Ukosefu wa maadili unatisha kwa kasi unayoporomoka Tanzania

Ukosefu wa maadili unatisha kwa kasi unayoporomoka Tanzania

Wazazi wa hiyo miaka uliyoitaja ndio wameshindwa kulea hawa watoto unaowaona leo hawana maadili.

Wazazi wenye maadili huzaa na kutoa watoto wenye maadili. Nyoka hawezi zaa jongoo.
Mbona kuna watoto wenye maadili, kumaanisha walilelewa na wazazi kimaadili.

Mzizi wa wa matatizo yote ni wazazi walioshindwa kutimiza majukumu yao. Ndio walioharibu hiki kizazi.
Jukumu la mzazi ni malezi kwa mtoto. Mtoto unavyomlea ndivyo anayokua.

Kusema sijui mambo ya utandawazi ni uongo na kisingizio cha kipuuzi cha wazazi walioshindwa majukumu yao.

Mtoto anajilea mwenyewe tangu akiwa mdogo unategemea nini?

Unakuta mzazi hajazeeka, hata miaka 60 haijui na haumwi ati anamtegemea mtoto amtunze, mtoto anitafute, upuuzi tuu.

Kila siku nasema hapa, lakini wapumbavu wanateteana na kuona kama nakosa adabu.
Nitakuwaje na adabu na watu waliokimbia majukumu yao?
Umeeongea point tupu.shida iliyopo ni wazazi wenyewe imagine mtoto wa umri miezi6 anaachiwa house girl mama anarudi saa2-3 usiku kesho anaondoka sa12 asubuhi halafu mtoto akifikisha umri wa miaka 3-4 anapelekwa yule anaanza kulelewa huko Kwa kisingio Yuko shule kumbe umeshindwa kumlea wewe.
Umeshindwa kumlea mtoto wako ni nani atakae kulelea? Kulea mtoto ni wajibu wa mzazi hutaki kulea acha kuzaa
 
Bila ya shaka, wengi wa wale wenye umri iliozidi miaka 40 watanielewa.

Tanzania yetu iliyokuwa inasifika ndani na nje ya nchi kwa maadili na nidhamu imeenda "arijjojo", wale waliowahi kucheza na vishada (kites) watanielewa nikisema "arijojo".

Nakumbuka miaka ya nyuma, kuna vijana nilikuwa nawasiliano nao sana US, wakati huo nami naishi nje ya Tanzania, akanambia kuna rafiki yake anatafuta mchumba nimtafutie, nikamwambia mbona wachumba wapo wengi na vijana siku hizi hakuna anaetaka kutafutiwa, akanambia hujanielewa, hataki mchumba tu, anataka mchumba kutokea Tanzania. Akanielewesha nikamuelewa, nikamuunganisha na watu Dar., Nafurahi kusema akapata mke na mpaka sasa wanazeeka pamoja, watoto zao wameshafikia umri wa kujukuu, kama bado, sina mawasiliano nao ya mara kwa mara.

Hiyo siyo point yangu bali ni mfano tu. Kama hayo yalikuwa mengi sana si kutokea Ulaya tu, hata nchi za jirani walitamani kuoa mwanamke wa Kitanzania, sababu kuu ikiwa ni maadili.

Leo hayo kukutana nayo ni nadra sana, sisemi yamekwisha kabisa, lakini yameporomoka kwa kiwango kikubwa sana. Ni nini kilichotufikisha hapo? Nafahamu wengi sana maisha wanayokutana nayo ndivyo yalivyo, hawatoweza kunielewa kabisa, kwani hawana cha kulinganisha nayo hayo, sisi wa zamani tunaoyaona kuwa ni maadili mema.

Wewe unayenisoma, maadili mema kwako ni yepi? Tutajie japo moja tu. Inawezekana kabisa nnavyoviona mimi kuwa si maadili mema, kwako ikawa ni ajabu kwanini hilo hayo si maadili mema.

My take; Maadili mema hayafundishwi tu, bali huanzia kwa kuigwa, je ni wazazi na walezi ndiyo tulikosea?
Utanda wazi ndiyo chanzo cha yote hayo,hakuna mchawi mwingine!!
 
Ni Simba aliyevaa ngozi ya kondoo jichanganye uone
Kondoo wewe simba wewe.

Tumekuelewa kwa kukusoma kati ya mistari. Unamaanisha waleeeee.

"Huku hayuko kule hayuko ankula huu".
 
Utandawazi ndio umeharibu kila kitu, especially ujio wa smartphones
 
Back
Top Bottom