Ukosekanaji wa Haki kwenye Mhimili wa Mahakama, kunaweza kuwa kunachangiwa na Majaji/Mahakimu wenye uwezo mdogo kubaini haki?

🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏
 
Mkuu bagamoyo, asante kwa hii post, kwa ruhusa yako, naomba kuitumia kama mbolea kuboreshea baadhi ya mabandiko yangu ya kilio cha haki.

Natanguliza shukrani.

Paskali
 
Update
Wanabodi, hili ni bandiko la zamani likiuangazia uwezo wa baadhi ya Majaji wetu kutoa uamuzi wa haki kwa kukosa jicho la roho la kuangazia haki.

Hoja hii imeleta matokeo chanya ambayo nimeyaeleza hapa
Msikilize Rais Samia anesema nini kuhusu majaji P
 
This is a typical case ya this scenario Ukosekanaji wa Haki kwenye Mhimili wa Mahakama, kunaweza kuwa kunachangiwa na Majaji/Mahakimu wenye uwezo mdogo kubaini haki?

Any right thinking member of the society, akiyasoma tuu hayo mashairi, atagundua this man is insane!, huyu sio mtu wa kupelekwa jela, ni mtu wa kupimwa akili na kuanza matibabu!.

P
 
GT Pasco nilipoona unamtaja bwana Lakha nilipatwa na shauku ya kumfaham mtu huyu hakika nilipata wasaa wa kusoma kitabu Cha kesi ya uhaini hakika alikuwa mtu mwenye uwezo mkubwa sana.

Pia niligundua kwamba majaji wa kipindi kile walikuwa majaji hasa sio hawa tulio nao sasa wanatia mpaka aibu kuwasikiliza bila hata kusoma hukumu zao ambazo hata mtu asiye na basic ya Sheria akisoma anaona wazi kabisa kwamba hatuna majaji na mahakimu bali wahuni.
 
Kiukweli hili linasikitisha sana!.
P
 
Wanabodi, hili ni bandiko la kitambo, hoja yake ni uwezo mdogo wa baadhi ya majaji na mahakimu wetu kuwa na jicho la tatu, jicho la ndani, jicho la roho kubaini haki.

Hoja hii inathibitishwa na kinachoendelea ndani ya mhimili wa Mahakama sasa. Jaji Mkuu Prof. Ibrahim Juma, ametimiza umri wa kustaafu kwa mujibu wa sheria tangu Juni 15, lakini kufuatia kukoseana majaji Rufaa wenye uwezo wa kushika nafasi ya Jaji Mkuu, imebidi Jaji Mkuu Prof. Ibrahim Juma aongezewe muda kidogo wakati wa kumuandaa mrithi wake.

Hivyo hoja yangu hii inapata nguvu!, yaani licha ya kuwepo majaji kibao wenye sifa za kuwa Jaji Mkuu, lakini bado hawatoshi, hali inayopelekea Jaji Mkuu aliyemaliza muda wake, kuongezewa muda mpaka mrithi muafaka apatikane.

Kuongezewa muda huku, kukamuibua Jaji Stella Mugasha Profesa Ibrahim Juma kuendelea kuwa Jaji Mkuu, Rais Samia anavunja Katiba ya JMT? hivyo na mimi nikashauri Jaji Mugasha Apewe Maua Yake Kupinga Uvunjifu wa Katiba Ukomo wa CJ, ila Mbona Hili ni Dogo Tuu, Kubwa ni Katiba Yetu Imenajisiwa! Why Wako Kimya?!.

Kuna vitu watu tunasema humu, wana wanapinga!. Majaji Rufani wenye sifa za kuwa Jaji Mkuu, wangekuwepo wa kutosha, kusingelikuwa na need kumuongezea muda CJ aliyemaliza muda wake!.
P
 
Kuna vitu watu tunasema humu, wana wanapinga!. Majaji Rufani wenye sifa za kuwa Jaji Mkuu, wangekuwepo wa kutosha, kusingelikuwa na need kumuongezea muda CJ aliyemaliza muda wake!.
Mkuu, wewe umejuaje kuwa majaji wa Rufani waliopo hawana sifa?? Kwa nini hata huyo Mugasha uone hana sifa wakati ameichambua vyema ibara ya katiba na kuitetea kuhakikisha uvunjifu hauendelei kuishi?
 
watu hawaelewi tu. hakuna hakimu au jaji asiyekula rushwa. kama yupo ni wachache sana. ukiondoa majaji wa mahakama ya rufaa, waliobaki woote kwenye judiciary hata uwaongezee milioni mia kwenye mshahara watakula tu rushwa kwasababu mahakama za kiafrika ni rushwa rushwa rushwa.
 
Mkuu, wewe umejuaje kuwa majaji wa Rufani waliopo hawana sifa?? Kwa nini hata huyo Mugasha uone hana sifa wakati ameichambua vyema ibara ya katiba na kuitetea kuhakikisha uvunjifu hauendelei kuishi?
Huenda mheshimiwa Rais kaona ingeleta shida kuwa na CJ mwanamke (hata kama sifa anazo)
1. Rais
2. Spika
3. CJ tena!?
 
Huenda mheshimiwa Rais kaona ingeleta shida kuwa na CJ mwanamke (hata kama sifa anazo)
1. Rais
2. Spika
3. CJ tena!?
Kama tulikuwa nao, wote ni wanaume, kwanini iwe shida wakiwa wanawake?.
P
 
Mkuu, wewe umejuaje kuwa majaji wa Rufani waliopo hawana sifa?? Kwa nini hata huyo Mugasha uone hana sifa wakati ameichambua vyema ibara ya katiba na kuitetea kuhakikisha uvunjifu hauendelei kuishi?
Hili sio swali!. Nimesema waliopo wote hawatoshi ndio maana imebidi aliyepo aongezewe muda wakati mrithi wake akitafutwa!.
P
 
Hili sio swali!. Nimesema waliopo wote hawatoshi ndio maana imebidi aliyepo aongezewe muda wakati mrithi wake akitafutwa!.
P
Ni swali. Aliyeongeza muda hajasema sababu ya kumuongezea muda, wewe umekuja na hitimisho. Ndio napenda kufahamu nini kilichokufanya uwaze hivyo? Ungeweza kusema kuwa kapendelewa lakini umesema kuwa ni kwa kuwa wengine hawana vigezo.
 
Ni swali. Aliyeongeza muda hajasema sababu ya kumuongezea muda, wewe umekuja na hitimisho. Ndio napenda kufahamu nini kilichokufanya uwaze hivyo? Ungeweza kusema kuwa kapendelewa lakini umesema kuwa ni kwa kuwa wengine hawana vigezo.
Kiswahili ni kigumu, kigezo pekee cha mtu kuteuliwa Jaji Mkuu ni kuwa JR. Hivyo ma JR wote wamekidhi vigezo vya kuwa CJ, sasa inapotokea CJ aliyeyopo amemaliza muda wake, anaongezewa muda, maana yake ni waliopo in line of seniority hawatoshi, hivyo mchakato wa kumtafuta anayetosha ukiendelea. Tofautisha kukidhi vigezo na kutosha!.
P
 
Mkuu, mahakamani moja ya sababu ya kumtaka Hakimu au Jaji kujitoa kwenye kesi ni upendeleo. Wote, mdai na mdaiwa, mnakuwa na haki sawa ya kusikilizwa lakini kwa makusudi au kwa sababu azijuazo Jaji au Hakimu anaamua kumpa haki zaidi mmoja wenu (anampendelea). Sasa hata kwa JM ningetegemea nyongeza yake isiyostahiki ioneshe kuwa ni upendeleo, lakini wewe umehitimisha kuwa hawatoshi, na hautoi sababu ya kufikia hitimisho hilo. Masuala ya kutosha hayapo kikatiba.
 
“Hawatoshi” 🤔. Code muhimu sana hii ya chama inayoeleweka na wanachama kindakindaki. Katiba haihusiki kabisa hapa.
 
sina mashaka na uwezo wa mahakimu au majaji wetu Tanzania, BUT sina imani nao kabisa kwa sababu wana itikadi za CCM ya Ole Sabaya, na Pole pole, ya Bashiru, ya Makonda nk. Tangu CCM iingiwe na roho ya ku inflict pains to innocents mahakimu wetu wamekuwa wakiakisi nia hiyo. Hata kama kesi ya kubambika ya Mbowe, au ya masheikh, au ya wale waliohukumiwa maisha kutokana na kesi ya uchaguzi kufutwa bado BADO JINSI KESI HIZO ZILIVYOENDESHWA NA MAJAJI WETU HATUTASAHAU. HIVI KWELI MTU ALIYETUMIKA KUWAPORA WATU FEDHA KUPITIA PRE BARGAIN ANA KUWA JAJI????? Sidanganyiki. sina shida na CCM shida yangu ni roho tesi iliyowaingilia.
 
Mkuu unataka kuitenga CCM na dola (mahakama) na watendaji wake? Hapo umeshadanganyika! Hiyo roho tesi iliyomo ndani yao ndio CCM yenyewe!

Huwezi kupewa nafasi ya maana katika serikali ya CCM kama huwezi kuwa na “roho ya kutu” mara ikibidi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…