Ukweli kuhusu waasisi wa TANU na harakati za kupigania uhuru

Status
Not open for further replies.
watoto wa mjini bana,wakibahatisha kuukimbia umande,basi inakuwa taabu-eti,"pepo mbaya naona kakatiza hapa"
 
Ungekuwa credible kama ungesema haya mapema. Pepo mbaya aliishaingia hapa. Na ataambiwa kuwa tumemstukia bila kificho.

Amandla.......

FM Mkuu achana na hawa kina AMI wasio na uelewa cha nini kinachoongelewa, they were never contributors to this debate intellectually in the first place.
 
FM: It is OK let us move on. Insha Allah napitia kumbukumbu zangu ili niweze kuweka moja ya kufurahisha wanaukumbi tustarehe na yale ya kale yaliyofanywa na wazee wetu:

UAMUZI WA BUSARA WA TABORA
Kumbukumbu ya Uchaguzi wa Kura Tatu 1958

na Mohamed Said

KITABU KIPYA KUHUSU HISTORIA YA KUDAI UHURU WA TANGANYIKA

Katika moja ya misiba ya Tanzania ni kutokuandikwa kwa ukweli historia ya wazalendo walopigania uhuru wa nchi hii. Vitabu vichache vilivyoandikwa vimejikita zaidi katika kujipendekeza kwa viongozi walio madarakani kuliko ukweli wenyewe ulivyokuwa. Hii imeifanya historia ya Tanzania kuwa sawasawa na mchuzi uliokosa viungo. Matokeo yake chakula kinakuwa doro hakina ladha. Sasa ni miaka hamsini toka siku ile kwa mara ya kwanza TANU katika mkutano uliofanyika Tabora ilipoamua kuingia katika uchaguzi mkuu wa kwanza licha ya masharti magumu yaliyowekwa na serikali ya kikoloni. Masharti ya kibaguzi na kudhalilisha ambayo TANU ilipania kuyakataa na kususa kushiriki katika uchaguzi ule. Endapo hilo lingetendeka chama pinzani cha wazungu United Tanganyika Party (UTP) ingepata mteremko na kuzoa viti vyote na hivyo kuingia katika Baraza la Kutunga Sheria. TANU ingebaki nje ya ulingo wa siasa na ikawa msemea pembeni.

Katika kitabu hiki mwandishi anaeleza yale ambayo hayafahamiki kwa wengi ni kwa nini suala la kura tatu lilitishia kuigawa TANU pande mbili. Moja likiwa na Mwalimu Nyerere rais wa TANU na jingine likiongozwa na Zuberi Mtemvu, Sheikh Suleiman Takadir, Ramadhani Mashado Plantan na wazalendo wengineo. Katika kitabu hiki mwandishi anamchukua msomaji na kumkutanisha na wazalendo ambao lau kama wanahistoria wa leo wamewapuuza ukweli unabaki palepale kuwa bila ya kuwataja hawa katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika na hata historia ya Mwalimu Nyerere mwenyewe basi historia hiyo si tu itakuwa haijakamilka bali itakuwa historia ya uongo.

Mwandishi wa kitabu hiki kwa hakika ni mpiga hadithi kwa jinsi anavyowaleta wazalendo katika kurasa za kitabu. Mathalan anawajulisha wasomaji wake Mshume Kiyate, dalali wa samaki katika soko la Kariakoo lile la zamani la miaka ya 1950. Katika soko lile mkuu wa soko alikuwa Abdulwahid Sykes mmoja wa wazalendo 17 walioasisi TANU. Pale sokoni ndipo palipotoa wanachama wa mwanzo wa TANU mmoja wapo akiwa Mzee Mshume Kiyate, mzee aliyeheshimika sana mjini. Wangapi wanaojua leo mchango wa hali na mali wa Mzee Mshume Kiyate kwa Mwalimu Nyerere binafsi na katika Baraza la Wazee wa TANU?
 
Another fool! Jazba ipi ya KIDINI? Unataka kudai kuwa nawaona wapuuzi kwa sababu ni waislamu? Upuuzi nao una dini? Basi, iko kazi.

Amandla......
Hee! Fundi sasa unatukana kila mtu,mimi,Mohammed,Yaya.Hata wenzako akina Lole wakikupoza husikii tena.Mimi sikupendelea iwe hivyo lakini najuwa umeuona huu mjadala wa kutetea kudhulumiwa kwa waislamu sasa umekuwa moto kwako.Nilikushauri mapema kaa kimya.
Nakukumbusha tena kuwa hivyo munavyojidai navyo na kutukoga waislamu musingevipata kama si upendeleo na kudhulumiwa sisi.Ukristo hauna historia ya kufanya haya.Mambo kama haya ni mambo ya waislamu katika imani yao.Hili nalo utabisha?.
 
Wanaukumbi tutulize na tuendeleze mjadala kwa taratibu hapana haja ya kuparurana. Haya ni mawazo na ghitilafu ni jambo la kawaida sana. Ingekuwa sote tunakubaliana kwa kilajambo dunia ingechosha na kuchusha. Hebu msomeni Mzee Mshume. Huyu Mzee akikaa Mtaa wa Tandamiti karibu na Mtaa wa Gogo ilipokuwa moja ya nyumba za baba zangu. Nyumba yetu ilikuwa Gogo namba sita na nyumba ya mwisho mtaani ilikuwa nyumba ya mama yake Abdu Mgunya mmoja wa marafiki zangu utotoni. Hapa kwao ndipo ilipokuwa club ya Kilwa Jazz katika miaka ya 1960. Nje ya nyumba hii pakichezwa bao na ni hapo ndipo nilpomjulia Abdallah Kassim Hanga. Akija pale kucheza bao takriban kila siku. Sasa turudi kwa Mzee Mshume Kiyate. Someni kwa furaha:

Napenda nianze dibaji ya kitabu hiki kwa kisa nilichoelezwa na
mmoja wa wazalendo wa nchi yetu – Ahmed Rashad Ali – kutokana
na kisa alichohadithiwa na Mwalimu Julius Nyerere mwenyewe.
Siku hiyo , Ahmed Rashad alikuwa pamoja na Dossa Aziz na Lucy
Lameck. Ilikuwa mwaka wa 1965 siku ile Ian Smith alipojitangazia
uhuru. Ahmed Rashad wakati ule alikuwa Katibu Mkuu Msaidizi
Idara ya Habari. Walimkuta Mwalimu Nyerere nyumbani kwake
Msasani anaandika. Ahmed Rashad anasema katika kutafakari mambo
yaliyokuwa yakiendelea Rhodesia Mwalimu Nyerere aliwahakikishia
kuwa Uingereza haitofanya lolote dhidi ya Ian Smith kwa kujitangazia
uhuru wa maguvu. Ahmed Rashad anasema Mwalimu Nyerere neno
alilotumia ni kuwa hawa ni mtu na mjomba wake. Inawezekana
labda Mwalimu Nyerere kwa kukumbuka historia ya kudai uhuru wa
Tanganyika aliwajua vyema Waingereza na fikra zao na kwa ajili hiyo
akakileta kisa hicho cha TANU. Mwalimu Julius Nyerere alikiita kisa
hicho ‘the TANU spirit' – yaani moyo wa TANU – vile ulivyokuwa
wakati wa harakati za kudai uhuru. Mwalimu Nyerere alisema kuwa
siku moja wakati wa kudai uhuru alikuwa anatoka nyumbani kwake
Magomeni Majumba Sita kwa miguu kuelekea Kariakoo ili kupata
mahitaji yake. Mwalimu Julius Nyerere alisema kuwa katika safari
hiyo mfukoni mwake alikuwa hana hata senti moja.

Akiwa njiani karibu na sehemu inayoitwa Mwembe Togwa,
Mwalimu alikutana na Mzee Mshume Kiyate. Mzee Mshume alikuwa
mfanyabiashara wa samaki katika soko la Kariakoo. Mzee Mshume
alikuwa mzee aliyeheshimika sana mjini Dar es Salaam na alikuwa
mmoja wa wazee katika Baraza la Wazee wa TANU. Mwalimu
Julius Nyerere akamfahamisha Mzee huyo kuwa anakwenda sokoni
Kariakoo lakini hakuwa na fedha za kununulia mahitaji yake. Mzee
Mshume Kiyate aliingiza mkono katika koti lake, akatoa shilingi mia
mbili na kumpa Mwalimu Julius Nyerere. Ukitaka kujua thamani ya
fedha hiyo kwa wakati ule, naitoshe kujua kwamba ilimgharimu mtu
shilingi mia tano tu kujenga nyumba ya vyumba sita katika eneo la
Kariakoo.

Kutokana na hali hii Mzee Mshume aliona itakuwa ni kumtwisha
Mwalimu Julius Nyerere mzigo ikiwa atakuwa anashughulika na
kuwatafutia wanawe chakula na wakati huohuo akiwa na jukumu la
kufanya kazi za TANU. Ndipo Mzee Mshume alipojitolea kuihudumia
nyumba ya Mwalimu Julius Nyerere kwa chakula. Alifanya hivyo hadi
uhuru ulipopatikana. Baada ya uhuru Mwalimu Nyerere alimwomba
Mzee Mshume aache kufanya hivyo lakini alikataa. Badala yake
akamtafadhalisha Mwalimu Nyerere aendelee kupokea chakula chake
na kile ambacho kinatolewa na serikali kwake yeye kama mkuu wa
nchi, alimwomba Mwalimu awakirimu wageni wake. Mzee Mshume
Kiyate ni mfano wa aina ya viongozi wa TANU waliokuwepo wakati
wa kudai uhuru. Mzee Mshume alifanya mengi katika kudai uhuru na
hata baada yake.

Kisa hiki kwa mara ya kwanza kabisa kilihadithiwa hadharani
na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, marehemu Ditopile
Mzuzuri Mkiwaona, kada wa Chama Cha Mapinduzi. Ditopile
alikieleza kisa hiki kama alivyokieleza Mwalimu Nyerere kwa
Ahmed Rashad kwa nia ile ile ya kuonyesha moyo wa TANU. Kwa
bahati mbaya waandishi wa magazeti wakapotosha kisa kizima.
Badala ya kutoa umuhimu kwa moyo wa ukarimu wa Mzee Mshume
na kumueleza kama mzalendo aliyejitolea katika kupigania uhuru,
magazeti yakageuza maneno ya Ditopile kuwa masimango kwa
Mwalimu Nyerere, yaani alikuwa akilishwa chakula bure. Kwa ajili
hii nafasi ambayo ingeliweza kutumiwa ili kueleza umuhimu wa Mzee
Mshume na historia ya TANU ikapotezwa.

Baada ya maasi ya wanajeshi wa KAR tarehe 20 Januari 1964
kuzimwa na Jeshi la Kiingereza, TANU ilifanya mkutano mkubwa sana
katika viwanja vya Jangwani Dar es Salaam. Mzee Mshume kwa niaba
ya wazee wa TANU alipanda jukwaani na kumvisha Nyerere kilemba
kama ishara ya kumuunga mkono. Picha ya mzee Mshume akimvisha
Nyerere kilemba ilichapishwa katika magazeti mengi. Halikadhalika,
picha nyingine mashuhuri ya Mzee Mshume na Mwalimu Nyerere ni
ile iliyopigwa Novemba 1962 wakati wa Uchaguzi Mkuu.

Picha hiyo inamuonyesha Mzee Mshume akiwa amevaa koti,
kanzu na kofia na huku amemshika Mwalimu Nyerere mkono
akimsindikiza kupiga kura. Magazeti ya Chama na Serikali – Uhuru
na Daily News yamekuwa yakiitumia picha hii kila baada ya miaka
mitano katika uchaguzi wa rais kama njia ya kuwahamasisha watu
kupiga kura na kumchagua Mwalimu Julius Nyerere. Kwa bahati
mbaya picha ile siku zote hutoka bila maelezo na kwa hiyo wengi
hawafahamu yule mzee aliyefuatana na Mwalimu Julius Nyerere
kuwa ni nani. Kadhalika, si wengi wanaoufahamu mchango wa Mzee
Mshume Kiyate katika kupigania uhuru wa Tanganyika kwa sababu
Mwaka 1995 Jiji lilipoamua kubadilisha jina la mtaa aliokuwa akiishi
Mshume Kiyate – yaani Mtaa wa Tandamti ili uitwe Mtaa wa Mshume
Kiyate kama ishara ya kumuenzi na kuthamini mchango wake katika
kupinga ukoloni, baadhi ya magazeti yalipinga kitendo hicho. Je, ni
nani wa kulaumiwa endapo wananchi wenyewe hawajui historia ya
ukombozi wa nchi yao?
 
SOA: Usitusimange ndugu yetu sisi tunaasili ya kusoma hata kabla Mjerumani na Muingereza hajatia mguu Tanganyika. Una khabari kuwa Krapf alipata mshangao mkubwa alipomkuta Chifu Kimweri wa Vuga yuko katika mahakama yake akiandika na kusoma hati za Kiarabu? Chifu Kimweri na wanawe wote walikuwa wanajua kusoma na kuandika. Huna khabari Chifu Mkwawa alikuwa akiandikiana barua na Sultan wa Zanzibar kwa hati za Kiarabu? Tena alikuwa hampi mtu uongozi katika himaya yake hadi amesilimu na kuwa Muislam? Mmoja wa makamanda wake akiitwa Yusuf.

Babu yangu mzaa mama Sheikh Mohamed Mvamila alikuwa maisha yake yote hadi anaondoka duniani akiandika barua kwa irabu za Kiarabu na alisomesha watu wengi sana katika madrasa yake. Mama zangu wote wamejua kusoma na kuandika bila hata kuingia darasa kama wengi wanavyolijua darasa. Na mimi alianza kunifundisha kusoma kama alivyofundishwa yeye na hayati Sheikh. Babu yangu ni Mzaramo wa Mkamba lakini baada ya Vita Kuu ya Kwanza alihamia Musoma akiwa kijana mdogo sana. Alizaa watoto wanne wote hapo Musoma na alifundisha dini huko hadi Mungu alivyomuhitimisha. Hilo suala la kuogopa umande kwetu halikuwapo. Naweka kipande hiki hapo chini kwa faida ya wanaukumbi:

Missionaries became envious of the level of civilisation and literacy advancement achieved by Muslims through the Arabic script taught in the ‘madras' system of education not only at the coast in Zanzibar, Bagamoyo, Kilwa or Mikindani but also in far way places in the interior, like Usambaa, Tabora Kigoma, Ujiji were Islam was firmly established. Missionaries in collaboration with the colonial government initiated plans to subvert whatever progress Muslims had made. The first step taken by the British when they took over the country from Germany after the First World War was to abrogate the Arabic script, which was in use for many years in favour of the Roman script. By a mere stroke of a pen people who were educated were overnight reduced to illiterates. These instant, British and missionaries made illiterates were the poets of yesterday and the ‘ulamaa' who had intellectually held their own against missionaries defeating them in debates with ease. The vacuum created by the abrogation of Muslim education system was filled with missionary education with the British colonial government as the overseer. Knowledge was now disseminated from the class room with missionaries as teachers instead of the ‘maalim' in the ‘madras'. Tanganyika was now open for evangelisation.
 


Heshima kwako Mohamed Said,

Kwanza naomba kujipa pongezi mwenyewe kwa kufikisha post 1000 jamvini.

Mkuu MS hii habari niliwahi kuisikia siku nyingi kidogo bila shaka Mzee Mshume Kiyate ni miongoni mwa mamilioni ya wazee wetu walijitolea kwa hali na mali kupigania uhuru wa Tanganyika bila kujali dini au kabila.Wapo wazee wengi sana waliojitolea kwa hali na mali kupigania uhuru wa Tanganyika ambao michango yao haijulikani sana kwa watanzania wengi wa kizazi cha leo na kesho.

Nimefurahi sana kujua kwamba walikuwepo wazee wetu wenye moyo wa upendo,hekima na uzalendo wakati huo,kitu ambacho ni nadra sana kukisikia au kukiona siku hizi [wakati wetu].Historia itaendelea kumuhenzi mzee Mshume Kiyate kwa wema wake na upendo wake alioutenda kwa faida ya Tanzania ya wakati ulee na sasa.Nina hakika Mzee Mshume alitoa msaada kama mzalendo halisi wa wakati wake.Mzee Mshume angeweza kutoa sadaka msikitini au kanisani lakini hekima ilimuongoza kumsaidia Mwl Nyerere ambae alikuwa na majukumu ya kuhamashisha kudai uhuru wa mtanganyika bila kuwa na mshahara.Mungu ambariki Mzee wetu Mshume kwa kazi nzuri na yenye faida kubwa kwa watanzania wote hata leo.Wanahitajika akina Mzee Mshume wengi wakati wetu ili kuliepusha taifa letu na dhambi ya ubaguzi wa kidini na ukabila ambao Mwl Nyerere aliupigania sana wakati wa uongozi wake.

Mungu ibariki Tanzania,Mungu ibariki Afrika iwe moja.
 


This can only be a piece of MS's fertile imagination.
The Arabs taught cramming of the Quran and nothing else.
And pls do not let us to believe that ,Okay, come the white man, Islamic "education" or what ever stood in its place just melted away into insignificance?
MS you should have the courage to admit that Ismaic converts were grilled with the view that the white man is an infidel, thus one can not gain much from him.Please do agree that Islamic converts actually resented modern education and thought it was opposing Islam.
You find this today as we speak.
Alas and behold, several years later muslims come to find that they have missed the development boat and are refusing to be passengers in the same development boat, as christians.They want their own boat!!!

There is more to this issue than what we are being told by MS and co.
 
Mnaolalamika kuwa Fundi Mchundo ametumia matusi kumuita Ami na Ya ya kuwa wapuuzi, mlikuwa wapi huyo huyo Ami alipomuita Mkandara mpuuzi? Huyo pepo mbaya mnamuona sasa wakati mmegeuziwa kibao? Hao jamaa wawili ni wapuuzi, fools na kama nilivyosema awali, kunguni ( na hapa nilyemtukana ni kunguni) katika jamii yetu. Unafik haupendezi. Huyu Mohamed Said asiyeacha kujiita muungwana alikuwa wapi wakati huyo mpuuzi Ami akimuita Mkandara mpuuzi, kwa sababu tu ametofautiana nae? Badala yake, aanamsifia:

Ami: Ahsante sana kwa uchambuzi wako. Mungu atakulipa Insha Allah.
Unafik kwa watu wazima haupendezi. Hawa kunguni niliacha kuwajibu lakini naona hawataki kujifunza. Watu ambao hawaogopi kusema uongo wazi wazi hawastahili heshima ya kujadiliana nao!

Amandla......
 
Ngongo: Ahsante kwa mchango wako na kwa namna ulivyomsifia Mzee Mshume. Nashukuru kuwa na wewe umeuona mchango wake katika kupigania uhuru wa Tanganyika. Mzee Kondo akiwa Mayor wa Dar es Salaam aliubadili mtaa alokuwa akikaa Mzee Mshume wa Mtaa wa Tandamti na kuupa jina la "Mtaa wa Mshume Kiyate." Wakubwa wamekataa kukibadili kibao hicho sasa karibu miaka kumi. Wanadai kilichomsukuma Mzee Kondo kumuenzi Mzee Mshume ni udini. Waandishi wa magazeti nao hawakuliachia hilo karibu. Walikwenda kwa Nyerere kumuuliza mawazo yake. Magazeti yalitoa taarifa kuwa Nyerere kasema yeye asihusishwe na mambo hayo. Sarah Dumba wa RTD akenda kufanya majadiliano na Mzee Kondo kuhusu mitaa iliyobadilishwa majiuna na kupewa majina ya wazalendo waliopigania uhuru wa Tanganyika: Kleist Sykes, Tatu bint Mzee, Makisi Mbwana, Omari Londo nk. Mzee Kondo akasema hao wanaolalamika kama hawawajui watu hao basi watuulize tutawaeleza walikuwa nani.

Wakati Mshume anaumwa amelazwa Muhimbili alikuwa akiwauliza wanae, "Hivi jamani Mheshimiwa mmempelekea habari kuwa mimi naumwa?" Mzee Mshume kafa na kuzikwa TANU haina habari. Jina lake kwa kipindi kirefu lilisahaulika hadi lilipoibuka upya katika kitabu changu mwaka 1998. Katika kila picha alopiga Nyerere wakati wa kupigania uhuru akiwa na wazee wa Dar es Salaam pembeni yake utamuona Mzee Mshume Kiyate.
 
Si kitu na tusameheane kama huko nyuma tumekoseana hii ndiyo silka ya binadamu aliyekamilika ni Mwenyezi Mungu peke yake. Tuendelee na mjadala kwa faida ya ukumbi wetu, wanaukumbi na wasomaji walio kimya wakifuatilia mjadala. Tutambue kuwa mwisho wa siku watatuhukumu kwa yale tuliyosema.
 
Size: 203 × 152 Type: 10KB JPG







Mwalimu alijitahidi sana tena sana kuji Identify na waswahili na kuwatetea ili na wao wafaidike na huduma muhimu za kufuta adui njaa, ujinga na maradhi katika miaka ya awamu ya kwanza. 1961-1985.

Na hata Azimio la Arusha ilikuwa juhudi za kuwaweka wananchi on an equal footing.
He was probably carried away with it to the extent ya kuvaa kama waswahili wa kawaida.
Hiki kibargashia , Mwalimu alikivaa kwa muda mrefu sana katika harakati zake za urais.
 
Wanaukumbi mjadala umekuwa mkali sana. Ghadhabu zinapanda ni wajibu wetu kuzipoza. Naweka hapa chini siku za mwanzo za TANU ilipokuwa inajaribu sasa kuvuka mipaka yake kutoka Dar es Salaam pale New Street na kwenda katika majimbo. Katika majimbo ya mwanzo kwa TANU kwenda ilikuwa Jimbo la Kusini. Soma kwa furaha:


Jimbo la Kusini, 1955

TAA mjini Lindi ilikuwa chini ya uongozi wa Suleiman Masudi Mnonji aliyekuwa Rais na Katibu wake alikuwa Mohamed Waziri. Mnonji alikuwa fundi cherahani na Waziri alikuwa mchoraji wa ramani za nyumba. TAA ilichelewa kuanza mjini Lindi. TAA ilianzishwa Lindi mwaka 1953 wakati uongozi wa TAA mjini Dar es Salaam si tu ulikuwa unaigeuza TAA kuwa chama cha siasa bali ulikuwa ukifanya mipango kumpeleka mjumbe wake Umoja wa Mataifa kudai uhuru. Masudi Mnonji alikuwa na uzoefu wa kutosha katika siasa. Baada ya Vita Kuu ya Pili alikuwa amejaribu kuanzisha vyama vya wafanyakazi katika mashamba mbalimbali ya mkonge kusini mwa Tanganyika. Vilevile aliwakusanya wapishi na madobi mjini Lindi waanzishe umoja wao. Ilikuwa kupitia juhudi zake binafsi TAA ijapokuwa ilichelewa, ilikuja kuanzishwa mjini Lindi na Mnonji alijitolea nyumba yake katika mtaa wa Makonde kama ofisi ya chama. Mnonji kwa kutambua umuhimu wa kuwa na uongozi ulioelimika vizuri, alimleta Nangwanda Sijaona kutoka Nachingwea aje aishauri TAA jinsi ya kufanya mambo kwa utaalamu.

Wakati huo mjini Lindi kulikuwa na chama cha wafanyakazi bandarini Dockworkersí Union chini ya uongozi wa Mussa Athumani Lukundu, chama ambacho kwa kiasi chake kilianzisha vuguvugu la siasa za vyama vya wafanyakazi. Ingawa vyama hivi viwili, yaani TAA na Dockworkersí Union vilikuwepo katika mji mmoja, siasa za hiki chama cha pili cha wafanyakazi bandarini hazikupitia TAA kama ilivyokuwa mjini Dar es Salaam. Hii kidogo ilidhoofisha mwamamko wa siasa kwa wananchi. Jimbo la Kusini lilikuwa katika usingizi mzito wakati sehemu nyingine Tanganyika zilikuwa zikipiga hatua kwenda mbele zikiandaa vita dhidi ya utawala wa kikoloni. Chanzo cha usingizi huu mzito huko kusini ulikuwa na asili yake katika historia ya Tanganyika.

Vita vya Maji Maji vilipoanza kusini ya Tanganyika mwaka 1905 kwa nia ya kuwafukuza Wajerumani kutoka Tanganyika, zile sehemu zenye Wakristo wengi zilikataa kujiunga na vita na badala yake wakajiunga na majeshi ya Wajerumani na kupigana bega kwa bega na dhidi ya wazalendo. Hii ilitokana na sababu ya kuwa uasi dhidi ya dhulma wa Wajerumani ulianza katika maeneo yenye Waislam wengi na vita vikachukua sura ya vita vya Kiislamu dhidi ya Wazungu ambao dini yao ni Ukristo. Kwa kuwa wamishonari walikuwa washirika wa wakoloni, walichukuliwa kama maadui na hivyo ikawa vituo vyao vinashambuliwa na wapiganaji wa Maji Maji. Kutokana mashambulizi haya, Wakristo walivichukua Vita Vya Maji Maji kama vita dhidi ya Ukristo. Harakati za Maji Maji zilishindwa na Wajerumani walifanya fisadi kubwa dhidi ya wananchi na viongozi wao. Jambo hili liliacha kovu kubwa katika fikra za wananchi na kwa upande wa Wakristo ambao walinusurika na ghadhabu ya Wajerumani, wengi wao wakajiweka mbali na aina yoyote ya kupinga ukoloni.

Kufuatia historia hii Waafrika waliokuwa kusini ya Tanganyika sasa wakiwa chini ya utawala wa Waingereza na kuwa chini ya himaya ya wamishonari walipumbazwa kiasi kwamba waliogopa siasa. Baada ya Waafrika kushindwa vita kwa silaha kali za Wazungu sasa Kanisa likaona ndani ya fadhaa ile fursa yao kutawala sehemu hiyo kwa kutoa vishawishi kama vile shule na hospitali. Kwa hiyo Wamishionari na Waingereza walionekana kama mabwana wema wenye kuwajali raia zao kinyume na serikali katili na ya kidhalimu ya Wajerumani. Vuguvugu la siasa kama ilivyokuwa Vita vya Maji Maji, lilianza katika maeneo ya Waislam kufuatia mfumo ule ule kama ilivyokuwa katika upinzani wa ukoloni wa Wajerumani. Wakristo katika Jimbo la Kusini waliiona TANU kama walivyoviona Vita Vya Maji Maji, kama harakati nyingine za Waislam zilizowa zinakuja tena kwa mara ya pili kuvuruga amani na utulivu. TANU ilipoanza ikawa inavuma kuwa safari hii Waislam walikuwa wamemua kuanzisha vita dhidi ya Waingereza kama walivyoanzisha vita na Wajerumani.

TANU ilipoanzishwa mjini Dar es Salaam na hisia za utaifa zilipokuwa zikipanda pole pole katika fikra za wananchi katika sehemu nyingi za Tanganyika, Jimbo la Kusini lilikuwa bado usingizini likiishi katika zama za kale. Mnonji na Waziri, kwa sababu ya utu uzima wao, daraja yao katika jamii na hasa kutokana na kuhusika kwao katika siasa za pale mjini, walikuwa na nguvu kubwa katika TAA. Wakati TANU imeshachukua nafasi ya TAA, uongozi wa TAA Lindi haukutaka kufungua tawi la TANU. Mtu wa kwanza kuutanabaisha uongozi wa TAA mjini Lindi juu ya mageuzi yaliyokuwa yakitokea Tanganyika na kuanzishwa kwa chama kipya cha siasa mjini Dar es Salaam alikuwa Abdallah Juma Makopa, kijana kutoka Tanga akifanya kazi ya ukarani Posta ya Lindi. Makopa aliwaendea Mnonji na Waziri na kuwajulisha kuhusu kuanzishwa kwa TANUmjini Dar es Salaam na aliwashauri waanzishe TANU pale Lindi. Jambo hilo lilipingwa moja kwa moja na Mnonji, Waziri, Said Nassoro, Abdallah Mhuji na wanachama wengine wa TAA.

Chama cha Waafrika ambacho kilianzishwa siku nyingi mjini Lindi na kwa hakika ndicho kilikuwa chama cha pekee kushughulikia maslahi ya Waafrika sehemu za kusini kilikuwa African Welfrare Association ambacho mlezi wake alikuwa John Nevi, Mjaluo kutoka Kenya na katibu wake alikuwa Casian Njunde, Mngoni wa Songea. Makopa aliposhindwa kukishawishi kile kikundi cha wazee wa TAA aliwaendea Yusufu Chembera na Rashid Salum Mpunga. Chembera alikuwa na umri wa miaka thelathini na nne na Mpunga alikuwa kijana wa miaka ishirini na saba. Chambera alikuwa amesoma hadi shule ya msingi na Mpunga alikuwa amemaliza madras. Chembera alikuwa akifanya kazi katika kantini ya Lindi Welfare Centre, wakati Mpunga alikuwa dereva wa lori aliyeajiriwa na mfanyabishara wa Kihindi. Makopa aliwashauri Chembera na Mpunga juu ya uwezekano wa kuwahamasisha wananchi wawaunge mkono ili tawi la TANU lifunguliwe pale mjini. Aliwaambia alitaka sana kufanya hivyo yeye mwenyewe lakini asingeweza kwa sababu yeye alikuwa mtumishi wa serikali na hakuwa akifahamika sana mjini. Uongozi kama wao ndiyo ungeweza kuaminiwa na wananchi na usingetiliwa mashaka. Makopa, Chembera na Mpunga walikubaliana kuwa kabla ya kuanza kufanya kampeni waziwazi kwa ajili ya TANU, lazima wawaandikishe wanachama wachache kama waasisi wa chama. Mpunga na Chembera walimwandikisha kijana mmoja akiitwa Abdallah Faraj na katika muda mfupi waliweza kuwapata takriban wanachama kumi na tano walioridhia kujiandikisha kama wanachama waasisi wa TANU.

Baada ya kuandikisha wanachama waasisi mkutano wa siri uliitishwa katika Welfare Centre ambako ndiko alikokuwa akifanya kazi Chembera. Chembera aliwaeleza kwa ufupi wale wanachama wa mwanzo kuhusu malengo na madhumuni ya chama hicho kipya cha siasa. Mkutano huo ulichagua kamati ya watu watatu yaani, Makopa, Chembera na Faraj ili kuwakabili Mnonji na Waziri kuwaleza kuwa TAA haipo tena nchini Tanganyika. Lengo lilikuwa kuwasadikishia kuwa ilikuwa kazi bure na kupoteza wakati kujaribu kuihuisha TAA mjini Lindi wakati ambapo Tanganyika nzima ilikuwa ikisonga mbele na TANU. Baada ya mjadala mrefu sana na mkali wa wale vijana watatu na ule uongozi wa TAA wa wazee, walikubaliana TANU lazima isajiliwe mjini Lindi.

Uchaguzi ulifanyika na Shaaban Msangi, kijana wa Kipare akifanya kazi kwa Smith Mc Kenzie, alichaguliwa rais na Ahmed Seif, katibu. Mpunga, Chembera, Mnonji na Idd Toto walichaguliwa wajumbe wa kamati. Ahmed Seif alikuwa kijana ambaye ndiyo kwanza amemaliza shule, yeye alikabidhiwa kuendesha ofisi kwa niaba ya uongozi. TANU mjini Lindi ilimwajiri ili kukiandaa chama kiweza kufanya kazi zake kwa ufanisi. Hassan Mohamed Kinyozi aliajiriwa kama mhudumu wa ofisi. Hawa wawili walikuwa ndiyo wafanyakazi wa kwanza wa TANU waliokuwa wakilipwa mshahara katika Jimbo la Kusini na wakawa miongoni mwa wafanyakazi wachache sana walioajiriwa na TANU kwa wakati ule. Mnonji alitoa nyumba yake katika mtaa wa Makonde kuwa ofisi ya kwanza ya TANU Jimbo la Kusini. Baada tu ya kuanzishwa kwa TANU, Athumani Mussa Lukundu, kiongozi wa Lindi Dockworkersí Union, aliunganisha chama chake na TANU. Jambo hili, kwa TANU lilikuwa la kuitia moyo sana kwa sababu Dockworkersí Union ilikuwa na wananchama wengi na hatua ile iliongezea TANU nguvu.

Baada ya muda mfupi tu toka kufunguliwa kwa TANU Mkutano Mkuu wa Kwanza wa TANU wa mwaka 1955 ulifuatia. Tawi la Lindi lilikuwa tayari lina uhusiano na makao makuu ya TANU mjini Dar es Salaam, na lilikuwa likitarajia kuhudhuria mkutano huo na kukutana na Julius Nyerere na uongozi mzima wa TANU pale makao makuu Dar es Salaam. Mpunga, mwanachama muasisi wa TANU, na Ali Ibrahim Mnjale waliteuliwa kuhudhuria mkutano huo kama wajumbe kutoka Jimbo la Kusini. Halmashauri ya TANU ya Lindi iliwaelekeza wajumbe hawa wafikishe ombi rasmi kwa makao makuu ili Julius Nyerere aje kufanya ziara kusini kwanza, kukutana na wananchi na kufanya kampeni kwa ajili ya TANU na pili aje kupambana na propaganda dhidi ya TANU zilizokuwa zikitawanywa na Yustino Mponda. Mponda akitumia uhusiano wake na serikali ya kikoloni na nafasi yake kama mjumbe wa Baraza la Kutunga Sheria kutoka Newala; na vilevile akitumia ushirikiano wake wa muda mrefu na kanisa ambao bila shaka yoyote lilikuwa serikali ndani ya serikali kule kusini, alikuwa ameanza kampeni yake ya kuipinga TANU. Hili lilikuwa likiathiri msukumo wa uanachama. Mponda alikuwa mmoja wa wajumbe waliotumwa na Gavana Twining kwenda Umoja wa Mataifa Februari, 1955 kwa niaba ya serikali ya kikoloni kwenda kuipinga. Uongozi wa TANU huko Lindi ulitaka Nyerere aende kupambana na Mponda akiwa katika uwanja wake mwenyewe, ndani kabisa ya ngome ya Ukristo wa Kikatoliki katika Tanganyika.

Mkutano mkuu wa mwaka wa TANU ulifanyika katika ukumbi wa Hindu Mandal mjini Dar es Salaam. Siku kabla ya mkutano TANU ilimwalika Gavana Edward Twining kwenye tafrija katika Ukumbi wa Arnatouglo lakini alikataa kistaarabu na akamtuma Chief Secretary, Bruce Hutt, kumwakilisha. Baada ya mkutano, wakati wajumbe wengine wanaondoka kurudi kwenye majimbo yao, Mpunga na Mnjawale walibakia nyuma kukutana na uongozi wa makao makuu wa Julius Nyerere, Sheikh Suleiman Takadir, John Rupia, Ali Mwinyi Tambwe, Said Chamwenyewe, Oscar Kambona na wengineo. Mpunga na Mnjawale waliwafahamisha viongozi wa makao makuu kuhusu hali mbaya ya siasa Jimbo la Kusini. Mbali na kampeni za kuipinga TANU za Mponda, katika ziara yake Lindi Gavana Twining aliwatahadharisha Waafriika wa Tanganyika wasijihusishe na wafaanya fujo wanaotaka kuzusha vuruguí. Twining alikuwa akitoa onyo hili akiikusudia TANU ambayo ilikuwa imeanzishwa mwaka uliopita. Hotuba hii ya Gavana iliwatisha wananchi kujiunga na TANU. Mpunga na Mnjawale walisisitiza kuwa kuja kwa Nyerere mjini Lindi kulitakiwa haraka sana kukabiliana na vyote viwili, kwanza ile hotuba ya gavana na pili zile kampeni za kupinga TANU zilizokuwa zikiendeshwa na Liwali Yustino Mponda.

Wakati huo Abeid Amani Karume aliyehudhuria ule mkutano alimwalika Nyerere afanye ziara Zanzibar. Kitu cha kustaajabbisha ni kuwa, Nyerere alionekana kuiafiki zaidi ziara ya Zanzibar kuliko ile safari ya kwenda kusini kuiimarisha TANU. Mpunga alimsisitizia Nyerere umuhimu wa yeye kwenda Lindi ambako kunaweza kuwa ndiyo chanzo cha TANU kupata ufanisi Newala, Songea, Tunduru na Masasi ambako kulikuwa na upinzani mkubwa dhidi ya TANU. Kanisa lilikuwa likiwazuia Wakristo kujiunga na TANU. Sheikh Suleiman Takadir, Said Chamwenye, John Rupia, Ali Mwinyi Tambwe wote waliunga mkono ule ujumbe wa Lindi juu ya suala hili. Baada ya kufikia makubaliano, Mpunga na Mnjawale walipewa barua ya kuthibitisha safari ya Nyerere. Ziara ya Nyerere ilikuwa ianze muda mfupi kutokea hapo kwa kuwa ilikuwa ndiyo siku za mwisho za kiangazi. Barabara sehemu ya kusini ya Tanganyika zilikuwa hazipitiki wakati wa masika, zikiitenga kabisa kusini toka sehemu zilizobaki za nchi. Ali Mwinyi Tambwe na Rajab Diwani walifuatana na Nyerere kwenda Jimbo la Kusini kuondoa wasiwasi na woga uliozushwa na Gavana Twining na kibaraka Yustino Mponda.

Nyerere na msafara wake ulipokelewa na uongozi wa TANU wa Lindi huko Mbanji, kijiji kidogo nje ya mji. Msafara wa Nyerere ulipowasili Mbanji ilikuwa kiasi cha saa moja jioni hivi na giza lilikuwa linaanza kutanda. Mbali na Mpunga na wale wajumbe wawili waliokutana na Nyerere mjini Dar es Salaam mwezi uliopita, hakuna hata mtu kati ya umma ule uliokuja kupokea ujumbe kutoka makao makuu ya TANU aliyekuwa anajua Nyerere anafanana vipi. Mpunga, dereva wa lori, alijibagua kutoka kwa lile kundi la watu akawa amesimama pembeni ili Nyerere apate kumuona. Baada ya Nyerere kumtia Mpunga machoni, Mpunga alimwendea kumsalimu Nyerere, Tambwe na Diwani; kisha aliligeukia lile kundi la watu kumtambulisha Nyerere kwa wananchi akilitaja jina lake kwa sauti kubwa. Baada ya hapo aliutambulisha ule ujumbe wa Nyerere. Nyerere na ujumbe wake ulisindikizwa kwa shangwe na kundi la watu hadi ofisi ya TANU kwenye nyumba ya Mnonji. Kupakana na ofisi ya TANU ilikuwepo nyumba ya seremala mmoja, Issa bin Ali Naliwanda. Hii ndiyo nyumba iliyochaguliwa alale Nyerere na ujumbe wake, si kwa sababu ilikuwa nzuri kupita zote. Ilichaguliwa na kupewa heshima hii kwa sababu ilikuwa karibu sana na ofisi ya TANU na hivyo basi ilirahisishia TANU kazi ya ulinzi wa Nyerere. Siku iliyofuata ilikuwa Jumapili na Nyerere aliwaomba wenyeji wake apelekwe kanisani kwa ajili ya ibada.

Kanisa Katoliki mjini Lindi ni jengo la fahari lililoko ufukweni katika Bahari ya Hindi. Lindi ulikuwa mji wa Waislam. Mbali na mlio wa kengele za kanisa hakuna mtu pale mjini aliyekuwa akishughulishwa na kile kilichokuwa kikifanyika kwenye viwanja vya kanisa. Watu wachache waliokuwa wakienda kusali kanisani walikuwa Wakristo waliokuja Lindi kutoka sehemu nyingine za Tanganyika kufanya kazi katika ofisi za serikali. Ghafla mahala hapa palipokuwa pweke, palipopuuzwa kwa miaka na Waislam wa mjini, pakawa muhimu kwa sababu rais wa TANU ambae alikuwa Mkatoliki alikuwa na haja ya kuhudhuria ibada pale kanisani. Hakuna mtu katika uongozi wa TANU wa Lindi aliyejua ndani ya kanisa lile kulikuwa vipi wala hapakuwa na yoyote kati yao aliyewahi kuingia ndani ya kanisa, si Lindi wala mahali popote pale. Uongozi wa TANU wa Waislam mjini Lindi haukumwamini Mkristo yoyote kumsindikiza Nyerere kanisani ili kumpa ulinzi. Baada ya kujadili suala hilo kwa urefu hatimaye iliamuliwa kuwa Mpunga na wanachama wachache Waislam wenye kuaminika lazima wamsindikize Nyerere kanisani na wengine wabakie nje kulinda mlango.

Jumapili hiyo Nyerere aliingia ndani ya kanisa Katoliki mjini Lindi akifuatwa nyuma na walinzi wake Waislam wakiongozwa na Salum Mpunga, dereva wa lori shupavu. Misa hii ëmaalumí ilidumu katika fikra za wale Wakristo waliokuwepo pale kanisani kwa miaka mingi kwa kuwa tukio hilo liliwagusa sana Wakristo walioshuhudia mkasa ule ndani ya kanisa la Lindi. Hii huenda ilikuwa mara ya kwanza na ya mwisho kwa Nyerere kumsalia Mungu wake huku akiwa amesimamiwa na Waislam.

DC mkoloni alikataa kutoa kibali kwa TANU kufanya mkutano wa hadhara. Akiwa amekasirika sana, Shabaan Msangi aliitisha mkutano wa dharura wa tawi uliohudhuriwa na Nyerere na Tambwe. Baada ya mkutano huo Tambwe alikwenda kumwona DC. Ruhusa ilitolewa, na adhuhuri hiyo siku ya Jumapili, katika kiwanja ambacho Wazungu walikuwa wakicheza gofu, ambako mwaka mmoja uliopita Gavana Edward Francis Twining alitoa hotuba iliyowavunja moyo Waafrika, Nyerere alihutubia mkutano wa hadhara. Kamwe haijapata kutokea kabla ya siku ile katika historia nzima ya Jimbo la Kusini, watu wengi kiasi hicho kujumuika mahali pamoja. Wazungu na Wahindi pamoja na askari, watu wakiwa wamekaa na wengine wamesimama katika jua kali walikuja kumsikiliza Nyerere akihutubia. Ili kuhakikisha amani na usalama pale mkutanoni serikali iliweka askari waliouzunguka uwanja mzima wa mkutano. Nyerere aliwafikishia watu ule ujumbe wa TANU wa kuwa, kutawaliwa ni fedheha, na Waafrika wa Tanganyika lazima wadai uhuru wao. Uingereza ilikuwa ikiitawala Tanganyika chini ya udhamini kwa niaba ya Umoja wa Mataifa, na wakati ukiwa muafaka inabidi Uingereza ikabidhi nchi kwa wananchi wenyewe. TANU ilikuwa imewasili Jimbo la Kusini.
 
Kama Mkristo ninachokumbuka ni kuwa kuna wakati hatukubaguana kidini kwa kuangalia majina kwani hatukujali hata majina tuliyowapa watoto wetu wa kuzaa. Nyakati hizo haikuwa taabu kwenye familia ya Kikristo kukuta watoto wanapewa majina kama Abdalla, Shakila, Hamisi, Juma, Mwajuma na mengine mengi tu ya Kiislamu na hasa kwa wale walioshi sehemu za pwani kama Dar es Salaam. Pia Wakristo wengi tu hawakuona taabu kununua nguo kama kanzu, vikoi, baragashia, buibui na katu watu hawakubaguana kwenye sherehe kama za vifo, harusi, Iddi, Krismasi na Pasaka.

Huo ulikuwa ni wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere na watu walitanguliza utaifa kwanza lakini kwenye miaka ya sabini akatokea mdudu mbaya kwa umbo la mkufunzi kutoka nchi ya Pakistani. Hawa akina Mohamed Said ni matokeo ya mbegu ya chuki iliyopandikizwa na Mpakistani huyo miongoni mwa vijana hawa wakati huo baadhi yao wakiwa tayari chuo kikuu. Kwa sababu tulikuwa na utawala thabiti mikakati hii ya kutaka kutugawa kidini na kupandikiza mbegu ya chuki iliweza kuzimwa bila kuleta madhara lakini mwaka 1985 akaingia Mzee Rukhsa and all hell broke loose !

Mohamed Said anajua hawangeweza kufanikiwa kwa namna yoyote ile Mwalimu alipokuwa hai kwani Watanzania kwa ujumla wao bila kujali dini au rangi waliutambua na kuuenzi mchango wake. Siyo tu aliongoza harakati za kupigania uhuru bali juhudi zake zilizofuatia za kupigania umoja na usawa wa Watanzania bila kujali dini, rangi,jinsia au mali. Uthibitisho ulionekana hata kwa kipofu jinsi Watanzania walivyomlilia siku mwili wake ulipopokewa uwanja wa ndege kutoka Ulaya hadi anazikwa kijijini kwake Butiama.

Najua Mohamed Said na kundi lake wamesubiri hadi watu wamesahau machungu waliyokuwa nayo wananchi kwa kupotelewa na jemadari wao na Baba wa Taifa ili waanze hizi chokochoko zao za kebehi na dharau zao. Bahati mbaya ni kuwa wingu la udini limewafunika macho na kuwaziba masikio hadi wanashindwa kutambua hatari itakaikabili Taifa wakiendelea na hizi hadithi zao za hatari. Lakini baya zaidi ni ukosefu wa utawala ulio thabiti na makini unaoruhusu wenda wazimu kama akina Mohamed wasiojua hata kile wanachokitafuta kuchezea amani na umoja wa Watanzania. Pamoja na yote nina matummaini hawatafanikiwa.
 

Umenena mkuu Mag3, hawajui hamasa wanayoiamsha.
Nimejaribu kuwakumbusha kuwa sheria moja ya fizikia,Action and reaction are equal and but opposite in direction.
Na hapo mambo yatakapokuwa wasijekuwa wa kwanza kuvaa mabomu viunoni!!
Maana destruction wanaiweza sana badala ya kujenga shule.
 
Mag3: Hapana ndugu yangu kwa hilo unanionea tena sana. Mimi kwa bahati mbaya ama nzuri niko katika hali ya kuyajua usiyoyajua wewe. Awali ya yote chanzo cha mimi kunyanyua kalamu ni pale nilipogundua historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika (na hili nimelisema mara nyingi kuwa ni historia ya wazee wangu) imepotoshwa na ipo katika hali ya kupotezwa kabisa. Nikajagundua kuwa kisa cha historia hiyo kutopendeza machoni mwa Wakubwa ni kuwa ni historia ya Waislam na harakati za kuung'oa ukoloni Tanganyika. Hapo ndipo nilipokujatanabahi kuwa kumbe tatizo ni dini. Kuanzia hapo nikaanza sasa utafiti na kuandika na kutoa mihadhara. Yaliyokujafatilia baada ya hayo yalinisadikishia kuwa historia haipendezi kwa Wakubwa kwa kuwa wao hawana cha kuonyesha. Sasa sidhani kama ni kosa kwa mtu kuweka kumbukumbu za wazee wake. Kama wao wenyewe TANU hadi CCM hawakuitaka historia hii basi si kitu lakini mimi nina wajibu wa kueleza yale ninayoyajua kuhusu kipindi kile na kuwapa heshima wanayostahili wazalendo waliopigania uhuru wa nchi yetu. Hiki ndicho ninachofanya sasa hapa ukumbini na ni kwa kuwa nimechelewa kufika hapa. Historia hii hivi sasa ni maarufu inasomeshwa kote Ulaya na Marekani wanakofundisha African History, Politics and Islam. Na taarifa nilizopata hivi karibuni ni kuwa hata katika vyuo vyetu hapa nchini baadhi ya walimu wanaisomesha.

Hivi kweli ndugu zangu mnaamini kwa dhati na ithibati ya nyoyo zenu kuwa amani anadumu kwa kutoeleza mchango wa Kiyate Mshumi, Abdulwahid Sykes, Titi Mohamed na wengine na amani hiyo itadumu kwa kueleza mchango wa Nyerere peke yake katika kupigania uhuru wa nchi yetu? Nchi gani imeingia vitani na chanzo ni kuwa watafiti walirekebisha historia? Hapa tunakuwa tunajitisha sisi wenyewe na kitu ambacho hakina kitisho hili ni zimwi la bure mnaloliogopa. Mbona nimeisomesha hii historia kwa zaidi ya miaka kumi na sijasikia mahali popote mtu kenda hata kurusha jiwe?

Je, ndugu zangu mngependa historia hii tuifute ibakie ileile ya Nyerere peke yake?

Ama hilo la sisi kujenga shule ulotushauri mbona nimetoa mifano mingi ya shule tolotakajenga na tukapigwa vita na wakubwa kuanzia Chuo Kikuu mwaka 1968 kilichosababishwa EAMWS kuvunjwa na Nyerere, mradi wa OIC kujenga Chuo Kikuu serikali ikakataa, mradi wa Darul Iman Kibaha serikali ikahujumu, Shule ya Masjid Quba nk. Au ndugu zangu nyinyi hamuamini? Hivi hii hali ya sisi kuhangaika wakati nyinyi mnafaidi fursa zote mnadhani sisi tunaipenda?

Serikali ndiyo ina majibu ya maswali yetu Waislam lakini imekaa kimya imewaachia nyinyi mtujibu.
 

AFRICA,TANZANIA - The Late Tanzanian President Mwalimu Julius Nyerere with Senator Boby Kennedy when he visited Tanzania on his 1966 tour of Africa.

Many people , and I think Mohammed Said included, do resent the fact that Mwalimu could intellectually connect with almost ANY learned person in this world and give him or her his sincere piece of view in world politics.
They all regarded him almost in awe, for his intellectual prowess.


 
1966 ni baada ya uhuru, tuwekee picha kabla ya uhuru, kama hutoona vibarakashia vitupu
Usiwe na wasi wasi Mkuu Mwalimu aliweza ku-connect na hata waliokuletea Uislamu intellectually.Mwalimu hakuchagua rafiki kutokana na dini bali aliangalia sana msimamo wa usawa wa kibinadamu.
Hao jamaa kushoto wana ndevu hata za kumzidi Osama, au babu zako.
Hapa ni kabla hata ya uhuru
 
WANAUKUMBI: Hapa naweka ushahidi wa dhulma kwa kila mtu auone kama nilivyouleleza katika kitabu changu. Nyerere kakisoma kitabu na wote wahusika naamini wamesoma niliyosema. Huu ni mwaka wa kumi na mbili halijatoka jibu la kukanusha au hata kuandikwa kitabu cha kupinga kitabu changu. Soma na tafakari na tuendelee kujadiliana:

Uthibitisho wa Njama Dhidi ya Uislam
Hivi sasa kuna vitabu viwili vilivyoandikwa na Wakristo wenyewe vinavyothibitisha kuwa Wakristo wametumia nyadhifa zao katika serikali kuuhujumu Uislam na Waislam. Jan P van Bergen katika kitabu chake, Development and Religion in Tanzania,(1981) [1] ametoboa siri kuhusu uadui aliokuwa nao Rais Mstaafu, Nyerere dhidi ya Uislam na Waislam. Kitabu kinaeleza kwa ufasaha jinsi Nyerere wakati alipokuwa madarakani alivyokuwa akifanya mikutano ya siri na viongozi wa Kanisa kuweka mikakati ya kuupa nguvu Ukristo. Katika mikutano hiyo Nyerere aliwahakikishia viongozi wa Kanisa kuwa anaaunga mkono Ukristo. Kitabu hicho kinaeleza jinsi Nyerere alivyotimiza ahadi yake hiyo kwa Kanisa kwa kuhakikisha kuwa anawapa Wakristo nafasi za juu katika serikali na chama. Kitabu hiki kilikuwa kinauzwa Catholic Bookshop, Dar es Salaam. Lakini ilipokuja kudhihirikia Kanisa kuwa kitabu hiki kilikuwa kinatoa habari nyeti na siri za Kanisa kuhusu njama dhidi ya Waislam, kwa haraka sana kikaacha kuuzwa. [1] Hadi hivi sasa kitabu hicho ni marufuku kuletwa tena Tanzania.

Kitabu cha pili ni cha Dr John C. Sivalon, Kanisa Katoliki na Siasa ya Tanzania Bara 1953 Hadi 1985 (1992). [1] Kitabu hiki kinaeleza njama ndani ya serikali kuuhujumu Uislam. Sivalon anafichua kuwa kuanzia mwaka 1961 baada ya Tanganyika kupata uhuru, Kanisa lilikuwa na hofu mbili. Hofu ya kwanza ilikuwa umoja wa madhehebu za Kiislam kati ya Sunni, Bohora, Ismailia na Ithnasheri. Hofu ya pili ilikuwa kuhamishwa kwa makao makuu ya EAMWS kutoka Mombasa kuja Dar es Salaam. Kanisa lilikuwa linahofu kuwa mali walizokuwanazo Waasia Waislam zikitiwa katika harakati za Waislam ambao walikuwa na nguvu kubwa katika uwanja wa siasa zitaathiri maslahi ya Ukristo katika Afrika ya Mashariki. Kwa ajili hii Kanisa likatanganza kuwa Uislam ni adui wake na ikaanza mikakati ya hujma dhidi ya Uislam ili kuudhoofisha. [1] Kuna kazi mbili zilizoandikwa na Waislam kuhusu uhusiano baina ya serikali na Waislam. Kazi ya kwanza ni tasnifu ya Kiwanuka, ëThe Politics of Islam in Bukoba Districtí (1973); [1] kazi ya pili ni makala ya utafiti ëIslam and Politics in Tanzaniaí (1989) [1] iliyoandikwana mwandishi wa kitabu hiki. Ilikuwa baada ya kusoma tasnifu ya Kiwanuka na kuona jinsi ukweli wa kuvunjwa kwa EAMWS kulivyopoteshwa ndipo kama Muislam na kama ada ya Uislam inavyodai kuwa pande mbili za mgogoro zote lazima zisikilizwe, ndipo nilipoamua kufanya utafiti na kuandika tatizo lile kwa mtazamo wa Waislam. Ukweli ambao kwa miongo miwili ulizuiwa usifahamike kwa Waislam. Kiwanuka anadai na kuafiki kuwa Nyerere alikuwa na haki ya kutumia vyombo vya dola dhidi ya Waislam kwa kuwa kama asingefanya hivyo nchi ingekuwa na mamlaka mbili, yaani ya Waislam na ya serikali. Kwa ajili hii aliamua kuivunja EAMWS ili ëkulinda umoja wa kitaifa.

Halikadhalika ipo ëKwikima Reportí (1968)[1] ambayo imeeleza kwa ufasaha tatizo la EAMWS, chanzo chake na mchango wa serikali katika kuhujumu umoja wa Waislam. Taarifa hii inafaa kutumika leo kama dira ya kuelewa tatizo la Waislam wa Tanzania kama ilivyokuwa wakati ule ilipotolewa kwa mara ya kwanza. Taarifa ya Kwikima inaeleza jinsi TANU, serikali na Waislam wachache katika TANU walivyodanganyika kudhani kuwa katika kuisaidia serikali kuivunja nguvu EAMWS walikuwa wanatimiza uzalendo na maslahi ya taifa. Rejea hizi tano ni muhimu kwa wanafunzi wa historia ya siasa Tanzania; na kwa mtafiti yeyote anaetaka kujua chanzo cha chuki baina ya Waislam na serikali na chanzo cha hisia kali za kidini zinazoikumba nchi yetu kuanzia miaka ya 1980. Rejea zote hizo za vitabu, makala za utafiti na taarifa mbalimbali, ingawa zimeandikwa na waandishi tofauti na kwa muelekeo tofauti zote hizi zinadhihirisha kitu kimoja ñ kuwepo kwa njama zinazoendelea kwa zaidi ya karne moja dhidi ya Uislam na Waislam, kwanza zilikuwa zikifanywa na wakoloni walioitawala Tanganyika na sasa zinafanywa na Wakristo wananchi kuhakikisha kuwa Uislam haupati nguvu.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…