DR Mambo Jambo
JF-Expert Member
- May 10, 2012
- 11,622
- 26,005
Dini haziluenezwa kwa Maridhiano ya Mezani!Atheist idea haikuwepo zamani hakuna uthibitisho hata kidogo ,kwa sababu mpaka leo haina nguvu.
Kama ilikuwepo ilikuwa na nguvu ndogo sana ,tena mno kiasi kwamba haikuwa na uwezo wa kujitosheleza kushawishi watu.
Nadharia ya uwepo wa Mungu ilikuwa mwanzo kabisa kushinda etheist ndio maana ilikuwa rahisi kwa dini kukua ,watu walikuwa na idea za kuabudu Miungu ,mizimu yaani kifupi vitu visivyoonekana.
Ilikuwa rahisi kwa dini kuchukua nafasi kuliko atheist kwa vile ni mfumo ambao hauna mashiko wala haujitoshelezi .
Kama waafrica walipinga ukoloni kwa nn wasipinge dini kama zimeletwa? Kama watu walipogania uhuru , resistance kibap ila mbona hawakupigana kuondoa dini?
Atheists wapo serious kuamini watu wengi duniani wanafuata uongo!?
Watu wengi wamepoteza maisha zaidi ya watu mamilioni..
Kwa wakristo Dini zimeenezwa in the name of Crusades and War na Heresy killing through burning people alive..and Empire Creation na kuweka sheria za kanisa kuwa Ndiyo kipimo cha maadili na sheria za kiutawala...
Kwa Waislamu It was through Jihad and Empire Creation ma kuziweka Sheria za Dini kuwa kipimo.cha maadili na sheria za kiutawala..
Kwahyo wengi waliamua kusali/Kuswali kuhofia maisha Yao na hasa kufa,Kunyongwa au kuchomwa moto.hadharani...
Nakupa mifano ya kidini kwanza!
Kipindi cha Musa, Musa alikuja na sheria na Amri akasema yoyote asiyeshika Sheria hizi atauwawa na kuuliwa na watu aisha kwa kupondwa na mawe au kupewa adhabu yoyote..
na waliokuwa hawaishiki kiukweli waliuliwa!..
swali ni kuwa unafikiri Nani angeendelea kuamini anachokiamini wakati usalama wa Maisha yake upo hatarini?
Kipindi cha mtume..Baada ya watu wasioshika Dini walikuwa wakipatiwa adhabu kali sana..
Na ndo maana Mtume anakiri Kuwa kulikuwa na wanafiki katika Dini..Unafikiri kwa sababu gani?
Unafiki unakuja pale mtu anapoogopa Adhabu ila ndani ya moyo wake hayupo pamoja na nyinyi...
Nataka nikupe mfano mwingine..
Chukulia sasa Hivi nikuulize wewe ni kabila gani utanitajie lile babu yako alilokuwa nalo ila babu yako na babu yako hujui alikuwa ni kabila gani na ukitrace kabila lake utakuta kuwa Kabila hilo alijipachika baada ya kufika maeneo hayo na kukaa kwa muda mrefuu..
Sasa hapo naamaanisha nini Kwakuwa wale atheists waliopinga ,walizaa watoto na watoto wao waliwakuta wazazi wao wakibehave Unafiki kwa kusali na wao pia waliamini wazazi wao wanasali..
Na wao wakarithisha kusali kwa watoto wao bila kuuliza wala kuhoji..
Na hivyo ndivyo dini ilivyosambaaa..
Na kuhofia Upoteaji wa Dini..
Ndipo ikaanzishwa Hofu ya KUCHOMWA moto kwa wanaotenda Dhambi kitu ambacho kabla ya hapo hakikuwepo..
Ukienda kwa Wayahudi hakuna Theology ya Kuwa kuna siku ya Hukumu watu watachukuliwa na kuuliwa na watu watapelekwa motoni wwngine peponi...
Kwa maelezo hayo mafupi ni kwamb Dini ni mfumo wa Kurithishana kutoka kizazi Kilichokuwa na uoga kuja kizazi chetu bila kuchunguza ukweli walioturithisha kama ulikuwa ni code au Ni maneno ya Hadithi!