta zimeliwa kabisa nilinunua vitu vya mtoto chocolate 🍫 korosho na biscuits sikukuta niliishia kuguna tu sikutaka ugomvi nikasep ata ukiangusha pesa kwenye gar wakaikuta ni ya kwao hawakupi
Umepigaje hapo!!
beats or bites!
 
Fanya Practical ewe mwenye gari:

Nunua Chocolate ama biscuits kidogo zipake pilipili kichaa za kutosha nenda nazo car wash, ziache kwenye gari halafu uone hao TUMBILI wadokozi watakavyolia na kusaga meno..

Hutaua ila utawakomesha!

Baadae waambie zilikua za kutegemea panya nyumbani
Kuna Kambi Moja mashambani huko handeni, jamaa walikuwa Kila mara wanaenda Kambi ya jirani kuiba unga wa ugali maana msimamizi mlevi mlevi tu.
Mlevi akashauriana na walevi wenzie JINSI anaibiwa unga wake wakamshauri aweke simu ya panya then yeye msosi akawa anakula kijiweni..... Siku tatu nyingi wale waizi waliharisha nusu kifo... Na mwenyekiti akaitwa, wanaulizwa mmekula nini wanasema wameiba unga kwa Kambi ya jirani. Mlevi kuulizwa anasema yeye sumu alitegea panya maana wanamsumbua sana Kambini... Kesi ikwapi hapo?
 
Unashangaa mtu gari yenyewe Ist anataka akaioshe Car wash, si akaoshee nyumbani kwake kwenye beseni (In Mpoki's voice)
 
Pimbi yule aliniibia shuka la kimasai wkt na tip nilikua namuachia Na nikaja kukutana nae ziwa duluti amelivaa.
 
1- Hakikisha vitu vyako ulivyoacha ndani ya gari:-

- USB flash, Charger, hela, na vitu vingine vidogovidogo ni vyema ukavitia ktk mfuko maalumu ukashuka navyo. Huwa si rahisi kubaini kama vimeibiwa kwa haraka mpaka utakapotoka eneo la tukio.

-Mtindo wa kubadiri vitu au kuiba kabisa hasa Carpets, jana nimeenda kuosha "Mkweche" wangu, wakati anarudishia Carpets hakuweka zote maana hii gari ina Carpets mbili mbili. Yeye akaweka moja moja zingine akasema hazikuwepo, alikuta hivyo. Na mimi sikubishana nae nikasema sawa nikaondoka.

-wengi wanapewa ORDER na watu kwamba nitafutie kitu fulani ambacho kiuhalisia madukani si rahisi kukipata au ni ghali sana, mfano kuna rubber zinazozuia vumbi matope etc ktk baadhi ya sehemu hasa nyuma ya gari huwa wanazichomoa, fuse mbalimbali etc kuna jamaa yangu aliacha gari kuosha akaenda kunywa pombe, walimbadirishia Control box, kurudi gari haiwaki (Baadae kule garage ndio wakagundua Control Box imechapwa)

Spika ndogo ndogo zinazokaa nyuma ya gari ktk baadhi ya magari huwa wanazibandua, wewe huwezi jua siku hiyo hiyo.

2- Kujifanya madereva wakiona gari kali, nzuri au imekaa mkao wa kipekee:-

Hii imenikuta hivi karibuni, nimeenda kuosha gari, akataka nimuachie funguo ya kuisogeza nikamuuliza unaiweza hii gari? Akaitikia ndio naiweza naendesha malori ije inishinde hii?. Kwa confidence yake mie nikamuachia funguo nikakaa pembeni. Baada ya kuosha nikasikia gari imewasha huku imekanyagiwa mafuta (Full Throttle). Akatia gia gari ikaruka na kuzima, bahati nzuri mbele kulikuwa na Tank ambalo halina maji so lile TANK lilisogezwa kwa umbali tu. Nikaenda kumuuliza imekuwaje? akasema alitak kwenda nyuma, badala aweke Reverse yeye akaweka gia namba 5. (Hii gari ni Manual ya 6 gears, na gearbox yake imegeuka sio ordinary) yeye kwa kukariri kwake akataka aniingize hasara.

Tuwe makini na hawa WAOSHA magari hasa ktk kipengele cha kusogeza gari.

3- Kutumia Pressure ya maji katika sehemu ambayo haina haja:-

Anaweka high pressure ktk sehemu sensitive kama ktk taa hasa upande wa nyuma kwenye waya, kama gari yako rangi yake imevimba kidogo atatia pressure hapo mpk rangi inabanduka. Yaan hawaangalii pakutumia high pressure na low pressure.

4- Kuosha Engine (INJINI) bila uangalifu:-

- Kuna magari ni very sensitive ktk maji, hasa haya ya umeme. Unakuta mtu anaenda kupigilia high pressure ktk engine bila tahadhari mwisho wa siku anakuletea faults zisizo na maana. Ni heri uoshe kwa mvuke au afute tu engine-bay yote.

5- Wanasoma Documents zako:-

Nilifanya research fupi tu baada ya kufuta kitambulisho changu na kukificha nyuma ya siti pia nilikiweka katikati ya Documents zingine huku nikiziunganisha ndani ya bahasha, nilifanya maksudi.

Baadae wakati nimerudi home nikacheck zile Documents nikakuta zimewekwa ndivyo sivyo na ile ID imeshikwa shikwa inaonyesha Fingerprints. Nikajisemea hawa kumbe nikiacha vitu vyangu humu wanapekua pekua instead of kufanya wanachotakiwa kufanya.

Ni hayo tu, Je wewe ulikutana na Changamoto gani kwa hawa Waosha Magari?

Rejea:- Muosha Magari apatisha ajali gari lenye thamani zaidi ya Milioni 100. Akutwa anaruka sarakasi

Kwa mtu Kama Mimi na Brand yangu nikienda kwa car wash, na respect my home boy waliyonayo kwangu Sijawahi Kuwa na wasiwasi, they treat me with absolute respect!

Mjini lazima Uwe na watu ambao wanatahisisha Maisha yako na sio uishi kwa wasiwasi kila, labda kwa nyie waajiriwe, kwa sisi watafuta Pesa tunaitaji akili na ubunifu watu kwenye mambo ya msingi ya kimaisha!

Naweza enda Car wash naongea na simu, nikashuka gari inanguruma Bado, nikachukua taxi Bado naongea na simu, hata maagizo Sijaacha, baadae naambie Bocy tukuletee au unakuja!?
 
hilo la kujifanya wao wadereva ndio kwa vigar vya auto. ukienda na manual uwe mwangalifu. na kupiga pressure maji wao akishawasha ile mashine hajui sehem ya ku adjust wametutia hasara rrang ikavimba ikabid ikakwanguliwe bonet zima. hata wale vijana wa electric wanapenda kufungua sensor na kuziiba
 
Back
Top Bottom