Uko tayari? Dar es Salaam mpya inakuja. Serikali kutwaa eneo la mita za mraba 233,000. Maeneo ya Sinza, jirani na Mlimani City, Boko, SIMU2000 kuguswa

Uko tayari? Dar es Salaam mpya inakuja. Serikali kutwaa eneo la mita za mraba 233,000. Maeneo ya Sinza, jirani na Mlimani City, Boko, SIMU2000 kuguswa

Unajua mnapenda kujadili vitu vya kufikirika sana. Story za hivi ndio mnapenda. Hilo tangazo na sijui ramani nani kakueleza?

Mm nakueleza uhalisia, pesa ya kulipa watu fidia kwa sqm200000+ inatoka wapi? Ubungo maziwa pale Kuna eneo linatakiwa kuchukuliwa na kulipwa fidia kwa ajili ya BRT depot, toka 2022 hadi leo kesi imeenda mahakamani sababu ya mgogoro wa pesa za fidia kwa wananchi 90 tu. Ni bilion 8 lakini mvutano wake sio kitoto. Leo eneo Kama sinza kwa sqm 200000 unategemea nn? Mnahisi pesa zipo tu?

Wawekezaji walipe fidia kubwa kwa eneo kama Hilo ili kuweka kitu gani kitachorudisha pesa iliyowekwa? Na huyo mwekezaji ni nani? Nakumbuka enzi za JK kulikua na hizi story za kigamboni itatengenezwa kama Dubai.

Nadhani ni Bora tujadili vitu halisia na sio hisia.

Atakayetaka kununua ndiye atakayelipa fidia lakini kumbuka sio lazima iwe fidia ni kwamba wanaolipwa fidia ni maeneo serikali itakayoyataka kwa miuondombinu yake, wengine wote ni kwamba wamepewa ruhusa ya kuuza nyumba/assets zao! Watakasubiri fidia ni barabara zitakapopita na mali za umma zitakapojengwa, wengine wote watauza kwa raia na makampuni yanayotaka

Na miradi ya namna hii kama ina mikopo na misaada inakuja? Who knows, serkali hii ina maovu mengi lakini pia sio lazima kila kitu kiwe kiovu. Itakuwa mpango huu umechukua miaka na wataalam wa nje na ndani kuuandaa hadi umefikia viwango vya hatua hizi, wakati ni ukuta tusubiri na tuone kama hii ambitious project/program itafanana na zingine ila napongeza kwa maono haya hata kama yatachukua miaka 100 yatabaki kwenye historia
 
H

Mimi najichanganya au wewe?
Wewe unaamini sababu ni rent kubwa, mm nakuambia sababu sio ukubwa wa rent Bali uchumi tulionao hauruhusu.

Hata rent ilishushwa bado sehemu kubwa itabaki wazi sababu uchumi wa watu hauruhusu. Wewe umeandika nadharia. Mambo ya kufikirika zaidi ikiwa uhalisia hauendani kabisa

Unasema yajazwe maghorofa hapo kwenda juu, bila kujua wataojenga hayo maghorofa watapata hasara sababu uchumi wa watu upo chini. Ndio nikakutolea mfano hapo sinza Kuna psssf tower ipo wazi hadi leo hii
Mkuu,

Kujengwa kwa makazo nako kitachochea uchumi kujua kama kutafanywa kqa mkakati.

Ni kiasi cha serikali kujipanga kutumia wakandarasi wa ndani, kudhibiti mzunguko wa oesa uwe ndani.

N8mekuambia waliopo hapo hawahitaji kuhamishwa, wakioewa nyumba hapohapo ghorofa linajengwa la ghorofa 25, ghorifa za chini unawapa waliopo hapo wanazimikiki iutright wewe serikali au muwekezaji unachujua juu huko, hapo aliyepo sasa.

Hiyo tiwwr ya Sinza iki wazi kwa sababu iko moja, ina rent za juu sana, ni commercial property.

Ukijenga nia za hivyo, kwa residential apartments, kwa mpango wa kurudisha hela miaka mingu, huna sababu ya kuweka rent kubwa.

Ukiwa na special mortgage ya miaka 30 hapo hata wafanyakazi wa serikali unaweza kuwauzia apartments
 
Atakayetaka kununua ndiye atakayelipa fidia lakini kumbuka sio lazima iwe fidia ni kwamba wanaolipwa fidia ni maeneo serikali itakayoyataka kwa miuondombinu yake, wengine wote ni kwamba wamepewa ruhusa ya kuuza nyumba/assets zao! Watakasubiri fidia ni barabara zitakapopita na mali za umma zitakapojengwa, wengine wote watauza kwa raia na makampuni yanayotaka

Na miradi ya namna hii kama ina mikopo na misaada inakuja? Who knows, serkali hii ina maovu mengi lakini pia sio lazima kila kitu kiwe kiovu. Itakuwa mpango huu umechukua miaka na wataalam wa nje na ndani kuuandaa hadi umefikia viwango vya hatua hizi, wakati ni ukuta tusubiri na tuone kama hii ambitious project/program itafanana na zingine ila napongeza kwa maono haya hata kama yatachukua miaka 100 yatabaki kwenye historia
Mkuu umeandika mambo ambayo hayaeleweki, nimesoma lakini nimeshindaa kuelewa.

Ngoja nikuulize hivi pengine tutaelewana. Ni Nani amekuambia kuna huo mradi wa kujenga upya hilo eneo? Au umetoa wapi hizi habari za eneo hilo kutakiwa kupangwa upya au kujengwa upya?
 
Ifutwe yote tu, temeke yote, yaani mitaa ya uswahilini yote, mwananyamala, kijitonyama, gongo la mboto, mbagala, tabata, bunju, tegeta, ukonga. Uswazi yote zukumiza mbali. Peleka bagamoyo, kisarawe, chalinze ili ijulikane tu jiji linapangwa upya
 
Hapo kwa individual hawezi kufanya huo uwekezaji ila inakuwa ni kampuni ya commercial real estate wanaweza kufanya hivo gradually sio kwa mkupuo.

Unajua pale buguruni nyumba hazijajengwa kwa ustaarabu sasa mfano ukinunua nyumba za chini kama 10 kwa hata milioni 300 kwasababu zile nyumba ni choka mbaya, hapo unaweza pata eneo kubwa ukapandisha apartment za kwenda juu za ghorofa 10 ambapo hapo unaweza kupata apartment za kutosha hata zaidi ya 50
Unajua mnaongea mambo ya kufikirika sana. Hiyo commercial real estate yenye mtaji mkubwa wa kununua na kujenga upya kata nzima ni ipi hiyo?
 
ningependa kuanzia mori kijiweni mpaka ile ya kutokea tandale magomen mpaka pale kwenye makabur waichkue ipangwe upya
 
Hizo ni alinacha, rejea bonde la msimbazi watu wamelipwa hela isiyozidi milioni mbili na kutakiwa waondoke. Usidhani msimbazi ni kwa ajili ya kujenga njia za mafuriko tu mpango uliopo ni kuwapa wawekezaji yale maeneo wajenge maghorofa lakini wamiliki halali wa hayo maeneo wamelipwa pesa kiduchu.

Huo mpango tegemea vilio na kusaga.meno kwa wamiliki wa hayo maeneo, subiri kidogo utaona watu wazima wanalia kama watoto wadogo including huyo mjomba wako.

Nchi hii unajengwa uchumi nyang'anyi sio uchumi jumuishi.
Siongelei uchumi uliopo.

Nimepanua mawazo zaidi kuongelea uchumi unaowezekana kuwepo.

Hii ndiyo tofauti yako wewe na mini.

Wewe umeifunga akili yako kwenye uchumi uliopo mpaka unashindwa hata kuzungumzia uchumi unaoweza kuwepo.
 
Hata hayo makaburi wayahamishe tu ili viwanja vipatikane, makaburi ya kinondoni, kisutu, chang'ombe, mburahati na mengine, si ndiyo wanataka kupanga jiji upya? Kazi wanayo
 
Mkuu,

Kujengwa kwa makazo nako kitachochea uchumi kujua kama kutafanywa kqa mkakati.

Ni kiasi cha serikali kujipanga kutumia wakandarasi wa ndani, kudhibiti mzunguko wa oesa uwe ndani.

N8mekuambia waliopo hapo hawahitaji kuhamishwa, wakioewa nyumba hapohapo ghorofa linajengwa la ghorofa 25, ghorifa za chini unawapa waliopo hapo wanazimikiki iutright wewe serikali au muwekezaji unachujua juu huko, hapo aliyepo sasa.

Hiyo tiwwr ya Sinza iki wazi kwa sababu iko moja, ina rent za juu sana, ni commercial property.

Ukijenga nia za hivyo, kwa residential apartments, kwa mpango wa kurudisha hela miaka mingu, huna sababu ya kuweka rent kubwa.

Ukiwa na special mortgage ya miaka 30 hapo hata wafanyakazi wa serikali unaweza kuwauzia apartments
Unaongea mambo ya kufikirika zaidi. Hayo ni maeneo ya watu binafsi, kuyachukua ni kuwalipa fidia sababu wakati unajenga wao hawatakuwepo au unafikiri utajenga bila kubomoa nyumba zao?

Hakuna namna nyingine zaidi ya kukipa fidia waliopo. Wahame alafu ndio uanze huo ujenzi. Hayo ya kukubaliana mje mgawane, huo muda hao wakazi wote wanakua wanaishi wapi?
 
Mkuu umeandika mambo ambayo hayaeleweki, nimesoma lakini nimeshindaa kuelewa.

Ngoja nikuulize hivi pengine tutaelewana. Ni Nani amekuambia kuna huo mradi wa kujenga upya hilo eneo? Au umetoa wapi hizi habari za eneo hilo kutakiwa kupangwa upya au kujengwa upya?

Tumuulize mtoa mada mkuu! Nimechangia kama mpita njia anayekerwa na status quo tu mkuu sina maslahi yoyote
 
Unaongea mambo ya kufikirika zaidi. Hayo ni maeneo ya watu binafsi, kuyachukua ni kuwalipa fidia sababu wakati unajenga wao hawatakuwepo au unafikiri utajenga bila kubomoa nyumba zao?

Hakuna namna nyingine zaidi ya kukipa fidia waliopo. Wahame alafu ndio uanze huo ujenzi. Hayo ya kukubaliana mje mgawane, huo muda hao wakazi wote wanakua wanaishi wapi?
Kwani wapi nimekataa kulipa fidia?
 
Dar inapangwa upya, Sinza inasukwa upya, maeneo jirani na Mlimani City yanasukwa upya. Serikali inaenda kutwaa eneo la ukubwa wa mita za mraba 233,000 na kulipanga upya.

Maeneo kama Sinza yana viwanja vya 20/20, na maeneo hayo kwa sasa ndio ujenzi mkubwa wa maghorofa unakuja. Ni vyema serikali imeyatwaa maeneo hayo ili iyamiliki, ifute ramani ya eneo hilo, ifidie, kisha ilipange upya, na kugawa viwanja vikubwa kwa uwekezaji mkubwa.

Kama ujenzi ungeendelea kwa hali ilivyo, maeneo hayo yangekuwa hayana mvuto, na yenye msongamano.

Hii iende mpaka Tandale kwa awamu, tuipate Dar tunayoitaka.
View attachment 3171283
Mipango mizuri sana, kwenye utekelezaji ndipo tutaona NIA na usahihi wake
 
Back
Top Bottom