Ukraine: Iron Dome ya Israel haiwezi mudu kuzuia makombora ya Urusi, Iron Dome imeundwa kuzuia makombora dhaifu yatengenezwayo gereji kwa tech duni

Unakaribia kuvua nguo wewe!

Sio kwa kuchanganyikiwa huko 🤣🤣😇😇😇😜😜🤪🤪🤪
 
hayo ni makombora ya kupambana na HAMAS sio Urusi....waache ujinga ujinga wao hao ukraine
Hizbullah na katyusha zake alipata sifa sana2006 wakat iron dome ilipiga mzigo mpaka inapata moto inaishia kujam[emoji41][emoji41][emoji41]
 
Hii ya iron dome kuwa ya makombora ya wapalestina mnaisema leo ,siku zote mlikuwa mnaisifu hakuna kitachokatiza, Leo aibu imewapata.
 
Kwani ile zile mbinu za kinjekitile ngwale hazitufai tena mpaka tuanze kukumbatia vya wazungu?
 
Niliona hiyo report but they are unreliable kwenye kazi hiyo. Unajua zile infrared seeekers, radar na guidance ya over the horizon haifanyi kazi ground. Hiyo ni dalili ya kukosa makombora fulani kwa haraka wakati huo, na pia ni njia ya kudump S-300 missiles kama zinaisha matumizi ila S-400 sio ya zamani missiles zake zitakuwa na muda bado. Ni gharama sana unaingia

Its better waendelee kutumia anti ship missiles za zamani kama walivyofanya wiki chache nyuma maana meli iko kwenye surface tena zile zina accuracy kubwa kwani meli hutembea majini na inakuwa sehemu hakuna different geographical features
Warusi wanapenda silaha zenye secondary capabilities
 
Israel huwa hawatoi hovyo silaha zake, hata Marekani walipoioatia Iron Dome battery moja ya majaribio waligoma kutoa keys hivyo Marekani haiwezi kufanya integration na mifumo yake ya ulinzi kuwa na layer ya defence. Sasa waligoma kutoa keys kwa Marekani iliyochangia gharama za development ya huo mfumo ndio waje kuutoa kwa Ukraine.

Achana na Iron Dome ya kina Hamas na Hezbollah. David's Sling ndio mfumo wa makombora ya kisasa ambao hata huwa hautumiki ovyo kwa kuwa maadui wa Israel wanatuma mabati hewani hayana hata guidance. Kwa sasa hata Iron Dome wanaona ni dharau kuitumia, unatumia missile ya $30,000 kufanya interception ya bati la $600 hewani. Sasa wako wanadevelop mfumo wa kutumia laser, gharama ni umeme tu na spare parts
 
Kwanza Iron Dome tangu mwanzo haikutengenezwa kutungua Makombora ya ballistic au cruise ilitengenezwa maalumu kujilinda dhidi ya maroketi na mizinga na kwenye kazi hiyo ipo vizuri ikiwa na ufanisi wa zaidi ya 90%.

Kwenye masuala ya Ulinzi wa anga Israel NI moja ya nchi yenye mifumo imara Sana ya kujilinda Kama Arrow 2&3,David Sling,Barak-8,nk.

Wakati wa Vita ya Armenia na Azerbaijan mfumo wa Israel wa Barak-8 ulitungua Makombora ya Iskander ambayo yalivurumishwa na Armenia kushambulia Azerbaijan. Haya Makombora yalikua yakiogopeka Sana kwamba yanaweza kukwepa tactical air defense za Azerbaijan sababu kwenye flight path yake kombora linafanya maneuver za kutosha lakini yalitunguliwa na Barak 8
Israeli Barak-8 missile shot down Russian Iskander missile - Defence View

Mwaka 2017 baada ya F-15 za Israel kufanya mashambulizi ndani ya Syria,Syria walirusha Makombora ya S-200 kujaribu kuzitungua wakati zinarudi kwenye mission lakini Makombora ya S-200 yalitunguliwa na mfumo wa Arrow 2 na ndio ilikua mara ya Kwanza kutungua kombora tangu ianze kufanya kazi miaka ya 2000. Iliwashangaza experts wengi wa kijeshi kwamba ni mara ya Kwanza Kwa Air defense kutungua kombora la air defense nyingine ya adui.

Israel's Arrow anti-missile system 'in first hit'
 
😆labda uwe nachuki zako kutoka kwenye quran na sunnah, ila kiukwel israel wako vizur sana,.
Bro tafuta nyuzi zangu kuhusu Israel ndio utaelewa msimamo wangu Iron Dom haiwezi kuzuia ballistic kama alivyosema waziri za.Ulinzi wa Ukraine.

Labda David Slings au other anti air to ground missiles
 
Hata F14, F15 na F16 pamoja na F35 za Israel huwa wanazifanyia modifications na kuongezea some electronics features zinazowafaa wao
 
Hata F14, F15 na F16 pamoja na F35 za Israel huwa wanazifanyia modifications na kuongezea some electronics features zinazowafaa wao
Modification ya F-35 ya Israel inaitwa Adir na ndio nchi pekee imeruhusiwa na Marekani kufanya ujanja kwenye hiyo ndege. Waisraeli suala la kuamini mtu kwenye ulinzi wao hawataki. Kwenye cyber wako vizuri sana
 
Nakumbuka hii scenario. Bila Israel kuingia makubaliano na Russia kuhusu ruhusa ya Syrian airspace tungeona mengi na haya maajabu yanayoshuhudiwa hapa yengeshajulikana muda.

Ni kama Turkey ilipofikia makubaliano na Russia kuhusu patrols za Northern Syria. Hizi Bayraktars zilianzia kazi uko tukahisi bahati mbaya, hapo zilitoka kuonyesha uwezo kule Libya nako tulihisi wamebahatisha. Tukakaa kidogo zikaonekana Nagorno-Karabhak nikaamini rasmi zina uwezo
 
Modification ya F-35 ya Israel inaitwa Adir na ndio nchi pekee imeruhusiwa na Marekani kufanya ujanja kwenye hiyo ndege. Waisraeli suala la kuamini mtu kwenye ulinzi wao hawataki. Kwenye cyber wako vizuri sana
Hapo sawa kumbe kuna watu hawajui hii ishu
 
Modification ya F-35 ya Israel inaitwa Adir na ndio nchi pekee imeruhusiwa na Marekani kufanya ujanja kwenye hiyo ndege. Waisraeli suala la kuamini mtu kwenye ulinzi wao hawataki. Kwenye cyber wako vizuri sana
Na wamezimodify kwelikweli sasa hivi zinaweza kufanya long range mission mfano zinaweza kuruka moja Kwa moja toka Israel zikaenda mpaka Tehran na kurudi bila ya kua refueled mid air na tankers. Na wametengeza mabomu yake yenye uzito wa tani moja maalum Kwa kubomoa miundombinu iliyofukiwa chini ya ardhi
 
Lakini hizi drones sio sophisticated Kama za Marekani au Israel lakini nashangaa kwann Urusi zimewapa Sana shida kule Ukraine.l,maana kuanzia speed, electronics mpaka payload hazifikii kabisa hata zile Predator za USA
 
Lakini hizi drones sio sophisticated Kama za Marekani au Israel lakini nashangaa kwann Urusi zimewapa Sana shida kule Ukraine.l,maana kuanzia speed, electronics mpaka payload hazifikii kabisa hata zile Predator za USA
Ukileta Predator inaweza shambuliwa na S-300 au S-400 maana ni high flying na ina radar cross section kubwa kiasi. Hizi Bayraktars ni medium na zina some stealth features ndio maana hazishikiki kirahisi. Sasa ona wanashindwa kuzua vizuri Bayraktar alafu wanataka wazuie F-35 na F-22
 
Na wana external tanks wametengeza ndio maana range yake kubwa. Lazima wapate corridor kutoka nchi moja ya Kiarabu wapite ndio waingie Iran kwa kutumia F-35, kama walivyofanya mission ya Iraq kwenye Osirak nuclear site miaka ya 1970 sijui 80
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…