Chuma,
Huyo Jumbe alikataa kitu gani kwa Nyerere?.. ikiwa yeye aliweza kuivunja warsha ya waislaam akiwa makamu wa rais iweje tena ni kosa la Nyerere hali yeye Muislaam ambaye alikuwa na uwezo wa kukataa kama huyo Aziz..Nionyeshe hata hadithi moja ya Nyerere kuhusiana na waislaam ambayo kaifanya pasipo Waislaam wenyewe kuhusika kutoa maamuzi..
Hii habari mimi siikubaliani nayo kwa sababu ina malengo makuu ya Udini, ni sawa na kesho Chadema washinde uchaguzi huu atokee Mchagga mmoja aanze kudai wao Wachagga ndio wameiwezesha Chadema kusimama kwa sababu tu ya waasisi wake ati ndio iwe historia ya chama kwa kuchukua kabila moja na sii Watanzania waliojiunga na Upinzani...Nina hakika Chadema wasingefika hapa walipo leo kama sii kuungana na watanzania wengine kupambana na CCM Kisiasa na sio kikabila, hii ndio argument yangu..
Na ikumbukwe tu kwamba historia ya TANU ilianza tokea Kariakoo kama chombo cha kidini ambako asilimia kubwa kama sii yote ya wakazi na wanchama wake wakati huo walikuwa Waislaam. Lakini walipotaka kubadilika na kuwa chama cha kisiasa yalitokea Mapinduzi ndani ya chama cha kidini na AbdulWahid na Mwapachu kumpindua Kreist ktk uongozi na kukifanya chombo hicho kiwe cha kisiasa na sio cha kidini tena.
kwa hiyo Historia ya Uislaam inakwisha baada ya Mapinduzi na Uzalendo unaingia kwani ndipo Wakristu walipojiunga kwa sababu lengo ni kupigania Uhuru. Kabla ya hapo mtu asikudanganye kwamba Waislaam walikuwa wakipigania Uhuru..Na nazidi kukataa hii habari ya Uislaam kwa sababu hata hao kina Mtenvu na wapinzani wa TAA wakati ule walikuwepo Waislaam, sasa iweje tuchukue moja la kufurahisha lakini lenye machungu tunawaachia Wakristu.
Haya huyu Mohamed said anasema wazi yeye hakumuogopa Nyerer na aliandika kitabu chake Nyerere akiwa hai iweje mtu huyu kaweza kuandika mabaya yote ya Nyerere asifikichwe isipokuwa wale Mawaziri wenye wadhifa na hadhi kubwa Kitaifa wamwogope Nyerere ktk maswala ya kupinga kuonewa kwa waislaam. Na hata kama ilikuwa kweli navyojua mimi miaka ya 60 kufikia Uhuru hadi tunapata Uhuru asilimia kubwa ya viongozi wa chama wenye sauti ndani ya chama walikuwa Waislaam. Sioni ubavu wowote wa Nyerere kuweza kuwadidimiza Waislaam wakati ule zaidi ya Waislaam wenyewe kushindwa kutekeleza ya dini ndani ya siasa za chama.
Yoote yazungumzwe lakini ukweli unasimama vipi.. Hadi mwalimu anaondoka madarakani ni asilimia chini ya 10 - ooh no to be exact only 5% ya wanafunzi waliomaliza darasa la saba ndio walipata nafasi ya kwenda shule za Secondary. Tazameni record ya shule zetu utakuta kwamba ni mikoa ya Pwani tu ndio ilikuwa na wanafunzi wengi Waislaam wakati bara sii ajabu kabisa kukuta vijana wawili wa Kiislaam ktk darasa la wanafunzi 45.
Na shule za bara alitoka mwanafunzi mmoja au wawili tu toka kila shule kwenda Secondary wakati Mkoa wa Pwani ulichukua hesabu kubwa ya wanafunzi walioingia secondary. Wakuu fikirieni asilimi 5 ya wnafunzi kwenda secondary utaweza vipi kuwaridhisha Umma..na sababu kubwa ni kwamba hatukuwa na nafasi za kutosha secondary kulingana na shule za msingi hivyo sii lazima watu wali fail mitihani isipokuwa nafasi ndizo zilikuwa adimu.
Sasa mimi Mkerewe naweza kusema kwamba Nyerere aliwapendelea sana watu wa Pwani kuliko sisi bara ama kwa lugha nyingine aliwapendelea zaidi Waislaam (Wazaramo na Manyema) kuliko sisi Wakerewe na Wabara wavaa kaptula kwa kuwapa wao nafasi nyingi zaidi ya mikoa mingine. Hii sio lugha ya UTaifa, sii lugha ya watu wanaojiita Watanzania kama jamii moja isipokuwa ni lugha ya watu wanaojiona wao ni tofauti na wengine hivyo kuwafanya wao wabaguzi.
Sasa nikuambieni navyoiona picha mimi.. Ubaguzi wa kidini umeanza wakati wa Mwinyi (awamu ya mwisho) na kushamiri baada ya Nyerere kuondoka. Na hakika naamini kabisa kwamba Kighoma Malima alifanyiwa Ufisadi kuondolewa kwa sababu mfumo wa Elimu yetu ulianza kubadilika ghafla na Udini kutumika zaidi kuingia elimu ya juu. Na hakika kama juhudi zake zilivyunjwa nguvu yoyote ile basi mhusika mkubwa ni alikuwa rais Mwinyi - Muislaam mwingine ambaye hakupenda kuona Waislaam wakifanikiwa.
Aloandika Kighoma Malima yote yanahusiana na wakati huu (baada ya Nyerere), utawala huu wa CCM ambao umekuja kumbatia Udini zaidi kiasi kwamba alipotaka kujitoa na kuingia Upinzani alionekana mwiba wa takoni. Binafsi naamini kabisa Mkapa asingeweza kusimama na Malima ktk uchaguzi uliofuata hivyo waka Mkolimba kumaliza ubishi. Malima aliondolewa sii kwa sababu ni Muislaam isipokuwa alikuwa tishio la Upinzani kwa CCM (Siasa) na waliopitisha kuondolewa kwake wapo Waislaam.
Haya ni mawazo yangu
Huyo Jumbe alikataa kitu gani kwa Nyerere?.. ikiwa yeye aliweza kuivunja warsha ya waislaam akiwa makamu wa rais iweje tena ni kosa la Nyerere hali yeye Muislaam ambaye alikuwa na uwezo wa kukataa kama huyo Aziz..Nionyeshe hata hadithi moja ya Nyerere kuhusiana na waislaam ambayo kaifanya pasipo Waislaam wenyewe kuhusika kutoa maamuzi..
Hii habari mimi siikubaliani nayo kwa sababu ina malengo makuu ya Udini, ni sawa na kesho Chadema washinde uchaguzi huu atokee Mchagga mmoja aanze kudai wao Wachagga ndio wameiwezesha Chadema kusimama kwa sababu tu ya waasisi wake ati ndio iwe historia ya chama kwa kuchukua kabila moja na sii Watanzania waliojiunga na Upinzani...Nina hakika Chadema wasingefika hapa walipo leo kama sii kuungana na watanzania wengine kupambana na CCM Kisiasa na sio kikabila, hii ndio argument yangu..
Na ikumbukwe tu kwamba historia ya TANU ilianza tokea Kariakoo kama chombo cha kidini ambako asilimia kubwa kama sii yote ya wakazi na wanchama wake wakati huo walikuwa Waislaam. Lakini walipotaka kubadilika na kuwa chama cha kisiasa yalitokea Mapinduzi ndani ya chama cha kidini na AbdulWahid na Mwapachu kumpindua Kreist ktk uongozi na kukifanya chombo hicho kiwe cha kisiasa na sio cha kidini tena.
kwa hiyo Historia ya Uislaam inakwisha baada ya Mapinduzi na Uzalendo unaingia kwani ndipo Wakristu walipojiunga kwa sababu lengo ni kupigania Uhuru. Kabla ya hapo mtu asikudanganye kwamba Waislaam walikuwa wakipigania Uhuru..Na nazidi kukataa hii habari ya Uislaam kwa sababu hata hao kina Mtenvu na wapinzani wa TAA wakati ule walikuwepo Waislaam, sasa iweje tuchukue moja la kufurahisha lakini lenye machungu tunawaachia Wakristu.
Haya huyu Mohamed said anasema wazi yeye hakumuogopa Nyerer na aliandika kitabu chake Nyerere akiwa hai iweje mtu huyu kaweza kuandika mabaya yote ya Nyerere asifikichwe isipokuwa wale Mawaziri wenye wadhifa na hadhi kubwa Kitaifa wamwogope Nyerere ktk maswala ya kupinga kuonewa kwa waislaam. Na hata kama ilikuwa kweli navyojua mimi miaka ya 60 kufikia Uhuru hadi tunapata Uhuru asilimia kubwa ya viongozi wa chama wenye sauti ndani ya chama walikuwa Waislaam. Sioni ubavu wowote wa Nyerere kuweza kuwadidimiza Waislaam wakati ule zaidi ya Waislaam wenyewe kushindwa kutekeleza ya dini ndani ya siasa za chama.
Yoote yazungumzwe lakini ukweli unasimama vipi.. Hadi mwalimu anaondoka madarakani ni asilimia chini ya 10 - ooh no to be exact only 5% ya wanafunzi waliomaliza darasa la saba ndio walipata nafasi ya kwenda shule za Secondary. Tazameni record ya shule zetu utakuta kwamba ni mikoa ya Pwani tu ndio ilikuwa na wanafunzi wengi Waislaam wakati bara sii ajabu kabisa kukuta vijana wawili wa Kiislaam ktk darasa la wanafunzi 45.
Na shule za bara alitoka mwanafunzi mmoja au wawili tu toka kila shule kwenda Secondary wakati Mkoa wa Pwani ulichukua hesabu kubwa ya wanafunzi walioingia secondary. Wakuu fikirieni asilimi 5 ya wnafunzi kwenda secondary utaweza vipi kuwaridhisha Umma..na sababu kubwa ni kwamba hatukuwa na nafasi za kutosha secondary kulingana na shule za msingi hivyo sii lazima watu wali fail mitihani isipokuwa nafasi ndizo zilikuwa adimu.
Sasa mimi Mkerewe naweza kusema kwamba Nyerere aliwapendelea sana watu wa Pwani kuliko sisi bara ama kwa lugha nyingine aliwapendelea zaidi Waislaam (Wazaramo na Manyema) kuliko sisi Wakerewe na Wabara wavaa kaptula kwa kuwapa wao nafasi nyingi zaidi ya mikoa mingine. Hii sio lugha ya UTaifa, sii lugha ya watu wanaojiita Watanzania kama jamii moja isipokuwa ni lugha ya watu wanaojiona wao ni tofauti na wengine hivyo kuwafanya wao wabaguzi.
Sasa nikuambieni navyoiona picha mimi.. Ubaguzi wa kidini umeanza wakati wa Mwinyi (awamu ya mwisho) na kushamiri baada ya Nyerere kuondoka. Na hakika naamini kabisa kwamba Kighoma Malima alifanyiwa Ufisadi kuondolewa kwa sababu mfumo wa Elimu yetu ulianza kubadilika ghafla na Udini kutumika zaidi kuingia elimu ya juu. Na hakika kama juhudi zake zilivyunjwa nguvu yoyote ile basi mhusika mkubwa ni alikuwa rais Mwinyi - Muislaam mwingine ambaye hakupenda kuona Waislaam wakifanikiwa.
Aloandika Kighoma Malima yote yanahusiana na wakati huu (baada ya Nyerere), utawala huu wa CCM ambao umekuja kumbatia Udini zaidi kiasi kwamba alipotaka kujitoa na kuingia Upinzani alionekana mwiba wa takoni. Binafsi naamini kabisa Mkapa asingeweza kusimama na Malima ktk uchaguzi uliofuata hivyo waka Mkolimba kumaliza ubishi. Malima aliondolewa sii kwa sababu ni Muislaam isipokuwa alikuwa tishio la Upinzani kwa CCM (Siasa) na waliopitisha kuondolewa kwake wapo Waislaam.
Haya ni mawazo yangu