Ukiweka milioni 200 kwenye fixed deposit unapata mrejesho wa 1.5m kwa mwezi

Ukiweka milioni 200 kwenye fixed deposit unapata mrejesho wa 1.5m kwa mwezi

Kiwanja cha 30M upate apartment za kupangisha usd 500!? Unaota ndoto ya mchana[emoji23][emoji23][emoji23] maana hizo bei ni mikocheni mbezi msasani huko utapata kiwanja cha 30M?!
Unaniambia mim au unamwambia mtoa mada?
 
Kwa kipato cha 1.5m hapo mbona unatoboa kabisa , mwez wa 1unachukua laki 5 unakodi shamba eka 10, mwez wa 2 unachukua laki 8 kwa ajili ya kusafisha na kupanda mpunga shambani, mwez wa 3 unachukua laki 4 kwa ajili ya palizi, baada ya miezi miwili mbele unavuna eka zako kumi za mpunga ambapo kwa wastani wa gunia 10 kwa eka unapata jumla ya gunia 100, kwa bei ya shamba gunia 1 unauza sh elf 80 , kama utauza magunia yote mia utavuna sh mil 8 fasta . Hiyo yote inatokana na faida ya kuwekeza fixed deposit kwamba hela ya kula nyumbani inakuwepo na hapo hapo unapata muda wa kunafanya uwekezaji mwengine juu yake.
 
Nikikutaga nyuzi kama hizi na pia comments za wachangiajI; binafsi naona wa-Tz tuna shida mahali.

Hiyo pesa inatosha kukufanya uwe bilionea chap!

Hiyo ni pesa nyingi sana hapa Africa!
 
Mwenye hiyo pesa tuingie nae mkataba kila mwezi nampa milioni5..

Yaani m200 ikuingizie 1.5 m kwa mwezi!?.
 
nikiweza kumili 200 m hapo siwezi kukosa hata 10 m kwa kwezi, nahiyo ni kwa uchache. Tuache uvivu na kufikiria kupata pesa kiwepesi tufanyeni kazi.
 
Benki hutumia hela zako na kununua treasuries BOT.
Kuwa mjanja, nunua treasuries from BOT.
Robo yake, nunua ardhi. Hasa shamba ambalo utaliendeleza kwa kulipima na kuwa viwanja.
Usijenge nyumba kwa ajili ya biashara, labda kama ni fremu.
Mkuu ufafanuzi kdg sie std7 tunachelewa kujua mengi nilitaka uniambie hiyo treasures ya b.o.t unifafanulie pia na nikitaka kuwekeza njia sake na taratibu zinakaaje?

Nawasilisha
 
Option nyingine ni kuwekeza kwenye real estate. Ukipata kiwanja location inayoeleweka unaweka. Kwa milioni 200 unasimamisha apartments za kueleweka. Hata kwa US$500 kwa mwezi kama ziko 5 utaiona faida.
Duh! hiyo 200m si shillingi jamani? Kama ni shillingi za Tanzania, zinawezaje kutoa apartments 5?
Kwa ufahamu wangu mdogo hiyo M200 utapata nyumba moja tu yenye hadhi ya kupata USD 500 pm, tena hapo kiwanja ulishakua nacho na kiko good location sio Vingunguti.
Ukitaka kununua na kiwanja kwenye hela hiyo hiyo, hautapata nyumba ya kupangisha kwa USD 500 pm. labda laki 5 za kitanzania. Pengine inawezekana mikoani (sina uzoefu nako) lakini kwa DSM sio rahisi.
 
Tena inawezekana benki ya posta ikaongezeka kwani nasikia wanatoa interest rate ya 13% per annum, ngoja nifuatilie zaidi nimshauri mstaafu fulani hivi akawekeze huko.
Wale waliokuwa wanauliza interest inayolipwa na benki kwa fixed deposit account. Niliongea na mmoja aliniambia wastani wa malipo ni kama hivyo ilivyo.

Hii inawafaa wasioweza kuzungusha pesa kwa njia ya biashara. Una uhakika wa kula kila mwezi na pesa yako iko pale pale.
Hakuna kitu hapo, utaweka pesa mara watatoa visingizio unapewa pungufu
 
Uzi mzuri umekaribisha michango mizuri kama kuwekeza kwenye hati fungani n.k.
Nimepata kitu toka kwa wajuzi wa biashara na fedha.
 
Option nyingine ni kuwekeza kwenye real estate. Ukipata kiwanja location inayoeleweka unaweka. Kwa milioni 200 unasimamisha apartments za kueleweka. Hata kwa US$500 kwa mwezi kama ziko 5 utaiona faida.
Apartment 5 kwa mil 200?...tena za kulipiwa 500$usd, tena na kiwanja kinunuliwe hapo hapo kwenye pesa hiyo?
 
Back
Top Bottom