Lole Gwakisa
JF-Expert Member
- Nov 5, 2008
- 4,768
- 2,361
Gole Gwasika,
Mkuu hapa ndipo nisipokuwbaliana na wewe na watu kama wewe ndio Mohamed Said anawafananisha na Nyerere - Utanisamehe pia.
Ni lazima kwanza usome habari kisha fanya utafiti kujua kilichotokea na sio ku copy na ku paste hali hujui historia ya nchi. Kupingana na TANU wakati wowote au chama chochote haina maana unatokana na ubishi wa Waislaam bali ndio demokrasia ya kweli mtu kuchagua viongozi wako, kukubaliana na malengo ya chama na hata kuweza kuweka Upinzani kwani hakuna binadamu aliye kamili.
Sasa kama wewe unaamini wapo Miungu Watu ambao wanatakiwa kufuatwa tu kama sisi ni kondoo, hii haiwezi kuwa hoja kwa waumini wengine ambao wanaamini hakuna tena kondoo ila sote ni Umma mmoja.
Na Imani yako wewe haiwezi kuwa sifa kwa waumini wengine, la muhimu kwako amini unachoamini wewe kwa tafsiri yako na kaa pembeni kunywa maji ukisikia kiu. Hii habari ya WAO hivi na SISI ni hivi kisha unadai watu kupendana ndio Unafiki huu mkuu wangu. Na hakuna msikiti ambao Muislaam anakatazwa kuingia - HAKUNA kitu hiyo..samahani tena.
Haswaa Mkuu Mkandara, dhamira yangu ya kurebute maandishi ya muheshimiwa Mohammed Said si kuwa anaandika mambo ambayo hayakuwapo, la hasha yalikuwapo.Lakini pamoja na aliyoandika yalikuwepo mengine asiyopenda kuyaelezea.Yeye anatoa conclusion kutokana na msimao wake wa udini na yale aliyohadithiwa na kusikia na kuwauliza wengine wa dini yake.
Na ndio maana ya kusoma , kuna maandishi mengi tu ya kuonyesha kuwa kile anachokidhamiria ni potofu na pamoja na maandishi yake , yapo mengi tu ya kumpinga.
Na mimi sikuanza na kuongea u MIMI, lakini muheshimiwa huyu ndo kaadika kitabu cha WAO, kitu ambacho ni msingi mkubwa wa ubaguzi Tanzaia ya leo.
Kama kuna WAO basi kuna SISI, hilo halijipingi.
Katika moja ya sheria za fizikia kuna ambayo isemayo , nairudia FOR EVERY ACTION THERE IS AN EQEAL AND OPPOSITE REACTION.
Hatuishi kwenye ombwe.
Mkuu Mkandara mimi naheshimu sana msimamo wako wa kuwa pro-active ,liberal na ambao ni endelevu na hauko subjective.
Sasa katika post no2 tu mchangiaji mmoja kapost:
History should be used to build a better future!!!!! but Sheikh Mohamed Said's motive is to destroy the national unit(y).
Mwalimu hakuwa malaika na alifanya makosa mengi tu tena ya kibinadamu, lakini leo waTanzania hatuchinjani wala kubaguana, and this his major acheivement.
Simpingi Ndugu Mohammed Said kwa sababu ni muislamu , hapana , nampinga kwa sababu ya kuanzisha dhana ya kutazama kila kitu katika miwani yake ya udini na jinsi walivoonewa na wakristo.
Naleta hizi postings vile vile kurefresh your view of the other side.
Narudia tena , kueleza matatizo kila mtu anaweza lakini si mtoa mada wala wanao msaidia katika udini wanao toa solution kwa matatizo yalipyopo.
Mwezi mmoja baada ya mjadala kuanza na hii ni post ya 443 hakuna fununu ya jibu wala uelekeo.
Lazima vile vile tujue kiini cha mjadala wenyewe, kiini kinachotokana na mihadhara ya Mohammed Said kwa vijana wadogo ambao hawakuwapo wakati wa ukoloni.
Wrong conclusions zikirudiwa rudiwa , kijana wa leo anaweza kufikiri ndio ukweli.
Worse still,udini unapochukua umuhimu zaidi katika mambo yote ya kijamii basi hatuna Taifa moja, na huo ndio UMIMI na WAO on a national scale.
Sasa ni juu ya mtoa mada ambaye ni responsible awabebe watanzania wote au awabwage kwa yale anyoyatumikia.