View attachment 1841771View attachment 1841772
Wanabodi,
Kama kawaida yangu, kila siku za Jumatatu, huwaletea makala za "Kwa Maslahi ya Taifa", ambayo huchapishwa na gazeti la Nipashe la Jumapili, ambazo ziko kwa mtindo wa maswali, majibu ya maswali hayo, utayapata wewe mwenyewe, na kisha tutawatafuta wahusika, ku balance hii mada, hivyo kwa mada hizi za mhimili wa Mahakama, mtu wa kubalance tuhuma hizi ni Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma.
Baada ya makala kuhusu Ofisi ya DPP, wiki hii, naugeukia Mhimili wa Mahakama.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati akiwaapisha Majaji wapya 28 wa Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani, Rais Samia alisema na hapa ninanukuu
“Tatizo la ucheleweshwaji wa kesi katika Mahakama zetu bado lipo,
kama mnavyosema Wanasheria haki inayocheleweshwa ndio haki inayokataliwa, hivyo ni imani yangu kuwa baada ya upatikanaji wa Majaji hawa ucheleweshaji wa kesi Mahakamani utapungua na hatimaye haki kupatikana kwa wakati,” alisema Mhe. Rais Samia.
Rais Samia akaendelea kwa kuitaja Ibara ya (107) A ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Mamlaka ya utoaji haki ni Mahakama, “hivyo jukumu lililopo mbele yenu ni kubwa sana, basi ni vyema mkatekeleze majukumu yenu mliyopewa kwa uaminifu, mkaongoze vyema na mkaongozwe na utu na nafsi zenu katika kuwatumikia wananchi,” Mwisho wa kunukuu.
Kwa upande wake, Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma alimshukuru Mhe. Rais kwa uteuzi wa Majaji hao wapya huku akiwa na imani kuwa idadi hiyo italeta mabadiliko makubwa ambayo yataonekana mara moja.
Jaji Mkuu, Prof. Juma alisema “Mhe. Rais napenda nichukue fursa hii kukushukuru kwa kutupatia Majaji hawa, idadi hii itasaidia kupunguza mzigo wa mashauri kwa Majaji waliopo na hivyo kusaidia kuleta mabadiliko ambayo yataonekana mara moja,” alisema Mhe. Jaji Mkuu.
Prof. Juma, aliendelea “Mhe. Rais idadi ya Majaji inapanda na kupungua kulingana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kustaafu kwa Majaji pamoja na Majaji wengine kupangiwa majukumu mbalimbali, hivyo bado tunaomba kuendelea kupatiwa Majaji kadri nafasi zinapopatikana ili kuendelea kutoa huduma ya haki kwa kuwa wananchi wengi kwa sasa wanafahamu haki zao na hivyo kufungua kesi kwa wingi,” alieleza Jaji Mkuu.
Kwa vile hoja yangu ya makala hii ni kuangazia uwezo mdogo wa baadhi ya Majaji na Mahakimu wetu, kutokuwa na jicho la ndani, lenye uwezo wa kuona haki, kunakochangia ucheleweshaji wa kesi na ukosefu wa haki, naomba kutoa historia fupi ya maisha yangu na jicho la ndani.
Mimi Paskali Mayalla, zaidi ya kuwa mwandishi wa habari na mtangazaji, mimi pia mtu wa mastori, yaani stori teller, hivyo kwa wapenzi wa mastori, unaweza kufuatilia sehemu hii ya Mastori ya Pasco Mayalla, ila wewe kama sio mtu anayependa mastori, unaweza ku skip hii segment ya mastori
Mastori ya Pasco Mayalla
Lengo la simulizi hii ni kuwadurusu baadhi ya majaji na mahakimu wetu, jee wana uwezo wa kubaini hatia kwa kutumia jicho la ndani?, jee kwenye utoaji wa humuku zao, wanazingatia "utu na nafsi"?, na sio kutegemea tuu vifungu vya sheria na ushahidi pekee?. Ili jinai itendeke ni lazima kuwepo kwa mambo mawili, actus reus (kitendo cha jinai) na mens rea, (nia ya kutenda jinai). Jee mfumo wetu wa kupata majaji na mahakimu wetu, unahusisha amplitude test kubaini uwezo wa hao majaji na mahakimu kutumia jicho la ndani la utu na nafsi kubaini nia ovu ya kutenda jinai?. Jibu ni hapana!.
Tanzania ili mtu kuwa hakimu, ni kwanza kuhitimu shahada ya sheria, na kuomba ajira ya uhakimu, kwenye kuajiriwa, kupitia Tume ya Kuajiri ya Mahakama iliyo chini ya Jaji Mkuu, ila kwenye hadidu za rejea, hakuna amplitude testi yoyote kupima uwezo wa waombaji kuwa na jicho la ndani la kubaini jinai, na matokeo yake ndio baadhi ya hawa mahakimu kwenye mahakama zetu wenye uwezo mdogo, na matokeo yake ni kwa baadhi yao, kutokuwa na uwezo wa kutoa hukumu za haki huku wengine wakituhumiwa kula rushwa!. Udhibitisho wa tuhuma hii ya uwezo mdogo wa mahakimu wetu kutoa hukumu za haki ni mlolongo wa rufaa, na matokeo ya rufaa nyingi kukubaliwa.
Ili kuwa Jaji wa Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani ni Tanzania, ni kwanza kuwa mwanasheria, kisha jina lako likapendekezwa na Tume ya ajira ya Mahakama, na kupelekwa kwa rais, mtu unateuliwa kuwa jaji, napendekeza, ili Tanzania tupate majaji kama Lord Denning, tuongeze vigezo vya mtu kuteuliwa Jaji. Kila mtu anaweza kuwa mwanasheria, lakini sio kila mwanasheria anaweza kuwa Jaji. Mfano mzuri ni mtu aliyekuwa DPP kinara wa ukandamizaji wa haki, halafu mtu huyo anateuliwa kuwa Jaji, unategemea nini?!. Kama akiwa DPP alifanya madudu yote yale ambayo sasa ndio yanafumuliwa, akiwa Jaji, atatenda haki?. Unless kama wakati akiwa DPP, baadhi ya maamuzi yake ilikuwa ni kufuata maelekezo, then sasa akiwa Jaji, atakuwa Jaji mzuri, lakini kama akiwa DPP alishindwa kutenda haki, haitegemewi akiwa Jaji atatendaje haki!.
Nchi za wenzetu hadi wana vifaa maalum vya kubaini kama mhusika anasema uongo, (lie detectors), Majaji wetu na Mahakimu lazima wawe na uwezo huo, ili kuepuka kuwatesa watu kwa kuwasweka ndani miaka mingi watu wasio na hatia. Yako mazingira mtu anakutwa na ushahidi wa kuhusika na jinai fulani, na wengine hadi kuhukumiwa kunyongwa, na akiisha nyongwa ndipo ushahidi unakuja kupatikana kuwa amehukumiwa kwa makosa. Majaji na Mahakimu wetu, wakiwa na jicho la rohoni, wataweza kuiona haki na kutoa hukumu ya haki hata kama ushahidi utaonyesha kuhusika.
Kwa maoni yangu, tatizo la msongamano wa kesi, sio idadi ya majaji na mahakimu, bali ni ubovu wa sheria zetu na uwezo mdogo wa baadhi ya majaji na mahakimu kukosa jicho la roho kubaini hatia, na udhaifu wa vyombo vyetu vya upelelezi. Mfano kwa tukio kama lile shambulio la Lissu, hata sisi tuu waandishi wa habari za uchunguzi, tungehitaji IJ ya siku moja tuu, kubaini chanzo cha wasiojulikana hao, na kukitumia kama lead kuwabaini, lakini kwa vyombo vyetu vya uchunguzi ni mpaka leo hakuna taarifa zozote!.
Kwa kesi kama ya kina Rugemalila, sisi waandishi wa habari za uchunguzi, tungehitaji siku 7 tuu, kuwawekea ushahidi wote mezani, lakini vyombo vyetu vya uchunguzi, ni zaidi ya miaka 4 sasa na bado kesi haijaanza kusikilizwa!, kwenye mazingira kama hayo, hata tungekuwa na majaji 100, wangefanya nini?.
Kwa bahati mzuri, mimi nimebahatika kuwa mwanafunzi wa Prof. Ibrahim Juma, hivyo namfahamu vizuri kwa kauli, uwezo na matendo, jicho hilo la rohoni analo, na kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, Mahakama ndio mhimili rasmi wa utoaji haki Tanzania, hivyo nina imani kubwa na Mhimili wa Mahakama chini ya Jaji Mkuu, Prof. Ibrahim Juma, licha ya changamoto za utoaji haki, inauwezo wa kuwapatia haki Watanzania.
Kufuatia mhimili wa mahakama kushiriki Maonyesho ya Saba Saba, makala ya wiki ijayo, nitawaletea ushiriki wa Mahakama kwenye Saba Saba.
Paskali
Update
Wanabodi kuanzia sasa, kwenye hoja zangu ninazoibua, zile ambazo zimepatiwa majibu nitakuwa natoa update ya hoja husika na jibu la hoja iliyopatiwa majibu.
Kwenye bandiko hili nilitoa hoja kuhusu uwezo wa majaji wetu kuwa na jicho la ndani la kubaini haki.
Hoja hii imeleta matokeo chanya ambayo nimeyaeleza hapa
Msikilize Rais Samia anesema nini kuhusu majaji
P